NATO wamefikwa na Nini? Mbona waliweza Kuwait na wakaweza Kosovo,wanashindwa Nini Ukraine?

NATO wamefikwa na Nini? Mbona waliweza Kuwait na wakaweza Kosovo,wanashindwa Nini Ukraine?

Kuna msemo unasema ni rahisi kuwa namba 1 ila ni vigumu kubaki namba moja wakati wote, USA ilishakua namba 1 hivyo anajitahidi kubaki na. 1....shida inakuja wanaotaka hiyo na. 1 ya USA ndiyo hawachangi karata vizuri.

Ebu fikiria suala la Rusia kutaka kuweka silaa karibu na USA kupitia CUBA ilimalizwa ki diplomasia bila USA kupoteza baadhi ya resources zake na Rusia waliondoa hizo silaa. Kama Rusia walijua maadui zake wanataka kuweka Silaa karibu yake akishindwa nini ushawishi?

Ukubwa pia unapimwa kwa busara siyo uwezo wa kumpiga mtu makonde tu.
Kongole kwako, umenena vema sana.
 
hivi weweeeee unaijua 'geopolitics' za ulaya na urusi weweeeee? Hayo mataifa ya ulaya yamekuwa 'overrated sana' kumbuka kuna mchina yupo nyuma ya mrusi! By the way, waarabu wanamsapoti urusi katika hili unasemaje hapo sasa!
hivi weweeeee unaijua 'geopolitics' za ulaya na urusi weweeeee?
Hayo mataifa ya ulaya yamekuwa 'overrated sana' kumbuka kuna mchina yupo nyuma ya mrusi! By the way, waarabu wanamsapoti urusi katika hili unasemaje hapo sasa!

WAARABU WANA NN HAO CHA MAANA!?
OHOO WESTERN WAPO OVERRATED ILHALI HAO NDIO WALIOUNDA UN NA MKASHOBOKA KUJIUNGA NA KUWEKA BENDERA ZENU MAKAO MAKUU PALE NEW YORK.
Bank ya dunia ipo kwao.
Mashirika makubwa ya fedha yapo kwao.
Utasemaje wako overrated!?
Hiyo China uisemayo wewe haijitoshelezi kuisaidia Russia ikainuka .
Ndugu mtake msitake uchumi wa dunia umeshikiliwa na hao mabwana.
 
Yaani wewe inaonekana haya mambo ya siasa za kimataifa yamekupita kushoto...Yaani marekani na NATO wamuangamize Russia![emoji849] Utakuwa umeamua kuchekesha kama huyo rais mchekeshaji wa Ukraine.
Kifupi ni kwamba marekani na NATO wameshajaribu kuingia Russia mara 2, kwenye world war I na World war II, walipigwa vibaya sana na hawatothubutu tena. Ndo maana unaona wamemuacha Ukraine mkiwa ahangaike na mwenyewe
Sometimes it's better not to drop your comment if you know you don't have a bit of substance to drop here. Sasa lini USA alijaribu kuingia Russia wakati wa WW 1& 2 akashindwa. Mbona mnatufanya mazuzu humu. Kwani ukija na hoja zenye ushahidi wa kihistoria tutakataa?
 
Sometimes it's better not to drop your comment if you know you don't have a bit of substance to drop here. Sasa lini USA alijaribu kuingia Russia wakati wa WW 1& 2 akashindwa. Mbona mnatufanya mazuzu humu. Kwani ukija na hoja zenye ushahidi wa kihistoria tutakataa?
Safi Sana.. WWI Urusi alipigana ndani ya muungano unaoitwa wa Allies, na ule muungano unaoitwa wa Central (ulioongozwa na ujerumani) walipotaka kuingia Russia walikwama. Kwenye world war ii Russia alipigana kwenye muungano wa allies tena na axis walipotaka kuichukua Russia walishindwa..sasa key point yangu hapo hizo nchi zinaunda NATO sasa hivi kama Germany, Hungary, Czechoslovakia, Turkey nk kwenye world war ii walikuwa upande wa Axis ( mjerumani) na walijaribu kuiteka Russia wakashindwa. Kwahiyo kuwepo marekani na hao kwenye NATO will not make any difference
 
