Nawaonya vijana wa leo mnaofungua makanisa kila kukicha acheni mara moja kama hamna wito, Injili sio biashara.

Nawaonya vijana wa leo mnaofungua makanisa kila kukicha acheni mara moja kama hamna wito, Injili sio biashara.

Kuzimu imeingia makanisani kwa sasa kupitia haya makanisa yaliyotokea Marekani mengi yalianzishwa ili kuharibu Ukristo.
Aliyeanzisha music wa Rap na haya makanisa ya kufokafoka ni mtu mmoja ndio uzao wa uharibifu makanisani.
 
Unawaonea bure .

Shida ni waumin wa dini ya kikristo
Mbona vijana wa kiislam hawafungui misikit wala kujiita masheikh?

Niny wenyew mmeifanya kazi ya Mungu NI kazi Kama kazi nyingine na si huduma.
Tutaendelea kusali wabadilike
 
Pana motivation speakers na pana mens of God ipo haja ya mamlaka kuwakategorize.
Mfano kiboko ya wachawi yeye kabase kuuwa wachawi so ni wewe tu unachagua unataka injili kavu za kina mbarikiwa, Cassian,mwangila au unataka zile za kupokea makontena
Wengi wao ni motivational speaker wamejivisha utumishi kwa kivuli cha kanisa wapige hela
 
Naandika Uzi huu moyo wangu ukibubujikwa na machozi.

Kuna vitu vinafanyika kwenye madhabahu mpaka mtu unaogopa, na huhitaji PhD Ili kujua wengi wa hawa leo waliojipa unabii ambao sina hakika hata kama walipitia kwenye vyuo vya biblia wakapikwa wakapikika.

Sio mavazi wanayovaa, si lugha wanazotumia vyote havisadifu Ile injili ya kweli tuliyoachiwa na Bwana wetu Yesu Kristo. Kinachoendelea ni wazi watu wanatumia matatizo ya watu kwa kivuli cha unabii waliojivika kufanya biashara makanisani. Ndipo ule unabii wa neno la kwenye biblia la Hosea 4:6 unatimia kwa kusema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"

Katika kitabu cha Mathayo 7:15; neno la Mungu linasema "Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini ndani ni mbwa-mwitu wakali". Hili halina ubishi wengi wa waanzilishi wa makanisa hii leo hasa vijana hawana wito wa kweli ndani yao na neno la Mungu haliko ndani yao bali wana agenda zao kujipatia fedha. Haiwezekani mtu akiweza tu kuhubiri prosperity gospel au kutoka motivation akawa maarufu na ana jina basi anafungua kanisa.

Ukizikiliza hata mahubiri yao mengi hasa clips mbali mbali kutoka TikTok huoni wanakemea dhambi na kuhubiri wokovu 100%, bali wake base kwenye mahubiri ya mafanikio katika maisha, mahusiano ya kimapenzi inshort wanawapa waumini wao wanachotaka kusikia ni tofauti kabisa na wale wahubiri wa barabarani ambao wao nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe.

Nimeshtushwa zaidi kusikia mtu mmoja anaitwa gudlove eti na yeye ana mpango wa kufungua kanisa lakini ukitizama baadhi ya clip zake huko mitandaoni unaona hawa watu waaleta mzaha na neno la Mungu. Ndipo ninasema vijana kama hamna wito acheni kupotosha watu kisa tu una jina au pesa.

Injili ya 2009 kurudi nyuma VS Injili ya 2010 up to date.

Wengi wa vijana tulionza kujitambua mwishoni mwa miaka ya 90 hadi kufikia 2008/2009 tukipelekwa kwenye mikutano ya Injili na wazazi wetu mfano kwa Egon Falk au Christopher Mwakasege watakubaliana nami kwamba Injili iliyokuwa inahubiriwa kipindi kile ni tofauti na hii unayohubiriwa na hawa vijanawa sasa. Mfano mzuri Christopher Mwakasege bado anaefanya mikutano yake hadi leo.

