Nchi za mabeberu wana Ramani zinazoonyesha maliasili ilipo Tanzania na nchi nyingine mbili. Wao wanaamini walitukabidhi tuwatunzie lakini si zetu

Nchi za mabeberu wana Ramani zinazoonyesha maliasili ilipo Tanzania na nchi nyingine mbili. Wao wanaamini walitukabidhi tuwatunzie lakini si zetu

Afu ww umezidi matusi sana hapa jamvini, alafu hunaga mambo ya maana ni upumbavu tu na kulobulobu kwenye hoja
Hapana.

Inawezekana pia na wewe huwa unamsoma ukiwa umekwishaweka akili hasi kwa michango yake.

Hebu kwa mfano, katika hayo aliyoandika hapo, ni matusi gani aliyoandika hadi ikabidi umjibu hivyo?

Hebu msome tena vizuri bila hasira naye, utaona kwamba kuna maana sana katika hayo aliyoandika, na wala hakuna "upumbavu tu na kulobulobu..."
 
We jamaa muongo sana eti wanakuanzia mbali sana huko mbali sana ni wapi huko. Nchi inongozwa na wahuni na majizi na mikataba yote wanayoingia ya rasilimali za nchi ni kuwaneemesha wao. Kumbuka mabilioni ya Uswiss na mikataba mingine yote IPTL, Richmond, Dowans, Escrows etc ilijaa wizi na ufisadi wa kutisha na nchi imeporwa trillions kwa sababu ya majizi wanaojifanya Viongozi na kuwa na Bunge DHAIFU.
Hizi nchi hazikupigi wala kukutisha ila hukuanzia mbali sana.
 
Mistari hii mitatu inaeleweka sana, na ina maana haswa.

Andiko, kama kweli ni lako, hukulitendea haki mkuu.

Umelivurugavuruga sana na mambo mengi yasiyoendana, tena kwa sehemu tofauti tofauti katika andiko lenyewe.

Hii mistari yako mitatu hapa..., ngoja nikuongezee ushahidi wa unayoyasema:

Maongezi ya hivi karibuni, kati ya Biden na BoJo kwenye simu, huku Biden akimhimiza BoJo na wao waanzishe kitu kama kile alichokifanya Jinping, the "Belt and Road". $650 Billion ikiwa kianzio cha juhudi hizo za kumpiku Jinping.

Na pia usisahau juhudi za yule Magufuli wa U'beparin' (Trump); hata yeye alikuwa kwenye mbio hizo hizo, ndio maana akina Uhuru Kenyatta wakaitwa White House, na akina Betchell wakitaka kujiingiza na barabara ya Nai-Momba, ili kupunguza nguvu za SGR ya mchina.

Haya mambo yapo sana, lakini tunatakiwa tuwe na ufahamu nayo vizuri, tusiwe watu wa kupiga tu kelele za "Mabeberu..., mabeberu", huku hata kuelza watu waelewe inatuwia vigumu.

Maana hasa ya kutumia neno hilo mara kwa mara kunaondoa uzito wake. Inabaki kama njia ya kuwatishia watu tu... wakimbie; hata bila ya kueleza sababu za ubeberu wenyewe tunaouona ukipangwa.

Sasa sijui kama utanielewa hapa, lakini nimejaribu kujieleza kadri niwezavyo. Nitajaribu njia nyingine kama bado sieleweki.

Ndio, mambo haya yapo
Naamini mada yangu imeeleweka kwa alietaka kuelewa.

Wewe kama yakuchanyanga ipotezee.
 
We jamaa muongo sana eti wanakuanzia mbali sana huko mbali sana ni wapi huko. Nchi inongozwa na wahuni na majizi na mikataba yote wanayoingia ya rasilimali za nchi ni kuwaneemesha wao. Kumbuka mabilioni ya Uswiss na mikataba mingine yote IPTL, Richmond, Dowans, Escrows etc ilijaa wizi na ufisadi wa kutisha na nchi imeporwa trillions kwa sababu ya majizi wanaojifanya Viongozi na kuwa na Bunge DHAIFU.
Lakini si kulikuwa na safari nyingi za nje kutafuta wawekezaji?

Au ushasahau?

Na hili la Bunge kuuona mkataba nitajie nchi gani yafanya hivyo kujadili mikataba kama ya kuuziana silaha wapi Wabunge wanapewa wasome?

Maana hata madili kama ya Uingereza au Mmarekani kumuuzia silaha Saudi Arabia au Israel haijawahi kusomwa na Wabunge na ikawa scrutinised.
 
