Ni somo lako tuu ndilo linawapa taabu au ni pamoja na baadhi ya masomo mengine au yote? Kama ni masomo yote, then hapo tatizo linaweza kuwa pana zaidi. Lakini kama ni somo lako tuu, then tatizo linaweza kuwa wewe au labda hilo somo ni gumu zaidi kupita masomo mengine.
Ila nakumbuka baadhi ya walimu ambao wanafundisha masomo ambayo ni compusory huwa wanajidai sana halafu wananoko sana kwa sababu wanajua whatever the case, wanafunzi hawezi kulikimbia somo.
Obvious lazima shule/chuo kitakuwa na standards za ku-set mitihani ambazo kama mwalimu unatakiwa uzifuate. Kama ni mwalimu unayeamini kwenye standards na quality, huwezi kupanua goli ili tuu wanafunzi wengi wafunge magoli. Bali utawafundisha skills za kufunga magoli kama Messi.
Prevention is always better than protection. Quality is always better than quantity. Mfano angalia sasa jinsi tunavyohangaika na elimu yetu iliyoshuka.
Nisisahahu huwa pia kuna mtindo wa wanafunzi kwa sababu fulani kuamua kumchukia mwalimu na automatically kuchukia hata somo analofundisha. Nakumbuka form one na two nilikuwa napenda sana biology na nilikuwa napasua, lakini kuanzia form three nililichukia hilo somo kisa mwalimu. The same happened nilipokuwa elimu ya juu; module moja niliipenda sana lakini nilipohudhuria lectures tatu tuu nikaona lecturer mzinguaji nika-switch kwenye module nyingine ambayo sikuipenda saaana lakini jinsi mwali alivyokuwa anafundisha mpaka leo nazikumbuka lectures zake. Major topics zimenikaa kichwani mpaka leo.