Ndani ya mwaka mmoja Rais Samia ailetea Tanzania zaidi ya trillion 43

Ndani ya mwaka mmoja Rais Samia ailetea Tanzania zaidi ya trillion 43

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
unnamed.jpg

"Ndani ya mwaka mmoja ailetea Tanzania zaidi ya trillion 43"

Ikiwa ni mwaka mmoja na miezi kadhaa tangu Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kushika atamu, kumekuwepo na mijadara inayozungumzia juu ya mwenendo wa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kusafiri ng'ambo tofauti za nje ya nchi ikilinganishwa na ziara afanyazo ndani ya nchi ikiwa ni tofauti na mtangulizi wake hayati Magufuli. Mijadara mingi sana imekuwa ikiendeshwa katika mitaa na mitandao ya kijamii kuhusu safari hizi afanyazo Mhe Rais.

4 July 2022 akiwa katika utiaji saini wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) Katika hotuba yake alisema kuwa;
"Wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, Rais anasafiri tu hakai. Badala ya kutembelea mikoa anatembelea tu nje, lakini matokeo yake ndiyo haya. Nikienda mkoani tunajenga siasa ya ndani, hakuna maendeleo. Nikienda nje nakwenda kutafuta fedha kwa ajili ya maendeleo"-Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.

Ukweli ni kwamba usio lijua ni sawa na usiku wa giza, wengi wao wamekuwa wakikosoa ziara hizo pasipo kujua ni matunda gani kama taifa tunafaidika kutokana na ziara hizo, pengine ni kutokuwa na ufatiliaji wa kutosha au lah!

Sasa nikujuze ni hii ambayo itakushangaza sana, unajua ziara hizo afanyazo Mhe raisi zimeitengezea nchi ya Tanzania zaidi ya trillioni 40? Haya yamesemwa na Katibu Mkuu Uwekezaji

" Katika kipindi cha mwaka mmoja na miezi kadhaa ya awamu ya sita, Economic Diplomacy imeweza kuingiza katika mfumo wetu wa uchumi dola bilioni 19, hizo huwezi kuzipata popote katika mfumo mwingine'- Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Prof. Godius Kahyarara.

Ikiwa ni Uwekezaji wa ndani dola bilioni 9 ambazo ni sawa na trillioni 20, pamoja na mauzo ya nje ni dola bilioni 10 ambazo ni sawa na trillioni 23.

Hayo ndiyo matunda ya ziara afanyazo Mhe Rais Samia Suluhu Hassan!
 
Ikumbukwe kuwa hii yote ni Mikopo tutakayoilipa sisi na vitukuu vyetu!
 
Kama kazi ya raisi ni kukopa tu..hiyo kazi ni rahisi sana.

Anakopa zinapigwa....hakuna hatua yoyote, unaambiwa urudishe😅

Ila Hangaya ni muhimu akajua
'Kukopa harusi ila kulipa matanga'
 
Hangaya hajui kusimamia matumizi ya serikali!
Hayo majumba yanayojengwa hapo Dodoma na watumishi wa serikalini yanatokana na mishahara yao?
Samia amka nchi inaangamia; unawaumiza wananchi wa chini kwa kushabikia wafanyabiashara wapandishe bei ya bidhaa huku ukiwatwisha tozo wananchi hao hao!!
Uko upande wa wananchi au wafanyabiashara?
Magufuli alikuwa upande wa wananchi ndio maana wanamkbuka.
 
Hizo T 43 ameziokota, amepewa au amekopa?, maendeleo yaliyoletwa na na hizo fedha yako wapi?
 

"Ndani ya mwaka mmoja ailetea Tanzania zaidi ya trillion 43"

Ikiwa ni mwaka mmoja na miezi kadhaa tangu Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kushika atamu, kumekuwepo na mijadara inayozungumzia juu ya mwenendo wa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kusafiri ng'ambo tofauti za nje ya nchi ikilinganishwa na ziara afanyazo ndani ya nchi ikiwa ni tofauti na mtangulizi wake hayati Magufuli. Mijadara mingi sana imekuwa ikiendeshwa katika mitaa na mitandao ya kijamii kuhusu safari hizi afanyazo Mhe Rais.

4 July 2022 akiwa katika utiaji saini wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) Katika hotuba yake alisema kuwa;
"Wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, Rais anasafiri tu hakai. Badala ya kutembelea mikoa anatembelea tu nje, lakini matokeo yake ndiyo haya. Nikienda mkoani tunajenga siasa ya ndani, hakuna maendeleo. Nikienda nje nakwenda kutafuta fedha kwa ajili ya maendeleo"-Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.

Ukweli ni kwamba usio lijua ni sawa na usiku wa giza, wengi wao wamekuwa wakikosoa ziara hizo pasipo kujua ni matunda gani kama taifa tunafaidika kutokana na ziara hizo, pengine ni kutokuwa na ufatiliaji wa kutosha au lah!

Sasa nikujuze ni hii ambayo itakushangaza sana, unajua ziara hizo afanyazo Mhe raisi zimeitengezea nchi ya Tanzania zaidi ya trillioni 40? Haya yamesemwa na Katibu Mkuu Uwekezaji

" Katika kipindi cha mwaka mmoja na miezi kadhaa ya awamu ya sita, Economic Diplomacy imeweza kuingiza katika mfumo wetu wa uchumi dola bilioni 19, hizo huwezi kuzipata popote katika mfumo mwingine'- Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara. Prof. Godius Kahyarara.

Ikiwa ni Uwekezaji wa ndani dola bilioni 9 ambazo ni sawa na trillioni 20, pamoja na mauzo ya nje ni dola bilioni 10 ambazo ni sawa na trillioni 23.

Hayo ndiyo matunda ya ziara afanyazo Mhe Rais Samia Suluhu Hassan!
Watakuita chawa mkuu, siku hizi hoja zikiwaumiza wanakimbilia kutukana watu kwa kuwabatiza majina ya chawa.
 
Hangaya hajui kusimamia matumizi ya serikali!
Hayo majumba yanayojengwa hapo Dodoma na watumishi wa serikalini yanatokana na mishahara yao?
Samia amka nchi inaangamia; unawaumiza wananchi wa chini kwa kushabikia wafanyabiashara wapandishe bei ya bidhaa huku ukiwatwisha tozo wananchi hao hao!!
Uko upande wa wananchi au wafanyabiashara?
Magufuli alikuwa upande wa wananchi ndio maana wanamkbuka.
Hakuna njia rahisi ya kuleta maendeleo, vyovyote atakavyofanya lazima kuna upande utalalamika. Afanye anavyoona yeye inafaa nchi kuendeshwa.
 
Back
Top Bottom