Nawachukia baadhi ya wanaume kuanzia leo

Nawachukia baadhi ya wanaume kuanzia leo

pole DA na punguza hasira. Tafuta kitu unachopenda zaidi ukifanye ili kupunguza hasira.
 
Yamenifika kooni BAK mpaka nataka kutapika mtu hakuheshimu wala kukujali hata kidogo potelea mbali ngoja nitoe nyongo nisisikie kichefuchefu tena

Pole sana.inaelekea yameanza siku nyingi. Kama utakumbuka nilikutumia PM kukuuliza mbona umeadimika hivyo? Si ajabu ndio ulikuwa tayari katika wakati mgumu. Pole sana DA
 
Nimekuja maana naona hawa kina Sipiyu nao wanakuongezea tu hasira!

Ila kweli kama kuna sehemu tulivu nenda ukajikalie na kutembea tembea kidogo akili yako itulie!Au kama unaweza hata kukimbia kidogo hua inasaidia sana kushusha munkari!!

Hasira hazitamjenga, badala yake zitazidi kumbomoa
Kanitaka niondoke ktk hii thread lakin SITAONDOKA HATA
 
Sasa wewe badala ya kupoint out makosa ungemtuliza ili hizo hasira zipungue na hitaji la kutukana nalo litoweke.Sio kila kitu unachambua kifilosofia....wakati mwingine unachohitajika ni kumwambia tu mtu POLE...USIJALI...YATAPITA and the likes na sio unaanza na sijui hasira zisikuendeshe sijui mambo gani gani.

Ningekuwa karibu yako ningekufanyaje sijui umenisaidia kupunguza hasira nilizonazo leo. Thanks Baby Stay Blessed
 
pole swthat, wanaume ndivyo walivyo mwaya, hawabebeki, hawapendeki, hawana shukrani n.k. Tafuta mahal nenda kapumzishe akil, utapata sukar bure.
 
Ungekuwa karibu ningekueleza kaniudhi balaa na hasira mpaka nataka kuzimia hapa nilipo mori umepanda mpaka basi acha tu

Ngoja nikae mbali na wewe kwanza hasira zikiisha ntakuona mida nikushauri la kufanya....maisha yenyewe mafupi kwanini mtu akupe shida na foleni zooote hizi loh
 
Pole sana.inaelekea yameanza siku nyingi. Kama utakumbuka nilikutumia PM kukuuliza mbona umeadimika hivyo? Si ajabu ndio ulikuwa tayari katika wakati mgumu. Pole sana DA

Yameanza siku nyingi lakini today im nimefika kiwango cha mwisho kwanini lakini mtu humuheshimu mwenzio humjali humthamini???
 
Hasira hazitamjenga, badala yake zitazidi kumbomoa
Kanitaka niondoke ktk hii thread lakin SITAONDOKA HATA
Acha sifa basi mazeee...
Ingekua watu hatuhitaji kua na hasira once in a while Mungu angetunyima uwezo wa kukasirika.Sasa ye hasira zake anazimaliza kwa maneno yasiyomuumiza yeyote hapa...hapo tatizo liko wapi?!Kama hujagurahia anavyojiexpress mwache...kama ye inamsaidia. shida iko wapi?!
 
Kwanini hamna huruma?
Kwanini hamthamini wanawake?
Kwanini hamna heshima na adabu?
Kwanini Hamthamini michango yetu kwenye familia??
Kwanini Mnamadharau?
Kwanini hamjali maumivu msababishayo kwa mkeo?
Kwanini hamjali hisia tulizonazo??
Kwanini mawasiliano mwanamke tu ndo aanze??
KWanini hamjali msaada mnaopewa??

NAWACHUKIA NAWACHUKIA NAWACHUKIA NAWACHUKIA MILELE SIWAPENDI


JF Ingeruhusu matusi nadhani hasira yangu ingeishia hapa leo.............ukoje wewe mwanaume upendweje?? Usaidiweje?? Ujaliweje?

Ngoja nika............oohh gooooshi nilale tu
Mtu asiniulize nini kimenikuta but nimeumizwa vya kutosha today nasema kilichonisibu

Pole pole dada. Max amesema anapitia na jukwaa hili pia kucheki posts zote kama ziko sawa. Inaonekana umefikia the point of not return. Ila pole sana. Ila mchukie huyo tuu, sio baadhi unless waliokutendea baya ni "baadhi"
 
Sasa wewe badala ya kupoint out makosa ungemtuliza ili hizo hasira zipungue na hitaji la kutukana nalo litoweke.Sio kila kitu unachambua kifilosofia....wakati mwingine unachohitajika ni kumwambia tu mtu POLE...USIJALI...YATAPITA and the likes na sio unaanza na sijui hasira zisikuendeshe sijui mambo gani gani.

Kitu gani nimechambua kifilosofia???
Kumwambia hasira hazifai ndo kumchambua kifilosofia?
 
Acha sifa basi mazeee...
Ingekua watu hatuhitaji kua na hasira once in a while Mungu angetunyima uwezo wa kukasirika.Sasa ye hasira zake anazimaliza kwa maneno yasiyomuumiza yeyote hapa...hapo tatizo liko wapi?!Kama hujagurahia anavyojiexpress mwache...kama ye inamsaidia. shida iko wapi?!

Mama Mchungaji thanks sina cha kuongeza naweza kuharibu bure
 
Acha sifa basi mazeee...
Ingekua watu hatuhitaji kua na hasira once in a while Mungu angetunyima uwezo wa kukasirika.Sasa ye hasira zake anazimaliza kwa maneno yasiyomuumiza yeyote hapa...hapo tatizo liko wapi?!Kama hujagurahia anavyojiexpress mwache...kama ye inamsaidia. shida iko wapi?!

Humu ndani tunafundishana na kuwekana sawa pale tunapoona tumekosea
Kama mimi kumwambia hasira hazifai wakati amekasirika basi litakuwa somo
Lakin hasira hizo hizo zisitumike kuhalalisha kufanya unavyotaka, kama kutoa matusi
 
pole swthat, wanaume ndivyo walivyo mwaya, hawabebeki, hawapendeki, hawana shukrani n.k. Tafuta mahal nenda kapumzishe akil, utapata sukar bure.

Hapo kwenye red hata wachaga?
 
Back
Top Bottom