Ndoa ilimpa kilema cha maisha binti

Ndoa ilimpa kilema cha maisha binti

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
25,258
Reaction score
48,589
Sehemu 1

Naitwa Mamujee, ni mzaliwa wa Musoma. Sijabahatika kusoma sana, niliishia kidato cha pili sababu ya kukosa mtu wa kunisomesha pindi tu nilipofiwa na baba yangu. Mama yangu alifariki kitambo sana tangu nilipokuwa darasa la nne. Baba yangu alipofariki tu, mimi nikachukuliwa na shangazi yangu anayeishi Dar es Salaam, huku kaka yangu akipelekwa kwa shangazi yangu mwingine anayeishi Arusha. Tumezaliwa wawili tu, mimi na kaka yangu.

Nilipofika Dar kwa shangazi, nilipokelewa vizuri. Shangazi yangu alikuwa mwalimu wa shule ya msingi. Pale nyumbani tuliishi na mjomba pamoja na watoto wa shangazi watatu. Kiufupi, pale nilikuwa kama house girl, kazi zote za nyumbani zilikuwa zangu. Watoto wa shangazi walilelewa kama mayai, hawawezi kufanya kazi yoyote. Tuliishi vizuri na shangazi huku nikiendelea kuwa mfanyakazi pale nyumbani, lakini sikujali kwa sababu nilijua mimi ni yatima sina pa kwenda, hivyo nikavumilia.

Ilikuwa imepita kama mwaka tangu nije Dar, nikawa mwenyeji na nikazoea jiji vizuri japo sikuwa mtu wa kujichanganya sana. Siku moja niliamka nyumbani na kuanza kufanya usafi kama kawaida. Shangazi na wanae walikuwa wametoka. Nilikuwa bize sana na kazi zangu, sikujua kama mjomba yupo ndani. Nilipomaliza kazi, nikaingia bafuni kuoga ili nijiandae niende Solomon.

Niliporudi chumbani kwetu nikivaa, ghafla mlango ulisukumwa kwa nguvu. Mjomba akaingia chumbani na kunikamata kwa nguvu huku akinifunika mdomo. Mjomba alinibaka! Nililia sana. Sikuwahi kukutana na mwanaume tangu nimezaliwa, na mjomba ndiye alikuwa wa kwanza. Niliumia sana. Baada ya tukio hilo, mjomba alinitishia kuwa nisithubutu kumwambia mtu yeyote, la sivyo angeniua.

Nililala chumbani nikiwa na maumivu makali hadi shangazi aliporudi. Alinikuta nikiwa chumbani bila hata kupika chakula. Akaniuliza, "Mamujee, mbona hujapika chochote na umelala? Kulikoni?" Nikamjibu nalia, "Naumwa." Akaniambia niende nikanunue dawa. Niliposimama kuchukua hela kwa shangazi ili nikanunue dawa, nilitembea kwa shida huku nachechemea. Shangazi aliponiona nashindwa kutembea vizuri, akaanza kuwa na wasiwasi.

Akaniuliza, "Umefanya nini huko chini hadi unashindwa kutembea?" Alinipiga sana akinituhumu kuwa nimeanza umalaya, akidai nimtajie mwanaume aliyenifanya hivyo. Niliomba msamaha huku nikilia na kumwambia mimi si malaya, lakini hakunielewa kabisa. Kipigo kilipozidi, niliamua kumwambia shangazi ukweli kuwa mjomba ndiye aliyenibaka.

Badala ya kunielewa, shangazi aliniita muongo na kusema namsingizia mumewe. Alidai mimi ni malaya tangu utoto na nimerithi umalaya wa mama yangu. Hakutaka kunielewa wala hakutaka kumsubiri mjomba ili amuulize. Aliniambia nitoke nyumbani kwake mara moja. Aliingia chumbani, akabeba begi langu na kuniita nje. Akaniambia niondoke na kunipa shilingi elfu 60 ili nitumie kama nauli ya kunifikisha Musoma.
 