Safi Sana.. WWI Urusi alipigana ndani ya muungano unaoitwa wa Allies, na ule muungano unaoitwa wa Central (ulioongozwa na ujerumani) walipotaka kuingia Russia walikwama. Kwenye world war ii Russia alipigana kwenye muungano wa allies tena na axis walipotaka kuichukua Russia walishindwa..sasa key point yangu hapo hizo nchi zinaunda NATO sasa hivi kama Germany, Hungary, Czechoslovakia, Turkey nk kwenye world war ii walikuwa upande wa Axis ( mjerumani) na walijaribu kuiteka Russia wakashindwa. Kwahiyo kuwepo marekani na hao kwenye NATO will not make any difference
Nice explanation! Lakin unasahau kua au maybe hujui mataifa gani yalikua frontline kupigana na aggressors wa WW 2? Russia na Marekani uadui umeanza rasmi na kuiva baada ya ya WW 2, baada ya USSR kushida ulaya mashariki kwa kumtandika Germany na Marekani kushinda Far East kwa kumtandika Japan. Sasa mbona kama hapa wote walishirikiana kuleta balance na amani duniani kwenye hii vita, lini Marekani alijaribu kuingia Russia kwenye huu wakati wa WW 2?
 
Nice explanation! Lakin unasahau kua au maybe hujui mataifa gani yalikua frontline kupigana na aggressors wa WW 2? Russia na Marekani uadui umeanza rasmi na kuiva baada ya ya WW 2, baada ya USSR kushida ulaya mashariki kwa kumtandika Germany na Marekani kushinda Far East kwa kumtandika Japan. Sasa mbona kama hapa wote walishirikiana kuleta balance na amani duniani kwenye hii vita, lini Marekani alijaribu kuingia Russia kwenye huu wakati wa WW 2?
Nimemchanganya marekani na NATO kama kitu kimoja, hata hivyo marekani amekua akijaribu kuingia Russia by the back door kwa kutumia nchi jirani za Russia kwa muda mrefu sasa ( Georgia, Crimea nk). Lakin amekwama
 
Nimemchanganya marekani na NATO kama kitu kimoja, hata hivyo marekani amekua akijaribu kuingia Russia by the back door kwa kutumia nchi jirani za Russia kwa muda mrefu sasa ( Georgia, Crimea nk). Lakin amekwama
Sina shida na wewe kuchanga mkuu. Shida yako ni kutoa evidence isiyo support huo mchanganyo wako. Refer ulichoandika hapa chini[emoji116]

"Kifupi ni kwamba marekani na NATO wameshajaribu kuingia Russia mara 2, kwenye world war I na World war II, walipigwa vibaya sana na hawatothubutu tena."
 
Marekani na NATO yake wamefyata mikia, wamezoea kuonea dagaa tu hao! Wanajua mrusi anapomchapa m'ukrane, kimsingi anayelengwa hapo ni m'marekani' na NATO' yake! Akijichanganya tu imekula kwake! Ila vita isee isikie tu kwa mbali...siyo kabisa i see! Mungu azinusuru nyika!
Wala Nato hawaiogopi urusi tatizo urusi ina silaaa za nyuklia endapo akipigwa na nato anaweza kuzitumia na kuleta maafa makubwa kwa dunia

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Marekani na NATO yake wamefyata mikia, wamezoea kuonea dagaa tu hao! Wanajua mrusi anapomchapa m'ukrane, kimsingi anayelengwa hapo ni m'marekani' na NATO' yake! Akijichanganya tu imekula kwake! Ila vita isee isikie tu kwa mbali...siyo kabisa i see! Mungu azinusuru nyika!
Huyo Russia anayesumbuliwa na ka nchi kama Ukraine kwa siku ya 12 leo hajauteka hata mji mkuu ndo apambane na mataifa makubwa yenye silaha za kisasa?

Putin hadi anatishia kutumia nyuklia ni dalili tosha ameelemewa.

NATO na Marekani hawashindwi kuingia vitani hata kidogo ila ni mbinu ya kumdhoofisha Russia kiuchumi kwanza hadi atie adabu.

Vita vya siku hizi havihitaji physical battle angalia Mchina yupo tuli anajiimarisha kimya kimya kiuchumi.
 
Tatizo chizi anamiliki mabomu ya nuklia na ametishia kuyatumia.
 
Wala Nato hawaiogopi urusi tatizo urusi ina silaaa za nyuklia endapo akipigwa na nato anaweza kuzitumia na kuleta maafa makubwa kwa dunia

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
Si bora unyamaze sio kuchangia. Kwani hizo silaha zimetengenezwa kama mapambo? Si zimetengezwa kwa ajili ya kutumika?

Mpo katika mapambano unamchaguliaje adui silaha? Kwani NATO hawana hizo silaha? Siku nyingine shirikisha ubongo bro unavyochangia ili kuepusha kudharaulika hata na watoto wako kama wamo humu, mtoto anaona mchango dhaifu kama huu bila kujua ni wa mzazi wake anakushambulia na kukudharau
 
Si bora unyamaze sio kuchangia. Kwani hizo silaha zimetengenezwa kama mapambo? Si zimetengezwa kwa ajili ya kutumika?

