Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Hadithi za kwenye kahawa hizi! Trillion 3000? Afrika haiwezi kuwa na hiyo hela!
Watu bilioni 1.5 wanafanyakazi usiku na mchana, kwa miaka zaidi ya 60 ya uhuri, na bado hatuna hata ambulance tu za kueleweka ni shida.., pesa zote zinaenda wapi? Commomwealth sisi mtego wetu upo IMF na World bank.., kataa kukopa pesa uone kitakachokupata,uliza Djibouti walifanywa nini baada ya kugoma kukopa. Yaani. Unakopa Trillion 2 kwenye makaratasi, mkopo wenyewe hauji, ila unatakiwa ulipe Trillion5 na riba, mnamuonea mama wa watu bure kumuuliza pesa alizokopa zimeenda wapi, mnamuonea bure! Hakuna anaependa kufa jamani, huo ushujaa alikuwa nao jiwe tu! Tuombe sana aje mwingine atakaekuwa tayari kufa, kama Burkinafaso walivyompata yuke dogo..
 
Fake news, hizo nchi kwanza hazina uwezo wa kugenerate hizo dollar billioni 500 kwa mwaka za kulipa kadeni na bado zijiendeshe

Hakuna Siri sa ivi duniani kwenye ulimwengu wa kidijitali, labda uniambie hua wanalipana hizo pesa kwenye magunia, ila kama ni transactions za kibenk ingekua ishajulikana kitambo tu,

Btw, nchi Gani hizo mbili ambapo wafaransa walifanya ivo?
Madini ya uranium yanayotoka pale Niger kwenda ufaransa kwa mwaka unajua yanagharimu kiasi gani?. Ukilijua hilo utajua sio lazima utoe hela ili ulipe deni.
Ushawahi kujiuliza kwa nini ufaransa hataki kuyaachia makoloni yake afrika iwe kwa jasho au kwa damu?

Sijui lolote kuhusu huo mkataba ila najua sub sahara Afrika inaongozwa na vilaza na inanyonywa sana
 
Fake news, hizo nchi kwanza hazina uwezo wa kugenerate hizo dollar billioni 500 kwa mwaka za kulipa kadeni na bado zijiendeshe

Hakuna Siri sa ivi duniani kwenye ulimwengu wa kidijitali, labda uniambie hua wanalipana hizo pesa kwenye magunia, ila kama ni transactions za kibenk ingekua ishajulikana kitambo tu,

Btw, nchi Gani hizo mbili ambapo wafaransa walifanya ivo?
Guinea chini ya Sekou Toure mwaka 1958 walikiona cha mtema kuni
 
Tutajie hizo nchi mbili zilizogoma


Haya yote yalifanyika Katika nchi ya Africa na ni siri? (hiyo nchi haijulikani)? Je hayo maji yalitumika na kama yalitumika hali za hao raia vipi si walikufa wote au?

Kwangu hii naona ni ngumu kumesa
Hii kitu ipo,miaka miwili nyuma nilimsikia baruani muhuza kupitia radio U-FM akihojiwa kuhusu haya mapinduzi hasa ya nchi za Afrika Magharibi na alisema wazi kabisa juu ya hiyo fidia inayolipwa kwa mfaransa kila mwaka ndyo chanzo cha hayo mapinduzi
 
Jamaa liongo hili! Sijui kama linakuwa hesabu liliyoiweka hapo kwa hela ya madafu inaitwa quadrillion. Ambazo ni sawa na trillion 1000!
 
Kwa sasa naandika kwa kifupi sana, ila nitaleta andika kamili kesho au baadae.

Nitaanza na Francophone Africa. mnafahamu kwamba Ufaransa iliwasainisha makoloni yake yote mkataba unaoitwa ‘Agreement for the continuation of colonialism’ kabla hajawapa ‘uhuru feki’?

Msingi wa mkataba huu ni kwamba Ufaransa anadai alipwe kwanza fidia ya maendeleo yote ya kiutawala na miundo mbinu ambayo aliwekeza kwenye nchi hizo ili aweze kuondoka.

