kibaha apo mwanzoni almaarufu mkoani kuna sehemu ina itwa mwanalugali mbele ya shule hiyo ya sekondari kuna mradi wa viwanja vilivyo pimwa na ni sehem ina weza kukufaa upo interested nikuunge na wahusika uka angalie hivo viwanja ukivutiwa uweze kufanya maamuzi?Toa namba
Ni uelekeo wa geza maxmum kutoka ferr mpk kweny kiwanja main ni km 22-23 na eneo maarufu mwembe mdogo chuo cha afya cha kigamboni
Viwanja vinauzwa kigamboni mwembe mdogo karibia na chuo cha afya kigamboni college
1. Umbali kutoka ferry mpk site ni killometer 23
2. Viwanja vimepimwa ila vipo katika michakato ya hati kwahy ukinunua unapata kwa jina lako rasmi
3. Umeme umefika tayar kumetulia hali ya hewa ni safi sana
Meter 8* 22 mil 1.5
Meter 15*20mil 2.5
Meter 35*35 mil 5
Kuhusu punguzo ondoa shaka kila kitu ni maelewano.
shukrani kwa maelezo mkuu
Kiwanja bado sijapata eneo nililoridhika nalo, wananipeleka porini wakati mimi nataka nijenge na kuhamia. Nimepandisha dau sasa hivi, milioni 20 kwa size ya 800 sqm ila isiwe porini
chamaz ya upande upi mkuu maana ninayoijua mie ya opposite uwanja wa azam had kurudi huku karibu na mbagala maji matitu.. imekuwa new squatter in town. ndo paliniboa ila kama kuna sehem ina viwanja vizur na mitaa ya kueleweka tufahamishane tuko interested
VigwazaMi Nina milio1 napata wapi kiwanja
[emoji23][emoji23]Njoo chato
KwaniniAkanunue kiwanja tuu,asiguse nyumba za jenga uza atapata depression.
Nmependa haya maelekezoKwa bajeti ya milioni 20 sqm 800 utapata kiwanja kizuri tu na eneo karibu, katika mengi mengi ya kuzingatia pia usisahau yafuatayo
- Usiwe na haraka kumbuka nyumba ni kitu cha kudumu hivyo jipe muda viwanja vipo vingi, heri uchelewe lakini upate eneo lisilo na shida.
- Usikubali kulipa 100% lipa kwa installments hata kama zitakuwa chache hii itapunguza chances za full kutapelewa.
- Hakikisha umefanya utafiti kwanza kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Utafiti namaanisha kwa kuhoji majirani, mjumbe wa eneo (jua jina lake kwanza kabla ya kumwendea, jua na anapoishi, hii ni kuepuka kupata mjumbe feki.
- Kwa kuwa umesema unafanyia kazi nyumbani na kama unahitaji internet jiridhishe kuwa internet kwa eneo unalotaka kununua ina signals strenght ya kutosha.
- Angalia ukubwa wa barabara ulizopakana nazo je zina ukubwa wa kutosha maana kuna viwanja unauziwa barabara ina mita 3 hii ina maana kiwanja chako mwisho wa siku kitamegwa kupisha barabara za mitaa/mtaa so kiwanja kitapungua ukubwa.
- Hakikisha kiwanja kinafikika tena bila shida majira yote iwe jua iwe mvua iwe mafuriko. Epuka kununua kiwanja uelekeo ambao inabidi uvuke mto au mfereji na wakati kwenye huo mto au mfereji hakuna daraja lililojengwa. Hata kama mfereji/mto utakuwa mdogo vipi acha kununua hicho kiwanja maana siku mvua kubwa ikinyesha hakika utakuwa kisiwani.
