Naweka dau laki 3; Yanga hatoki kwa Al Hilal

YN

WAKITOBOA HAPO NITAAMINI KUWA WAO NI TIMU BORA AFRICA.. HUKO HAKUNA MAMBO YA ILE MICHONGO YA KUGAWA PESA KWA WAAMUZI NA TIMU PINZANI BILA KUSAHAU VUMBA ZA USHIRIKINA KAMA WANAVYOFANYAGA WAKIWA BONGO, NAWAKUMBUSHA WASISAHAU NA ZILE SINDANO WANAZOCHOMAGA WACHEZAJI WANAOWATEGEMEA ILI KUONGEZA NGUVU KIPINDI CHA PILI. TUKUTANE CAF!!
 
Mkuu mbona umefika mbali sana.

Upinzani wa timu usitufanye tukaharibu utu na ustaarabu wetu.

Kama mchizi alikukera ni vyema ungemchana tu..

Tuendelee kudumisha utani pasipo kuvunjiana heshima.

Ni mtazamo tu.
Inashangaza sana,hata sijamkera popote zaidi ya mambo ya mpira.
 
Tutoke kwenye ushabiki wa hivi, Mimi sio shabiki wa Yanga ila natamani kuziona timu zote tatu za Tanzania zikitinga Groups Stage kwa maslahi mapana ya nchi.

Nimeona umoja wa mashabiki wa Al Hilal natamani na huku tuwe wamoja na sio kuombeana njaa
 
Mimi sio mshabiki wa Yanga, lakini napenda kusema ukweli. Yanga ya sasa hivi ni bora kuliko timu yoyote ya Tanzania. Hata Simba kwa sasa hatuna viwango vya ubora wa Yanga. Sababu za msingi ni hizi:

1. Kwa aina ya kocha waliyenaye sasa Yanga, uwezo wake (kumsoma adui ndani ya mechi na kuibadili timu kucheza ndani ya mechi), hicho ndio kiwango cha kucheza mechi za kimataifa.

2. Ubora wa wachezaji kama Fiston Mayele katika kufunga, Aziz Ki katika kugawa mipira na Feitoto katika kusukuma timu kushambulia, Yanga wanaweza kuifunga timu yoyote hapa Afrika. Narudia tena, Yanga ya sasa wanaweza kuifunga timu yoyote hapa Afrika.

Kiwango cha uchezaji wa kiushindani kinachoonyeshwa sasa na Yanga, bila ushabiki ninapenda kusema wazi, ni kiwango tunachokiona kwa timu za hatua ya robo fainali. Sio mtoano wala makundi kunakoweza kumsimamisha Yanga, labda hatua ya robo fainali. Al hilal sio timu tishio kwa Yanga, sijaona kitu kipya au kitu cha ajabu.
 
Uchambuzi makini
 
ahahaha

Naunga mkono hoja
 
Dah kumbe utopolo wanatumia dawa za kuongeza nguvu
 
Tuwekee uthibitishobwa haya madai
 
Unaijua Al hilal kweli kama kibonde vipers alikubamiza 2 Al hilal si atakupiga 3mara 2
 
Hakuna hata mtu mmoja ashawahi leta ushahidi wa haya unayooandika maana kila siku yanaandikwa

Mpira mchezo wa wazi wote tunaona kama ni ubora wa timu unaonekana wazi haina haha ya kutafuta visababu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…