Sasa angalia utaratibu wa huduma ya Mwakasege na huu utaratibu wa wahubiri wa kisasa, wahubiri wa siku hizi pesa, mafanikio, na mahusiano ndio main topic kwenye mahubiri yao Toba, ubatizo na wokovu wa kweli utausikia kwa nadra sana au usisikie kabisa na inafika muda waumini wanalazimishwa kutoa pesa. Ukisoma 2 Petro 2:3 inasema "Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao Toka zamani haikawii, Wala uvunjifu wao hausinzii" Ndio maana hao wenye makanisa Ili uweze kuwaona lazima utoe pesa hii ni Injili au biashara??

Na wengi wao wana utajiri wa kufuru na wanaishi maisha ya anasa wakati hao waumini wao waliopotea kwa kukosa maarifa wanaishi kwenye ufukara wa kutupa. Kinachoumiza pia kuna nchi nyingine manabii na mitume hao wananajisi madhabahu wa kuwavua nguo waumini wao ama hata kuwashika sehemu zao za siri kwa kigezo cha kufanya maombezi ya uponyaji.

Kama wanayafanya mambo haya hadharani ni nini kinachoendelea huko maofisini mwao wanapojificha eti bila hela huwezi kuwaona?? Na kuna member humu aliwahi kulalamika mke wake anamsikiliza zaidi mchungaji/mtume wake kuliko yeye. (There must a be a problem and mchungaji is a problem)

Na hata kwaya nazo huko makanisani hasa haya kisasa yanayoendelea ni ushetani mtupu yaani leo hii kwaya kucheza Amapiano kanisani sio issue, watu wanakata viuno na viongozi wa kanisa hawakemei wapo kimya mpaka unajiuliza wanaburudika au?? Na mbaya zaidi the so called Praise and worshipping team nguo wanazovaa kuna muda unaogopa wewe unayetazama. Hii ndio Injili aliyosema Yesu katika Marko 16:15 kuwa tuenende ulimwenguni mwote tukaihubiri Injili kwa kila kiumbe?

Lakini pia nilishutuka kuona Pastor Kapola kanisani kwake wanawake wamevaa skin jeans zimechora miili yao guys let's have some respect we can't worship our Almighty God in this way.

Sio wote hawana wito ila wengi wao ukiona tu anachofanya maarifa ya asili yanakataa sababu ni utapeli wa wazi wazi. Mfano Nabii Olivia wa kule Sinza aliwahi kumwambia mtu aliyekuwa anamuombea kuwa apige kelele, haya maigizo ndio yanapaka matope hata wale wenye wito wa kweli.

Vijana wote tunaoifahamu kweli ya Kristo tutumie akili zetu na elimu zetu kukemea utapeli unaofanywa na vijana wenzetu kisa tu wapate utajiri wa haraka kwa staged miracles. Hii haikubaliki na MUNGU HADHIHAKIWI.
Umeandika vizuri lakini nikuambie ukweli: HAO MANABII, MITUME, WALIMU n.k wa aina hiyo na mambo yao hayo SIYO UKRISTO. NI USHETANI ULIOPAKWA JINA LA YESU. NI MAKUFURU. Wote wanaofuata upumbavu huo jwa hao wahubiri wanakufuru. Watakiona cha moto. Ukristo halisi umejengwa kwenye misingi iliyoachwa na mitume na si huu upumbavu unaoendelea leo. NI USHETANI MTUPU NA WOTE WANAOKIMBILIA MIUJIZA HUKO WOTE NI WAFUASI WA SHETANI WANAOLITAJA BURE JINA LA YESU KRISTO.
 
Naandika Uzi huu moyo wangu ukibubujikwa na machozi.

Kuna vitu vinafanyika kwenye madhabahu mpaka mtu unaogopa, na huhitaji PhD Ili kujua wengi wa hawa leo waliojipa unabii ambao sina hakika hata kama walipitia kwenye vyuo vya biblia wakapikwa wakapikika.

Sio mavazi wanayovaa, si lugha wanazotumia vyote havisadifu Ile injili ya kweli tuliyoachiwa na Bwana wetu Yesu Kristo. Kinachoendelea ni wazi watu wanatumia matatizo ya watu kwa kivuli cha unabii waliojivika kufanya biashara makanisani. Ndipo ule unabii wa neno la kwenye biblia la Hosea 4:6 unatimia kwa kusema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"

Katika kitabu cha Mathayo 7:15; neno la Mungu linasema "Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini ndani ni mbwa-mwitu wakali". Hili halina ubishi wengi wa waanzilishi wa makanisa hii leo hasa vijana hawana wito wa kweli ndani yao na neno la Mungu haliko ndani yao bali wana agenda zao kujipatia fedha. Haiwezekani mtu akiweza tu kuhubiri prosperity gospel au kutoka motivation akawa maarufu na ana jina basi anafungua kanisa.