Nimesomaaa,ila nilipofika kwenye hii sentensi "uranium ambavyo ni malighafi muhimu kwa utengenezaji wa betri za magari, simu za mkononi" hapo nikashtuka!nadhani panahitaji tupate ripoti ya CAG!
 
Mkuu! Sisi hatuna uwezo wa kushindana na hao unaowaita mabeberu wakidhamiria kufanya yao! Hatuwezi kuwazuia! Ila tunaweza kukaa nao meza moja tukaweka mambo sawa..
Hakuna Cha mabeberu Wala nini ila ishu ya mabeberu inaletwa na viongozi wetu. Hawataki weka Sera ambazo mwananchi wa kawaida anaweza faidika nazo hawachez na fursa. Tuchukulie kwa upandé wa viwanda tuchukulie utengenezaji wa magari hasa mabasi, Sera zetu mbovu zimeua viwanda vyote vya kuchonga mabasi tumebaki ni wagaizaji lakin ukiwasikiliza viongozi wetu always ni mabeberu.
Tuje kwenye upandé wa kilimo, nchi zote zinazotuzunguka zinauhaba mkubwa wa chakula hasa mchele ila kwa sabab ya Sera mbovu mchele unaozea mashamban hivyo kuwafanya makulima waendelea kuwa maskini.
Africa nzima hakuna nchi inayojitosheleza kwa kilimo Cha ngano na nahitaji ni makubwa Sana lakin Sera zetu mbovu hakuna uzalishaji wq ngano kabisa. Ngano mpaka mwez Jana China inauzwa usd 310 kwa tonne jumla, lakin hakuna mzalishaji kutoka Africa.
Kodi na tozo zetu bado ni chini lakin bado zinaweza tulipa kuliko wenzetu.
Ni Africa tu mkulima anaweza akauza Mahindi kg 350 na ikamlipa tofaut na wenzetu. Ila Sera zetu mbovu Sana .
Wakati wenzetu kupanda eka moja ya mahindi atatumia usd 100 pamoja na mbegu, Africa inaweza fika karibia Mara mbili ya hapo na bado ikalipa. Wakati kuvuna Mahindi kwetu itahitajika tsh40000 ya kuvuna na 40000 kupukuchua Mahind kwa eka wenzetu watahitaji Lita 90 za mafuta kuvuna eka 20 za Mahindi yaliyopukuchuliwa wastani wa 9000 kwa eka lakin bado hawawez uza Bei tunazouza.
Kwa mifano hiyo sisi tuna nafasi nzuri ya kuendelea kuliko hao mnaowaita mabeberu.
Mabeberu ni viongozi wetu wazungu wanalihitaji soko letu
 
Sasa kwani ukienda nje kusaini mikataba inahusiana vipi na kusaini mikataba ya kifisadi? Acha kubadili subject na kutaka kuingiza mambo ya Marekani kuhusu mikataba ya rasilimali za Watanzania.
Lakini si kulikuwa na safari nyingi za nje kutafuta wawekezaji?

Au ushasahau?

Na hili la Bunge kuuona mkataba nitajie nchi gani yafanya hivyo kujadili mikataba kama ya kuuziana silaha wapi Wabunge wanapewa wasome?

Maana hata madili kama ya Uingereza au Mmarekani kumuuzia silaha Saudi Arabia au Israel haijawahi kusomwa na Wabunge na ikawa scrutinised.
 
Afu ww umezidi matusi sana hapa jamvini, alafu hunaga mambo ya maana ni upumbavu tu na kulobulobu kwenye hoja

Yaani ww utukanwe na nani, utukanwe ili ujipatie umaarufu? Hapa unapewa ukweli unaokuumiza. Hizi Id za 2020 zilikuja rasmi kulinda siasa Chafu,na kuendekeza propaganda mfu za awamu ya majizi ya Kura, kuelekea uchaguzi mkuu. Na mimi Id hizi za wanafiki nimezipa vitasa vikali, hivyo sishangai huu mrejesho.
 
Kwa bahati mbaya sana sisi watanzania tumejikita kwenye kuangalia maisha ya leo tu, tunatumbua kila kitu kifisadi, anayejaribu kuangalia ya kesho pia anageuzwa adui ,

Itatuchukua muda sana kuja kushtukia mambo kama haya na hata tukifanya hivyo itakua tayari tumechelewa.

Inasikitisha sana lakini ndivyo tulivyo.
 
Lakini si kulikuwa na safari nyingi za nje kutafuta wawekezaji?

Au ushasahau?

Na hili la Bunge kuuona mkataba nitajie nchi gani yafanya hivyo kujadili mikataba kama ya kuuziana silaha wapi Wabunge wanapewa wasome?

