Nateseka sana na complicated U.T.I. Naelekea kukata tamaa, nisaidieni niondokane na mateso haya

Nateseka sana na complicated U.T.I. Naelekea kukata tamaa, nisaidieni niondokane na mateso haya

Kutoka moyoni kabisa SIJAWAHI KUFANYA HIVYO iwe kwa mwanamke au kwa mwanaume. Ninahitaji sana msaada wa utatuzi,, ningekuwa nimeshawahi hata mara moja ningesema wazi maana nahitaji kupata ufumbuzi.
Kaka, mimi ni mwanamke nilishasumbuliwa sana na UTI Japo yangu sio hiyo complicated, bali ilikuwa sugu, nilikunywa sana antibiotics, nilichoma sana pawercef ila tatizo linarudi wiki tu baada ya kumaliza dose, maumivu ya tumbo kwenye kinena yalinisumbua mpaka nikahisi nina tatizo kwenye kizazi ikabidi nikamuone gynecologist nikakuta kizazi hakina shida, yeye mwenyewe akabaini ni UTI inanisumbua, akanipa dawa bila mafanikio, nikahamia upande wa tiba miti(medicinal plants) nimekunywa blacks seeds oil na kalinji seeds powder mpaka nimepona. Kuanzia mwaka juzi mpaka leo nikipima UTI sina. Nenda maduka ya asili wana dawa nyingi za kutibu hayo maradhi kaka ulizia unga wa habat soda au mafuta ya habat soda uwe unakunywa katika chai au uji, maduka ya asili yaliyo karibu nawe utapata
 
Tatizo, kuna vitu watu mnafanya halafu mnapokuja kuomba ushauri huwa mnaongea kama haya maradhi yamewakuta tu......

Naomba nikuulize, huwa hauli nyuma yaani kula mwanamke hata mwanaume kinyume na maumbile haujawahi fanya hiyo kitu?!

Sent using Jamii Forums mobile app
sasa hilo swali lako litamsaidiaje huyu bwana maana diagnosis ishapatikana na details zote za tatizo zipo pamoja na majibu ya vipimo vyote alivyopima, issue ni tiba
 
Kaka, mimi ni mwanamke nilishasumbuliwa sana na UTI Japo yangu sio hiyo complicated, bali ilikuwa sugu, nilikunywa sana antibiotics, nilichoma sana pawercef ila tatizo linarudi wiki tu baada ya kumaliza dose, maumivu ya tumbo kwenye kinena yalinisumbua mpaka nikahisi nina tatizo kwenye kizazi ikabidi nikamuone gynecologist nikakuta kizazi hakina shida, yeye mwenyewe akabaini ni UTI inanisumbua, akanipa dawa bila mafanikio, nikahamia upande wa tiba miti(medicinal plants) nimekunywa blacks seeds oil na kalinji seeds powder mpaka nimepona. Kuanzia mwaka juzi mpaka leo nikipima UTI sina. Nenda maduka ya asili wana dawa nyingi za kutibu hayo maradhi kaka ulizia unga wa habat soda au mafuta ya habat soda uwe unakunywa katika chai au uji, maduka ya asili yaliyo karibu nawe utapata
Asante sana dada yangu kwa ushauri, nitautafuta unga/mafuta hayo.
 
Unaishi na mke? Je, ulishampeleka kwa madakatar bingwa kupimwa yeye kama ana infections njia us uzaz?


NB: mwanamke anaweza kuwa na infections za hzo UTI bila kuonekana rahis zaid ya mwaka,unajikuta unakarbia kupona,unakutana nae,unawachukua wadudu
Mke ninaye. Alishawahi kupima mwenyewe na hakuwa na UTI.
 
unatakiwa utumie dawa hizi

1.cefixeme2na secnidazole single dose

baada ya hapo utumie hizi dawa

Azithromyce1od 6/7

metronidazole2tds7/7

gynozol1od3/7

fluconazole 150mg 1od1/12

Natumaini ukitumia dawa hizi utapona kabisa
 
Nenda ukapime na tezi dume mana hizo dalili kama zinafanana
 
"UTI in men is always considered complicated and treatment should be targeted at the likely bacteria".

Nenda hospital kapime kipimo cha urine culture kujua ni bacteria gani wanakusumbua ili upate dawa sahihi. Pia utaongezea na Doxycyline tabs.

Lazima afanye culture and sensitivity ili kujua dawa iko sensitive au resistant, kuna mda doxy zinakua resistant so lazma ifanyiwe sensitivity kujua itamtibu au vp
 
Mimi sishauri mtu atumie dawa bila kufanya urine culture and sensitivity, matibabu ya kuhisi kwamba dawa flani itatibu hayawezi kumsaidia mgonjwa.

Utampa mgonjwa several antibiotics bila mafanikio ni lazima mgonjwa anayekua suspected na UTI afanye kipimo hicho cha culture and sensitivity lengo ni kujua dawa zipi zitakua sensitive na dawa zipi zitakua resistant based on CLSI reference.

Natamani diagnosis ya UTI iwe kwenye Algorithm ya wizara kama ilivyo diagnosis ya HIV ingesaidia watu wengi kutotumia dawa bila kuwa na uhakika. Leo hii mtu anaenda hospital saa 2 asubuhi anapimwa mkojo majibu yanatoka nusu saa baadae au dak 45 anaambiwa ana UTI anapewa na vifurushi vya dawa?? Saa ngapi imefanyika sensitivity kujua labda Gentamycin aliyopewa itaitibu hiyo UTI? Ciprofloxacin aliyopewa itaitibu hiyo UTI?

Angalia mfano wa ripoti hii mgonjwa amefanyiwa sensitivity na kila dawa imekataa, ingekua ni kwa matibabu ya kuhisi kwamba apewe dawa flani si angemaliza dawa zote hizo bila mafanikio?
IMG_20201224_082125_139.jpg
 
Sawa,hii urinal culture na sensitivity wanapima wapi na bei yake ya vipimo ni laki ngapi?
 
Sawa,,hii urinal culture na sensitivity wanapima wapi na bei yake ya vipimo ni laki ngapi?
Kwa dar nafahamu muhimbili wanapima na aga khan wanapima nadhani pia hindu mandal watakua wanaipima na Regency pia referral hospital kama amana nadhani watakua wanafanya. Muhimbili na aga khan hospital nina uhakika kipimo hicho kinafanyika kwa sababu ni sehemu ambazo nimefanya kazi.

Kwa bei sasa hapo zinatofautiana kutokana na hospital ila naamini haizidi 50,000 tsh, kwa hospitali za serikali bei itakua ni pungufu ya hapo. Sina uhakika na bei kwa sababu kwa hospital kama aga khan kuna watu maalum wa billing ndio wanajua bei za mambo zote hizo.
 
Choma sindano saba za ceftriazone kwa siku sindano moja hiyo dawa ni komakoma.
Moja ya dawa ambayo imezidi kuwa resistant kwa watu wengi ni hiyo Ceftriaxone, hivyo makampuni ya kutengeneza dawa yakaiboresha na kuiongezea dawa nyingine in combination. Hiyo combination ndio iko super kwa sasa sijawahi kuona ikifeli. Now wameleta inaitwa Cetriaxone+Sulbactam+Disodium EDTA. Ila ceftriaxone yenyewe kama yenyewe imeshaanza kupungua makali ishu ya antibiotic resistant inazidi kushika kasi.

Kikubwa akafanye sensitivity kujua dawa ipi itamtibu asibahatishe.
 
Back
Top Bottom