Naufunga mjadala: Zuchu ni mwandishi bora wa nyimbo kuliko Lady Jaydee

Naufunga mjadala: Zuchu ni mwandishi bora wa nyimbo kuliko Lady Jaydee

sinza pazuri

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
3,344
Reaction score
9,066
20241019_134953.jpg

Kwenye pen game hakuna msanii wa kike wa bongofleva amewahi kufikia uwezo wa Zuchu toka bongofleva izaliwe nasema hakuna.

Jide ni msanii mkali, anauwezo mkubwa kafanya hitsong nyingi namheshimu kwa ilo ila huu mjadala nimeuona uko kuwa Jide anaweza andika kumzidi Zuchu haupo sahihi.

Jide ni mkongwe ila ngoma nyingi ameandikiwa, Zuchu 97% ya ngoma zake anaandika mwenyewe.

Nafikiri mnaona uhandishi wa Zuchu hata wasanii wa kiume wengi hawamuwezi.

Nyimbo kama Raha, Kwaru, Nisamehe, Naringa ni uhandishi wa kiwango cha juu sana cha sanaa.

Huu mjadala usiendelee popote nimeumaliza rasmi.
 
Jay Dee si kumlinganisha na Zuchu.
Jay Dee huyo anamzaa huyo Zuchu, heshimu amekaa kwenye game muda wote huo na bado anapambana na watoto wa 2000s.

Kitu ambacho hatuna uhakika Zuchu atafika hapo...

Kama ulishawahi ingia shows za Jay Dee utakiri Zuchu hawezi kufanya live performance kwa kuimba kama Jay Dee....
 
Sio kweli japo una uhuru wa maoni mkuu ukitaka kujua ufundi wa jide kasikilize yahaya

"Wa nok nok " || Jide x dojo x kaya
"Kama Jana '" || Kibla x jide
" Sawa na wao ". || Jide
Together remix Jide & spicy ⚡⚡

20241019_141214.jpg
 
Jay Dee si kumlinganisha na Zuchu.
Jay Dee huyo anamzaa huyo Zuchu, heshimu amekaa kwenye game muda wote huo na bado anapambana na watoto wa 2000s.

Kitu ambacho hatuna uhakika Zuchu atafika hapo...

Kama ulishawahi ingia shows za Jay Dee utakiri Zuchu hawezi kufanya live performance kwa kuimba kama Jay Dee....
Upo nje ya mada mkuu. Hii mada haizungumzii nani ni mkongwe.

Mada inahusu kalamu.
 
Jay Dee si kumlinganisha na Zuchu.
Jay Dee huyo anamzaa huyo Zuchu, heshimu amekaa kwenye game muda wote huo na bado anapambana na watoto wa 2000s.

Kitu ambacho hatuna uhakika Zuchu atafika hapo...

Kama ulishawahi ingia shows za Jay Dee utakiri Zuchu hawezi kufanya live performance kwa kuimba kama Jay Dee....
Unadhani wataelewa hawa watoto wa juzi?
 
Nimesikiliza nyimbo za Jide na nimesikiliza nyimbo za Zuchu

Jide apewe heshima yake kama legend

Ila huyu Zuchu anajua sana, muziki ni vibe hapa ndipo Jide anaposhindwa kwa Zuchu

Pili utunzi, Zuchu anakuimbia nyimbo zenye mahadhi tofautitofauti na ujumbe tofauti-tofauti kitu ambacho Jide hawezi. Zuchu anaweza kuwapa vibe watoto, vijana mpaka watu wazima

Kusema Rihanna ni mkali zaidi ya Mariah Carey au JLo haimanaanishi unamkosea heshima Mariah au JLo kisa RiRi ni wa karibuni

Jide ni legend hatuwezi kusahau mchango wake katika kiwanda cha bongo fleva, moja ya msanii mkali sana chorus alizitendea haki sana akiwa kwenye ubora wake

Machozi itabaki kuwa bonge la ngoma la Jide in my books
 
Nje ya Mada, mbona huku AudioMack kila nikimtafuta Jide simpati, msaada tafadhali au mwenye ngoma yake ya Forever aloimba na msechu sijui anitumie
 
Back
Top Bottom