Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 24,831
- 45,154
Unamfumua mtu risasi ya ubongo ukijua kbs hastahili ila ni tamaa ya mali zake?Changamoto huwa ni kuthibitisha kwamba nilikutuma.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unamfumua mtu risasi ya ubongo ukijua kbs hastahili ila ni tamaa ya mali zake?Changamoto huwa ni kuthibitisha kwamba nilikutuma.
kwa bahati mbaya, polisi hata wapate mateso au maumivu gani huwa hawatetewi, wanachukiwa, though kwa upande mwingine kazi yao inafanya wengi tulale usingizi. tung'ate na kupiliza, ni watoto wetu hao, kaka zetu, dada zetu, mama zetu na kadhalika.(Ameandika Malisa G. )
SSP Christopher Bageni atanyongwa hadi kufa. Ndivyo mahakama ya rufaa ilivyoamua. Maamuzi ya leo ni ya mwisho ktk mwenendo wa kesi yake. Hana pengine pa kukata rufaa, pa kukimbilia, wala pa kupinga. Mahakama imeamua anyongwe hadi afe. Jaji Stellah Mugasha amegonga nyundo. Itz over.
Hawezi kukata rufaa tena kwa sababu hukumu ya leo ni review ya hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo September 16, 2016, ambapo alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Benard Luanda. So hakuna mahakama ya kujadili tena shauri lake, labda Rais ampe msamaha.
Kwa wasiokumbuka Bageni alikua Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Kinondoni. Mwaka 2006 yeye na wenzie wakiongozwa na aliyekua Kaimu RPC Dar, Abdalah Zombe, walituhumiwa kupanga njama za kuwauwa wafanyabiashara watatu wa Morogoro.
Zombe anadaiwa ndiye aliyeongoza wenzie kwenye mpango huo, baada ya kujulishwa kuwa wana madini na fedha kiasi cha shilingi milioni 200.
Walikamata gari waliyokua wameikodi. Wakamuongoza dereva hadi msitu wa Mabwepande. Wakapora madini pamoja na fedha zote walizokua nazo. Kisha wakawafunga vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi. Kisha wakawapiga risasi za kisogoni na kuwauwa wote akiwemo dereva wa taxi waliyemkodisha.
Kesho yake Zombe akaita media na kusema wameua majambazi yaliyokua yanarushiana risasi na Polisi. Rais Kikwete akaunda tume ya Jaji Kipenka kuchunguza. Ikabainika hawakuwa majambazi. Kilichouma zaidi walikua ndugu wa familia moja. Mama mmoja alipoteza wanae watatu. Watoto wa familia 4 wakapoteza baba zao, na wake wanne wakawa wajane kwa tamaa za polisi.
Zombe alifanikiwa "kuchomoka" kwenye kesi hii baada ya kusota rumande kwa miaka kadhaa. Lakini Bageni alipatikana na hatia akahukumiwa kunyongwa. Akakata rufaa ikafeli, akaomba review ya kesi, na rulling imesomwa leo kuwa ANYONGWE HADI KUFA.
Waliomtuma hawapo nae Segerea, wala hawatanyongwa pamoja nae. Atanyongwa peke yake. Wanaohangaika nae saivi angalau kumfariji ni familia yake. Zombe hayupo, OCD wake hayupo hata IGP wa wakati huo hayupo. Ni yeye mwenyewe, na atanyongwa mwenyewe.
Hii iwe fundisho kwa wote wanaotumwa kufanya maovu leo e.g kuteka, kuua na kupoteza watu. Ipo siku utajikuta peke yako. Anayekutuma hatakuwepo. Utasimama wewe mwenyewe kutoa hesabu ya maovu yako. Kama si hapa duniani basi hata mbinguni, lakini ipo siku utalipa. Kama ambavyo wema ni mbegu, na ubaya pia ni mbegu. Humea, hukomaa, na ni lazima UVUNE.!