Mpo katika mapambano unamchaguliaje adui silaha? Kwani NATO hawana hizo silaha? Siku nyingine shirikisha ubongo bro unavyochangia ili kuepusha kudharaulika hata na watoto wako kama wamo humu, mtoto anaona mchango dhaifu kama huu bila kujua ni wa mzazi wake anakushambulia na kukudharau
Mkuu nadhani we ndo una matatizo ya kutoshirikisha akili vizuri.

Just a reminder; Bomu la nyuklia limetumika mara mbili tu katika historia ya Dunia Kule Nagasaki na Iroshima, hivyo kila mtu anajua scale ya uharibifu wa hilo bomu. Na kwa taarifa yako Nuclear weapons are owned by super powers for being used as "Deterrence" weapons and not as war weapons. And such detterence reasons apply in situations like these of Ukrane's, hence bringing equal balance between world's powers.

Akitokea mmoja akatrigger huu mzigo wa Nuclear hata wewe hapo ulipo iwe bonyokwa au katavi hutasalimika. Narudia tena hutasalimika! So sometimes ni heri tusiropokee kwenye kuchangia mambo ya muhimu.

Bila Nuclear msuguano wa vita kati ya mataifa ungekua mkubwa zaidi ya hivi uonavyo leo. Lakin kumiliki silaha za Nuclear kunafanya wakubwa wa dunia waheshimiane na kucompromise ili Dunia ibaki mahala salama kwa viumbe hai.
 
Wazungu ni wanafiq tu, Mara zote wanajidai kulinda haki za raia mahali pengi duniani hususani bara la Africa mbona sasa hivi moto unawaka kwao na hawafanyi yale waliyokuwa wakiyafanya kwenye baadhi ya Nchi kama Libya,Syria, Lebanon..Africa ya kati na kwingine

Wameingilia baadhi ya nchi na hatimaye viongozi walioko madarakani hawakubaliki kila uchwao tunashuhudia mapinduzi ya kijeshi.

Tunataka kuona Umoja wa Ulaya na Nato zikiichukulia hatua kali Urusi kama, Wao kama Baba wa Demokrasia lazima waonyeshe mfano.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo zamani,Sadam huseini wa Iraq alifanya kama anavyofanya Putin wa Urusi Leo kwa kuivamia nchi ya Kuwait.
Marekani na washirika wake wakaivamia Iraq na kuipiga Hadi ikatoka Kuwait.

Miaka kadhaa baadae Slobodan Milosevic wa Yugoslavia aliwapiga kishenzi waasi na raia waliokua wanataka kujitenga wa mji wa Kosovo Huku wakikimbia bila kujua wanakimbilia wapi.
Yalikua ni mapigano ya kikabila.

NATO wakaingilia kati na kushusha kipigo Cha mabomu Cha Hali ya juu katika miji na vijiji vya Yugoslavia upande wa Serbia iloyokua ikiongozwa na Milosevic aliekua anawashusgia vipigo vikali sana wakosovo,na hatimae Milosevic akasalimu amri.

NATO walifanya hayo hayo kwa Yugoslavia Huku umoja wa mataifa ukipinga kuwa damu itamwagika sana, bila idhini ya umoja wa mataifa NATO walipiga mabomu sana upande wa Serbia.

Marekani alipiga Tena Iraq yeye na washirika wake kwa madai kuwa Iraq ilikua imeficha silaha za maangamizi.(weapons of Mass destruction) WMD.

Wamarekani na washirika wake na wapambe wao walishiriki vita hizo na hatimae Wakamkamata Rais wa Iraq akiwa mzima na kumkabidhi kwa wairaq wasio mpenda wakamnyonga.

Muamar Ghadafi wa Libya nae hakuweza kukwepa mkono mmoja wa Baadhi ya Wanachama wa NATO Marekani na Ufaransa .

Baada ya kuonekana Gadafi anaua raia wake kwa wingi kutokana na guvu ya jeshi lake ,ilibidi Marekani na Ufaransa wakatimia madege kudhoofisha uwezo wa jeshi la Libya na hatimae Gadafi kuzidiwa na kukamatwa na mwisho kuuwawa.

Leo najiuliza NATO wamefikwa na nini?
Matendo anavyofanya Urusi huko Ukraine yanafanana kabisa na matendo ya akina Milosevic,Saddam na Ghadafi.
Marekani na NATO waliweza kushusha mabomu na kuwamaliza nguvu maraisi hao.

