Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Huyo muungwana anataka bandari ile ile ya kizamani isiyokuwa na teknolojia ndio iendelee kuwepo miaka yote, kisa ni zile dhana potofu kwamba bandari ni nyeti kwa uchumi wa taifa.
Unajitoa akili na kumchanganya kwa maksudi huyo mwenzako kwa malengo yale yale ya upotoshaji kama siku zote ulipokuja humu kwa jina hilo la bandia kutetea mradi huo huo ambao wewe unajisifu mwenyewe kuwa kinara wake.

Nimekueleza mara kadhaa juu ya jambo hili hili, lakini umekomalia tu na msimamo huo huo wa upotoshaji.
 
basi bwana. Siwezi kukusaidia zaidi ya hapo.
Kumbe uelewa nao kwako ni shida kabisa. Ulivyo andika hapo ndivyo nilivyo maanisha mimi?
Wewe si umetaka bandari tusimpe mtu(dp) bali tuwekeze wenyewe atakachowekeza dp,kwanza tusomeshe watu wa kufanya hizo kazi...hili linashangaza sababu ticts wanaendesha bandari kwa miaka 25 sasa,au hatutakiwi kumpa mwarabu tu!?..ndiyo nikahoji kipindi hiki tunasomesha watu wawe na ujuzi wa dp,nani atakua akiendesha bandari!?..pili,ulidai tutie nguvu kusimamia utendaji,toka uhuru tumeshindwa kutia hiyo nguvu,miaka 63 tutaweza leo?!..tatu kwa nini hela za kuwekeza bandari Ili mwarabu asichukue tusiziwekeze kwingine?..maana kea mwarabu tutaweza kuongeza pato bandari kwa 67%+
 
Wewe si umetaka bandari tusimpe mtu(dp) bali tuwekeze wenyewe atakachowekeza dp,kwanza tusomeshe watu wa kufanya hizo kazi...hili linashangaza sababu ticts wanaendesha bandari kwa miaka 25 sasa,au hatutakiwi kumpa mwarabu tu!?..ndiyo nikahoji kipindi hiki tunasomesha watu wawe na ujuzi wa dp,nani atakua akiendesha bandari!?..pili,ulidai tutie nguvu kusimamia utendaji,toka uhuru tumeshindwa kutia hiyo nguvu,miaka 63 tutaweza leo?!..tatu kwa nini hela za kuwekeza bandari Ili mwarabu asichukue tusiziwekeze kwingine?..maana kea mwarabu tutaweza kuongeza pato bandari kwa 67%+
Mkuu 'Gallow', naona unaning'ang'ania huku huelewi ninacho eleza.
Sasa ngoja nikueleze kwa kifupi sana na kwa utulivu. Fungua akili yako, acha kuniangalia kama mpinzani wako.

Ni hivi: Mimi naamini kwa dhati ya moyo wangu yote, kwamba waTanzania kwa sasa, hapa tulipo fikia, tunao uwezo wa kutosheleza kabisa kufanya mambo mengi sana sisi wenyewe bila ya kuhitaji kutegemea watu toka nje waje watufanyie kazi tunazoweza sisi. Kinacho kosekana ni uongozi wa kusimamia juhudi zetu hizi.

Ngoja nieleze tena mfano huo wa Bandari.

Tuliamua kwenda kukopa pesa World Bank ili tuiboreshe Bandari yetu iweze kufanya kazi vizuri. Kazi ilifanyika ya kukarabati kilicho hitajika kukarabatiwa. Uendeshaji wa Bandari tukaona hatuwezi. Tukawapa DP World mkataba wa miaka 30 au hata zaidi. Kwanza nieleze hili; kwa nini hatuwezi kuendesha bandari? Tunaambiwa na viongozi wetu kwamba wizi ni mwingi hapo Bandarini; viongozi wetu hawa wanaona ni kazi kubwa sana kuzuia wizi hapo. Ni kazi isiyo wezekana hadi tumtafute mwekezaji aje azuie wizi!

