Natarajia kununua gari yangu ya kwanza, naomba ushauri

Update: Asante sana kwa maoni yenu na ushauri wenu kwa kuwa sikutoa update mwezi wa 11 mwishoni niliamua kuchukuwa Subaru forester XT ile second generation version ya JDM . So far am loving it sijui kwa huko mbele.

Kama nilivyosema nyuma sina mizunguko mingi mara experience yangu ni nikijaza full tank natumia almost mwezi mzima kama siku 25 alafu najaza full tena
 
Ya mwaka gan mkuu
 
Cha kuchekesha nimeamua kushare na nyie majuzi nilimuazima sister aende nayo church alivyonirudishia akasema gari ilitaka kumuingiza mtaroni nikamuuliza kwanini anasema alikanyaga mafuta gari ikaruka mbele sana nikajua huyu alikanyaga mafuta kwa ghafla rpm ikawa juu turbo ikaingia ndio maana gari iliruka mbele ghafla , gari ya sis anayoendesha kila siku ni Vitz
Kama sio dereva mzuri inakutupa hii
 
Nataka ninunue Toyota Allex CC 1490 unanishauri nini?
 
Hajui subaru ukigusa ishafika mwisho wa safari, vitz na Ist mpaka ukanyage sana
 
Ukipata note jichange uchukue ile ya 2008 au 2010 utaenjoy
Hahaha unajuwa mm nataka ile ya Forester ya 2007 ila STI inayokuja manual ya gia 6 .Sema bei zake zimesimama sana aisee
 
Full tank unajaza kwa shingap?
 
Kiukweli sina accurate value maana huwa naona yanakaribia kuisha najazilizia mfano mara ya mwisho ilikuwa nilitoa 120K ila ww piga hesabu forester karibia zote ni tank ni lita 60 piga kwa litre moja itakuwa shs ngap
 
Kiukweli sina accurate value maana huwa naona yanakaribia kuisha najazilizia mfano mara ya mwisho ilikuwa nilitoa 120K ila ww piga hesabu forester karibia zote ni tank ni lita 60 piga kwa litre moja itakuwa shs ngap
chief
ulimvua mtu au uliagiza,

weka na bei kabisa kama hutojali
 
Nilichukuwa 12.9M ilikuwa kwa mjeda mmoja aliagiza mwaka jana Japan sema yeye kaenda course nje ya miezi 6 Kaamua kuuza ilikuwa jumla na km 80,000. Nimepata na document zake kama user manual na vingine sijapata muda kuvipita
 
Kaka pia kuna kitu unasahau, kwenye maamuzi ya kununua gari, fuel efficiency, resale value etc…ni mojawapo ya vigezo. Kuna vigezo vingine pia. Mf. Kuna swala la status. Kwamba madmax anasukuma BMW (wenyewe wanaita bima), ni kigezo kwa wengi wetu, ingawa siyo Mara nyingi tunakiweka wazi.

Wengi tunaponunua Europe cars au high end SUVs, kuna vigezo Vingi vinatusukuma. Lakini ile feeling kwamba jamaa anaendesha VW, range, au BM, ina maana kubwa kuliko kuendesha Subaru au Crown. Lakini pia, ukienda kuomba tender kwenye ofisi ukiwa unasukuma range (hata kama imechoka) na anayekwenda na crown…….jibu unalo.

Again, sipingi ushauri wako, lakini kwenye maisha kuna level unafika unataka kuwa tofauti na wengine. Pia, kuna level ya maisha, costs za kufanya maintenance ya Chuma kama hizo, zinakuwa kawaida. Siyo big deal.

Ni kama ukute jamaa anakunywa beer ya 10,000 pale mlimani city, wakati opposite na pale beer ni 2000, unafikiri anasukumwa na nini? By the way na hao ni vipato vya kawaida tuu au vijana waajiriwa wa benki zetu hizi za akina Azania na Mkombozi…so is life!
 
elf 25 mwez mzima? 😳
 
Kwa upande wangu naona kitu muhim sana ni kujuwa gari utakuwa unalitumia hasa kwa lipi kama ni daily driver au kwa long trips na kujuwa pia running costs za hio gari ili usilione chungu likishakuwa kwenye umiliki wako
 
Achana na gari old model kijana....jichangechange utumie gari recent kidogo zenye upgrade ya vitu vingi including safety features...buy a car inayoweza kukulinda pia siku lolote likitokea
Recent which?? wew nunua gari ya kujifunzia kama ndo unaanza maisha hizo za mzungu au gari weseee inakula kama ina wazimu aiseee utayachukia magariii, kamata IST..VITZ yani humooo premior nayo inavumilia shida unanunua mzungu hujui hata kuna suala la kuangalia oil kila siku?? maji unajisahau mpaka gari inachemshaaa service ndo unapitisha miezi 6 mbeleee
 
Unatarajia matumizi ya gari yako yawe yapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…