Agy pole. Ila ngoja nikushauri nikupe ushauri tofauti.
Yawezekana hawakufanyii makusudi, kupishana huku jukwaani ni kawaida sana. Kujibiana shombo ni kawaida sana. Sasa pengine wewe unahisi wanafanya hivo kwa sababu wamekusaidia.
Na hata kama wapo wanaofanya hivyo labda ni mmoja au wawili pasikufanye ukaona watu wote 10+ wanakufanyia hivyo.
Kuhusu kuwalipa, hauwezi kuwalipa kabisa. Nakazia kwamba HAUWEZI KUWALIPA KAMWE. kwa sababu ile sio hela tuu walikupa Bali walikufanyia WEMA, WALIKUINUA KIPINDI UMEANGUKA, WALIKUFANDILI. Hela utawapa lakini hela sio kitu , Fadhila walizokutendea hauwezi kuzirudisha kwa sababu hazirudishwi kwa pesa.
Usizire. Muombe Mungu akupe uvumilivu na ujasiri. Na pia jaribu kuishi kama hamna kilichotokea.
Watu waliokufanyia WEMA lazima wanajisikia vibaya kwa hivi unavyoviandika, mara utawarudishia, Mara unawajua wote. Kila mtu anaweza akawa anahisi unamwona adui kisa alikusaidia.
Kosa la mtu mmoja au wawili lisikufanye uone watu wote waliokusaidia wanakunyanyasa.