Uchaguzi 2020 Naunga mkono aliyoyazungumza Lissu kwenye “ufunguzi wa kampeni” mengi aliyoyasema hatukuyafahamu. Nashauri afanye hivyo kila mkutano

Uchaguzi 2020 Naunga mkono aliyoyazungumza Lissu kwenye “ufunguzi wa kampeni” mengi aliyoyasema hatukuyafahamu. Nashauri afanye hivyo kila mkutano

Ni sahihi kabisa.

Lisu ni lazima kwanza auseme uovu wote ulifanywa awamu hii, halafu baadaye aeleze yeye atafanya nini, tofauti na uovu uliofanywa na awamu hii.

Aeleze jinsi alivypshambuliwa, sababu ya kushambuliwa kwake, alivyonyimwa matibabu, wabunge wa CCM walivyozuiwa kwenda kumwona, polisi walivyoamua kutochunguza.

Aeleze wengine waliopatwa na madhila ya aina mbalimbali kama vile Ben Sanane kwa kuhoji elimu ya jiwe, Azory kwa kuweka wazi mauaji ya raia, madiwani waliouawa kwa kukatwa mapanga na watu wa CCM.

Aeleze jinsi hela za umma zinavyotapanywa kwa kununua ndege, kujenga uwanja wa ndege Chato, majengo makubwa kama ya TRA kujengwa Chato badala ya Geita, bohari ya kanda ya madawa kujengwa Chato, n.k.

Aeleze pia dalili za upendeleo zinazoonekana kama vile teuzi mbalimbali kuegemea kanda moja, ndugu kuwekwa kwenye nafasi kubwa za serikalini, n.k.

Kisha azungumzie jinsi Serikali yake itakavyofanya kuwapunguzia madhira ya awamu ya 5, na kisha mifumo itakayozuia kiongozi mwingine kuliingiza Taifa tena kwenye madhira kama ya sasa.
 
Hapana aisee. Hata nafsi inakusuta. Ila bado ana chance kubadili upepo.
Hana haja ya kubadili upepo hata kidogo. Kwanza jana ni kwasababu wameamuwa kutafuta haki kwanza iliyopokwa na tumeccm
 
Ni mtu mjinga asiyetambua kuwa upande ule mwingine Kuna kivuli Cha ushetani kimewavaa .

Wana mioyo ya ajabu yenye chuki kisa tu madaraka .

Ubinadamu umeachwa mbali .

Hawa watu wanadhani wataishi milele Wala hawajui kitakachowapata wajukuu zao .

Tangulizeni ubinadamu Basi
Maghufuli akishinda, ina maana watanzania wengi wana mambo ya kishetani, jambo ambalo sikubaliani nalo hata kidogo. Watanzania ni watu wenye huruma na ubinadamu. Kenya wenyewe huwa tunawashangaa!
 
Kazi anayo kubwa aisee kama ataamua kiwa mwl wa uraia
Maana kila anakopita lazima amwage notes kwa wananchi huku wenzake wakichanja mbuga kumwaga sera zaoo hahahaaa


Ualimu sio kazi nyepesi mjue, hadi wakuelewe watu ushapoteza muda mwingi wa kumwaga sera haahaaaa,

Lisu inabidi aachane na Uraisi ili aitumikie nafasi ya ualimu vyema aisee
Kazi na dawa.
 
Maghufuli akishinda, ina maana watanzania wengi wana mambo ya kishetani, jambo ambalo sikubaliani nalo hata kidogo. Watanzania ni watu wenye huruma na ubinadamu. Kenya wenyewe huwa tunawashangaa!
Sijataja jina hapa usiletee Mambo ya kiduanzi
 
Chama pendwa kilipofikia kwa sasa!
Egmtp-WWoAE_XGt.jpg
 
Sikujua kwamba aliyemuwahisha TL hospitali ni binti wa Mzee Juma Jamaldin Akukweti[r.i.p].

Juma Akukweti alikuwa mbunge wa Tunduru na alipata kuhudumu ktk serikali za Raisi Mkapa.

Huyo binti alikuwa msaidizi wa TL ktk bunge la 2010 to 2015, na sasa hivi ni msaidizi wa Dr.Tulia Ackson.

Sasa huyu binti wa Akukweti alikwenda kuitwa na msaidizi wa nyumbani wa TL, na pamoja na dereva, wakamkimbiza hospitali.

Bila msaada wa haraka wa hao watatu, nadhani tungekuwa tunazungumza habari nyingine leo.
Yah huyu mzee alifariki kwa ajali ya ndege huko mikoa ya nyanda za juu kusini km sijakosea!
 
Arejeshe na ajenda ya kupambana na ufisadi, ccm wanafanya kampeni kwa pesa ya ufisadi trillioni 1.5 na pesa ya vitambulisho vya machinga.
 
Sikujua kwamba aliyemuwahisha TL hospitali ni binti wa Mzee Juma Jamaldin Akukweti[r.i.p].

Juma Akukweti alikuwa mbunge wa Tunduru na alipata kuhudumu ktk serikali za Raisi Mkapa.

Huyo binti alikuwa msaidizi wa TL ktk bunge la 2010 to 2015, na sasa hivi ni msaidizi wa Dr.Tulia Ackson.

Sasa huyu binti wa Akukweti alikwenda kuitwa na msaidizi wa nyumbani wa TL, na pamoja na dereva, wakamkimbiza hospitali.

Bila msaada wa haraka wa hao watatu, nadhani tungekuwa tunazungumza habari nyingine leo.
Yote hayo hata mimi sikuyafahamu. Pia sikufahamu kuwa serikali ya Kenya ilimpatia ulinzi rasmi.
 
Arejeshe na ajenda ya kupambana na ufisadi, ccm wanafanya kampeni kwa pesa ya ufisadi trillioni 1.5 na pesa ya vitambulisho vya machinga.
Naam, hii ya ufisadi asiache hata kidogo. Bado yule mkaguzi mkuu wa serikali aliyegunduwa ufisadi hajazungumziwa. Watanzania hawakuruhusiwa kuongea lolote maana kesi za uhujumu na kupotezwa ni kawaida kabisa na ccm huwa wanafurahia na kuchekelea. Sijui ni watanzania wa aina gani hawa?🤦🏾‍♂️
 
..amewataja Khadija Akukweti, Amina Abrahman Kanyama, na Adam Mohamed Bakari, ndio waliomuwahisha hospitali Dodoma.
 
Lisu yuko very focused na strategic. Wafungue mawazo/fikra watu kwanza wajitambue kuwa wanaonewa! , ni watumwa, HAKI ZAO ZA BINADAMU ZIMEKUFA etc, then baadaye tandaza sera! AU awe anaanza na sera, then dakika 20 za mwisho ni kuwafungua watu wanavyonewa, wanavyoibiwa na Jiwe, wanavyokosa haki zao etc etc

Kabisa Mkuu. Hapa Lissu na team yake wakazie
 
..amewataja Khadija Akukweti, Amina Abrahman Kanyama, na Adam Mohamed Bakari, ndio waliomuwahisha hospitali Dodoma.

Majina hayo yanadhihirisha waislamu wana mchango mkubwa katika historia ya Lissu. Mambo hayo yanampa mtu mmoja kiwewe hadi anaamua kuendesha mchango wa ujenzi wa msikiti akiwa kanisani!!

Mfumo wa kisiasa wa nchi hii umekuwa designed makusudi kuhakikisha wapinzani hawawezi kuwaunganisha waislamu na wakristo katika chaguzi kuu.
 
Back
Top Bottom