Nawauliza wana Simba wenzangu, Mohamed Dewji aliwahi kufanikisha lipi kwenye soka?

Kama nawe huwa unachangia timu hela ya kukuwezesha basi nunua zile hisa 51 % zilizobaki ili usaidiane nae.
Unauliza alishindana na nani wakati pale kwenye mkutano walisema yeye alikua only bidder.
Au hukwenda hata kwenye mkutano?
Swadakta ! Unakijua kisa cha kuwa peke yake ?

Huu ni uzi fukunyuzi usije macho juu .
 
Wewe sio Simba na wala huna mchango wowote kwa Simba kama hujui Dewji kaifanyia nini Simba 2003 na kuendelea.unanonyesha ulivyo mbulula kwenye zabuni unauliza alipata Kura ngapi?zinakutosha kweli
Hii timu ina mashabiki duni sana !
 

1. Simba ya zamani alikuwa mfadhili yaani anafanya fadhila kwa faida ipi? mapenzi kwa timu au hata maslahi binafsi kidogo

2. Logically, kwenda singida united au kuanzisha African Lyon alikuwa anaepuka baadhi ya mambo yaliyomuondoa Simba. Lakini bado faida huko hasa kwa African Lyon hakuipata ajili ya upungufu kwa maana ya Brand. Imebidi aitafute tena Simba kwa ajili ya potential ya biashara ajili ya Brand. Angeweza hata kwenda Yanga kwa maana ya biashara kwa sababu Yanga pia ni Brand kubwa lakini ni rahisi ku deal na Simba kwa ajili ya mrengo wake kimpira.

3. Sasa suala la procurement sielewi unataka kusema nini yaani anaweza kuwa alishindwa ila akapendelewa? Naamini kwenye kukaribisha wazabuni kutakuwa kulikuwa na makabrasha ya zabuni ambako sifa zote zitakuwa ziliwekwa na namna ya kumpata mshindi. Unaweza kutafuta kule. Naamini ingekuwa vigumu kushindwa kwani naamini kulikuwa na kigezo kinachohusisha uelewa na/au uhusiano wa mzambuni na maendeleo ya klabu, shughuli zake, uhusiano wake na mambo ya kulipa kodi, ripoti za ki audit n.k., pato lake: kumbuka huyu amewahi kuwa tajiri na 1
kwa Afrika Mashariki. Sidhani kama kuna mtu angemshinda.

4. Ndiyo maana kulivyotokea uvumi Bakhresa anataka kuomba kununua hisa ilikuwa kasheshe kwa kuwa sifa zake zinalinganishika kidogo

5. Ukishaingia makubaliano ya kimkataba ulio wazi mafanikio yanaweza kupatikana kwani kuna bodi na watendaji wanaowakilisha maendeleo kwenye bodi na ndiyo maana kuna hiyo 50% or 51% ya share kwa maana asiburuzwe na wanachama na yeye asiwaburuze wanachama ndiyo effective checks and balance kwenye governance.

6.Matatizo yataweza kutokea hiyo ni kawaida lakini si sawa na kuwa na timu zina miaka 80, mashabiki sijui milioni ngapi lakini hazina viwanja wala pesa.
 
Mchakato ulipoanza ulikuwa wapi Ndugu yangu!! watu wameishafanya we ndo unaibuka na hoja zako ambazo zinaashiria dalili ya unafiki!!

Watu kwa pamoja wameamua kwamba wanataka mabadiliko sasa wewe kama unaona wamekosea na upingana nao unaweza kuwasilisha malalamiko yako kwenye chombo chenye ili kikutendee Haki wewe binafsi
 
MO.ajawahi kufanya lolote la maana kwa simba zaidi ya hii miaka miwili mitatu kukopesha mishahara na kununua nunua wachezaji lakini kwa kurudishiwa pesa zake .na kingine ni mshangiliaji mzuri achelewi kujichanganya barabarani kushangilia kifua wazi.kumbuka simba ina miaka zaidi ya sabini na aijawahi shuka daraja .ila african lion. Agip manyoni .mto singida na singida utd ziliwahi kushuka daraja na katika hizo timu zilishakua mkoani kwake
 
Yule ni mfanyabiashara, lazima aangalie penye faida. Nendeni naye vizuri mtamuelewa tu mkuu. Mpeni muda itapendeza [emoji3]
 
Namba 4 : Kwanini baada ya Bakhresa kujitokeza ikawa KASHESHE ? sasa kwa taarifa yako bakhresa na wengine waliojitokeza ambao wako 7 walinyimwa kabisa ushirikiano na walihujumiwa kwa maelekezo maalum.
 
Nilikuwa nashangaa pale waliposema kuwa Kuna mkutano wa kumtangaza mshindi wa zabuni.

Yaani utadhani alikuwa akishindanishwa na mwengine, kumbe ulikuwa mkutano wa kumkabidhi timu.
 
Kwani wewe umewahi kufanikiwa lipi?
 
Mjomba wengi wape , mimi ndio nimejitokeza hadharani , lakini wengi wanaugua ndani kwa ndani .
 
Kaziulize nd
 
Kawaulize ndala wenzako pumbav
 
Ha! Ha! Ha!!!
 
Mbona una point dhaifu sana ktk uwekezaji wa mpira kuna kitu kinaitwa fan base( wingi wa mashabiki) kama timu ina mashabiki wengi kila mwekezaji atataman kuwekeza apo kwa akili yako mbagala market na simba ni klabu ipi yenye fan base kubwa?
Kwa hiyo Manchester ilikuwa na fan base kubwa ndio maana yule mwarabu aliamua kuwekeza? Acheni kudanganya watu jamani fan base ni moja ya variables zinazomfanya mwekezaji awekeze kwenye mpira lakini sio determinant ya kila uwekezaji wa mpira. Vipi kuhusu brand name?
 
Nina maana Manchester City
 
Ww unavyoona vitu atakavyofanya mo kwa brand name ya simba vitaenda kununuliwa na mashabiki wa yanga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…