Mjeeeeeee,

Sehemu 2

Shangazi kanifukuza bila hata kuniulumia, hakujali kuwa nimebakwa na mumewe. Nilitoka pale huku nachechemea, sijasikia pakwenda, giza lilikuwa limeingia, nikatoka hadi stendi ya basi. Tulikuwa tunaishi Bunju, nikapanda gari hadi Ubungo ili nilale stendi asubuhi nipande gari za kwetu. Nilifika Ubungo vizuri huku nalia, nikiwa natembea kuelekea geti la kuingilia nikamsukuma mama mmoja, nilikuwa sijamuona, nilimsukuma kwa bahati mbaya. Yule mama alinirudishia alinisukuma kwa nguvu hadi nikadondoka chini. Nikamwambia, "Mama, mbona umenisukuma kiasi hiki?" Akaniambia tena, "Ukome unavyotembea, uwe unaangalia mbele, sio macho chini kama mwizi." Nikajiinua ili niondoke zangu. Wakati nanyanyuka, nilipoteza hela niliyopewa na shangazi kama nauli ya kwetu. Sikujua kama sina hela. Nilianza kupekua kila sehemu, lakini wapi. Nikaanza kulia pale tena kwa nguvu. Watu waliniuliza, "Nalia nini?" Niliwabia, "Nimepoteza nauli," ila hakuna aliyenijali.

Nilitoka pale stendi hadi maeneo yale. Niliondoka nikaanza kutafuta hela, lakini wapi. Nikatoka nikaanza kutembea, hata sijui naenda wapi. Nilifika mahali nikakaa chini huku nalia. Hapo sijakula chochote tangu asubuhi. Nikatamani nimpigie shangazi wa Arusha, lakini sikuwa na namba zao. Nilikaa pale hadi usiku mwingi ukaanza kuingia. Niliogopa nikasema hapa nitabakwa tena. Mamujee mm alipita dada mmoja amevaa vizuri tu. Nikamfata nikamsalimia vizuri, nikaanza kumuomba msaada. Nikamfata, "Naomba unisaidie japo pa kulala tu kwa siku hiyo." Yule dada aliniangalia juu mpaka chini, akaniambia, "Nitafute mtu mwingine, mimi sina msaada."

Yule dada alivyokuwa anatoa akaja kaka akaniuliza, "Binti vp? Mbona unaangaika usiku wote huu?" Nikamwambia, "Sina pa kwenda, nimetoka mkoani, nimekuja kufanya kazi za ndani. Sasa mtu niliyeambiwa atakuja kunipokea simuoni." Ilibidi nidanganye, kwani aliniangalia vizuri. Akaniambia, "Twende, nikakutafutie pa kulala, kesho nimtafute bosi wangu." Nikamfuata yule kaka, tulipanda basi hadi kwake. Tumefika kwake vizuri tukaingia ndani, alikuwa kapanga chumba na sebule. Akaniambia, "Nenda kaoge, mimi naenda kukutafutia chakula." Akanionyesha choo kilipo, nikavua nguo nikaenda kuoga. Nikavaa nguo zangu vizuri huku nina wasiwasi, sijui hatima yangu.

Kaka akarudi akabeba chips mbili na soda. Akanipa nikala, na yeye akaenda kuoga. Akaniuliza jina langu, nikamwambia naitwa Mamujee. Basi akaniambia, "Sasa ingia chumbani ulale." Niliogopa, nikasema hapana, nitalala hapa panatosha. Akaniambia, "Jee, noo, ingia chumbani ulale na mimi, nitalala hapa sebuleni." Nikanyanyuka japo kwa uoga, nikaingia chumbani. Wakati nashusha neti nilale, kaka akagonga mlango. Nikainuka kufungua huku natetemeka, akaniomba achukue shuka. Alivyotoka, nikafunga mlango kwa ndani, nikalala.

Asubuhi palivyokucha, nikaamka zangu. Nikatoka sebuleni, ila sikumkuta kaka. Nikaanza kufanya usafi ndani, kuanzia chumbani hadi sebule. Nikapanga kila kitu vizuri, nikaoga, nikachukua begi langu, nikakaa kwenye sofa nimsubiri kaka aje nimuage niondoke zangu. Kaka alikuja akaniita, "Jee vp, umeamka salama?" Nikajibu, "Ndiyo, shikamoo kaka." Aliitika vizuri, alibeba soda mbili na chapati. Akaniambia, "Jee, njoo tunywe chai." Mimi ni msera sina hata jiko. Tunaanza kula huku ananiuliza maswali, "Kwetu ni Musoma, sehemu gani?" Nikawa namjibu, "Vp kuhusu wazazi wako?" Nikamwambia, "Mimi ni yatima."