Sasa hivi masikini,ukweli nimeingiwa na huruma ,Ukraine inaadhibiwa na Urusi NATO hiihii ambayo ilimpa matumaini Zelensky inaangalia TU jinsi anavyofedheheshwa.

Zelensky Yuko chumbani kwake amevamiwa anapiga mayowe,makele,mwano na Kila aina ya kuomba msaada majirani na marafiki waliokua wanampa matumaini wamesimama pembeni mwa madirisha wanachungulia TU.

Sababu wanayotoa Haina mashiko,kuwa NATO ni kwa ajili ya Wanachama TU.

Ok basi tuache uanachama,tuaangalie na ubinadamu TU,kwa mfano Kuwait,Kosovo,na Libya hazikua Wanachama wa NATO lakini ubinadamu ulikuja na kuwaokoa watu wa nchi hizo.

Sasa kwa Nini NATO inakua na ubaguzi namna hii?

Ukweli sipendi vita,vita inaharibu Kila kitu.watu wasio na makosa ama hatia wanakufa bila sababu wanaacha makazi na kazi zao wanakimbilia kusukijulikana.

NATO- Kuiwait,Kosovo na Libya waliingilia kijeshi lakini nchi zote hizo hazikua Wanachama na kwingine hata umoja wa mataifa haukutoa baraka .

Anachokifanya Urusi Leo kwa Ukraine walifanya akina Sadam,Ghadafi na Milosevic.

Labda tofauti ni ndogo TU,Urusi yeye anasema anaharibu miundimbinu ya kijeshi tuu.
Ungekuwa unajua NATO nn wamekusudia kwa URUSI hata wewe ungefanya hivyo hivyo anavofanya Putin .Mimi namuunga mkono sana na yule Raisi wa Ukraina ndio mjnga wa mwisho kabisa kachuuzwa na NATO kaitia nchi yake ktk vita na kuharibu Infructure zote yaani namuona bonge la mbumbavu wa mwishoo any way tuombe vita imalizike na ipo dalili ya kumalizika israili wameingilia kati ya kupatanisha sababu raisi wa Ukraine ni Myahudi mwenziwao.
 
Iraq alipovamia Kuwait nilikuwa huko na nilishiriki
Kuwait ni rafiki mkubwa wa wazungu na wanamlinda kwa mkataba wa miaka dhahari

Kuwait wakati huo population ilikuwa 1m tu ukijumlisha na expatriates
Saddam alipovamia walikuwa askari zaidi ya 1m na mgambo na wale wa akiba walikuwa takriban 3m

Sasa ili kulinda maslahi ya Kuwait na washirika wengine kama Saudia, na GCC wengine ilibidi USA na [emoji636] wamuondoe Saddam hata kama ni rafiki yao maana Iraq na GCC yote bora hao wanawalipa hela ndefu sana

Sasa Ukraine anawapa nini?
Kama ni humanitarian sawa watasaidia wakimbizi ila kwa maslahi mzungu anaangalia tumbo lake tu
 
Sina shida na wewe kuchanga mkuu. Shida yako ni kutoa evidence isiyo support huo mchanganyo wako. Refer ulichoandika hapa chini[emoji116]

"Kifupi ni kwamba marekani na NATO wameshajaribu kuingia Russia mara 2, kwenye world war I na World war II, walipigwa vibaya sana na hawatothubutu tena."
Kitu unatakiwa kujua vita vyote vya world war I na World war ii, marekani alipigana either kwa kwenda front au kwa kutoa support kwa Allies. Hivyo kushindwa kwao ni kushindwa kwake.
 
Yaani Russia kama ni kupigana kwa mapanga basi anampiga Ukraine na panga lililo ndani ya Hala yake kwa kuwa hataki kumuua ndugu yake! Anamsubiri USA na wapambe wake wajitikeze ndio awachomolee panga!
Huyo USA unayemuabudu ni mhuni TU, anataka asaidiwe na Dunia yote kumdhoofisha Russia!
Hana hata huruma kwa wa'ukraine!
By the way wanaopigana Ukraine sio wukraine TU Bali mamluki wa magharibi waliovalia kiraia!
Huyo Russia anayesumbuliwa na ka nchi kama Ukraine kwa siku ya 12 leo hajauteka hata mji mkuu ndo apambane na mataifa makubwa yenye silaha za kisasa?

Putin hadi anatishia kutumia nyuklia ni dalili tosha ameelemewa.

NATO na Marekani hawashindwi kuingia vitani hata kidogo ila ni mbinu ya kumdhoofisha Russia kiuchumi kwanza hadi atie adabu.

Vita vya siku hizi havihitaji physical battle angalia Mchina yupo tuli anajiimarisha kimya kimya kiuchumi.
 
Back
Top Bottom