Maana hata madili kama ya Uingereza au Mmarekani kumuuzia silaha Saudi Arabia au Israel haijawahi kusomwa na Wabunge na ikawa scrutinised.
Kuna kamati za Bunge zinazofanya kazi kama hizo katika nchi nyingi, hasa hizo kubwa kubwa.

Haiwezi ikawa kazi ya waziri pekee, au hata siri ya Rais pekeyake.
 
Umeandika upumbavu mwanzo mwisho.

Hapana mkuu BAK.

Tusiende huko.

Pamoja na ugumu wa mada yake, lakini nadhani haistahiri maneno mazito kama hayo.

Amekwishajieleza kivingine, tena kwa kifupi zaidi, na nadhani anaeleweka.

Tafsiri ya makala aliyoifanya imeongeza ugumu wa makala yenyewe.
 
Nchi za Tanzania, Angola na Congo DRC ni nchi muhimu katika mstakabali mapinduzi ya viwanda barani Ulaya na Marekani.

Mwaka 2020 Uingereza walitangaza kuachana na magari yatumiayo mafuta ya diseli na petroli kufikia mwaka 2030 na wameazimia kuanza kutengeneza magari zaidi yatumiayo betri.

Hata hivyo tayari magari yatumiayo betri tayari yanatengenezwa katika nchi mbalimbali barani Ulaya.

Nchi za kibeberu au maadui wa maendeleo hawawezi kuiruhusu Tanzania iendelee kwa kuwa na viwanda vyake .

Pia Tanzania ina malighafi zote kutengeneza hata seti za televisheni, vioo vya madirisha na balbu.

Kuna mambo matatu makuu ambayo sisi binadamu twapaswa kufahamu.

Mambo hayo ni technical know what, technical know how and technical know why.

Darasani mwalimu hutufundisha kuhusu somo la jiografia, kisha kuingia ndani kufanya tathmini kutumia kifaa maalum cha Compass kwa kutumia ramani na hiyo ni technical how.

Pale uanzapo kujiuliza hii Compas imetengezwa vipi ndipo unapoingia kwenye technical know why.

Mabeberu wanakuambia kuwa Afrika kuna dhahabu tatu ambazo ni Tanzania, Angola na Congo DRC.

Mabeberu wanaendelea kuziangalia nchi tatu ambazo nchi za Tanzania, Angola na Congo DRC ambazo wana malengo ya muda mrefu hadi miaka 50.

Katika nchi hizo ni Tanzania ambayo wao mabeberu wana uwezo wa kuingia na kujichotea maliasili watakavyo.

Kutokea bandari ya Lobito iliopo Benguela kupitia Lusaka, Lubumbashi ni ukanda maalum ulojaa madini, mafuta na madini ya uranium ambavyo ni malighafi muhimu kwa utengenezaji wa betri za magari, simu za mkononi na mabomu ya nyuklia na mitambo yake.

Lango kuu la kuingia kwenda huko ndani au (interior) na kutokea ni Bagamoyo na ni njia rahisi kuliko kuzunguka Cape Town.

Ila mabeberu hao wakadai kuwa watakuja kwa mazungumzo na ikiwa mazungumzo yatashindikana basi watatumia mbinu zozote kuhakikisha wanafanikiwa azma yao.

Wazungu hao wanasema kuwa Tanzania ni nchi ya kuingia na kutokea Afrika kupitia Bagamoyo. Pia wanasema kuwa asilimia 60 ya biashara ya meli kuanzia mwaka 2050 itakuwa ndani ya bahari ya Hindi na hiyo ndio itakuwa Ocean of the future.

Hivyo, meli yaweza kutoka bandari ya Lobito kupitia Dar-es-Salaam hadi mfereji wa Suez bila shida na kwa uharaka zaidi.

Na hivyo ndivyo mfalme Leopold wa pili wa Belgium alivyokubaliana na wakoloni wa kijerumani kujenga reli ya kati ambayo ingesafirisha bidhaa zote za malighafi kutoka katikati ya Tanzania na Afrika kuelekea bahari ya Hindi.

Mfalme huyo alikuwa akivuna zao la mpira na kulisafirisha kwenda Ulaya kutengeneza bidhaa mbalimbali kama matairi ya magari, baiskeli na zingine yaani alikuwa "supplier" mkubwa.

Moja ya viwanda vikubwa ambavyo mfalme huyo alikuwa akiviuzia malighafi ya mpira ni kiwanda kinachotengeneza bidhaa za Dunlop.