Kwamba waTanzania hatuna uwezo wa kuelewa mambo ya kuendesha bandari? Kama na wewe unakubaliana na sababu ya kipuuzi hii, hapa ndipo tusipoweza kuelewana hata kidogo; kwa sababu hakuna 'rocket Science) ya kushindikana waTanzania wasiweze kuielewa kwa muda wa miaka 30??... Licha ya hapo; nimekupa na mfano kwamba ni katika dhana hiyo hiyo potofu, inayotokana na viongozi wabovu, kwamba tumekaa na TICTS zaidi ya miaka 25 na bado tukawa hatuwezi kujifunza namna ya kuendesha Bandar???
Kwa hiyo; maoni yangu ni kuwa kutakuwa na sababu nyingine zinazo fanya viongozi wetu na baadhi yetu, kama wewe na huyo tapeli "Mtamu Sana" ya kutaka kila mara tutafutew watu wa kutufanyia kazi, huku sisi tumebutaa. Huu siyo uongozi.

Na usije ukadhani kwamba napinga uwekezaji, la hasha; kwa sabau ya utapeli tu wengi mnakimbilia huko; kama mnavyo fanya kuhusu mambo ya Ujamaa au Ukabaila, haya ni maswala ambayo yanatumika tu sasa hivi kuchanganya akili za watu. Si Ujama, au Ukabaila unaoendesha nchi yoyote duniani. Hizo zilikuwa ni siasa za nyakati hizo, zimekwisha pitwa na wakati.. Nenda Marekani kama hutakuta vimelea vya ujamaa huko; na ukienda China utakutana na vimelea vya ukabaila huko, pamoja na wao kujitambulisha kuwa wakomunisti.

Tunacho takiwa hapa kwetu Tanzania ni kuwa na uongozi unao lenga kuwajengea uwezo waTanzania waweze kuendesha sehemu kubwa ya kujiletea maendeleo ya nchi yao. Viongozi wapo kutafuta watu watakao kuja kutuletea maendeleo, jambo ambalo haliwezekani kamwe.

Bandari tunaweza kabisa kuendesha wenyewe. Wizi siyo sababu ya sisi kukimbia kwenda kutafuta watu. Wengine wanasema waTanzania ni WAVIVU? Hii nayo ni sababu? Kama ni teknolojia ambayo hatuna, hatuwezi kuinunua/kuikodi? Hatuwezi kuajiri 'consultants' wenye ujuzi huo kwa muda nasi tukijifunza?

Lakini, hapana, kazi rahisi kwa viongozi wetu wabovu ni kuwapa wageni waendeshe Huu ni ujinga.

Ni siku nyingi nime pendekeza kwamba nafasi ya kwanza kabisa tunayotakiwa kupata mgeni aje atuendeshee shughuli zetu ni palepale nafasi ya juu kabisa serikalini. Tumtafute mtu/watu toka nje waje waendeshe shughuli zote za serikali tukimjumuisha na Rais mwenyewe. Hawa tulio nao kazi hawawezi.
 
Labda niulizie kulikuwa na maana gani Nyerere kutaifisha mali za watu, Viwanda,Makampuni na Majumba?
Ili kuwa ni shortcut ya kupata nyumba za viongozi wa chama na serikali. Pia kwa ya shughuli za kiserikali waseme wamejenga wao
Nhc zaidi ya 89% ni assets za wizi
 
Nimezaliwa miaka 1970, nimekutana na maisha magumu Sana, kulikuwa hakuna Sabuni, Sukari, Mafuta na hata nguo.

Watu walivaa magunia, kulikuwa hakuna vyakula na wakati tunapata uhuru aliikuta Tanganyika iko vyema kutoka kwa mkoloni nchi ikiwa vizuri.

Je, Uongozi ulimshinda?

Soma Pia: Kumuelewa vyema Hayati Mwalimu Julius Nyerere upeo uwe mkubwa
Nyerere alikuwa sio kabisa, na hii laana ya ukondoo yeye ndio kapandikiza kwenye nchi hii.
 
Mkuu 'Gallow', naona unaning'ang'ania huku huelewi ninacho eleza.
Sasa ngoja nikueleze kwa kifupi sana na kwa utulivu. Fungua akili yako, acha kuniangalia kama mpinzani wako.

Ni hivi: Mimi naamini kwa dhati ya moyo wangu yote, kwamba waTanzania kwa sasa, hapa tulipo fikia, tunao uwezo wa kutosheleza kabisa kufanya mambo mengi sana sisi wenyewe bila ya kuhitaji kutegemea watu toka nje waje watufanyie kazi tunazoweza sisi. Kinacho kosekana ni uongozi wa kusimamia juhudi zetu hizi.