- Hakikisha unajua unataka kiwanja maeneo gani yaliyo flat kama kigambon au yaliyo na milima milima kama kimara. Hii unaweza ukaona haina maana lakini ukipata kiwanja ambacho hakipo flat ujue itakuwa ikinyesha mvua kigogo tu inabidi urudishie mchanga uliosombwa na maji na vilevile kabla ya kujenga mara nyingi itakubidi ufanye kupasawazisha au ujenge kufuata bonde/mwinuko hii inaongeza gharama za ujenzi.Vilevile angalia kiwanja hakifanya maji kutuama maana unaweza kununua sehemu wakati wa kiangazi ikija masika maji ya mtaa yanajihadhi kwenye kiwanja chako! ila wakati wa kiangazi ahh pako safi.
- Ni vizuri kiwanja kisiwe mbali sana na barabara ya lami maana kama kipo mbali sana na lami na kwa mfano una gari ina maana gharama za matengenezo na mafuta zitaongezeka maana wakati wa masika daily unakanyaga madimbwi wakati wa kiangazi daily unakanyaga mashimo.
- Jua status yako maana kama unajiona una hadhi fulani basi itakubidi utafute maeneo yahadhi yako ambayo hata majirani zako na mijengo yao liyo mingi itakuwa ni ya hadhi fulani. Hii itaepusha kujisikis vibaya pindi ushajenga halaf unaona noma hata kuwapeleka ndugu marafiki zako maana majirani zako wengi wana hadhi fulani ambazo wewe huzipendi.
- Fanya utafiti kujua kama kiwanja hakina mgogoro kwa maana ya muuzaji na wanaomhusu na wasiomhusu i.e. majirani, ndugu, watoto, serikali.
- Epuka kununua kiwanja mahali mbapo kwa siku za usoni au hata siku za mbele sana serikali ina mipango ya kutumia hiyo ardhi, maana siku serikali ikiamka ikachukua hiyo ardhi utakuta umepoteza pesa, na muda wako.
- Kabla ya kunua angalia huduma za kijamii ambazo wewe ungependa ziwe karibu na wewe je zipo?
- Mtangulize Mungu, muombe sana asikuache ukanunua kiwanja ambacho kina shida za kiroho. Amini usiamini kuna watu maisha yao yamepata shida maana walinunua viwanja ambavyo vina shida katika ulimwengu wa roho.
Mcheki huyu anaitwa rajabu 0677 281 046Mkuu habari.
Naomba namba ya dalali wako mkuu.
Ile Chanika ni Manzese ya baadaye mkuuWakuu nimejipanga na bajeti ya milioni 5 hadi 8 kwa ajili ya kununua kiwanja, maeneo ya DSM au Pwani kulingana na upatikanaji utakavyokuwa, bahati nzuri mimi nafanyia kazi nyumbani so hata eneo likiwa nje ya mji halitaniletea shida endapo litakuwa na intaneti
Baada ya kufanya utafiti wangu nimeona maeno yenye viwanja vya angalau sqm 800 ni maeneo ya Kigamboni, ambapo unaweza kupata eneo la kujenga nyumba nzuri na uwanja ukabaki
Sasa kilichonishangaza ni maeneo ya Chanika kuwa na viwanja na nyumba za bei chee sana tena maeneo yenye watu wengi tu, hili ni kwa nini?
Pia naomba kujua ni taratibu gani za kufuatwa ili kuepeukana na matapeli
ChanikaDalali wa wapi huyu, Chanika?
dodoma unapataMi Nina milio1 napata wapi kiwanja
Mkuu njoo inbox kuna viwanja bibi yangu anauza vipo kerege kwa kiwete ni tambalareMkuu habari.
Naomba namba ya dalali wako mkuu.
Wajanja wanaunua viwanja along morogoro road kibaha hadi chalinze hii ni promising area.Kanunue Kigamboni utanishukuru baadae
Umbali ni dakika 7 kutokea bagamoyo Road na barabara inafikika vizuri sana hata kwa gariMwendo wa dakika 7 kutokea road gani, Bagamoyo road?
Anauzaje Bei ya kuanzia. Ukubwa wake?
Hivi ukitoka mapinga ndio unaingia kerege halafu Bagamoyo?