Kuna nchi mbili ziligoma kusaini , kilichowakuta kiliwaogopesha makoloni mengime yote na wakasaini. Wale waliogoma, Ufaransa aliondoka , lakini alichukua kila kilicho chake ambacho kinahamishika, vile ambavyo havihamishiki walivichoma moto vyote, waling’oa reli, walichoma moto majengo yote ya kiutawala, walichoma moto maghala yote ya chakula, walitia sumu visima vyote, waliharibu kila kitu! Ndio wakaondoka, kuona dhahama hiyo, wote waliobaki walisaini.

Kupitia mkataba huo wa siri wa kinyonyaji, nchi za Francophone Africa wanalipa Dollar Billioni 500 kila mwaka kwa Ufaransa, na sharti kuu ni iwe siri , wananchi wasiambiwe.

Marais wengi wapya wa nchi hizo kila walipoingia madarakani walikutana na mkataba huu, na hawakuamini walichokiona, na wakagoma kulipa, kila aliyegoma aliuwawa au kupinduliwa. Angalia histora ya Marais wa nchi hizo, utashangaa, wengi sana wameuwawa na kupinduliwa.

Burkinafaso mfano, walishamuuwaga Thomas Sankara, hata huyu Rais wao wa sasa, huu mkataba ulimuumiza sana roho, na akawafukuza wafaransa na kusema wazi kabisa , haogopi kufa, na hata majaribio ya mapinduzi wameshamfanyia majaribio zaidi ya 10, na bado wanaendelea kumuwinda. Ameina bora akatafuta alliance na Urusi, na wameingia military pact ya kumlinda kwa malipo kidogo. Inshort huyu Dogo kawaambia Ufaransa lije jua ije mvua, halipi hiyo pesa!! Na kawatimua nchini kwake!

Huo mkataba nitauleta na nitauchimbua msharti yake yalivyo makali, inaumiza sana. Dollar billion 500 kila mwaka wale mbwa wanavuna, inauma sana!

Chanzo cha hii habari. Siri imevuja vipi?
 
Tatizo kubwa tulilonalo Waafrika ni Elimu wengi huzani kitu chenye Thaman zaidi ni Pesa tu ndio maana watu wanauliza transaction zinafanyikaje, Viongozi wanaingia Mikataba mpaka ya 6% kwa 94% mnadhani yakua hawana akili kwa kiwango hicho, Mzungu anakwambia alishiliki kugundua mwisho wa siku anachukua 70% anakuachia 30% we unaona ina make sense?
 
Wanatoa wapi hayo mapesa?
1. Benki kuu za nchi hizo zinatakiwa (sio ombi, ni amri) kuweka asilimia 50% ya hazina yake yote katika benki za ufaransa.
Na serikali ya ufaransa ina haki zote za kutumia pesa hizo bila ruhusa kutoka nchi husika.
Pia ndio maana pesa zao (nchi nyingi Afrika magharibi: Senegal, ivory coast, mali, benin, niger, burkina faso etc) zinaitwa CFA Franc.

2. Right of First Refusal.
Ufaransa kama koloni lao la zamani wana haki ya kukataa kwanza kwa uwekezaji wowote ule unatakiwa kufanywa katika nchi hizo.

Mfano;
Benin kagundua kuwa ana madini ya urani(uranium) katika ardhi yake, taarifa inabidi ziwafikie serikali ya ufaransa kwanza, nayo itangazie makampuni ya uchimbaji madini kuhusu hiyo fursa. Kama makampuni na serikali itaona hiyo fursa haina tija kwao, wataikataa, hapo sasa ndio serikali ya Benin inaweza tangaza fursa hiyo kwa nchi wawekezaji wengine ambao si wafaransa.

Kwa ufupi ni kwamba, ufaransa kajibinafsishia hizo nchi milele.
 
Back
Top Bottom