Ngoja nieleze tena mfano huo wa Bandari.

Tuliamua kwenda kukopa pesa World Bank ili tuiboreshe Bandari yetu iweze kufanya kazi vizuri. Kazi ilifanyika ya kukarabati kilicho hitajika kukarabatiwa. Uendeshaji wa Bandari tukaona hatuwezi. Tukawapa DP World mkataba wa miaka 30 au hata zaidi. Kwanza nieleze hili; kwa nini hatuwezi kuendesha bandari? Tunaambiwa na viongozi wetu kwamba wizi ni mwingi hapo Bandarini; viongozi wetu hawa wanaona ni kazi kubwa sana kuzuia wizi hapo. Ni kazi isiyo wezekana hadi tumtafute mwekezaji aje azuie wizi!

Kwamba waTanzania hatuna uwezo wa kuelewa mambo ya kuendesha bandari? Kama na wewe unakubaliana na sababu ya kipuuzi hii, hapa ndipo tusipoweza kuelewana hata kidogo; kwa sababu hakuna 'rocket Science) ya kushindikana waTanzania wasiweze kuielewa kwa muda wa miaka 30??... Licha ya hapo; nimekupa na mfano kwamba ni katika dhana hiyo hiyo potofu, inayotokana na viongozi wabovu, kwamba tumekaa na TICTS zaidi ya miaka 25 na bado tukawa hatuwezi kujifunza namna ya kuendesha Bandar???
Kwa hiyo; maoni yangu ni kuwa kutakuwa na sababu nyingine zinazo fanya viongozi wetu na baadhi yetu, kama wewe na huyo tapeli "Mtamu Sana" ya kutaka kila mara tutafutew watu wa kutufanyia kazi, huku sisi tumebutaa. Huu siyo uongozi.

Na usije ukadhani kwamba napinga uwekezaji, la hasha; kwa sabau ya utapeli tu wengi mnakimbilia huko; kama mnavyo fanya kuhusu mambo ya Ujamaa au Ukabaila, haya ni maswala ambayo yanatumika tu sasa hivi kuchanganya akili za watu. Si Ujama, au Ukabaila unaoendesha nchi yoyote duniani. Hizo zilikuwa ni siasa za nyakati hizo, zimekwisha pitwa na wakati.. Nenda Marekani kama hutakuta vimelea vya ujamaa huko; na ukienda China utakutana na vimelea vya ukabaila huko, pamoja na wao kujitambulisha kuwa wakomunisti.

Tunacho takiwa hapa kwetu Tanzania ni kuwa na uongozi unao lenga kuwajengea uwezo waTanzania waweze kuendesha sehemu kubwa ya kujiletea maendeleo ya nchi yao. Viongozi wapo kutafuta watu watakao kuja kutuletea maendeleo, jambo ambalo haliwezekani kamwe.

Bandari tunaweza kabisa kuendesha wenyewe. Wizi siyo sababu ya sisi kukimbia kwenda kutafuta watu. Wengine wanasema waTanzania ni WAVIVU? Hii nayo ni sababu? Kama ni teknolojia ambayo hatuna, hatuwezi kuinunua/kuikodi? Hatuwezi kuajiri 'consultants' wenye ujuzi huo kwa muda nasi tukijifunza?

Lakini, hapana, kazi rahisi kwa viongozi wetu wabovu ni kuwapa wageni waendeshe Huu ni ujinga.

Ni siku nyingi nime pendekeza kwamba nafasi ya kwanza kabisa tunayotakiwa kupata mgeni aje atuendeshee shughuli zetu ni palepale nafasi ya juu kabisa serikalini. Tumtafute mtu/watu toka nje waje waendeshe shughuli zote za serikali tukimjumuisha na Rais mwenyewe. Hawa tulio nao kazi hawawezi.
Suala la wizi limeshindikana,siyo bandari tu hata mashirika mengine ya umma yalikufa sababu mojawapo no hiyo, dp world anaendesha hadi bandari za uingereza na USA,siyo kwamba uingereza hawawezi endesha bandari zao, watanzania hawawezi simamia mradi bila kuiba,hili huwezi kubadilisha,limethibiti kwa miaka zaidi ya 50,ikiwa ukimpa muwekezaji kunakua na tija zaidi na watanzania watapata ajira hapo,kwa nini uhangaike kuwekeza,hiyo nguvu kea nini usiwekeze kwingine?..kwa nini unaifanya bandari kama sehemu za siri na kumpa muwekezaji ni idhlali!?..umeambiwa mapato yatakua makubwa,kea nini hutaki!?..mtu anakuja kulima shamba lako mgawane mazao,amekuthibitishia na umehakiki kuwa atatoa gunia mia, utapata hamsini tofauti na ulipokua ukilima mwenyewe na kupata 15,kwa nini usinwache alime Ili nguvu zako za kulima uzipeleka kwingine!?
 
