Nchi Wahisani hawatakubali kutoa fedha zao iwapo watabaini wapinzani wa kutumika ndio wataongoza kamati za fedha za Bunge

Nchi Wahisani hawatakubali kutoa fedha zao iwapo watabaini wapinzani wa kutumika ndio wataongoza kamati za fedha za Bunge

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Ni Imani yangu walioweka sharti kamati za Bunge: PAC, POAC na LAAC ziongozwe na Wapinzani, walijua umuhimu huo wakiamini wapinzani wana nafasi nzuri zaidi katika kuibana serikali kwenye suala zima la matumizi ya fedha za Umma na zile zinazotolewa na wahisani.

Kwa sababu hiyo, naamini mpaka sasa wahisani hawa watakuwa wanafuatulia, na hivyo wana taarifa zote za nini kinaendelea hasa kuhusu tuhuma/ madai ya NEC kupeleka majina ya Wabunge wa viti maalum wa CHADEMA huku CHADEMA wakikana majina hayo.

Katika hili sakata, ninachotarajia kukiona ni wafadhili kusita kutoa fedha zao iwapo watajiridhisha juu ya madai hayo na watakuwa tayari tu kutoa hizo fedha pale kamati hizo zitapoongozwa na watu wanaostahili na si vinginevyo.

Kama tungekuwa na Uchaguzi Huru na wa Haki, na CCM wakashinda viti vyote, basi hapo hata wafadhili wengeona umuhimu wa kutazama upya jambo hili au kuangalia kanuni zinasemaje iwapo itatokea wapinzani wanashindwa kihalali katika Uchaguzi, lakini sio kwa Uchaguzi huu na zaidi si kwa hizi tuhuma za kutaka kufoji majina ya Wabunge wa viti maalum kutoka Upinzani ili wakaunde hizo Kamati.

Huu pia, kulingana na mtazamo wangu, unaweza kuwa ni mbinyo wa awali wa kulazimisha tuwe na mifumo huru ya Uchaguzi na hata kukazia madai ya Wapinzani kutaka Uchaguzi urudiwe.

Muda utaongea.
 
Kwa hiyo wahisani wasipotoa pesa tanzania inakufa?

Ni haki yao kutoa pesa au la. Hakuna anayewalazimisha na wao wasitulazimishe tukiamua kufanya tunavyotaka!

Tukinyimwa pesa na wahisani itatusaidia kutafuta njia zingine za kukabiliana na changamoto hiyo.
Sasa kwanini leo hii mnatuhumiwa kufoji majina wakati mna njia mbadala za kupata hizo fedha?!

Mmelikoroga, sasa mlinywe.
 
Tatizo mmekariri upinzani ni chadema pekee. Magu ana nafasi kumi akichukua queen sendiga,mbatia etc kisha jumlisha wa nkasi na wa Cuf upinzani ushakamilika kuongoza hizo kamati mnazolilia.
Wapinzani wa aina hiyo hawawezi kukubalika na kuaminiwa na wahisani.
 
Sasa kwanini mnahangaika kufoji majina wakati mna njia mbadala za kupata hizo fedha?!

Mmelikoroga,sasa mlinywe.
Yaani Rais ambaye kikatiba anaruhusiwa kuteua majina 10 ya watanzania kuwa wabunge halafu wahangaike na wabunge wa viti maalum wa CHADEMA!

Propaganda za majina waanzishe wenyewe halafu majibu ya propaganda mnatoa wenyewe!
 
Tatizo mmekariri upinzani ni chadema pekee. Magu ana nafasi kumi akichukua queen sendiga,mbatia etc kisha jumlisha wa nkasi na wa Cuf upinzani ushakamilika kuongoza hizo kamati mnazolilia.
Wahisani sio wajinga kiasi hicho watoe pesa zao kwa upinzani wa kuokoteleza wanajua kila kitu.
 
