Nchi za Afrika zimehimizwa kujifunza toka kwa China ili ziweze kupata maendeleo ya kasi

Nchi za Afrika zimehimizwa kujifunza toka kwa China ili ziweze kupata maendeleo ya kasi

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
57a8e229d19a72edff166e78df3c4c5.jpg

Nchi za Afrika zimetajwa kuwa zinaweza kujifunza kutoka kwenye mtindo wa maendeleo wa China kama zikitaka kupata maendeleo ya kasi.

Akiongea kwenye mahojiano maalum na Shirika Kuu la Utangazaji la China CMG, Profesa Waithaka Niraki wa Chuo Kikuu Cha Nairobi amesema, mbali na kujifunza kutoka kwenye mtindo wa maendeleo wa China, nchi za Afrika pia zinaweza kunufaika na teknolojia na hata kuweza kujiamini, huku akiwa na matumaini kuwa China inaweza kuwa tayari kuzisaidia nchi za Afrika kwa teknolojia na hata kuzipa moyo wa kujiamini kujiletea maendeleo.

Akizungumzia ripoti ya mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Kikomunisti cha China, Profesa Waithaka amesema ripori hiyo imejikita kwenye uongozi wa jumla, unaongalia nyanja zote za maisha, na sio tu pesa na utajiri.

Amepongeza njia ya kujiendeleza ya China na kuitaja kuwa ni njia muhimu inayotoa mafunzo ya kuleta masikilizano kwenye jamii, kushirikiana na mataifa mengine ya kuzipa uwezo nchi za Afrika.
 
Kwani Africa tumekosa nini hasa kinacho kwamisha maendeleo kama sio uongozi bora?
 
Toa elimu ya mzungu leta elimu ya wachina ,Toa na ujinga wa demokrasi pia .Hapo maendeleo ni lazima ila hii ya mzungu watu wanajifunza lugha na kukariri vifungu vya sheria hamna cha maana.
 
Toa elimu ya mzungu leta elimu ya wachina ,Toa na ujinga wa demokrasi pia .Hapo maendeleo ni lazima ila hii ya mzungu watu wanajifunza lugha na kukariri vifungu vya sheria hamna cha maana.
Tanzania hakuna demokrasia na ni chama kimoja ndicho kinacho tawala miaka nenda rudi na maendeleo hakuna sasa bado unataka kusingizia nini na huku bara la Afrika ndilo linaloongoza kwa utawala wa kiimla na ndio inavuta mkia kwa maendeleo sasa bado unataka kusingizia kitu gani. Bure kabisa.
 
Market Socialism ndio iliyoifanya China iwe Head Above Shoulders kwa wengine...., Kuhusu uchapaji kazi na Innovation from ancient times China have always been ahead even before the West....
 
Toa elimu ya mzungu leta elimu ya wachina ,Toa na ujinga wa demokrasi pia .Hapo maendeleo ni lazima ila hii ya mzungu watu wanajifunza lugha na kukariri vifungu vya sheria hamna cha maana.
Mchina mwenyewe anatumia elimu ya mzungu na nyingine anaiba kabisa. Demokrasia ni mfumo bora kabisa wa uongozi. Muda wa kuongozwa na wafalme kama viongozi proper ulishaisha siku nyingi.
 
Mchina mwenyewe anatumia elimu ya mzungu na nyingine anaiba kabisa. Demokrasia ni mfumo bora kabisa wa uongozi. Muda wa kuongozwa na wafalme kama viongozi proper ulishaisha siku nyingi.
Kasome mfumo wao wa elimu kwanza ndio utaelewa , tunayosoma sisi imeletwa na mzungu ila hao wazungu wenyewe pia hawaisomi ndio maana kuna international schools.
 
Kasome mfumo wao wa elimu kwanza ndio utaelewa , tunayosoma sisi imeletwa na mzungu ila hao wazungu wenyewe pia hawaisomi ndio maana kuna international schools.
Kuna mambo ya kipekee karibia kwa mfumo wa elimu wa kila nchi. Hata hivyo, kanuni nyingi za elimu, hasa sayansi zinafanana.
 
Back
Top Bottom