Kwa hiyo ukirudishwa Kijiji kwa mk, baada ya hapo ni nn kinaendelea?
Hacheni kutetea uovu kisa kuona italeta picha mbaya , bali inabidi tuonyeshe ukomavu wa akili na sio uoga wa kufuga ujinga.

Rafiki wa mchoga wakule sijui Georgia, wali assassinate yy na mkewe Tena hadhari, France pia nao walimla kichwa king na queen hadhari.
Yakawa mapinduzi ya democracy and Renaissance kushika hatamu.
Wa tz tatizo lao ni uoga TU

Hebu niambie nani ambaye ana usafi huo? Mnamsingizia Nyerere kama vile hakuna mwingine anayefanya. Ninachoona uongo wetu unasukumwa zaidi na udini kuliko uhalisia
 
Suala la wizi limeshindikana,siyo bandari tu hata mashirika mengine ya umma yalikufa sababu mojawapo no hiyo, dp world anaendesha hadi bandari za uingereza na USA,siyo kwamba uingereza hawawezi endesha bandari zao,
Hivi wewe kichwa chako ni ngumu kivipi? Nirudie hayo hayo mara ngapi ndipo uelewe?
Umelishwa takataka muda mwingi kiasi kwamba akili yote imegota kabisa kuelewa kitu?
Ni nchi gani hakuna wizi, nieleze hapa nisiendelee kukuona wewe kuwa kilaza wa ajabu sanma!

Tanzania ndipo kulipo vumbuliwa wizi usioweza kudhibitiwa? Chia hakuna wizi? Marekani hakuna wizi. Ni wapi pasipo kuwepo na wizi! Sasa kwa kweli unaudhi. Mwanzo nilidhani huelewi, kumbe ni kichwa ngumu tu asiyetaka kuelewa, kwa sababu wewe mwenyewe na wanao kufuga na kukuleta hapa ni wezi.

Sasa nieleze hao DP World wao wamegundua dawa gani ya kuzuia wezi, ambayo wengine hawawezi kuitumia! Hao DP World wana 'patent' na dawa hiyo?
Hovyo kabisa.

Kamuulize huyo mwenzako 'Steven Ntamusana kuhusu haya mnayo rudia rudiya ya Uingereza na sijui wapi kwingine walipo hao wajomba zenu wanao wapeleka nyinyi chooni.
Nchi hizo mnazo tolea mfano na wenyewe wanayo bandari moja wanayo itegemea kama sisi? Wao pia hawana uwezo wa kuendesha bandari kwa sababu tu ya sera za viongozi wa nchi hizo kuwa vihiyo wasiokuwa na akili kabisa kichwani?
Unaelewa sababu zinazo wafanya wakodishe baadhi ya hizo bandari; na unajuwa makubaliano ya ukodishaji wao ni sawa na wa Kimangungo wetu hapa?

Najuwa huwezi kujibu hata moja ya swali nililo kuuliza hapa.
Napoteza muda na lofa fulani tu anaye faidi makombo anayo tupiwa na wanaomleta humu JF kuvuruga akili za watu.
 
