Ndege vita za China na Urusi zatinga eneo la karibu na pwani ya Alaska (Marekani) kufanya doria

Ndege vita za China na Urusi zatinga eneo la karibu na pwani ya Alaska (Marekani) kufanya doria

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Jumatano ya 24th July 2024, ndege vita 4 zinazojulikana kama nuclear bombers za China na Russia ziliingia kufanya "strategic patrol" au "doria ya kimkakati" eneo la Alaska Air Defense Identification Zone (AADIZ) katika bahari ya Bering karibu na pwani ya Alaska Marekani.

Ndege 2 za China ziitwazo Xian H-6 strategic bombers na nyingine 2 za Russia TU-95MS strategic missile carriers zilionekana pwani ya Alaska. China na Russia wanasema walikuwa wanafanya 8th joint aerial strategic patrol.

20240725_182225.jpg
China-Russia 8th joint aerial strategic patrol nuclear bombers

Russia imekuwa ikifanya patrol katika eneo la bahari ya Bering, lakini safari hii kwa mara ya kwanza ilishirikiana na China kufanya doria (patrol) katika eneo hilo la Arctic.

Kitengo cha ushirikiano wa Marekani na Canada katika ulinzi wa anga US-Canadian North American Aerospace Defense Command (NORAD) kilituma ndege zao ili kuzizuia. Hata hivyo NORAD inasema ndege hizo hazikuwa tishio kwa usalama zilikuwa eneo la anga la kimataifa.

Beijing imesema doria hiyo haina uhusiano wowote na hali ya sasa ya kimataifa na kikanda (Geopolitical)

Kremlin imesema ushirikiano wa China na Russia katika eneo la Arctic ni wa amani na utulivu.

Ikumbukwe mapema mwezi huu China na Russia walifanya 4th joint naval patrol eneo la kaskazini na mashariki mwa Bahari ya Pacific. Maeneo ya karibu na washirika wa Marekani ambao ni mataifa ya Japan, South Korea na visiwa vya Philippines.

20240725_182553.jpg
China-Russia 4th joint naval patrol

China na Russia zimeendeleza uhusiano wa karibu tangu Moscow ilipowekewa vikwazo na nchi za Magharibi kufuatia uvamizi wake nchini Ukraine mnamo Februari 2022. Ushirikiano wa kina kati ya mataifa hayo mawili unatazamwa kwa wasiwasi na Marekani na nchi za Ulaya.

Nchi za NATO zilitoa tamko la pamoja mwishoni mwa mkutano wa hivi majuzi uliofanyika huko Washington na kuishutumu China kuwa "mwezeshaji madhubuti" (decisive enabler) wa vita vya Russia nchini Ukraine na kuitaka ikomeshe kuiunga mkono Russia kwa vifaa vya kutengeneza silaha na kisiasa.

20240711_111251.png
Tamko la NATO la kuishutumu China kwa kuisadia Russia katika vita vya Ukraine

Katika ripoti kuhusu usalama wa Arctic iliyochapishwa Jumatatu, Wizara ya Ulinzi ya Marekani ilionyesha wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa ushirikiano wa nchi hizo mbili, na kutabiri kuwa ushirikiano wao wa kijeshi utaendelea kuongezeka.
"Kitendo hiki cha China na Russia ni cha kichokozi, uchochezi ambao haujawahi kufanywa na wapinzani wetu."
Lisa Murkowski (Senator wa Alaska)

Marekani ni kwenda naye kibabe tu kama China na Russia wanavyofanya. Mbona Marekani hufanya joint drills na patrol akishirikiana na washirika wake katika eneo la Bahari ya Kusini na ya Mashariki ya China, kwani kuna ubaya China na Russia wakienda eneo la karibu na Marekani kufanya patrol?
 
Marekani ana washirika Kila Kona ya Dunia lkn haishi kulalamika.
Ana washirika ulaya,Afrika,uarabuni,mashabiki ya mbali na kwingineko.
Cha ajabu hataki kabisa Urusi awe na washirika.
Kuna watu wanasema ana bajeti kubwa kabisa ya ulinzi,Sasa kilio hicho ni Cha Nini?
Ndugu zangu hapa Kuna la kujifunza.
Ukiona hivyo ujue Marekani anaujua udhaifu wake.
 
Defence Budget ya USA 800 billion usd. Russia + China hata 300 billion hawafiki Budget yao.
Bajeti kubwa imeshindwa kuisaidia Marekani kuwashinda Watalaban ambao hawana jeshi la anga,jeshi la majini wala jeshi la maana la nchi kavu.

Bajeti kubwa ya Marekani ilishindwa kuwashinda wavietnam,
Bajeti kubwa ilishindwa kumtoa madarakani Bashir Al Assad wa Syria.
Bajeti kubwa ya Marekani pamoja na bajeti za washirika wake wa NATO kwa kushirikiana na Ukraine wameshindwa kuishinda Urusi, pamoja na kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo hakuna nchi duniania imewahi kuwekewa.
 
Sasa siwatasababisha Marekani mavi yanagonge kyupi
 

Attachments

  • IMG_20240725_144402.jpg
    IMG_20240725_144402.jpg
    38.3 KB · Views: 9
Marekani ana washirika Kila Kona ya Dunia lkn haishi kulalamika.
Ana washirika ulaya,Afrika,uarabuni,mashabiki ya mbali na kwingineko.
Cha ajabu hataki kabisa Urusi awe na washirika.
Kuna watu wanasema ana bajeti kubwa kabisa ya ulinzi,Sasa kilio hicho ni Cha Nini?
Ndugu zangu hapa Kuna la kujifunza.
Ukiona hivyo ujue Marekani anaujua udhaifu wake.
Marekani miaka hii bila kufanya kolabo na NATO, U.S vassal states na nchi nyingine washirika ni wa kawaida sana
 
Bajeti kubwa imeshindwa kuisaidia Marekani kuwashinda Watalaban ambao hawana jeshi la anga,jeshi la majini wala jeshi la maana la nchi kavu.

Bajeti kubwa ya Marekani ilishindwa kuwashinda wavietnam,
Bajeti kubwa ilishindwa kumtoa madarakani Bashir Al Assad wa Syria.
Bajeti kubwa ya Marekani pamoja na bajeti za washirika wake wa NATO kwa kushirikiana na Ukraine wameshindwa kuishinda Urusi, pamoja na kuiwekea vikwazo Urusi ambavyo hakuna nchi duniania imewahi kuwekewa.
Umesema vyema
 
Ajaribu kuigusa China au Russia kivita aone, mbona anaongelea mbali na kukimbilia vikwazo fake vya kiuchumi

China and Russia in America’s own backyard
mkuu ebu fikiria kama Finland ingefanya hayo karibu na Russia, Busara ni kitu kikubwa sana kwa binadamu.
 
Back
Top Bottom