Natamani ningefeli shule

Kesho kunani

Member
Joined
Sep 10, 2023
Posts
72
Reaction score
191
Kama ningefeli shule Ninayopitia Sasa bila Shaka nisingeyapitia.

Kama ningefeli shule bila Shaka ningeenda veta na Sasa ningekuwa na ujuzi Fulani.

Kama ningefeli shule bila Shaka jamii isingekuwa inaniangalia Kama inavyoniangalia Sasa,ningekuwa huru,nisingenyoshewa vidole ninapoendesha boda boda au ninavyopakia mchanga kwenye magari.

Kama ningefeli shule bila Shaka ningekuwa na amani, majuto niliyokuwa nayo ya kupoteza muda shule nisingekuwa nayo.

Kama ningefeli shule classmate wangu wasingejadili kila ninachofanya,maana saizi kila ninachofanya watu wanajadili , nikiuza viepe utasikia kunani kesho anauza chips siku hizi, nikiendesha boda utasikia kunani kesho kawa boda boda licha ya kufaulu kote kule.

Kama ningefeli shule bila Shaka nisingekuwa na ugomvi muda wote na mke wangu,maana naamini alinikubalia kwakuangalia ufaulu wangu,alijua nitakuwa mtu mkubwa na haijawa hivyo,kwasaaa ndani ya nyumba ni miguno na misonyoo isiyokuwa na mwisho.

Kama ningefeli shule bila Shaka ningekuwa na amani Sana.

Kunani kesho.
Kwasasa songea.
 
Dunia inanjia zake za kurekebisha mambo. Ukiwa patient and persistent, things will unfold.

I speak from experience.
 
Mwenzake mimi nimesoma water resources chuo cha maji na nimekaa home miaka miwili nika apply nikaenda changombe nikafeli nikaapply interview ya pili dodoma ukumbi wa asha rose migiro udom nikatoboa
 
We chapa kazi acha maneno mengi.
 
Only in one country: Tanzania. Only in one continent: Africa.

Huwezi kuta udhalilishwaji wa Elimu Ulaya na Marekani.
 
Ndo maana wasomi wengi wanahama mikoa waliyowahi soma hapo mwanzo.
 
Komaa boy, ila umaskini ni matokeo ya fikra si mazingira
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…