Kwa swali lako hili naona bado hujaniwia radhi! Hata hivyo, nimeisha timiza wajibu wangu. Nikirudi mazima sasa kwenye swali lako, ili nikupe majibu sahihi utayoyaelewa utalazimika kwenda kusoma ilani za vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi. Katika usomaji wako angalia ni chama gani kilikuwa na ilani yenye mwelekeo wa Tanzania unayoitaka.
Mkuu, inabidi uende ukazisome kweli, vinginevyo ukirudi hapa tutashindwa kuelewana kile tutakachokuwa tunaulizana.
Suala si ilani bali suala ni utekelezaji wa Ilani. Yapo yaliyokuwamo kwenye ilani iliyopita ya 2015 lakini hayakutekelezwa mpaka sasa!
Aidha, mbali na tatizo la utekelezaji wa ilani ya Chama, pia tatizo lilopo ni huyo mliyempa ridhaa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama. Tangu alipopewa ridhaa 2015-2020 yapo mazuri na mabaya kama binadamu. Lakini mabaya yake yamezidi kipimo na ni mengi na unayafahamu sina haja ya kuyaorodhesha kwa sababu balil insaan alaa nafsihi baswiira! Binadamu anajifahamu hakika nafsini mwake yupoje!
Tukija kwenye uchaguzi wa sasa umechafuka kwa ushahidi wa wazi na hauna kificho!
Binafsi ni mtu wa "ilmul haal" nimechanganya elimu ya kisekyula na elimu ya dini. Nimefundishwa kuishi na watu kwa wema, kuipenda jamii na kuipenda nchi. Nimefundishwa kumuokoa anayedhuluma na anayedhulumiwa!
Siwezi kukitetea chama kwa sababu chama hakitonisaidia chochote mbele ya Mungu! Siwezi kumtetea mtu kwa mapenzi yangu binafsi hata kama anafanya uonevu kwa kuwa ni miongoni mwa watu wangu!
Uchaguzi huu imefanyika dhulma ya wazi na uhujumu kwa kuchaguliwa viongozi ambao hawakuwa mahususi kwa wapiga kura. Pia umejeruhi wengi na kuwaua baadhi ya raia, na sikuona makosa yao isipokuwa walikuwa ni wenye kulinda kile walichokipigia kura na hakikuwa na athari hasi yoyote kiutendaji hata kama walikiuka utaratibu.
Dini yangu inaniambia; ikiwa nitafanya dhulma tu hata kama si kwa vitendo hata iwe kwa kusapoti tu basi nami nimechangia hiyo dhulma! Kama waliyopiga kura 50,000 wakadhulumiwa haki yao nikihusika basi natakiwa niwalipe hao wote haki yao. Sasa nikiangalia majeruhi na waliyouliwa sina mema ya kuwalipa wote! Dhulma kwangu ni dhambi kubwa na kuua unapata laana kwa Mungu.
Licha ya hivyo tunaishi kwenye sayari tofauti na tuna dini tofuati. Kwa hayo kwa roho njema tena kwa moyo mkunjufu nimeazimia kutokuchangamana na wewe kwenye mijadala na kukukoti pia kuanzia sasa na hii ni koti ya mwisho kutoka kwangu kuja kwako rasmi!
Mungu atubariki.