Naunga mkono uamuzi wa Donald Trump kuondoa misaada kwa nchi za Afrika

Naunga mkono uamuzi wa Donald Trump kuondoa misaada kwa nchi za Afrika

MImi naunga mkono hilo ili hizi nchi za kiafrica ziweze kubana matumizi na kutumia rasimali zake na kuwabana wezi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ikiwezekana wabunge na mawaziri mishahara yao ipunguzwe wakatwe maradufu kuchangia waathirika!
Kwa mara ya kwanza naona una andika jambo la akili na kizalendo kabisa👏
 
Baada ya Uchunguzi wangu wa kina nimeamua kwa dhati kabisa kuunga Mkono na Kupongeza Uamuzi wa Serikali ya Marekani kuondoa misaada yote kwa Nchi za kiafrika.

Hii ni kwa sababu misaada hiyo haikustahili kupewa Nchi hizo, kwa vile zinao uwezo wa kujihudumia zenyewe.

Kwa Mfano, Inawezekanaje kuipa msaada wa matundu ya vyoo Nchi ambayo Mawaziri wake wananunuliwa gari za LC300? unawezaje kusaidia Chanjo ya Polio Nchi ambayo Chama cha siasa kinanunua Mabasi zaidi ya 200 na Bodaboda zisizo na idadi kwa kisingizio cha kufanyia kampeni, Wakati inafahamika kwamba Wanaiba kura na Uchaguzi wote kwa Ujumla? Kwanza Wazungu walichelewa Mno kuchukua uamuzi huu Muruwa!

View attachment 3229455

Inawezekanaje kusaidia Nchi ambazo Wake ama Waume wa viongozi Wanalipwa mishahara mizito hata kama hawafanyi chochote?

Kwa kufupisha, Siungi Mkono watu kufa kwa kukosa ARV za Bure, lakini ni Aibu kuchimbiwa vyoo vya shule na Masoko huku Viongozi wanaokufa wanafumwa wamelundika Malundo ya Hela kwenye vyumba vyao.

Uamuzi huu uwe Fundisho kwa Wananchi Masikini waliochagua kuwa Machawa ili watupiwe Makombo.

MUNGU WABARIKI WAZUNGU
Infact,
Nchi nyingi za kiafrica zimeupokea uamuzi huo wa marekani kwa dhati na kwa mikono miwili, kwani ni hiyari yake kutoa au kutotoa misaada kwa waaFrica.

Hata hivyo,
misaada yenyewe iliambatana na nongwa nyingi sana, lakini pia ililenga kuifanya marekani kama ni watu wema sana, kumbe ni makatili na waovu watupu, lakini pia misaada yao ililenga tu kuzituhumu nchi za Africa kwa rushwa na ufisadi kitu ambacho si kweli, na ufisadi wa misaada yao ulifanywa na wao wenyewe.

Africa inajitosheleza kwa kila kitu, na Africa haijawahi kuilazimisha Marekani kutoa misaada popote.
Anaejiskia kutoa misaada popote ni hiyari yake kufanya hivyo au vinginevyo, haipo nchi inayo exist kwa misaada ya marekani Africa 🐒
 
Infact,
Nchi nyingi za kiafrica zimeupokea uamuzi huo wa marekani kwa dhati na kwa mikono miwili, kwani ni hiyari yake kutoa au kutotoa misaada kwa waaFrica.

Hata hivyo,
misaada yenyewe iliambatana na nongwa nyingi sana, lakini pia ililenga kuifanya marekani kama ni watu wema sana, kumbe ni makatili na waovu watupu, lakini pia misaada yao ililenga tu kuzituhumu nchi za Africa kwa rushwa na ufisadi kitu ambacho si kweli, na ufisadi wa misaada yao ulifanywa na wao wenyewe.

Africa inajitosheleza kwa kila kitu, na Africa haijawahi kuilazimisha Marekani kutoa misaada popote.
Anaejiskia kutoa misaada popote ni hiyari yake kufanya hivyo au vinginevyo, haipo nchi inayo exist kwa misaada ya marekani Africa 🐒
Kwamba hakuna ufisadi na rushwa Africa ?
 
Kwamba hakuna ufisadi na rushwa Africa ?
sio ya kiwango kilichokua kinasemwa na watoa misaada waovu na wenye gubu moyoni,

yaani unatoa misaada huku roho na moyo kwa pamoja vyakuuma 🐒
 
Umaskini uliopo Africa unasababishwa na viongozi kwa 80%
Gentleman,
uoga na uvuvi wako ndio umaskini wako.

kua maskini au tajiri ni uamuzi na hiyari ya mtu binafsi Africa na hususani Tanzania 🐒
 
Infact,
Nchi nyingi za kiafrica zimeupokea uamuzi huo wa marekani kwa dhati na kwa mikono miwili, kwani ni hiyari yake kutoa au kutotoa misaada kwa waaFrica.