Tatizo mmekariri upinzani ni chadema pekee. Magu ana nafasi kumi akichukua queen sendiga,mbatia etc kisha jumlisha wa nkasi na wa Cuf upinzani ushakamilika kuongoza hizo kamati mnazolilia.
Duuu!!!
Umeishia darasa la ngapi? Unajua maana ya wabunge wa kuchaguliwa na kuteuliwa? Kanuni za Bunge zinasema kuhusu wabunge wa kuchaguliwa na wananchi hawa ndiyo wanahitajika
 
Kwa akili yako mkuu wa Nkasi na wa CUF hujawaona hapo kwenye comment uliyoquote?
Duuu!!!
Umeishia darasa la ngapi? Unajua maana ya wabunge wa kuchaguliwa na kuteuliwa? Kanuni za Bunge zinasema nini kuhusu wabunge wa kuchaguliwa na wananchi hawa ndiyo wanahitajika
 
Shetani hakutokea tu kuwa shetani, Bali mawazo yake yalipokuwa yakizidu kuwaza vibaya juu ya mahali pake pa kujitawala, ndivyo wengi wa leo mnavyowaza vibaya juu ya mahali pao pa kujitawala!

Nchi yako wewe mwenyewe, usiku kucha, mchana kutwa kazi yako ni kuitabiria mabaya na kuiwazia mabaya tu!!

Mnatamani mabaya tu yatokee kwenye Nchi mliozaliwa, Nchi ambayo, watoto wako wanaishi, ukoo wako wote mnaishi!!

Mnatamani vita tu vitokee, hapa ndo akili za Mwanadamu zinapochanganyikana na za kishetwani, Wenye vita wanalilia Amani na wenye Amani wanalilia Vita!!

Duniani ni sehemu moja mbaya Sana ya kuishi, hasa shetani anapotaka kujitwalia wengi!!

Neno moja linanipa matumaini ya kuwa, Mwenye Haki mmoja akiwako, huwa sababu ya wengine wengi kupona!

Nakuhakikishia mwandishi kuwa, wahisani wote unaotamani wasiipe misaada Nchi uikaayo mwenyewe, wataipa Kwa kuwa shetani hawezi kushinda.
 
Yaani Rais ambaye kikatiba anaruhusiwa kuteua majina 10 ya watanzania kuwa wabunge halafu wahangaike!

Propaganda za majina waanzishe wenyewe halafu majibu ya propaganda mnatoa wenyewe!
Give me a break rais Magufuli ateue wapinzani 10? halafu waje wapinge maendeleo labda siyo Magufuli ninayemjua.
 
Shetani hakutokea tu kuwa shetani, Bali mawazo yake yalipokuwa yakizidu kuwaza vibaya juu ya mahali pake pa kujitawala, ndivyo wengi wa leo mnavyowaza vibaya juu ya mahali penu!

Nchi yako wewe mwenyewe, usiku kucha, mchana kutwa kazi yenu ni kuitabiria mabaya na kuiwazia mabaya tu!!

Mnatamani mabaya tu yatokee kwenye Nchi mliozaliwa, Nchi ambayo, watoto wako wanaishi, ukoo wako wote mnaishi!!

Mnatamani vita tu vitokee, hapa ndo akili za Mwanadamu zinapochangantikana na za kishetwani, Wenye vita wanalilia Amani na wenye Amani wanalilia Vita!!

Duniani ni sehemu moja mbaya Sana ya kuishi, hasa shetani anapotaka kujitwalia wengi!!

Neno moja linanipa matumaini ya kuwa, Mwenye Haki mmoja akiwako, huwa sababu ya wengine wengi kupona!

Nakuhakikishia mwandishi kuwa, wahisani wote unaotamani wasiipe misaada Nchi uikaayo mwenyewe, wataipa Kwa kuwa shetani hawezi kushinda
Mnafanya mabaya alafu mnataka matokeo mema. Hii ni akili au matoke?

Unaweza kupanda bangi ukavuna maharage?
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Mkuu akili yako ni ndogo sana. Ndio maana watanzania walisusa maandamano yenu.
Kama walisusa, kulikuwa na haja gani ya kukamata viongozi wa upinzani kabla hata ya hayo maandamano na kutisha wanaotaka kuandamana?
 
Back
Top Bottom