MImi sikuishi nao ila nilikuwa nawatembelea kwa mjomba.Karma lazima ifanye Kazi .
Nimekaa kota , hawa jamaa maisha yao huwa sio mazuri karma huwa zinasambaratisha familia zao na wao wenyewe . nimeishi nao nawaelewa Sana .dhulumati.
Kombani!!??Kwa hali ya siku hizi ambapo utekaji na maauji ni deep state sponsored sidhani kuna hakimu atakaye enda kinyume na Muhimili wenye mizizi mirefu zaidi.
Hata kesi hiyo ni sababu ya ushawishi wa marehemu mbunge Selina kwa Kikwete (waliouwawa walikuwa watu wa sehemu moja na Selina)
Selina Kombani?Kwa hali ya siku hizi ambapo utekaji na maauji ni deep state sponsored sidhani kuna hakimu atakaye enda kinyume na Muhimili wenye mizizi mirefu zaidi.
Hata kesi hiyo ni sababu ya ushawishi wa marehemu mbunge Selina kwa Kikwete (waliouwawa walikuwa watu wa sehemu moja na Selina)
Kuna mengi Sana Ila baada ya wao kuacha Kazi hufariki mapema sanaMImi sikuishi nao ila nilikuwa nawatembelea kwa mjomba.
Ukiona wana tembelea viyoyozi acha kuvitamani vina mengi
Bado tunasubiri wale wa mtwara nao wale kamba.(Ameandika Malisa G. )
SSP Christopher Bageni atanyongwa hadi kufa. Ndivyo mahakama ya rufaa ilivyoamua. Maamuzi ya leo ni ya mwisho ktk mwenendo wa kesi yake. Hana pengine pa kukata rufaa, pa kukimbilia, wala pa kupinga. Mahakama imeamua anyongwe hadi afe. Jaji Stellah Mugasha amegonga nyundo. Itz over.
Hawezi kukata rufaa tena kwa sababu hukumu ya leo ni review ya hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo September 16, 2016, ambapo alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Benard Luanda. So hakuna mahakama ya kujadili tena shauri lake, labda Rais ampe msamaha.
Kwa wasiokumbuka Bageni alikua Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Kinondoni. Mwaka 2006 yeye na wenzie wakiongozwa na aliyekua Kaimu RPC Dar, Abdalah Zombe, walituhumiwa kupanga njama za kuwauwa wafanyabiashara watatu wa Morogoro.
Zombe anadaiwa ndiye aliyeongoza wenzie kwenye mpango huo, baada ya kujulishwa kuwa wana madini na fedha kiasi cha shilingi milioni 200.
Walikamata gari waliyokua wameikodi. Wakamuongoza dereva hadi msitu wa Mabwepande. Wakapora madini pamoja na fedha zote walizokua nazo. Kisha wakawafunga vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi. Kisha wakawapiga risasi za kisogoni na kuwauwa wote akiwemo dereva wa taxi waliyemkodisha.
Kesho yake Zombe akaita media na kusema wameua majambazi yaliyokua yanarushiana risasi na Polisi. Rais Kikwete akaunda tume ya Jaji Kipenka kuchunguza. Ikabainika hawakuwa majambazi. Kilichouma zaidi walikua ndugu wa familia moja. Mama mmoja alipoteza wanae watatu. Watoto wa familia 4 wakapoteza baba zao, na wake wanne wakawa wajane kwa tamaa za polisi.
Zombe alifanikiwa "kuchomoka" kwenye kesi hii baada ya kusota rumande kwa miaka kadhaa. Lakini Bageni alipatikana na hatia akahukumiwa kunyongwa. Akakata rufaa ikafeli, akaomba review ya kesi, na rulling imesomwa leo kuwa ANYONGWE HADI KUFA.
Waliomtuma hawapo nae Segerea, wala hawatanyongwa pamoja nae. Atanyongwa peke yake. Wanaohangaika nae saivi angalau kumfariji ni familia yake. Zombe hayupo, OCD wake hayupo hata IGP wa wakati huo hayupo. Ni yeye mwenyewe, na atanyongwa mwenyewe.
