Habari wadau.
Ndoa changa za Kikristo ambazo mume na mke wanaanza kuishi mbalimbali baada tu ya kufunga ndoa zinashika kasi sana kwa kisingizio cha kazi ama ajira.
Ndoa inafungwa ila mume na mke hawaishi pamoja toka mwanzoni mwa ndoa.
Kuna ndoa ina miaka mitano ila mume na mke hawajawai ishi pamoja zaidi ya 1 month
Yaani katika hiyo miaka mitano ya ndoa mke na mume hawana bond yoyote.
Mke hajui hata mume anapenda kuvaa shati gani sababu hajawai ishi nae muda mrefu. Mume pia hajui pia hata mke anapenda kupika nini ama kuvaa nguo gani ama kusuka msuko gani maana hawajawai ishi pamoja.
Ndoa hewa mnazionaje?