Hata hivyo,
misaada yenyewe iliambatana na nongwa nyingi sana, lakini pia ililenga kuifanya marekani kama ni watu wema sana, kumbe ni makatili na waovu watupu, lakini pia misaada yao ililenga tu kuzituhumu nchi za Africa kwa rushwa na ufisadi kitu ambacho si kweli, na ufisadi wa misaada yao ulifanywa na wao wenyewe.

Africa inajitosheleza kwa kila kitu, na Africa haijawahi kuilazimisha Marekani kutoa misaada popote.
Anaejiskia kutoa misaada popote ni hiyari yake kufanya hivyo au vinginevyo, haipo nchi inayo exist kwa misaada ya marekani Africa 🐒
Mkuu kwanza hatoi misaada kwa kuipenda Africa. Bali anatoa viji misaada kuziba unyama waliofanyiwa waafrika utumwa.
Ukisikia Marekani aliendeleza kilimo,akajenga miundo mbinu kama miji,reli na barabara ni WAAFRIKA WATUMWA KUTOKA AFRIKA WALIOTUMIKA BURE KWA KARNE NA KARNE.
Sisi tuliosoma historia tunajua mbwa hao hawatupi misaada ila wananunua muda ili vizazi vipya wasahau unyama tuliofanyiwa.
Mtoa hoja namheshimu sana ila kwa hili ametanguliza ushabiki.
Miaka ya sitini yawezekana na sasa kulikuwa wanasheria nguli wa Kiafrika walikuwa wakipanga kesi ya kuitaka Marekani,Uingereza,Baadhi ya nchi Tajiri za Arabuni, Spain,Ubelgigi,France,Holland,Ureno,Germany, zilipe fidia ya unyama waliofanyiwa waafrika utumwa,ukoloni na wizi wa mali zao.
Eti mzungu kiazi anakusomesha uchumi na kukutia kasumba kwanini hu maskini ila hakwambii kuwa ana matani na matani ya dhahabu aliyopora Africa, ambayo uchumi wake ukiyumba kidogo anatoa vinoo vya dhahabu kidogo anauza kukabili tatizo.
 
Mkuu kwanza hatoi misaada kwa kuipenda Africa. Bali anatoa misaada kuziba unyama waliofanyiwa waafrika utumwa.
Ukisikia Marekani aliendeleza kilimo,akajenga miundo mbinu kama miji,reli na barabara ni WAAFRIKA WATUMWA KUTOKA AFRIKA WALIOTUMIKA BURE KWA KARNE NA KARNE.
Sisi tuliosoma historia tunajua mbwa hao hawatupi misaada ila wananunua muda ili vizazi vipya wasahau unyama tuliofanyiwa.
Mtoa hoja namheshimu sana ila kwa hili ametanguliza ushabiki.
Miaka fulani yawezekana na sasa kulikuwa wanasheria nguli wa Kiafrika walikuwa wakipanga kesi ya kuitaka Marekani,Uingereza,Baadhi ya nchi Tajiri za Arabuni, Spain,zilipe fidia ya unyama waliofanyiwa waafrika utumwa,ukoloni na wizi wa mali zao.
Eti mzungu kiazi anakusomesha uchumi na kukutia kasumba kwanini hu maskini ila hakwambii kuwa ana matani na matani ya dhahabu aliyopora Africa, ambayo uchumi wake ukiyumba kidogo anatoa vinoo vya dhahabu kidogo anauza kukabili tatizo.
Gentleman,
kula tana kwanza dah 👊

thank you 🙏💪
 
Magufuli alikuwa mbele ya muda.

Atayeathirika ni ombaomba Tundu Lisu
Tundu Lissu? Ndio huyu kaongeza na deni la taifa, ni Tundu Lissu ndio alisababisha hadi spika wetu mzuri kujiuzuru kwasababu spika Job Ndugai alikemea tabia ya kukopa kopa; huyu Tundu Lissu ndio anakwenda Ulaya na Marekani kukopa na kuomba omba pesa za kujengea vyoo vya watoto, Tundu Lissu na chama chake hawafai kabisa
 
Duh 🤣🤣🤣 haya mkuu
Yes,
kwasabb malipo na stahiki za mbunge au gavana moja tu wa marekani kwa mwezi yakiwekwa wazi ni ni sawa na bajeti ya wizara Fulani kwenye nchi moja ya kiafrica kwa mwaka 🐒
 
Yes,
kwasabb malipo na stahiki za mbunge au gavana moja tu wa marekani kwa mwezi yakiwekwa wazi ni ni sawa na bajeti ya wizara Fulani kwenye nchi moja ya kiafrica kwa mwaka 🐒
Unajua pamoja na hivyo daktari bado anamalipo mazuri zaidi?
 
Back
Top Bottom