Suala la wizi limeshindikana,siyo bandari tu hata mashirika mengine ya umma yalikufa sababu mojawapo no hiyo, dp world anaendesha hadi bandari za uingereza na USA,siyo kwamba uingereza hawawezi endesha bandari zao, watanzania hawawezi simamia mradi bila kuiba,hili huwezi kubadilisha,limethibiti kwa miaka zaidi ya 50,ikiwa ukimpa muwekezaji kunakua na tija zaidi na watanzania watapata ajira hapo,kwa nini uhangaike kuwekeza,hiyo nguvu kea nini usiwekeze kwingine?..kwa nini unaifanya bandari kama sehemu za siri na kumpa muwekezaji ni idhlali!?..umeambiwa mapato yatakua makubwa,kea nini hutaki!?..mtu anakuja kulima shamba lako mgawane mazao,amekuthibitishia na umehakiki kuwa atatoa gunia mia, utapata hamsini tofauti na ulipokua ukilima mwenyewe na kupata 15,kwa nini usinwache alime Ili nguvu zako za kulima uzipeleka kwingine!?
LOOooooh
Huko anakolima yeye apate gunia 100; kwa akili zako mbovu kabisa unadhani waTanzania wenye akili nzuri hawawezi kutumia njia hizo hizo na wao wakavuna hizo gunia 100! Hii ni mifano ya kumpa mtu aone uelewa wako ulivyo mfinyu?
Sitaendelea tena kuhangaika na wewe.
 
LOOooooh
Huko anakolima yeye apate gunia 100; kwa akili zako mbovu kabisa unadhani waTanzania wenye akili nzuri hawawezi kutumia njia hizo hizo na wao wakavuna hizo gunia 100! Hii ni mifano ya kumpa mtu aone uelewa wako ulivyo mfinyu?
Sitaendelea tena kuhangaika na wewe.
Uelewa wako mdogo, umeshindwa kuelewa la bandari tulioyishindwa kea miaka 60,nakupa mfano wa shamba ulilolima hovyo muda mrefu,napo huelewi, endelea kulia
 
Hivi wewe kichwa chako ni ngumu kivipi? Nirudie hayo hayo mara ngapi ndipo uelewe?
Umelishwa takataka muda mwingi kiasi kwamba akili yote imegota kabisa kuelewa kitu?
Ni nchi gani hakuna wizi, nieleze hapa nisiendelee kukuona wewe kuwa kilaza wa ajabu sanma!

Tanzania ndipo kulipo vumbuliwa wizi usioweza kudhibitiwa? Chia hakuna wizi? Marekani hakuna wizi. Ni wapi pasipo kuwepo na wizi! Sasa kwa kweli unaudhi. Mwanzo nilidhani huelewi, kumbe ni kichwa ngumu tu asiyetaka kuelewa, kwa sababu wewe mwenyewe na wanao kufuga na kukuleta hapa ni wezi.

Sasa nieleze hao DP World wao wamegundua dawa gani ya kuzuia wezi, ambayo wengine hawawezi kuitumia! Hao DP World wana 'patent' na dawa hiyo?
Hovyo kabisa.

Kamuulize huyo mwenzako 'Steven Ntamusana kuhusu haya mnayo rudia rudiya ya Uingereza na sijui wapi kwingine walipo hao wajomba zenu wanao wapeleka nyinyi chooni.
Nchi hizo mnazo tolea mfano na wenyewe wanayo bandari moja wanayo itegemea kama sisi? Wao pia hawana uwezo wa kuendesha bandari kwa sababu tu ya sera za viongozi wa nchi hizo kuwa vihiyo wasiokuwa na akili kabisa kichwani?
Unaelewa sababu zinazo wafanya wakodishe baadhi ya hizo bandari; na unajuwa makubaliano ya ukodishaji wao ni sawa na wa Kimangungo wetu hapa?

Najuwa huwezi kujibu hata moja ya swali nililo kuuliza hapa.
Napoteza muda na lofa fulani tu anaye faidi makombo anayo tupiwa na wanaomleta humu JF kuvuruga akili za watu.
Ulikua wapi miaka 30 iliyopita kutoa dawa ya wizi bandarini na uduni wa ufanisi!?..acha kujifanya una uelewa mpana wa mambo wakati ni mbumbumbu fanatic
 
Hebu niambie nani ambaye ana usafi huo? Mnamsingizia Nyerere kama vile hakuna mwingine anayefanya. Ninachoona uongo wetu unasukumwa zaidi na udini kuliko uhalisia
Sawa mkuu, ila mm sina dini, pia hakuna kiongozi aliye kamilika.

Wanatakiwa wajifunze kutokana na makosa,
Mfano kufanya marekebisho ya katiba iliyopo. Kuweka sera nzuri za uwazi na uwajibikaji kwa kila upande.

Si unaona Europe wamewekeza sana Kenya, ss huku ni wachina na wahindi ndio wawekezaji wakubwa,


Ukiangalia DSE Kuna companies 25 TU 😂, Ina maana Kuna ukwepaji mkubwa wa kodi kwenye hii nchi. Biashara nyingi zinafanyika kimagendo.eg GSM.