Ukizikiliza hata mahubiri yao mengi hasa clips mbali mbali kutoka TikTok huoni wanakemea dhambi na kuhubiri wokovu 100%, bali wake base kwenye mahubiri ya mafanikio katika maisha, mahusiano ya kimapenzi inshort wanawapa waumini wao wanachotaka kusikia ni tofauti kabisa na wale wahubiri wa barabarani ambao wao nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe.

Nimeshtushwa zaidi kusikia mtu mmoja anaitwa gudlove eti na yeye ana mpango wa kufungua kanisa lakini ukitizama baadhi ya clip zake huko mitandaoni unaona hawa watu waaleta mzaha na neno la Mungu. Ndipo ninasema vijana kama hamna wito acheni kupotosha watu kisa tu una jina au pesa.

Injili ya 2009 kurudi nyuma VS Injili ya 2010 up to date.

Wengi wa vijana tulionza kujitambua mwishoni mwa miaka ya 90 hadi kufikia 2008/2009 tukipelekwa kwenye mikutano ya Injili na wazazi wetu mfano kwa Egon Falk au Christopher Mwakasege watakubaliana nami kwamba Injili iliyokuwa inahubiriwa kipindi kile ni tofauti na hii unayohubiriwa na hawa vijanawa sasa. Mfano mzuri Christopher Mwakasege bado anaefanya mikutano yake hadi leo.

Sasa angalia utaratibu wa huduma ya Mwakasege na huu utaratibu wa wahubiri wa kisasa, wahubiri wa siku hizi pesa, mafanikio, na mahusiano ndio main topic kwenye mahubiri yao Toba, ubatizo na wokovu wa kweli utausikia kwa nadra sana au usisikie kabisa na inafika muda waumini wanalazimishwa kutoa pesa. Ukisoma 2 Petro 2:3 inasema "Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao Toka zamani haikawii, Wala uvunjifu wao hausinzii" Ndio maana hao wenye makanisa Ili uweze kuwaona lazima utoe pesa hii ni Injili au biashara??

Na wengi wao wana utajiri wa kufuru na wanaishi maisha ya anasa wakati hao waumini wao waliopotea kwa kukosa maarifa wanaishi kwenye ufukara wa kutupa. Kinachoumiza pia kuna nchi nyingine manabii na mitume hao wananajisi madhabahu wa kuwavua nguo waumini wao ama hata kuwashika sehemu zao za siri kwa kigezo cha kufanya maombezi ya uponyaji.

Kama wanayafanya mambo haya hadharani ni nini kinachoendelea huko maofisini mwao wanapojificha eti bila hela huwezi kuwaona?? Na kuna member humu aliwahi kulalamika mke wake anamsikiliza zaidi mchungaji/mtume wake kuliko yeye. (There must a be a problem and mchungaji is a problem)

Na hata kwaya nazo huko makanisani hasa haya kisasa yanayoendelea ni ushetani mtupu yaani leo hii kwaya kucheza Amapiano kanisani sio issue, watu wanakata viuno na viongozi wa kanisa hawakemei wapo kimya mpaka unajiuliza wanaburudika au?? Na mbaya zaidi the so called Praise and worshipping team nguo wanazovaa kuna muda unaogopa wewe unayetazama. Hii ndio Injili aliyosema Yesu katika Marko 16:15 kuwa tuenende ulimwenguni mwote tukaihubiri Injili kwa kila kiumbe?

Lakini pia nilishutuka kuona Pastor Kapola kanisani kwake wanawake wamevaa skin jeans zimechora miili yao guys let's have some respect we can't worship our Almighty God in this way.

Sio wote hawana wito ila wengi wao ukiona tu anachofanya maarifa ya asili yanakataa sababu ni utapeli wa wazi wazi. Mfano Nabii Olivia wa kule Sinza aliwahi kumwambia mtu aliyekuwa anamuombea kuwa apige kelele, haya maigizo ndio yanapaka matope hata wale wenye wito wa kweli.