Kaka aliumia sana akaniambia, "Jee, kaa hapa na mimi, nitakutafutia nauli urudi nyumbani. Maana hata ukirudi pale Ubungo, nina uhakika uwezi kumpata huyo bosi wako. Zaidi tu utafanyiwa vitu vibaya, maana hii Dar es Salaam sio kabisa." Aliniuliza, "Nauli ya kwenu sh ngapi?" Nikamwambia. Akasema, "Nisubiri apate mshahara." Tulikaa pale huku tukiangalia TV. Ilikuwa sio siku ya kazi, kaka hakwenda kazini. Mchana ilipofika alitoka, alivyorudi, akarudi akabeba jiko la gesi, sefuria tatu na hotpot mbili, ila havikuwa vipya. Akaniambia, "Amechukua kwa rafiki yake, tutumie kwa muda hadi nikiondoka, hatamrudishia maana sio vizuri kula mgahawani." Nikainuka, nikaviosha vizuri. Akanielekeza magenge, akanipa hela, nikaenda kununua vitu vya kupika.

Nilinunua vitu vyangu nikarudi, nikaanza kupika. Nakumbuka nilipika pilau, nikaweka kwa hotpot ili tule hadi usiku. Kaka alifurahi akaniambia, "Jee, kumbe unajua kupika vizuri?" Basi, siku ikaisha. Kesho yake kaka alikuwa anaenda kazini, akamwita mpangaji mwenziwe, ni mdada. Akamwambia, "Huyu ni ndugu yangu anaitwa Mamujee, naomba ushinde nae vizuri." Kaka akaondoka zake, nikabaki na huyo jirani. Ilivyofika jioni, nikaanza kupika chakula ili kaka akija tule.
 
Una uandishi mbaya sana hauweki alama zozote,hauna aya(paragraphs), yaani unaandika haraka haraka hata sentence zako zimechomelewa sijui una shida gani aisee.
 
3

Bc nikaandaa zangu chakula ili Kaka akija tule, Kaka akarudi ila hakuwa na raha kabisa, akaniambia Jee hii Dunia ni ya ajabu sana, cjui watu wapoje? Wanapenda kuwaza Negative kwa kila jambo? Nikamuuliza kivip Kaka? Akaniambia watu wamempigia cm mpenzi wake kuwa yeye amereta mwanamke ndani na kesho anakuja kujua mbivu na mbichi,, akaniambia nisijali ataniombea kwa yule jirani ili nilale nae,, bc nikawa mpole nikakosa cha kusema, asbh Kaka aliongea na yule jirani akakubali mm kukaa kwake,, bc kama kawaida nikafanya usafi ndani nikatoa begi langu kupeleka kwa jirani ili akija mwenyewe asinikute mule, bc tulikaa na yule Dada jirani huku tukipiga story mbali mbali, mara yule mpenzi wa Kaka akaja alikuwa na funguo zake akaingia hadi ndani, mie nilikuwa kimya na yule Dada jirani aliniambia nisiende kule maana yule Dada anajisikia sana asije akanionyesha ovyo,, Kaka akarudi akaja huku kwa jirani akanipa hela ya kula yeye akaenda ndani kwake,, nilikaa pale kwa jirani wa Kaka hadi wiki iliisha sikuingia ndani kwa Kaka ila Kaka alikuwa ananipa hela ya matumizi kama kawaida,, nakumbuka siku moja Kaka arirudi kazini akaja huku kwa jirani, akaniuliza Jee unapajua Kariakoo?? Nikamwambia hapana maana niliona kama mtego ananipa,, akanipa hela elfu 50 akaniambia nenda ununue vitu vyako muhimu kesho kutwa nakuletea ticket ya kwenda nyumbani,, bc yule Dada jirani akaniambia kunisindikiza kkoo,, bc nirifurahi sana kwa wema wa Kaka ila nilipata mawazo sana kuwa narudi Musoma naenda kukaa kwa nani? Nikasema bc kama shangazi yangu wa damu kanifukuza bc acha nirudi nyumbani
Asbh tulijiandaa na Dada jirani kwenda kkoo, tulifika vzr nikanunua chupi na sidiria na losheni tu nikabakisha hela kidogo ili nikifika Musoma niuze hata maandazi, bc tukawa tunarudi njiani tukielekea stendi gafra Dada jirani akapigiwa cm na mpenzi wake, akaniambia Jee ww nenda nyumbani mm nitakuja baadae, akanielekeza vzr na funguo alipo iweka, bc akaondoka na mm nikaenda stendi, nimesimama zangu stendi gafra ikaja gari mbele yangu nashangaa anaanza kuniita, nikawa sijamuelewa ni nani? Niliosimama nao stendi wakaniambia Dada unaitwa ww,, nikaenda yule Baba akaanza kutabasamu akaniambia panda twende nikupeleke hapo utakesha usafiri ni shida,, bc na ushamba wangu hata bila kuuliza unanipeleka wp nikapanda gari, nikamuelekeza ninapo enda akasema sawa,, Mara tukafika sehemu akapaki gari akashuka akaingia ndani, akanifata akaniambia haya njoo mara moja,, alikuwa mbaba mrefu kama muarabu IV, nikashuka akanipeleka hadi chumbani ilikuwa hotel, tukaingia ndani akaenda kuchukua vinywaji akaleta,, alinipa soda ila yeye alikuwa anakunywa pombe, niliogopa nikamwambia naomba niondoke, akasema subiri nitakupeleka, akaniuliza una CM? Nikamwambia hapana, akaniambia yeye kesho anasafiri kwenda Dubai ila anataka niwe mpenzi wake maana ameona Nyota yangu ni kali sana na itamfaa sana kwenye biashara zake kwa hiyo tuwe wapenzi,,, sikumuelewa chochote nilikaa kimya tu, nilienda chooni kukojoa nikaacha soda yangu ikiwa wazi, nilivyorudi akanilazimisha ninywe soda yngu, bc nikainywa mara nikaanza kupata kizungu zungu, na sikujua kinacho endelea, nilikuja kushtuka nipo uchi wa mnyama na nguo zangu zimekunjwa vzr zipo kwenye meza,, nikanyanyuka nikaanza kupata maumivu sehemu ya haja kubwa, nikasogea mezani ili nivae nikakuta vipimo vya ukimwi viwili vimegandamizwa na karatasi yenye maandishi"NIMEKUPENDA SANA MTOTO MZURI, HAYO HAPO NI MAJIBU YA UKIMWI YANGU NA YAKO TUPO VZR KUANZIA SASA MM NA WW NI WAPENZI,, HAPO CHINI YA NGUO ZAKO NIMEKUWEKEA CM PAMOJA NA HELA MILIONI TATU ZITAKUSAIDIA HADI NIRUDI SAFARI,, NIMEKUWEKEA LAIN KWENYE CM PLEASE USIBADILISHE,,,," niliogopa sana nikajikagua nikakuta nimeingiliwa kinyume na maumbile nikavaa nikachukua zile hela kweli zilikuwa milion tatu na CM ya smartphone pamoja na chaji cm ilikuwa mpyaa
Itaendelea
 
