Nawapongeza wasabato kwa kanisa lao kutovuma kwa skendo na drama

Nawapongeza wasabato kwa kanisa lao kutovuma kwa skendo na drama

'
wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi,

-hakuna biashara ya mafuta ya upako wala maji ya baraka'🤔
 
Pia wasabato wanaimba!

Sauti zinapangiliwa kiasi kwamba hata mimi mpagani najikuta nimekua kama mmoja kati ya Maselafi na Makerubi.

Hawavai ujinga, hawachezi kijinga. Hawa wanaifuata misingi ya imani kwelikweli.

Nawakubali sana Wasabato na waislamu!
wanaomba kistarabu bila fujo, hawakemei kwa sauti utadhani Mungu ni kiziwi,

-hakuna biashara ya mafuta ya upako wala maji ya baraka,
 
Unataka nikwambie kanisa gani la kisabato lenye pepo la ngono kwa hapa dar es salam, kuna mzee wa kanisa alikuwa anakula mke wa mwanamkondoo baadae akamtema akachukua mwnamke mwingine wa pale pale kanisani,sasa alichokosea alimpeleka guest ile ile alikuwa anaenda nayo yulee wa mwanzo , wapambe aakaenda kuchoma kwmb yule jaamaa uliekuwa unakuja nae zamani cku hizi anakuja na mwanamke mwingine , yule mama hakujalli kama ana mume na yule mzee wa kanisa pia ni mme wa mtu akaenda kuliamsha huko , kesi ikaenda kumuliwa kanisani ,sasa ktk kile kikao akatokea mjumbe mmoja alisimama upande wa mzee wa kanisa kupinga hoja kwmb huyu mzee hawezi fanya hivyo, mwisho wa cku mzee wa kanisa ikaonekana amepakaziwa,

Yule jamaa alitetea sanaaa akapewa uhasibu ktk shule inayomilikiwa na wasabato, hukoo kigamboni

Njoo nikupeleke hukoo kwenye wasabato ambao jumamosi maduka yao yapo wazi lkn wao wapo kanisani, njoo nikupeleke kwenye wasabato wenye biashara na nikuonyeshe waganga wao ni nani na nani, njoo nikuonyeshe michepuko ya wazee wa kanisa la kisbato,

Unapoambiwa mzee wa kanis fahamu hiki ni cheo tu lkn unaweza kut mzee wa kanisa ana miaka 35 ,

Sasa kuna mzee wa kanisa mmoja yeye yupo dar mkewe na familia wapo moshi, alichofanya alimchukua mfanyakazi wake wa ndani akaja nae dar huku dar hana mke amepanga akamfungia ndani kama wiki akila mzigo, baada ya akamrudisha kwao,
 
Wale waliotaka kwenda ulaya kububiri bila passport wala nauli ni wa wapi wale
 
Back
Top Bottom