Ndege ya Kwanza kutengenezwa Tanzania yazinduliwa

Ndege ya Kwanza kutengenezwa Tanzania yazinduliwa

Hizo ndege zenu mtaua watu
Ccm haijali kabisa haina tofauti na shetani
 
NDEGE YA KWANZA KUUNGANISHWA TANZANIA

1697326850600.jpg

Tanzania imeanza safari ya kuzindua ndege yake ya kwanza kabisa kutengenezwa nyumbani.
Kampuni ya "Airplanes Africa Limited" inazindua ndege ya kwanza kabisa Tanzania kuunganishwa nchini katika maenesho ya TIMEXPO 2023.

Ndege aina ya Skyleader600 imeundwa kwa ajili ya safari za kibiashara na uwezo wa kumudu gharama ya chini ya uendeshaji.

Poa kampuni ya AAL inapanga kupanua Skyleader500 kwaajili ya matumizi ya kilimo.

Kampuni hiyo iliyo Morogoro, ilionesha ndege ya kwanza kabisa kuunganishwa nchini Tanzania siku ya Jumatano. Tamasha la Skyleader 600’s lilifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee katika Maonesho ya Kimataifa ya Wazalishaji Tanzania (TIMEXPO), yaliyofanyika katika jiji kuu la Dar es Salaam.
Ndege hiyo imeundwa kupakia watu wawili akiwemo rubani.

David Grolic, mkurugenzi wa AAL alifichua kuwa shirika lake liliamua kuchukua fursa ya mazingira mazuri ya biashara ya Tanzania, na nia ya kutumia teknolojia mpya, kwa kuanzisha kuunganisha ndege nchini.

Chanzo: Business Insider
 
NDEGE YA KWANZA KUUNGANISHWA TANZANIA

View attachment 2782387
Tanzania imeanza safari ya kuzindua ndege yake ya kwanza kabisa kutengenezwa nyumbani.
Kampuni ya "Airplanes Africa Limited" inazindua ndege ya kwanza kabisa Tanzania kuunganishwa nchini katika maenesho ya TIMEXPO 2023.

Ndege aina ya Skyleader600 imeundwa kwa ajili ya safari za kibiashara na uwezo wa kumudu gharama ya chini ya uendeshaji.

Poa kampuni ya AAL inapanga kupanua Skyleader500 kwaajili ya matumizi ya kilimo.

Kampuni hiyo iliyo Morogoro, ilionesha ndege ya kwanza kabisa kuunganishwa nchini Tanzania siku ya Jumatano. Tamasha la Skyleader 600’s lilifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee katika Maonesho ya Kimataifa ya Wazalishaji Tanzania (TIMEXPO), yaliyofanyika katika jiji kuu la Dar es Salaam.
Ndege hiyo imeundwa kupakia watu wawili akiwemo rubani.

David Grolic, mkurugenzi wa AAL alifichua kuwa shirika lake liliamua kuchukua fursa ya mazingira mazuri ya biashara ya Tanzania, na nia ya kutumia teknolojia mpya, kwa kuanzisha kuunganisha ndege nchini.

Chanzo:
Hiyo si ndege bali kidege. Ulaya na Marekani vinatengenzwa uani kwa mtu
 
Ccm acheni elimu na technologia vijitegemee. Ok hao ni maorofessa pamoja na wanafunzi wao wameunda kitu kama hicho,pongezi kwao sio kwa serikali ya samia ambayo imeshindwa hata kizuia mgao wa umeme.
Ni nchi za wajinga tu zinazoweza kuoanisha siasa na elimu.
 
Siku elimu itakapotenganishwa na siasa.....tutaweza kutengeneza hata uji wa supu kwa kutumia kokoto.
 
Mimi nashauri kwa nature ya nchi yetu tungejikita zaidi kwenye sayansi ya kupunguza changamoto kwenye kilimo na ufugaji. Tungebuni ka app cha kusaka masoko mazuri ya bidhaa za kilimo na ufugaji ili kuwafurusha madalali wanao wanyonya na kuwadidimiza wakulima na marumbesa yao.

Kwa nature ya nchi yetu tungewekeza huko naamini tatizo la ajira lingepungua sana na tungetengeneza mamilionea wengi. Huku kwengeni hatutoweza kucompete na makapuni makubwa badala yake tunaweza jikuta tunaingia hasara tu. Simaanishi kwamba haiwezekani ila kwa sasa bado sana.
 
Back
Top Bottom