sehemu ya 4


Nilivaa nguo zangu vzr huku nalia, nikasema ee Mungu nimekukosea nn mm? Mbona matatizo kwangu yamekuwa mengi? Kila cku nimekuww mtu wa kubakwa tuu?? Nililia sanaa hadi macho yakawa mekunduu, nikachukua zile hela nikaweka kwenye chupi na ile CM nikaweka kwenye kitopu, nikatoka njee, nikakutana na muhudumu wa ile hotel, akaniambia Binti kuna usafiri wa bajaji hapo nje imelipiwa na Boss amesema ikupeleke nyumbani, nilitaka kukataa ila nikasema ngoja nipande tu, nikapanda ile bajaji nikamuelekeza dereva hadi ninapo kwenda, nilifika nyumbani bahati nzuri sikumkuta Dada jirani wala Kaka hakuwepo, nilifungua mlango maana funguo nilielekezwa na Dada ilipo, nikaoga nikavaa pensi zile hela na cm nikazificha kwenye pensi nje nikavaa sketi nikalala
Niliamshwa na Dada jirani akaniambia Jee mbona umelala mapema ivo? Amka tule alikuwa kabeba chips niliamka nikala mara Kaka akaja tukasalimiana vzr akanipa ticket ya safari, akaniambia amepata gari ya kesho kutwa kwhyo nijiandae kwa safari,, moyoni nilishukuru nikasema ngoja nirudi nyumbani maana huku mjini naishia kubakwa tuu najua sina wazazi ila sina jinsi nyumbani ni nyumbani,, bc Kaka aliniita nje tuongee, akaniambia Jee mdogo wng sio kama nakurudisha nyumbani ctaki ufanye kazi hapa Dar hapana, ila hii Dar sio sehemu salama ww ni mdogo sana ila nitakupa laki moja ya mtaji ukifika nyumbani ufanye biashara na ukiona umekwama kwa chochote bc utanipigia cm ili tujue cha kufanya, ww umekuwa ndugu yangu Sasa nililia mnooo nikasema sijawahi kupata upendo wa namna ile tangu Baba yangu alipofariki nimekuwa mtu wa kusukumwa sukumwa na kupigwa tuu ,, nilimshukuru Kaka mnoo akanipa hela laki na ishirini, ile ishirini nile njiani then laki nikafanye biashara, akanipa na namba yake ya cm tukaagana akaingia ndani kwake mie nikarudi kwa Dada jirani,, hapo sikutaka kumuambia Dada yaliyonikuta kabisa niliogopa asinione Malaya

