Natamani kuifanya familia yangu kuwa kama ya Bakhresa na ya akina Mo Dewji, nipeni muongozo

Dah! mkuu kama wewe ni mwanafamilia yani, sijui kwanini wanaamini katika kuajiriwa wakati mzazi wetu alikuwa mfanyabiashara mkubwa tu

Nilikuwa na mawazo hayo ya real estate lakini uchumi uko chini lazima tuanzie chini ndio tuwekeze zaidi
 
Familia zilizofaniliwa huwa wanaheshimu walichonacho na kuspend wisely

Mfano mtoto akiiba hela za baba akaenda kutumia ndivyo sivyo -hii inaitwa kujiibia .

Maana in future familia haitobaki na kitu
Hili nishaanza kulifanyia kazi mkuu walau kuweka utaratibu wa ukusanyaji mapato ili kuzuia mianya ya utapanyaji fedha baina ya wanafamilia
 
Ahsante kwa ushauri mkuu nitaufanyia kazi
 
Alipopitia Bakhresa sio Necessarily alipopitia Mo.., na wote hao ukisema wafanye walichofanya down to a T.., huenda outcome isiwe the same..., In short kuna so many happenstances in play...

Ushauri wangu kwako ni wewe binafsi ujiulize kwanini unaishi huenda unachokitaka / kitafuta sicho unachodhani....

 
Huna budi kuandaa long term plan, itakayokufanya uteseke sana kwa manufaa ya vizazi vyako, halafu mengine yaache kama bahati tu lolote linaweza kutokea katikakati hapo ukatoboa mapema na kufaidi utajiri wako.
Nilitamani kuendeleza alipoishia mzee kwani alipambana sana kufikia hatua alioiacha hakika ni hatua kubwa sana kwa mimi kuanza upya hadi kufika alipoishia mzee inaweza kuchukua umri wangu wote
 
Nenda YouTube andika neno fahari yetu bakhresa .utapata historia yake kutoka kwa mwanaye Abuubakar, pia wanakupitisha kiwanda kimoja kimoja na historia walipoanza hadi walipo. Utaongeza kitu
 
Kazanazo utafika
 
Sawa mkuu nitaisoma niielewe
 
Nilitamani kuendeleza alipoishia mzee kwani alipambana sana kufikia hatua alioiacha hakika ni hatua kubwa sana kwa mimi kuanza upya hadi kufika alipoishia mzee inaweza kuchukua umri wangu wote

Hapo ndio makosa tunafanya, unataka kuanza upya baada ya kuanzia alipoishia Mzee wako na kuendelea kwenda mbele.

Kama Mzee wako alijenga, huhitaji kujenga zaidi ya kuboresha hapo alipojenga na wote mkae hapohapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…