Natubu: Nilikuwa simuelewi Mwamposa, ila kwa idadi ya viwete walioponyeshwa Songea naanza kumuamini

Natubu: Nilikuwa simuelewi Mwamposa, ila kwa idadi ya viwete walioponyeshwa Songea naanza kumuamini

Kama kichwa cha habari hapo juu, ujio wa Mwamposa, Songea ni neema.

Umeleta uponyaji mkubwa sana, vilema wanatembea, vipofu wanaona, hiyo haina kupinga.

Mimi nilikuwa simuamini lakini kwasasa naanza kumuamini.

View attachment 2387081
SINA SHAKA NA UPONYAJI NA MIUJIZA YA MWAMPOSA

Labda swali ni jee anaponya kwa nguvu za yesu kweli au Kuna nguvu nje ya yesu??

Kwangu Mimi sina kilema nineyemfahamu aliyeponywa na MWAMPOSA ila
Nimeshuhudia ndoa iliyofungwa mwaka 2008 ikitaabika kupata mtoto Hadi mwaka 2022 wakaenda kwa MWAMPOSA Leo hii wanamtoto wa kiume.

Pia Rafiki yangu ametafuta mtoto kwa miaka 8 kwenye ndoa bila mafanikio
Mwaka 2022 alienda kwa MWAMPOSA huu ni mwezi wa pili sasa toka apate mtoto

Ninachoamini Mimi
MWAMPOSA sio tapeli, sio mwizi,sio mwigizaji. Utakachoomba utapewa

Swali jee hutenda kwa nguvu za yesu kweli???
 
Akina Moses Klora walifanyaga maigizo haya miaka ya 1990s, unashangaa vilema wanaopona ni wageni tupu. Wale uliowaina tangu utotoni mwako wanakuwa hawana Imani eti.

Hawaponagi kabisa fuatilia sana.
 
Usimkufuru Mungu
Acha ujinga hivi waafrika kwanini tunawaza mambo ya miujiza saa zote ndio maana tunapenda mambo ya uchawi uchawi, na umasikini hauwezi kuisha kwa akili za wapumbazi kama hawa washabiki wa manabii feki, muabudu muumba wako achana na hawa binaadamu wanaokudanganya kila siku, kuna mwingine kule lindi eti kaweka mgongo wake mwanasiasa apite juu sasahivi analialia ,ujinga umezidi bwana
 
Pumbavu kabisa wewe. Sijawahi kusali kanisani kwake na still ninaamini ni mtumishi wa kweli wa Mungu.

Napenda namna anavyokaa kimya na asimjibu yeyote. Pengine amepata darasa kutoka kwa mwalimu Mwakasege.
Nionyeshe picha ya mwalimu Christopher Mwakasege akiwa na watu wamebebeana magongo mapya
 
Back
Top Bottom