Cku ya safari iliwadia Kaka alinifata saa kumi alfajiri kunipeleka ubungo, tuliagana pale nilimshukuru Dada jirani kwa msaada wake kwangu pia nilichukua namba yake,,, nilipanda basi safari ya Musoma ikaanza rasmi,, hapo nina hela zangu pamoja na cm nimeweka kwenye pensi
Nilifika nyumbani salama kabisa, nikachukua pikipiki hadi nyumbani kwetu, Marehemu Baba yangu alikuwa na mji wake ambapo ndipo kwetu, alijenga tu nyumba za msonge wakazi wa Mara mtakuwa mnazifahamu, bc nilifika hadi nyumbani nikagonga hodi maana kulikuwa kunaonekana tu kuna watu wanaishi hapo,, nikakaribishwa na sauti ya mwanamke, alivyotoka nikamuona Mama mdogo ni mke wa Baba yangu mdogo ndugu yake Baba,, bc tukasalimiana vzr ila nikamuona kama hakufurahi iv, nikaenda hadi kwenye chumba changu nikaweka begi langu nikalala maana nilichoka sana tulilala njiani na basi, nilishutuliwa na sauti ya Baba mdogo aliniita kwa sauti kali sana Amamu!! Kijijini wananiita Amamu! Nilitoka nikamsalimia aliitika ila kakunja sura yake,, Ww dar ulitoka lini?? Mbona shangazi yako alituambia umetoka mda mrefu sana na huku ndio unafika leo ulikuwa wapi?? Kumbe kweli ww ni Malaya na umembaka mjomba wako huko dar?? Kwann unatupa aibu ww mtoto?? Kabla sijanyanyua mdomo kujibu, baba mdogo akaanza kunipiga, nilipigwa sana,. Nililia kuomba msaada lkn wapi hakunisikia wala kunionea huruma hadi nilipoteza fahamu
Itaendelea
 
