Nchi zenye Amani zaidi Africa

Nchi zenye Amani zaidi Africa

Wametumia kigezo gani kuiweka nchi kama Senegal, Liberia, Tunisia, Sierra Leone na kuiacha nchi iliyobarikiwa Amani kutokana na subira na uvumilivu wa watu wake Tanzania?

Nimeishi kwa karibia mwaka mzima Liberia na Senegal. Na mara kadhaa nimetembelea Ghana. Nchi kama Liberia, licha ya kumbukumbu mbaya ya vita vya huko nyuma, kwa sasa katika suala la utawala bora, wapo mbali sana kulinganisha na Tanzania. Kule kukiwa na tatizo dogo tu, hata lililomgusa mtu mmoja tu, na hasa kama tatizo lenyewe Serikali imehusika au kutajwa kuhusika, viongozi, hasa mawaziri watahangaika mpaka wamfikie huyo mtu ili wajue tatizo ni nini, na taarifa itatolewa kwa umma bila ya kuchakachuliwa. Hapa akina Makonda, licha cha kutajwa mara nyingi na watu wengi juu ya kuhusika kwake na utekaji, utesaji na uuaji wa watu wanaowakosoa watawala, lakini hawajawahi kuhojiwa hata siku moja!!

Nakumbuka kuna mkasa mmoja mdogo uliomhusisha mfanyakazi wetu, raia wa Madagaska, kuwa alisumbuliwa na maofisa wa polisi barabarani, habari ikatoka kwenye blog, siku 2 baadaye, mawaziri wawili wa wizara husika wakiambatana na maogisa wao wa chini wanne, walifika kambini kwetu usiku, tulikaa nao kwa masaa 6. Jamaa aliombwa msamaha, na polisi waliotajwa, wakati hayo yanaendelea walikuwa tayari wamesimamishwa kazi kwa uchunguzi. Na taarifa ya tukio lile ilitolewa kwa umma kama ilivyokuwa.

Tena Liberia au Ghana, ukifanya kosa hata la barabarani, omba tu msamaha, usithubutu kutoa chochote kumpa askari, ukitoa tu rushwa, hakika utaenda jela. Ukitoa rushwa, polisi anaona umempa nafasi ya kuthibitisha uaminifu wake. Utakamatwa hapo hapo. Kosa la mwanzo litasahaulika, la kutaka kuhonga polisi ndiyo litakuwa kubwa.
 
Hamia DRC mashariki ili ujue vizuri nini maana ya amani.

Polisi kwa kukosa uelewa wa vitu vidogo. Huelewi maana ya amani, utulivu, vurugu, vita, janga, etc. Kama umri unaruhusu, nenda ukasome upanue uelewa wako.

Kwa uelewa wako mdogo, popote pasipo na physical fighting basi pana amani!!
 
mbon
Kwa mujibu wa Africa fact zone hii hapa ndio Orodha ya nchi zenye Amani ya moyo
Africa's Most Peaceful Countries
1. Mauritius
2. Botswana
3. Sierra Leone
4. Ghana
5. Senegal
6. Madagascar
7. Namibia
8. The Gambia
9. Zambia
10. Liberia
11. Malawi
12. Tunisia
13. Equatorial Guinea
14. Angola
15. Morocco

Source: 2023 Global Peace Index.
sisi wazee wa kisiwa cha amani mbon hatujioni hapo!!!
 
Basi hamia Botswana

Wanaotakiwa kuihama nchi hii ni wale wanaoifanya nchi isiwe na maendeleo wala amani. Hao hawastahili kuwepo nchini kwa sababu kiuhalisia hao ni maadui wa Taifa. Wanaouza rasilimali za nchi kama njugu, hao hawastahili kuendelea kuishi nchini.
 
Wanaotakiwa kuihama nchi hii ni wale wanaoifanya nchi isiwe na maendeleo wala amani. Hao hawastahili kuwepo nchini kwa sababu kiuhalisia hao ni maadui wa Taifa. Wanaouza rasilimali za nchi kama njugu, hao hawastahili kuendelea kuishi nchini.
Bado hamjasema
 
Back
Top Bottom