Waafrika wengi sana raia wa Congo walikufa wakivuna zao hilo na wengine kukatwa mikono kwa kushindwa kufanya hivyo.

Bahari ya Hindi ni bahari ilojaaliwa kila aina ya maliasili kuanzia mafuta, gesi asilia na uranium. Leo hii twashuhudia jinsi magaidi wa kupandikizwa nchini Msumbiji wakitumika kama kivuli cha wizi wa maliasili hizi zinazoibwa usiku na mchana.

Mwandishi Robert Kaplan katika kitabu chake cha Monsoon - "The India Ocean and Future of American Power" anaitaja bahari ya Hindi kama New Great Game kama ndo njia ya China ikitumia meli zake kubwa za mafuta kusaka maliasili hiyo ndani ya bahari ya Hindi.

Lakini safari hii upo uwezekano mkubwa wa vita ndani ya bahari hiyo baina ya nch iza kibeberu yaani Marekani na China.

Kaplan anaelezea muungano wa nchi za Marekani, China na India katika bahari ya Hindi katika kufanya biashara, kuzuia vitendo vya utekaji meli yaani Piracy, kulinda njia za usafiri wa meli na kuitikia wito wa majanga ndani ya bahari hiyo.

Bila shaka kelele za ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni moja ya vielelezo vya mpango wa nchi za kibeberu.

Mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ulofumuliwa na hayati John Magufuli haukuwa mkataba uloweka maslahi ya taifa mbele na ulikuwa ni wa miaka 99.

Mkataba huo pia haukuwa unaruhusu maendelezo yoyote ya bandari zingine kama bandari ya Dar-es-Salaaam, Tanga, Zanzibar.

Hiyo ni kwasababu Bagamoyo ndo lango kuu la kuingiza na kutoa rasilimali zote zinatoka ndani ya Tanzania na maliasili zingine zinazotoka ndani ya Congo DRC na Angola.

Kwa vile nchi za kibeberu tayari wana ramani ya Afrika na sehemu zilipo maliasili basi Tanzania pamoja na Angola na Congo DRC na wanafahamu kuwa sasa hivi ujazo wa Uranium na madini mengine umefikia kiwango cha juu kiasi cha kuweza kuvunwa, basi sisi hatuna ujanja.

Tanzania tunapaswa kueleza wazi msimamo wetu na pia kueleza ni nini tunataka kwani mali tunayo.

Tanzania haina budi kulinda ukanda wa bahari ya Hindi hadi Msumbiji kuhakikisha usalama wake hauingiliwi kirahisi. Serikali pia inawajibika kueleza msimamo wake kuhusiana na mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.

Lakini si kuanza kuzunguka mbali na kuanza mijadala ya kupoteza muda huku tayari wenzetu wachache wamekaa tayari na mabeberu na wamepanga nini kinachofuata.

La sivyo tunakubali kuwa sie ni waangalizi tu wa rasilimali tulozikalia na tupo tayari kuzigawa bure au kwa ujira kiduchu.
Beberu asipo yahitaji hayo madini wewe mtu mweusi mwenzangu unaweza kuyafanyia nini?
 
Ndiyo. Hiyo ni tafsiri toka mahali fulani.

Lakini tafsiri yenyewe siyo ya kiustadi hata kidogo.
Mkuu, moja ya masomo niliyopiga kisawasawa ni history.

Kwa kuwa history is about past, present and future basi huwa najikumbusha ingawa si eneo langu ambalo ndio nina utaalam nilio nao.

Hii mada yangu sijaitafsiri kokote ni mtizamo wangu binafsi baada ya kuyaona na kuyasikiliza yanayoendelea chini kwetu, barani Afrika na mtazamo wa nchi ziloendelea juu ya Tanzania.

Pia ni tafakuri yangu juu ya kinachoendelea kule Msumbiji na hatima ya sisi waafrika.

Ningeitafsiri ningeweka chanzo ila nimetumia kitabu kimoja tu.
 
Umeandika upumbavu mwanzo mwisho.

Mkuu, punguza jazba, mwisho wa siku huu mjadala utaisha.

I respect Mr Assad ambae mara mojamoja huwa namsikiliza pale kijiwe cha Mnazimmoja akimwaga madini.

He has had a very distinguished career and he is well respected.

Lakini Prof Assad alisahau kwamba hii ni Tanzania ya CCM na ina namna yake ya kuendesha nchi.

Natarajia Freeman Mbowe kesho atatoa mwelekeo wa siasa za upinzani maana mfumo bado upo pale pale regardless nani ni raisi.
 
Back
Top Bottom