Japo wapo viongozi walioko madarakani wanadai Eti mbona Nyerere,hakubadilisha katiba kabla hajaondoka madarakani? Kwa hiyo 👆 na wao waachwe waendelee hivyo hivyo😲?
 
Hebu niambie nani ambaye ana usafi huo? Mnamsingizia Nyerere kama vile hakuna mwingine anayefanya. Ninachoona uongo wetu unasukumwa zaidi na udini kuliko uhalisia
Mkuu hao viongozi wa kidlni ni wasaliti wakubwa, dini hizi zilizo bariki ukoloni na utumwa Eti leo serikali inawapa kipaumbele kwenye kutoa maoni, kwani dini ina msaada gani kwa MTU mweusi, zaidi ya manyanyaso TU,MTU unaeijua history ya dini barani African na kungineko hawezi kuishobokea dini hata kidogo
 
Unajitoa akili na kumchanganya kwa maksudi huyo mwenzako kwa malengo yale yale ya upotoshaji kama siku zote ulipokuja humu kwa jina hilo la bandia kutetea mradi huo huo ambao wewe unajisifu mwenyewe kuwa kinara wake.

Nimekueleza mara kadhaa juu ya jambo hili hili, lakini umekomalia tu na msimamo huo huo wa upotoshaji.
Tafuta kujua maana za kisasa za bandari pia huu ni uchumi mpana wa kibepari tofauti na ule wa miaka ile enzi za serikali kumiliki njia kuu za uchumi.
 
Mkuu hao viongozi wa kidlni ni wasaliti wakubwa, dini hizi zilizo bariki ukoloni na utumwa Eti leo serikali inawapa kipaumbele kwenye kutoa maoni, kwani dini ina msaada gani kwa MTU mweusi, zaidi ya manyanyaso TU,MTU unaeijua history ya dini barani African na kungineko hawezi kuishobokea dini hata kidogo
Dini za kizungu zinatutaka tuishi kinafiki. Kuishi kwa kuheshimu mapokeo mengi na anayethubutu kwenda mwendo wa kwake binafsi huyo anaonekana ni adui wa kila mtu.

Zinatufundisha kutii aina fulani ya mafundisho bila kuhoji kwa kina, ukiwa huru unaonekana ni muasi mwenye haki ya kutengwa na jamii.
 
Dini za kizungu zinatutaka tuishi kinafiki. Kuishi kwa kuheshimu mapokeo mengi na anayethubutu kwenda mwendo wa kwake binafsi huyo anaonekana ni adui wa kila mtu.

Zinatufundisha kutii aina fulani ya mafundisho bila kuhoji kwa kina, ukiwa huru unaonekana ni muasi mwenye haki ya kutengwa na jamii.
Sio dini za kizungu TU, hata uislam, ni u dictator TU.
Dini zilitakiwa kufutwa kabisa nchini
 
Uelewa wako mdogo, umeshindwa kuelewa la bandari tulioyishindwa kea miaka 60,nakupa mfano wa shamba ulilolima hovyo muda mrefu,napo huelewi, endelea kulia
Hapa unaonyesha wazi kwamba umekwisha tambua ujinga wako uko wapi. Kilicho baki ni kutafuta njia ya kuondokana na aibu ya kushikilia maoni potofu uliyo kuwa nayo.
 
Ulikua wapi miaka 30 iliyopita kutoa dawa ya wizi bandarini na uduni wa ufanisi!?..acha kujifanya una uelewa mpana wa mambo wakati ni mbumbumbu fanatic
Unajuaje, pengine nilikuwa bado sjazaliwa!

Nipo sasa, kwa hiyo nina nafasi ya kulishikia bango swala hilo na kuwaonyesha nyinyi uhujumu mnao ufanya kwa nchi yetu hii.
 
Tafuta kujua maana za kisasa za bandari pia huu ni uchumi mpana wa kibepari tofauti na ule wa miaka ile enzi za serikali kumiliki njia kuu za uchumi.
Wewe unaimba tu kama kasuku; akili yako imegotea hapo hapo kwenye kuimba "ubepari" bila hata ya kutambua maana yake ni ipi hasa.
 
Back
Top Bottom