Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Hadithi za kwenye kahawa hizi! Trillion 3000? Afrika haiwezi kuwa na hiyo hela!
Watu bilioni 1.5 wanafanyakazi usiku na mchana, kwa miaka zaidi ya 60 ya uhuri, na bado hatuna hata ambulance tu za kueleweka ni shida.., pesa zote zinaenda wapi? Commomwealth sisi mtego wetu upo IMF na World bank.., kataa kukopa pesa uone kitakachokupata,uliza Djibouti walifanywa nini baada ya kugoma kukopa. Yaani. Unakopa Trillion 2 kwenye makaratasi, mkopo wenyewe hauji, ila unatakiwa ulipe Trillion5 na riba, mnamuonea mama wa watu bure kumuuliza pesa alizokopa zimeenda wapi, mnamuonea bure! Hakuna anaependa kufa jamani, huo ushujaa alikuwa nao jiwe tu! Tuombe sana aje mwingine atakaekuwa tayari kufa, kama Burkinafaso walivyompata yuke dogo..
 
Madini ya uranium yanayotoka pale Niger kwenda ufaransa kwa mwaka unajua yanagharimu kiasi gani?. Ukilijua hilo utajua sio lazima utoe hela ili ulipe deni.
Ushawahi kujiuliza kwa nini ufaransa hataki kuyaachia makoloni yake afrika iwe kwa jasho au kwa damu?

Sijui lolote kuhusu huo mkataba ila najua sub sahara Afrika inaongozwa na vilaza na inanyonywa sana
 
Guinea chini ya Sekou Toure mwaka 1958 walikiona cha mtema kuni
 
Tutajie hizo nchi mbili zilizogoma


Haya yote yalifanyika Katika nchi ya Africa na ni siri? (hiyo nchi haijulikani)? Je hayo maji yalitumika na kama yalitumika hali za hao raia vipi si walikufa wote au?

Kwangu hii naona ni ngumu kumesa
Hii kitu ipo,miaka miwili nyuma nilimsikia baruani muhuza kupitia radio U-FM akihojiwa kuhusu haya mapinduzi hasa ya nchi za Afrika Magharibi na alisema wazi kabisa juu ya hiyo fidia inayolipwa kwa mfaransa kila mwaka ndyo chanzo cha hayo mapinduzi
 
Jamaa liongo hili! Sijui kama linakuwa hesabu liliyoiweka hapo kwa hela ya madafu inaitwa quadrillion. Ambazo ni sawa na trillion 1000!
 
Chanzo cha hii habari. Siri imevuja vipi?
 
Tatizo kubwa tulilonalo Waafrika ni Elimu wengi huzani kitu chenye Thaman zaidi ni Pesa tu ndio maana watu wanauliza transaction zinafanyikaje, Viongozi wanaingia Mikataba mpaka ya 6% kwa 94% mnadhani yakua hawana akili kwa kiwango hicho, Mzungu anakwambia alishiliki kugundua mwisho wa siku anachukua 70% anakuachia 30% we unaona ina make sense?
 
Wanatoa wapi hayo mapesa?
1. Benki kuu za nchi hizo zinatakiwa (sio ombi, ni amri) kuweka asilimia 50% ya hazina yake yote katika benki za ufaransa.
Na serikali ya ufaransa ina haki zote za kutumia pesa hizo bila ruhusa kutoka nchi husika.
Pia ndio maana pesa zao (nchi nyingi Afrika magharibi: Senegal, ivory coast, mali, benin, niger, burkina faso etc) zinaitwa CFA Franc.

2. Right of First Refusal.
Ufaransa kama koloni lao la zamani wana haki ya kukataa kwanza kwa uwekezaji wowote ule unatakiwa kufanywa katika nchi hizo.

Mfano;
Benin kagundua kuwa ana madini ya urani(uranium) katika ardhi yake, taarifa inabidi ziwafikie serikali ya ufaransa kwanza, nayo itangazie makampuni ya uchimbaji madini kuhusu hiyo fursa. Kama makampuni na serikali itaona hiyo fursa haina tija kwao, wataikataa, hapo sasa ndio serikali ya Benin inaweza tangaza fursa hiyo kwa nchi wawekezaji wengine ambao si wafaransa.

Kwa ufupi ni kwamba, ufaransa kajibinafsishia hizo nchi milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…