Nawapongeza wasabato kwa kanisa lao kutovuma kwa skendo na drama

Nawapongeza wasabato kwa kanisa lao kutovuma kwa skendo na drama

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
- Kila siku hujisomea somo la wiki, ikifika jumamosi wanakusanyika kwa masaa takribani mawili kwenye vikundi vidogo kufundishana waliyojifunza na baada ya hapo ndio huingia wote kanisani kwenye ibada, hii ni nzuri kuzidi kukaa wiki nzima hujajifunza chochote kwenye biblia unasubiri tu ifike jumapili kwenda kwenye ibada kumsikiliza mchungaji.

- Ni nadra sana kusikia kuna vurugu kanisani mfano kwa viongozi wanaong'ang'ania vyeo mpaka kufikia kanisa kugawanyika, kwa kanisa kama kkkt walutheri zilitokea vurugu miezi michache iliyopita kanisa lilikuwa linafungwa na mapolisi wanaenda kutuliza ghasia, hali hii ilipelekea mpaka kuwe na kanisa jipya lingine.

- Hakuna shinikizo la kutoa sadaka, naona kuna makanisa yana mpaka vitabu vya madeni ya michango, usipochangia waweza usizikwe na kanisa.

- Mavazi ya kujisitiri kanisani wanajitahidi, nashangaa baadhi ya makanisa mwanamke anaenda na vazi la ajabu ajabu anajitetea kwamba Mungu anaangalia roho.

- wachungaji wao hawavumi kwenye skendo za kuchezea wake za waumini ama kulawiti watoto.

- Kwenye kwaya wanaimba kwa kutulia, nyimbo kama kwetu pazuri na mkono wa bwana hakuna purukushani za kucheza bolingo ama kutetema kama Mayele.

- Wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi.

- Hakuna biashara ya mafuta ya upako wala maji ya baraka,
 
Some time wanajikitaga wakina nani sijui.
 
Pia wasabato wanaimba!

Sauti zinapangiliwa kiasi kwamba hata mimi mpagani najikuta nimekua kama mmoja kati ya Maselafi na Makerubi.

Hawavai ujinga, hawachezi kijinga. Hawa wanaifuata misingi ya imani kwelikweli.

Nawakubali sana Wasabato na waislamu!
 
maelezo ya ziada tafadhali
Mathayo 26:26-28 "Nawalipo kuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega akawapa wanafunzi wake, akasema twaeni mle huu ndio mwili wangu. Akakitwaa kikombe akakishukuru akawapa akisema nyweni nyote katika haki kwa maana hi ndiyo damu yangu ya agano imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi."

Pasaka inatukumbusha kuwa Yesu alikufa kwa dhambi zetu na kwa niaba yetu. Imeandikwa 1Wakorintho 11:26 "Maana kila mwulapo mkate huu na kukinyea kikombe hiki mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo."
 
-Ni nadra sana kusikia kuna vurugu kanisani kwa viongozi wanaong'ang'ania vyeo mpaka kufikia kanisa kugawanyika.

-hakuna shinikizo la kutoa sadaka, naona kuna makanisa yana mpaka vitabu vya madeni ya michango usipochangia waweza usizikwe na kanisa.

-mavazi ya kujisitiri kanisani wanajitahidi, nashangaa baadi ya makani mwanamke anaenda na vazi la ajabu ajabu anajitetea kwamba Mungu anaangalia roho.

- hawavumi kwenye skendo za viongozi wa dini kuchezea wake za waumini ama kulawiti watoto.

- Kwenye kwaya wanaimba kwa kutulia, nyimbo kama kwetu pazuri na mkono wa bwana hakuna purukushani.

- wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi,
Unalinganishaje uzito wa punje ya Mchele na uzito wa gunia la Mchele [emoji23]
 
maelezo ya ziada tafadhali
Inausisha kula mkate ambao unawakilisha mwili wa mwana wa Mungu Yesu na kunywa divai ambayo ni kama damu yake Yesu na katika ili uwa wanashiriki wale waliosafi kwa maana waliotakaswa kwa njia ya ubatizo wa maji pekee kama hujabatizwa huruhusiwi kushiriki.

Ishu ya kutawazana miguu ilifanyika toka enzi za Yesu ivyo inaenziwa(maana yake nimesahau na vifungu vya bible pia nimesahau)..
 
Mathayo 26:26-28 "Nawalipo kuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega akawapa wanafunzi wake, akasema twaeni mle huu ndio mwili wangu. Akakitwaa kikombe akakishukuru akawapa akisema nyweni nyote katika haki kwa maana hi ndiyo damu yangu ya agano imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi."

Pasaka inatukumbusha kuwa Yesu alikufa kwa dhambi zetu na kwa niaba yetu. Imeandikwa 1Wakorintho 11:26 "Maana kila mwulapo mkate huu na kukinyea kikombe hiki mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo."
kumbe huwa ni sherehe yao ya pasaka, mbona inafanyikaga muda tofauti na hii iliyozoeleka ...

hako kautamaduni ka kuoshana migu nimekapenda,
 
-Ni nadra sana kusikia kuna vurugu kanisani kwa viongozi wanaong'ang'ania vyeo mpaka kufikia kanisa kugawanyika.

-hakuna shinikizo la kutoa sadaka, naona kuna makanisa yana mpaka vitabu vya madeni ya michango usipochangia waweza usizikwe na kanisa.

-mavazi ya kujisitiri kanisani wanajitahidi, nashangaa baadi ya makani mwanamke anaenda na vazi la ajabu ajabu anajitetea kwamba Mungu anaangalia roho.

- hawavumi kwenye skendo za viongozi wa dini kuchezea wake za waumini ama kulawiti watoto.

- Kwenye kwaya wanaimba kwa kutulia, nyimbo kama kwetu pazuri na mkono wa bwana hakuna purukushani.

- wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi,
Sabato woyooooooooooooooooo
 
-Ni nadra sana kusikia kuna vurugu kanisani kwa viongozi wanaong'ang'ania vyeo mpaka kufikia kanisa kugawanyika.

-hakuna shinikizo la kutoa sadaka, naona kuna makanisa yana mpaka vitabu vya madeni ya michango usipochangia waweza usizikwe na kanisa.

-mavazi ya kujisitiri kanisani wanajitahidi, nashangaa baadi ya makani mwanamke anaenda na vazi la ajabu ajabu anajitetea kwamba Mungu anaangalia roho.

- hawavumi kwenye skendo za viongozi wa dini kuchezea wake za waumini ama kulawiti watoto.

- Kwenye kwaya wanaimba kwa kutulia, nyimbo kama kwetu pazuri na mkono wa bwana hakuna purukushani.

- wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi,

-hakuna biashara ya mafuta ya upako wala maji ya baraka,
Duh mara hii umeshau Wasabato masalia?
 
kumbe huwa ni sherehe yao ya pasaka, mbona inafanyikaga muda tofauti na hii iliyozoeleka ...

hako kautamaduni ka kuoshana migu nimekapenda,
Hivi kipindi Mussa anamshinikiza Farao awaachie Wana wa Israel ulitambulika kuwa ni mwezi gani?
 
wapakwa mafuta wa mwamposa nao wanakuja soon kupinga
 
Back
Top Bottom