Nawafundishaje walimu ili waje kufundisha?

Nawafundishaje walimu ili waje kufundisha?

Me sio mwalimu ni PA ila fanya hivi chukua area of concerntration wape wajisomee kwa makundi alafu waje wafanye presentation kila kundi ila muda huo na we unatakiwa uwe unawafundisha kupia hizo presentation zao kwa kuwakosoa na kuwapa kazi warudie tena ili mladi wawe bize na somo lako alafu uwe unatoa quiz hii itasaidia sana
 
Unawapa testi za mara kwa mara

Kila baada ya vipindi viwili vitatu walime quiz

Test kila mara kuwafanya walisome zaidi somo lako

Halafu mitihani tunga ya kawaida maana walimu nyie kwa kupenda kutunga mitihani migumu hamjambo

Upo lakini???
 
Mmmmhhh in a man a wote ni vilaza Hamna kipanga hata mmoja? Basi chagua wafaulu wote au wafeli wote au Kata katikati.
 
Hebu ngoja kwanza nifikirie maana nahisi kama hii sredi imesheheni lugha ya picha...

Mwalimu na mwalimu wa mwalimu hebu ngoja kwanza...
 
Ukiona darasa nzima hawakuelewi basi teaching methodoloji unazotumia hazieleweki au hujui kupangilia mada.

Katika kufundisha angalua 10-20% inatakiwa waelewe hapo hap, 30+% inatakiwa waelewe baadae baada ya kurifaa ulichofundisha na notc, 20+% inatakiwa waelewe baada ya kueleweshwa tena na wenzao the rest wanaweza wasielewe kabisa. Soma cognitive theory of learning. Samahani lakini mimi sio Mwalimu correction is allowed.

Kuwapa review ya maswali ili wafauru ni kosa kubwa sana.
 
Babu Dark City umejaribu kutumia njia anuai m'badala kuangalia ikiwa malengo ya somo yanatimika....? Hebu Jaribu kuwashikisha katika kujifunza kwao....
 
Last edited by a moderator:
Chuo sio sehemu ya kuelewa, wanatakiwa wafaulu mtihani. Ndo maana kuna field
 
Ndugu zangu wana MMU,

Naomba mnisaidie jambo ambalo limenikwaza kidogo. Ngoja nijaribu kueleza mambo yalivyonibana,

Tuchukulie kwamba wewe ni mwalimu ambaye unafundisha wanafunzi ambao ni walimu watarajiwa (mwalimu wa walimu). Bahati mbaya somo lako linawapa taabu sana na hawaonekani kuelewa vitu vya msingi. Muda unaenda na wanatakiwa kufanya mtihani wa kumaliza masomo. Wewe mwenyewe ndiye unautunga na kusahihisha. Kwa vile muda wa kufanya mtihani bado kidogo, utawasaidiaje vijana wako ili walaulu? Na si kufaulu tu, ila huko mbele ya safari waweze kufundisha wanafunzi wao vizuri?

Je, utawapitisha hivyo hivyo....liwalo na liwe? Au utabanana nao hadi kieleweke? Kwamba hata wakifeli wote, potelea mbali kuliko kupeleka makapi uraiani?

Wenu katika kizungumkuti,

Babu DC!!

cc: Asprin, Kaizer, Fixed Point, King'asti, Mtambuzi, snowhite, gfsonwin, Mbu, Paloma, CHUAKACHARA, Mwanyasi, KOKUTONA, YNNAH, Arabela (sitakunyaka mdogo wangu), MwanajamiiOne, watu8..

No, huwezi kuwapasisha wanafunzi wasiokuwa na kiwango cha elimu tarajiwa. kurudia mwaka linaweza kuwa suluhisho la kupata muda wa watoto kujifunza kufikia kiwango.
 
Sorry lakn mkuu kwan unawafundisha masomo ya mapenzi au?
 
Very interesting.

Naamini sitachanganyikiwa zaidi.
 
No, huwezi kuwapasisha wanafunzi wasiokuwa na kiwango cha elimu tarajiwa. kurudia mwaka linaweza kuwa suluhisho la kupata muda wa watoto kujifunza kufikia kiwango.

Wakifeli wote na kukosa kibarua + mafweza, si nitakuwa source ya umaskini wao na familia zao?
 
Kama ningekuwa wewe ninacho Fanya let say zimebaki wiki mbili ninacho Fanya ni kuwafundisha kwa njia ya maswali!
Nahakikisha nime wapa maswali tofauti tofauti yanayo husiana na topic husika kwa njia ya group assignment kila Siku at least maswali matano!

Nina uhakika wakija kuingia kwenye mtihani wa mwisho watakuwa wameiva!
 
Back
Top Bottom