Vijana wote tunaoifahamu kweli ya Kristo tutumie akili zetu na elimu zetu kukemea utapeli unaofanywa na vijana wenzetu kisa tu wapate utajiri wa haraka kwa staged miracles. Hii haikubaliki na MUNGU HADHIHAKIWI.
Unahakikishaje na kuthibitishaje mahubiri yao sio ya kweli ila ya wachungaji wengine ni ya kweli?

Wakikwambia kwamba Bwana wao Yesu haangalii mavazi bali mioyo yao, utajibu ni nini?

Utahakikishaje na kuthibitishaje huyo Yesu anajali na kuangalia mavazi ya wahubiri wake?
 
Na kuna wengine wanauza mchanga,maji na mafuta ya nyonyo,keki na kujidai vina baraka kila kitu kinaanzia buku, jamaa kila akifanya mahubiri huwa na lori la bidhaa zake anadanganya waumini wanunue ndio watapata upako, waumini wake ni hohe hahe yeye anazidi kuporomosha mahoteli, majumba ya kuishi, kumiliki mashamba na vitega uchumi kibao-wajinga ndio waliwao. Mimi nasali haya makanisa makuu lakini sitaki kuzoeana na wachungaji, wachungaji hupenda kufanya urafiki na mtu anayeweza kuamua kuwa kesho nataka nile biriani au pilau,wengi wao ni omba omba kwa waumini,hawa ni tofauti na hawa wenye SACCOS zao (makanisa yao) hao wote ni matapeli, nimemuona kijana mmoja eti ae ni pastor anasifiwa na Mwijaku pembeni amepaki Hummer, kavaa visiruali vya kubana Domo kasingiziwa.
 
Na kuna wengine wanauza mchanga,maji na mafuta ya nyonyo,keki na kujidai vina baraka kila kitu kinaanzia buku, jamaa kila akifanya mahubiri huwa na lori la bidhaa zake anadanganya waumini wanunue ndio watapata upako, waumini wake ni hohe hahe yeye anazidi kuporomosha mahoteli, majumba ya kuishi, kumiliki mashamba na vitega uchumi kibao-wajinga ndio waliwao. Mimi nasali haya makanisa makuu lakini sitaki kuzoeana na wachungaji, wachungaji hupenda kufanya urafiki na mtu anayeweza kuamua kuwa kesho nataka nile biriani au pilau,wengi wao ni omba omba kwa waumini,hawa ni tofauti na hawa wenye SACCOS zao (makanisa yao) hao wote ni matapeli, nimemuona kijana mmoja eti ae ni pastor anasifiwa na Mwijaku pembeni amepaki Hummer, kavaa visiruali vya kubana Domo kasingiziwa.
Dhana nzima ya Mungu ilijengwa kwenye Uongo

Acha vijana watumie na wanufaike na dhana hiyohiyo iliyotumiwa na makanisa makubwa kuchota hela za watu kama Roman Catholic, KKKT, Anglican n.k

Hata kwenye hayo makanisa makubwa ni Hela za waumini tu ndizo huitajika and nothing else.

Kama huyo Mungu/ Yesu yupo kila mahali unaenda huko kanisani kufanya nini?

Huoni kwamba unaenda kutapeliwa tu hela zako utoe michango na sadaka kwa kigezo eti una mtolea Mungu?
 
Dhana nzima ya Mungu ilijengwa kwenye Uongo

Acha vijana watumie na wanufaike na dhana hiyohiyo iliyotumiwa na makanisa makubwa kuchota hela za watu kama Roman Catholic, KKKT, Anglican n.k

Hata kwenye hayo makanisa makubwa ni Hela za waumini tu ndizo huitajika and nothing else.

Kama huyo Mungu/ Yesu yupo kila mahali unaenda huko kanisani kufanya nini?

Huoni kwamba unaenda kutapeliwa tu hela zako utoe michango na sadaka kwa kigezo eti una mtolea Mungu?
Dhana ya dini kwangu haipo sana kwangu ni kama kusocialise tu, natoa sadaka ili nikiwa futi sita chini waje kuimba mapambio kuwafariji ndugu zangu na wanafamilia wangu wakati wakilia si kwa uchungu bali kwa jinsi watakavyoendesha maisha yao baada ya Bill Gates kuwa hawatamuona tena.
 