Hii iwe fundisho kwa wote wanaotumwa kufanya maovu leo e.g kuteka, kuua na kupoteza watu. Ipo siku utajikuta peke yako. Anayekutuma hatakuwepo. Utasimama wewe mwenyewe kutoa hesabu ya maovu yako. Kama si hapa duniani basi hata mbinguni, lakini ipo siku utalipa. Kama ambavyo wema ni mbegu, na ubaya pia ni mbegu. Humea, hukomaa, na ni lazima UVUNE.!
NakumbukaYaani alieita Waandishi wa Habari anaachiwa ananyongwa mtu mwingine na kumbuka hiyo kwenye hiyo kesi yupo askari alifia wakiwa jela kifo cha utata sana na huyo ndio alikua na ushahidi wa kesi yote..
Sio polisi tu hata wale wa HardTop HZ-1Kuna mengi Sana Ila baada ya wao kuacha Kazi hufariki mapema sana
Zombe alitoka kwa michongo sidhani kama dini inaplay part hapa.Story tu. Zombe alitoka sababu ya dini yake.
Ukweli mchungu ni kwamba Askari Polisi wengi zaidi ni Wahalifu wabaya Sana, wengi wao wamemwaga damu nyingi sana za watu wasio na hatia. Askari Polisi ambao ni raia wema watenda haki ni wachache Sana kupita kiasi. Polisi Wahalifu ndio ambao wameliteka Jeshi hilo.kwa bahati mbaya, polisi hata wapate mateso au maumivu gani huwa hawatetewi, wanachukiwa, though kwa upande mwingine kazi yao inafanya wengi tulale usingizi. tung'ate na kupiliza, ni watoto wetu hao, kaka zetu, dada zetu, mama zetu na kadhalika.
Wale jamaa walifanya ukatili wa hali ya juu sana aisee unaofanana na huu dogo wakampa kesi ya kuiba boda boda na kumuua wapo watu wakatili sana sijui kesi yao inaendeleaje?Bado tunasubiri wale wa mtwara nao wale kamba.
Nimeshangaa kwani hao wengine walikua hawana dini?Zombe alitoka kwa michongo sidhani kama dini inaplay part hapa.
Nakumbuka Sana jinsi huyo aliyewatuma akijibu hoja za baadhi ya watu. Alisema bila kusita kwamba yeye hatofanyiwa lolote na wala hatafungwa kwa vile anajua Sheria ilivyo. Hapakuwepo na ushahidi wa moja kwa moja wa kumuhusisha yeye na mauaji hayo.Ingependa na aliyewatuma akaunganishwa katika hiyo Kesi.
Kumuachia Huru Huyo Mkuu wao inafikirisha namna haki inavyotendeka.
Ingependa na aliyewatuma akaunganishwa katika hiyo Kesi.
Kumuachia Huru Huyo Mkuu wao inafikirisha namna haki inavyotendeka.
Yupo haiAliyewatuma ni Bwana Zombe. alishatangulia Jehanam
Ndio maana nasisitiza tukatae ulevi wa Dini.Nimeshangaa kwani hao wengine walikua hawana dini?
Namshukuru Mzee wangu alitoa huo ulevi nikiwa bado nakua kwa hiyo sina huo ujinga maana yeye alikua anasema kumuona mtu mwingine ni tofauti na wewe kwa sababu ya dini yake huo ni ujinga toeni ujinga kwa kutotofautiana kwa dini zenu..Ndio maana nasisitiza tukatae ulevi wa Dini.
Sio vibaya kuwa na dini ila kuendekeza dini sana kila unayemuangalia hutaiona status yake wala ubinadamu wake bali dini yake.
Hata isipofanya!Kwanza sheria yakunyongwa inafanya kazi kwa usahihi au ni maneno maneno tu .