NATO walalamika kuwa Prigozhin kuhamishiwa Belarus kunahatarisha zaidi usalama wa nchi za NATO za ukanda huo

Kama Putin alishindwa kuichukua Kyiv February Mwaka jana na jeshi rasmi akitokea Belarus kukiwa na msafara wa kilometa zaidi ya 60 wa vifaru huku Ukraine ikiwa haina silaha kama ilizo nazo leo basahu sahau kuichukua akiwa na jeshi la mamluki.
Ni mjinga tu anayefikiri putin alishindwa kuchukua ukraine.hakushindwa ila aliingia makubaliano na Ukraine kuwa asichukue Kiev acha kupotosha.
 
Natamani NATO ihusike moja kwa moja kwrnye vita hii ili Urusi na Belarus kwa pamoja zipigwe na majeshi ya NATO ili kuipa ahueni nchi ya Ukraine.
Ni mjinga tu anayefikiri NATO anauwezo wa kupiga urusi kwa sababu silaha za nuclear zitatumika na hakutakuwa na mshindi na dunia itaharibiwa kwa hiyo usifikiri kuna siku NATO wataingia vitani moja kwa moja na warusi acha wajiitie volunteers huko Ukraine.
 
Acha maneno dunia nzima inajua Nato ipo Ukraine na majeshi ya nchi hizo wengi wameuwa Kuanzia wamarekani na hata wafaransa nyie jidanganyeni eti Ukraine anapigana peke yake na Mrusi
 
Mwanamume kutua tu Belarus, NATO vijambio vinawapwita sasahivi mwendo wa vikao tu kama wanga
 
Kama Putin alishindwa kuichukua Kyiv February Mwaka jana na jeshi rasmi akitokea Belarus kukiwa na msafara wa kilometa zaidi ya 60 wa vifaru huku Ukraine ikiwa haina silaha kama ilizo nazo leo basahu sahau kuichukua akiwa na jeshi la mamluki.
Uwe unafuatilia mambo. Kilichorudisha ni mkataba wa makubaliano huko Turkey. Russia akaheshimu mkataba kama sehemu ya maridhiano akasitisha safari ya kiev makusudi.
 
Kama ni plan ,waliipanga vzr
 
Uwe unafuatilia mambo. Kilichorudisha ni mkataba wa makubaliano huko Turkey. Russia akaheshimu mkataba kama sehemu ya maridhiano akasitisha safari ya kiev makusudi.
Acha porojo wewe,

Javelin missiles ndio zilikimbiza vifaru vya Urusi Kyiv.
 

Libya alimpiga mwanachama gani wa NATO?? mbona walienda kumvamia kwa mbwembwe zote.??
 
Kwa hiyo NATO wanawaogopa hao wanamgambo hahaha
 
Libya alimpiga mwanachama gani wa NATO?? mbona walienda kumvamia kwa mbwembwe zote.??
Baraza la usalama la UN walipitisha azimio 1973 lilitoa kibali kwa NATO au muungano wa kijeshi wenye nguvu kuweka no fly zone Libya, Urusi ni wanachama wa kudumu wa baraza la usalama la umoja wa mataifa na hawakupinga hilo azimio.
 
Baraza la usalama la UN walipitisha azimio 1973 lilitoa kibali kwa NATO au muungano wa kijeshi wenye nguvu kuweka no fly zone Libya, Urusi ni wanachama wa kudumu wa baraza la usalama la umoja wa mataifa na hawakupinga hilo azimio.

Hii ndo no fly zone??

Vipi kuhusu Iraq? Alimvamia mwanachama gani wa NATO??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…