Nataka kununua mchele wa mwaka huu halafu niuuze baadaye

Nataka kununua mchele wa mwaka huu halafu niuuze baadaye

Mh! dunia ya Leo siyo ya kuamini mtu hivi hivi,chako kinakutoa uhai,miaka ya nyuma niliwahi kununua gunia za mpunga 500 nikaweka stoo za hawa watu wenye machine za kukoboa,chakushangaza muda uliposonga sana nikisubiri bei ipande, mwenye stoo akashikwa na tamaa za kutaka kuniua ili amiriki mpunga wangu ,nikiwa sijui hili wala lile,siku moja usiku saa sita nasikia watu wanagonga hodi kwangu nami bila kujua nikafungua mlango ,

Si kuamini macho yangu,nikapigwa chini ya ulinzi nakuambiwa tumetumwa tuje tukuue na bwana x, na ametupatia milioni moja,jamaa wakadai ili wasiniue niwape milioni moja na nusu wasiniue,nami bila hiyana ilibidi nifanye hivyo na baadae wakaniacha.

Ili kuamini ikiwa kweli wale watu walitumwa na jamaa au lah kesho yake kwenye muda wa saa nne jamaa mwenye stoo akiamini kuwa nimeshauawa nilienda mashineni na kukuta ameshaanza kukoboa mpunga wangu maana alikuwa na uhakika kuwa wameshanitoa uhai

Ogopa sana binadamu ,

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ulikumbuka kutoa sadaka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakupongeza kwa wazo zuri ingawa sijafahamu una lengo gani mara baada ya kununua huo Mchele.

Mimi nimenunua mchele siku kama 2 hivi zilizopita kutoka sengerema leo usiku mzigo unatua hapa mjini na lengo ni kuuza kwa jumla na rejareja.

My take:Mjasiriamali mwenye akili hutengeneza pesa wakati soko/hali imekuwa mbaya.
Unauzia qapi na bei gani nije nipate hata gunia mbili niweke kwenye kibanda vhangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poleni wanaJF kwa majukumu na mapambano ya CORONA tukumbuke kufuata maelezo ya wataalam.

Kama kichwa cha Habari kinavyoele naomba ushauri wenu wataalam wa Biashara ya Mazao. Nataka kununua mchele wa mwaka huu niuhifadhi niuze hapo baadaye.

Je, kuna athari yoyote?
Unataka mpunga au mchele??? Km mchele ninao super shinyanga
 
Hakikisha umenunua kwa bei ndogo kwa lengo la kuuza mwakani.. Mwaka huu kutakuwa na mavuno ya kutosha na soko la uhakika, hivyo bei zitakuwa za wastani.
Ila mwakani! Mmh....
Daah . . mkuu, mwaka huu ngoma itakua nzito kwa sababu World Food Programme imeshatangaza kwamba kuna uwezekano wa njaa mwaka huu. Anunue tu atapata boom mwishoni mwa mwaka huu
 
Kuna biashara zingine mtu kwa siku 7 anauhakika wa kupata laki 8 faida...every week...sasa kwa mwez huyu ana 2.4m...sasa ww umeweka mchele wako kwa miez hiyo yote uje uambulie 700@kg! Sijajua kwanini watu hatutaki badililka..wewe nunua mchele uza ..nunua uza hata ukipata faida ya 200@/sio mbaya!umedadavua vyema kbs
Aisee wewe mpambanaji sana, fursa nyingi ushazichangamkiaga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo muda boss! Unaizika hela yako kwa muda mrefu sana .anywys kupanga ni kuchagua
Muda wa MO na Backresa unaujua wewe,kule vingunguti walianza miaka na miaka mbona hawajalalamikia muda,Naomba tumuunge mkono wazo lake liko smart less compered na wasomi wengi
 
Muda wa MO na Backresa unaujua wewe,kule vingunguti walianza miaka na miaka mbona hawajalalamikia muda,Naomba tumuunge mkono wazo lake liko smart less compered na wasomi wengi

Mkuu afanye asifanye wala mimi hainiathiri chchote...kila mtu ana uhuru wa kuchangia! ...kwamba unadhani nilikua namkataza? Ameweka maoni watu tumetoa maoni yetu! Relax
 
Poleni wanaJF kwa majukumu na mapambano ya CORONA tukumbuke kufuata maelezo ya wataalam.

Kama kichwa cha Habari kinavyoele naomba ushauri wenu wataalam wa Biashara ya Mazao. Nataka kununua mchele wa mwaka huu niuhifadhi niuze hapo baadaye.

Je, kuna athari yoyote?
Unahujumu uchumi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu humu wanakatisha tamaa kabisaa hakuna biashara isiyokuwa na changamoto Cha msingi ni uvumilivu, Mimi hii biashara ya mchele nafanya sana hiyo interval ya miezi ndio nadeal nayo tena inalipa sana.

Nunua mpunga mzuri na uliokauka Bei inategemea ila Mimi nilipo shilingi inazaa shilingi weka stock subiri Bei ikae sawa then koboa mchele uza utaleta mrejesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu humu wanakatisha tamaa kabisaa hakuna biashara isiyokuwa na changamoto Cha msingi ni uvumilivu, Mimi hii biashara ya mchele nafanya sana hiyo interval ya miezi ndio nadeal nayo tena inalipa sana, nunua mpunga mzuri na uliokauka Bei inategemea ila Mimi nilipo shilingi inazaa shilingi weka stock subiri Bei ikae sawa then koboa mchele uza utaleta mrejesho

Sent using Jamii Forums mobile app


Mkuu hapa watu wanatoa maoni yao..wengine walishaifanya .wengine ndo hizo hofu za muda! Ni mhusika kuamua tu yeye na idea yake!/watu negative hatukosekani! Ukiskiliza ya watu hutafanikiwa..miluzi mingi....!
 
Back
Top Bottom