Mitazamo haitokuja badilika maana siku zote lazima kunaye anayemzidi mwenzie, hapo ulipo kuna wanaokuzidi na pia kunao walio nyuma yako. Haitokuja siku sote tuwe sawa hata tukijidanganya kivipi, ila cha msingi ni kila mmoja atie bidii na ashirikiane na wenzake. Kenya na Wakenya leo hii tumewekeza sana kwenye mataifa ya EAC, na pia tumeingiza pua SADC, lakini sasa Afrika inafunguliwa yote, yaani soko la walaji bilioni moja litakua mbele yetu, tushindwe wenyewe tu, ila kwa watu mliolemazwa na mifumo ya kunun'gunika na kununia kila kitu, mtaendelea kuwa watazamaji wa wenzenu wakijaribu na kuthubutu.
Ni kweli sio lazima tufaulu kwa mpigo mmoja, changamoto zitaibuka, lakini cha msingi tunathubutu sio kujifungia ndani kama mazombi na kuteseka kwenye umaskini wa kujitakia wenyewe.