Nataka kununua Heavy Motor Bike aina ya Kawasaki ila ushauri ninaopata kwa walionizunguka ndio napata uoga

Kwa nchi zetu hizi watu wa ovyo. Vyombo vya moto ni hatari lakini pikipiki ni hatari zaidi unakua hatarini mara elfu zaidi.
Watu wetu wengi wawapo barabarani hawafuati sheria ikichangia na ujifunzaji uendeshaji vyombo kiholela basi ni hatari tupu.
Nilisababishiwa ajali na mbweha mmoja, toka hapo nikaachana na pikipiki, unakua makini weee ila inatokea mpuuzi anakusababishia ajali. Sitosahau.
 
Pascal Mayalla zungumza jambo hapa Mkuu.
Mkuu Mgibeon , asante kuni tag,
Mkuu Villky_J , mimi ni bike lover, kwanza anzia hapa Pascal Mayalla apata ajali..... kisho soma shukrani zangu Waraka wa Pascal Mayalla - Asanteni Sana!
Umezungumza vitu viwili tofauti
1. Unatafuta usafiri wa gari mzuri, bajeti yako ya 7.M haiwezi kukupatia gari nzuri ila itakupatia bike nzuri. Hivyo kwa wengi humu wanaokushauri ni usinunue bike kwa ajili ya usafiri as an alternative kwasababu huna pesa ya gari zuri, kwasababu hiyo hiyo 7M, unaagiza Passo, Vitz na IST na unalipia hadi uhuru!.
2. Kununua bike as means of transport of choice for the love of it. Huku ndiko mimi nilipo. Kama wewe ni bike lover, kiukweli bike ni very addictive!. Hiyo bike niliyopata nayo ajali ni big bike yangu ya 5!, nilianza na Honda VT 250, nikaja VFR 750, nikaja CBR 1,100, na kumalizia na Buel Fire Bolt 1,200 hii niliifuata mwenyewe US nadhani ndio Buell ya kwanza Tanzania na mpaka leo 15 years later sijawahi ona Buell nyingine yoyote kwenye street za Bongo!.

Ushauri wangu.
Kama shida yako ni usafiri, hiyo 7.M yako inakupatia gari zuri tuu.
Kama ni mpenzi wa bike, just do what you love!, usisikilize maneno ya watu!.

Nina rafiki zangu 2 walinishangaa kununua hiyo bike ya mwisho na pesa niliotumia, wao walinunua magari mazuri, tumeisha wazika kwa vifo vya ajali, magari wameyaacha!, mimi nipo nadunda, na nimepanga at 60, nastaafu rasmi na kuweka barabani Bongo Harley-Davidson CVO Tri Glide!

P
 
Balaa kama Ractis ndio hazinivutii kabisa nilikuwa nataka ka subaru impreza sasa ndio hvy mambo yamegoma

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…