Ni kweli watanunua Mexico, Uganda, Zambia na Mozambique.Hivi kweli hanuna hata ufa mmoja tunaoeeza kuwafinya ili tuheshimiane,hawa jamaa wanatudharau sana, na Magu aliposema suala la chakula kwenda kwao kipindi kile, waziri wao wa kilimo na chakula alisema wakenya watanunua chakula toka mataifa mengine,sio lazima wanunue Tanzania. Wajinga sana.
China ndiko maambukizi yameanza....na imeruhusiwaAma kwa hakika mambo si shwari. Naona ndege za Tanzania nazo zimeanza kupata hitilafu kama ile ya Kenya
---
Akizungumza jijini Nairobi wakati akitoa taarifa kuhusu mwendendo wa maambukizi ya janga la Covid-19 nchini Kenya, Waziri wa Usafirishaji James Macharia amesema kuwa anga la Kenya halitafunguliwa kwa kila mtu. Orodha ikionesha wazi Tanzania ikiwa si mmoja wa nchi inayokaribishwa kwenye anga ya Kenya.
Macharia amesema ni raia wa nchi 11 pekee wa kigeni ndio watakaoruhusiwa kutua Kenya katika viwanja vyake vinne vya kimataifa vilivyopo Nairobi, Mombasa, Eldoret na Kisumu.
Nchi zilizoruhusiwa ni China, Korea Kusini, Japan, Canada, Zimbabwe, Ethiopia, Switzerland, Uganda, Rwanda, Namibia na Morocco.
Waziri huyo amesema nchi hizo zimedhibiti janga la Covid- 19 kwa kiasi cha kuridhidha.
Amesema nchi hizo zimepunguza maambukizi ya ugonjwa huo na raia wake wamekuwa wakipata dalili za kawaida za ugonjwa wa mfumo wa upumuaji.
''Tutaendelea kuboresha orodha yetu kwa kutegemea na hali ilivyo na mazingira. Hii ni orodha yetu kwa leo tutaipitia tena kesho na siku zinazokuja.''
''Abiria wote watakaowasili kwa ndege za kimataifa wakiwa na hati zinazoonesha kuwa hawana dalili za Covid-19 na wale waliopima saa 96 kabla ya safari hawatakaa karantini,'' alisema.
Mara tu orodha ilipotolewa, Wakenya kwa haraka waligundua kuwa Tanzania haimo.
Siku ya Jumatatu tarehe 27 mwezi Julai, Rais Uhuru Kenyatta alitoa kauli ambayo haikuilenga Tanzania moja kwa moja kuwa Kenya haifichi idadi ya watu wenye maambukizi ya Covid-19.
''Sisi tuko wazi na tunajua fika kuwa ugonjwa huu upo tofauti na majirani zetu ambao wanauficha ukweli huu,'' alisema Rais Kenyatta.
Chanzo: BBC
Ata ukiwepo hatuna kipimo na mtu akifa kwa huo ugonjwa atuwezi kuwataja kua amekufa kwa Covid-19Kamanda Twambie huo ugonjwa Tanzania uko wapi? Hahahahahhaha au kuna ndugu yako anaumwa?
KQ wametangaza kuanza safari za nje, na moja ya nchi wanakokwenda ni Tanzania, yaani Kilimanjaro, Dar, Zanzibar; pamoja na kwamba Waziri Macharia hakuihusisha Tanzania katika nchi zinazoruhusiwa.Partiner airlines zinakuja hapa! KQ na hizo wanagawiana wasafiri! Ikija BA, kwanini asiwakaie tiketi?
Msemakweli ni Mpenzi wa Mungu.mkuu samahani hii mambo ya kusema kenya ndugu zetu inanikera kweli, hawa ni jirani tu ambao wanaweza kuwa adui zetu vilevile kama ambavyo imewahi kutokea kwa uganda.
Hebu tueleze kidogo kwa nini corona inawachakaza wao lakini sisi imepoa!Ndiyo maana sijaona faida ya EAC.wivu was kike utawaua hawa.ngoja corona iwachakaze
For sure ,kahlenberg knew it .A vulture is a patient bird
Eti ndugu zenu! Damn, you are DISGUSTING!Sisi hatuna tatizo kenya ni ndugu zetu wana hasira zikitulia watatambua ukweli na hatuna mpango wa kuwazuia!
Good. Hii ndio safi Kabisa.Ilikua ni suala la mda tuView attachment 1523054
Nasikia tumeishajibu. Kuanzia kesho, Ndege kutoka Kenya marufuku kukanyaga KIA, JNIA wala Zanzibar. Na kama tumewajibu kweli namna hii akili zitawakaa wakenya. Hata hivyo, sifurahii mgogoro na nchi jirani, lakini jirani kama hajielewi hakuna namna ni kumsurubu tu kwa namna tunayoweza.Kwahiyo wao ndio wanakaribishwa? Ni kujisahau tu na mambo ya wanasiasa. We either fall apart or grow together. Ngoja tuone nani atakayepoteza
Correct.......James Hadley Chase novelA vulture is a patient bird
Jamaa ana vitabu vizuri sana japo ni vya zamaniCorrect.......James Hadley Chase novel