Unahakikishaje na kuthibitishaje mahubiri yao sio ya kweli ila ya wachungaji wengine ni ya kweli?

Wakikwambia kwamba Bwana wao Yesu haangalii mavazi bali mioyo yao, utajibu ni nini?

Utahakikishaje na kuthibitishaje huyo Yesu anajali na kuangalia mavazi ya wahubiri wake?
Nashukuru kwa swali zuri,

Nitakujibu kwa ushahidi wa kibiblia.

Kuhusu mahubiri yasiyo ya kweli:
Katika 2 Timotheo 3:16 inasema "Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu makosa yao, na kwa kuadabisha katika haki"
Hivyo mahubiri yeyote ambayo hayana mlengo wa utukufu wa Mungu hayo hayafai, mfano kuna mtu anajiita Nabii aliwahi kusema siwezi kuacha kuangalia chupi ya muumini wangu kisa nahubiri mtu kama huyu hawezi kuwa na mahubiri ya kweli.

Kuhusu mavazi:
Katika 1 Timotheo 2:9 inasema "Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujistri, pamoja na adabu nzuri na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, Wala kwa dhahabu na lulu, Wala kwa nguo za thamani"
Hivyo hata kama Yesu anaangalia moyo lakini sababu usijistri na kuvaa kwa adabu kama maandiko yanavyosema.
 
Na kuna wengine wanauza mchanga,maji na mafuta ya nyonyo,keki na kujidai vina baraka kila kitu kinaanzia buku, jamaa kila akifanya mahubiri huwa na lori la bidhaa zake anadanganya waumini wanunue ndio watapata upako, waumini wake ni hohe hahe yeye anazidi kuporomosha mahoteli, majumba ya kuishi, kumiliki mashamba na vitega uchumi kibao-wajinga ndio waliwao. Mimi nasali haya makanisa makuu lakini sitaki kuzoeana na wachungaji, wachungaji hupenda kufanya urafiki na mtu anayeweza kuamua kuwa kesho nataka nile biriani au pilau,wengi wao ni omba omba kwa waumini,hawa ni tofauti na hawa wenye SACCOS zao (makanisa yao) hao wote ni matapeli, nimemuona kijana mmoja eti ae ni pastor anasifiwa na Mwijaku pembeni amepaki Hummer, kavaa visiruali vya kubana Domo kasingiziwa.
Natamani Ile kweli ya Kristo ndio ihubiriwe no matter what
 
Dhana nzima ya Mungu ilijengwa kwenye Uongo

Acha vijana watumie na wanufaike na dhana hiyohiyo iliyotumiwa na makanisa makubwa kuchota hela za watu kama Roman Catholic, KKKT, Anglican n.k

Hata kwenye hayo makanisa makubwa ni Hela za waumini tu ndizo huitajika and nothing else.

Kama huyo Mungu/ Yesu yupo kila mahali unaenda huko kanisani kufanya nini?

Huoni kwamba unaenda kutapeliwa tu hela zako utoe michango na sadaka kwa kigezo eti una mtolea Mungu?
For what I know you need to give us proof to support what you said.
 
Nashukuru kwa swali zuri,

Nitakujibu kwa ushahidi wa kibiblia.

Kuhusu mahubiri yasiyo ya kweli:
Katika 2 Timotheo 3:16 inasema "Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu makosa yao, na kwa kuadabisha katika haki"
Hivyo mahubiri yeyote ambayo hayana mlengo wa utukufu wa Mungu hayo hayafai, mfano kuna mtu anajiita Nabii aliwahi kusema siwezi kuacha kuangalia chupi ya muumini wangu kisa nahubiri mtu kama huyu hawezi kuwa na mahubiri ya kweli.

Kuhusu mavazi:
Katika 1 Timotheo 2:9 inasema "Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujistri, pamoja na adabu nzuri na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, Wala kwa dhahabu na lulu, Wala kwa nguo za thamani"
Hivyo hata kama Yesu anaangalia moyo lakini sababu usijistri na kuvaa kwa adabu kama maandiko yanavyosema.
Biblia si ushahidi bali hadithi zisizo na uthibitisho wowote ule.

Ni sawa na Hekaya za Abunuwasi uziite ushahidi bila kuthibitisha uwepo wa Abunuwasi mwenyewe.
 
Back
Top Bottom