Nataka kununua mchele wa mwaka huu halafu niuuze baadaye

Kuna jamaa yangu kaweka milioni 500 ya kukusanya mpunga tu,,yaani mwaka huu watu wenye pesa ndefu nao wameingia kukusanya mpunga

Hapo ni sawa..lakini sio kukusanya kilo 5000! No .kuna mishe zingine hyo hela inaingia fast tu jamani.
 
Hivi unanunua mchele let say kwa 1000@kg! May...then dec uje uuze kwa 1800-2000@kg! Means nahangaikia 1000@kwa miezi yote hiyo!!!!!!!!
Ndio ambayo Said Salim Bhakressa alihangaikia hadi sahivi anawauzia ving'amuzi vya tv mnaangalia na kumlipa 10,000 kila mwezi.

Huku vijana wake wakisimamia land reclamation na kukita project ya Fumba land katika fukwe la zanzibar.
 
Ndio ambayo Said Salim Bhakressa alihangaikia hadi sahivi anawauzia ving'amuzi vya tv mnaangalia na kumlipa 10,000 kila mwezi.

Huku vijana wake wakisimamia land reclamation na kukita project ya Fumba land katika fukwe la zanzibar.


Ah jombaa miaka ile deals zilikua nje nje .chocho sana...sio sasa aisee..nakataa! Sema ni bora kuliko kukaa bila mishe!
 
Kuna watu hawajali time value for money kabisa.

Mambo ya Present Value, Future Value na Payback period hayakufundishwa kwa bahati mbaya.

Unaambiwa sikuzote mradi mzuri ni ule unaorejesha hela ya msingi mapema kuliko unaochelewesha.

 
Zingatia kuwa thamani ya pesa leo, haitakuwa sawa na thamani ya pesa kesho au hata mwaka ujao!

Wanaofungasha vyakula na kwenda kuuza Dar sio wapuuzi.
 
Kama unachanel ya wateja mtoa mada uza tu huo mchele hayo mambo ya kusubiria bei ipande itakupotezea pesa kwan mchele kila siku watu wanakula watajibana kwenye kuvaa na kujenga lakn syo kwenye kula binafsi nipo lindi vijijin huku ninauza mchele kwa rejareja.

Kuna bosi mmoja anachukua mchele ifakara na kuupeleka masasi huwa anashusha humo njian kwa wateja yaan mwaka mzima anakimbiza tu alafu anapita na semi mzima then baada ya wiki unashangaa tena anapita na semi so hii biashara ya mchele inafaida sana kwa hawa wazee wa jumla na tena ukiwa h
Kama huna tamaa ya kupata faida kubwa utakimbiza sana.
 
Hapo nakubaliana na ww..usihifadhi ww uzs
 

Mkuu tunaweza kufanya mawasiliano mkuu ?
 
Asante kumpa ushauri. Kwani hao wadudu hawaingii kwenye mpunga?
Kwenye mpunga hawaingii, mpunga hata miaka mitatu, unatunza tu, ila mchele miezi mitatu tu, lazima tu uwaone, na huwa sio kuwa wanatoka nje bali huwa wanatokana na uvundo uvundo wa mchele, ni kama funza funza hivi.
 
Nunua mpunga ndo unahifadhika
 
Wakuu kwa nimevutiwa na hii biashara lkn sipaoni pa kuanzia nahtaj Abc ya hili jambo

Mfano nina milion 4 na nipo dar nahtaj kuleta mchele kutoka mikoan niaziae wapi na je mtaji wa kuanzia unatosha.

Natanguliza shukran, wakuu njoon
 
Wazo zuri unaweza kuja kuuza katika kipindi cha sikukuu kama Christmas na zingine ambapo bei inakuwa nzuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…