Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Nchi za Afrika za Francophonie na Common wealth zinalipa Trillion 3000 kila mwaka kwa Ufaransa na Uingereza kama fidia ya faida za ukoloni

Kwa sasa naandika kwa kifupi sana, ila nitaleta andika kamili kesho au baadae.

Nitaanza na Francophone Africa. mnafahamu kwamba Ufaransa iliwasainisha makoloni yake yote mkataba unaoitwa ‘Agreement for the continuation of colonialism’ kabla hajawapa ‘uhuru feki’?

Msingi wa mkataba huu ni kwamba Ufaransa anadai alipwe kwanza fidia ya maendeleo yote ya kiutawala na miundo mbinu ambayo aliwekeza kwenye nchi hizo ili aweze kuondoka.

Kuna nchi mbili ziligoma kusaini , kilichowakuta kiliwaogopesha makoloni mengime yote na wakasaini. Wale waliogoma, Ufaransa aliondoka , lakini alichukua kila kilicho chake ambacho kinahamishika, vile ambavyo havihamishiki walivichoma moto vyote, waling’oa reli, walichoma moto majengo yote ya kiutawala, walichoma moto maghala yote ya chakula, walitia sumu visima vyote, waliharibu kila kitu! Ndio wakaondoka, kuona dhahama hiyo, wote waliobaki walisaini.

Kupitia mkataba huo wa siri wa kinyonyaji, nchi za Francophone Africa wanalipa Dollar Billioni 500 kila mwaka kwa Ufaransa, na sharti kuu ni iwe siri , wananchi wasiambiwe.

Marais wengi wapya wa nchi hizo kila walipoingia madarakani walikutana na mkataba huu, na hawakuamini walichokiona, na wakagoma kulipa, kila aliyegoma aliuwawa au kupinduliwa. Angalia histora ya Marais wa nchi hizo, utashangaa, wengi sana wameuwawa na kupinduliwa.

Burkinafaso mfano, walishamuuwaga Thomas Sankara, hata huyu Rais wao wa sasa, huu mkataba ulimuumiza sana roho, na akawafukuza wafaransa na kusema wazi kabisa , haogopi kufa, na hata majaribio ya mapinduzi wameshamfanyia majaribio zaidi ya 10, na bado wanaendelea kumuwinda. Ameina bora akatafuta alliance na Urusi, na wameingia military pact ya kumlinda kwa malipo kidogo. Inshort huyu Dogo kawaambia Ufaransa lije jua ije mvua, halipi hiyo pesa!! Na kawatimua nchini kwake!

Huo mkataba nitauleta na nitauchimbua msharti yake yalivyo makali, inaumiza sana. Dollar billion 500 kila mwaka wale mbwa wanavuna, inauma sana!
===========================


View: https://www.instagram.com/reel/DDCUYpYRcBx/?igsh=cmg0MjFpZTBxY2Zu


=========================
Update: 31/01/2025
Thambo mbeki aeleza kushtushwa baada ya kuiona mikataba hii


View: https://www.youtube.com/live/KMldcBNRJOs?si=yEBxFL6TMyZoEf1d

Haya Mambo richa ya kuwa mzungu ni katili,ukikataa asikulambe, anakutwanga, lakini lazima kuna wenyeji wanatumika kufanikisha hili,
 
Back
Top Bottom