Nawezaje kuacha kazi huku nina mkopo benki?

navache

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
499
Reaction score
368
Heshima zenu wakuu

Nipo Pwani ya kupambana na ninataka kuchoma meli. Lakini tatizo kuna mpinzani mmoja ananivuta shati nyuma. Mpinzani huyo ni mkopo toka benki moja hivi mjini.

Hoja yangu ni hii kwenu wajuzi wa taratibu za utumishi bila kusahau wazoefu wa uhalisia.

Je, nikiacha kazi bila kufuata taratibu watamalizana na mwajiri au watamalizana na mimi?

Uhalisia ukoje?
 
Huwa wanapiga piga simu kukukumbusha uwalipe ila hakuna wakukufuata labda ujipeleke isitoshe mkopo una bima so hiyo ndo hasara inayotakiwa kufidiwa na bima
Okay asante mkuu
 
Hela ya magu hailiwi kaka
Kukopa haruc kulipa matanga

Fanya tu ulipe au utajitafutia matatizo[emoji1321]
 
Nashukuru kwa ushauri wako mkuu. Lakini je nikiwa nje ya system huwa kuna utaratibu wa kulipa? Au ni lazima nibakie kwenye system?

Mkuu hutokopeshwa kama upo nje ya system na huo mkopo ulipo kopea
Usijidanganye ati huwa wanapiga tu simu wala hawakufatilii,
Nakushauri tu ufanye mbinu mbadala ya kulilipa hilo deni
Siku hizi wanaingizwa matatizoni kuanzia mkopaji hadi na familia inawekwa matatizoni
Usijipe kamoyo ati utakacha au kubadili namba za simu
Mkuu dawa ya deni ni kulipa tu popote uendapo ulipe tu
 
Huo ni mkopo wa mtumishi wa serikali sio wa biashara
Dhamana yake ni kazi...na ndio mana akisepa hata wadhamin hawasumbuliwi kabisa ...

Mi nimeshuhudia wengi wengi tu wasepa zao na hakuna shida walopata....
 
Mjanja wewe, Ila wao ni wajanja kuliko wewe. Wakikukosa jina lako linapelekwa creditors Beaural. Huko likipelekwa unaorodheshwa kama bad debtor, mikopo utaisikia tu redioni kama bombadia Morogoro. Labda ukopeshwe Na baba mkwe wako
[emoji15] [emoji15] [emoji15] hapo kwa baba mkwe sasa... Usikute yeye ndiye anakopa kwangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…