Sehemu 5

Nilipata fahamu nikajikuta nipo chumbani kwangu tena chini, nilijaribu kujiinua nikashindwa mwili wote ulikuwa unauma, nikalala pale chini hadi asbh hakuna hata aliyekuja kunitazama asbh ilivyokucha nikajitahidi kujinyanyua mwili mzima ulikuwa umevimba, nikajisachi nione hela zangu zilikuwa vile vile pamoja na cm maana niliweka mfuko wa pensi ndani nje nikavaa nguo kama kawaida, nilitoka nje sikumkuta mtu, nikaenda kuoga nikavaa nguo zangu nikatoka ili nikatafute chochote nile nilikuwa na njaa sana, nikaenda hadi kwenye mabanda nikaagiza chai nikanywa, wakati narudi nyumbani huku natembea kwa shida nikakutana na msichana mmoja tulikuwa tunasoma wote ila yeye alinitangulia kidato, anaitwa Ghati, tulisalimiana vzr yeye tyr kamaliza shule na matokeo yametoka alikuwa ameferi, bc tuliongea akaniambia nasikia ulikuwa dar? Vp mbona umerudi huku tena? Nikamuhadisia mkasa wangu wote hadi kubakwa na mjomba, ila kuhusu yule Mwarabu nilimficha niliogopa asijue nina hela, bc alinihurumia sana akaniambia bora ungebaki dar ukatafuta hata kazi za ndani au bar kuliko kuja huku,, tuliongea mengi tukaagana na Ghati nikarudi home, nimetoka home nikamkuta Mama mdogo nikamsalimia akaniambia Baba yangu mdogo ana maongezi na mm kwhyo nimsubiri nikamwambia sawa nikaingia Chumbani
Nimekaa chumbani nikatafakari sana nikasema bora niondoke hapa nitafute sehemu niende, cjui niende Arusha kwa Kaka yngu ila sipajui na mawasiliano sina, nikatafakari sana nikasema nikiondoka hapa naenda wapi? Nikiwa na mawazo mengi gafra nikaitwa nje nikatoka alikuwa Baba mdogo, nikakaa chini kumsikiliza,, akaniambia kama nimerudi pale bc nitafata sheria za pale, kuanzia Sasa natakiwa nilime shamba na sitakula chakula hadi ucku yaan nikiamka asbh kesho naenda shambani siruhusiwi kula chakula hadi ucku labda ninywe maji tu na ole wangu nilete uvivu pia siruhusiwi kwenda popote Zaid ya shambani na ole akute nimetoka,, nimeenda kufanya umalaya wangu bc ataniua, niliitika nikasema sawa Baba mdogo, nikarudi chumbani nikalia sana nikasema potelea mbali acha niondoke zangu kama kubakwa bc nikazidi kubakwa hadi nife kuliko kuteseka huku tena na ndugu wa Baba yangu nilisubiri giza liingie nitoroke,, nikiwa chumbani nawaza hayo akaja Mama mdogo akaniambia nitoke nikachote maji, bc nikatoka kwenda ramboni kufata maji, nikiwa bado nasomba maji maana nasomba maji na baiskeri, nikapata wazo nichukue baiskeri hadi center ili nikaweke chumba kabisa ili usiku nikitoka nyumbani nipate pa kulala ( gesti) bc nikaacha madumu hapo ramboni nikakimbiza baiskeri hadi center, nikatafuta gesti nikalipia, nilitoa kwenye zile hela nilizopewa na Kaka dar nilikuwa maziwa kwenye maziwa sikuzichanganya na zile zingingine, nikalipa chumba elfu kumi nikaandikisha jina nikasema nitarudi ucku kulala, bc nikakimbiza baiskeri hadi ramboni nikabeba maji yangu hadi nyumbani, nikaingia jikoni nikapika fasta huku nina mipango yangu kichwani, giza lilipo ingia nikatoa begi langu nikalificha nyuma ya nyumba kisha nikarudi ndani, nikatenga chakula vzr tukala, nikawaacha wao wanaangalia taarifa ya habari nikatoa vyombo nje ili nijifanye naviosha nilipotoka ndio kimoja sikurudi ndani nilifata begi langu nikabeba kichwani viatu mikononi huku natembea kwa shida hadi mbele mbele kidogo nikachukua pikipiki hadi center nikamwambia nishushe nikaogopa kumpeleka hadi pale gesti, nikatembea tena hadi gesti, nilivyofika mapokezi walinipa funguo nikaingia ndani
Nilishusha mapazia vzr na kufunga mlango vzr pale gesti ndipo nikatoa cm yangu ili niichaji ,, nikaiangalia vzr cm yangu ilikuwa iPhone nikaweka chaji nikalala, japo kuwa usingizi ulikuwa wa wasiwasi sana, ilivyofika saa kumi na moja alfajiri nikaamka nikaoga nikachukua begi langu na cm yangu nikaweka tena kwenye pensi pamoja na hela zile nyingi nikabakisha hela zile za Kaka niliweka kwenye maziwa nikatoka nje nikachukua pikipiki hadi stendi ya Mabasi ,, basi za Dar zilikuwa zimejaa nikaamua nipande zinazoishia mwanza kisha nilale gest asbh nipande za Dar,, nilifika Mwanza mida ya saa tisa ilikuwa mapema sana nikakata ticket vzr gari ya Dar lux, nikatafuta gesti nikalipia nikaenda kupumzika,, nimekaa zangu pale Mwanza gest ndipo wazo la kuwaza cm yangu likanijia,, nikawasha nikaanza kuangalia angalia japo sikujua kuingilia vzr ile cm lkn ilikuwa imewekwa hadi wtsap,, nikatoka nje nikaagiza chips na soda pamoja na maji, wakati nipo nasubiri chips nikawa naongea na Muhudumu akaniambia KAMA nina safiri nisiwe na shida watu wote wanaolala hapo ambao wanasafiri asbh wanafatwa na gari la hio gest wanapelekwa hadi stendi, bc nikamwambia na mm nina safiri bc watanigongea asbh akasema sawa niwe na amani tu,, nikarudi home kwangu nikafunga mlango vzr nikakaa kucheza cm,, Mara cm ikaja likatokea jina Mahamood" mhhh niliogopa ila nikapokea,, halow Mamujee hujambo?? Nikamwambia cjambo shikamoo,, Marhaba, habari za Tanzania? Nikamjibu nzuri,, akaniambia nilikutafuta sana kwann hukuwasha CM?? Nilikaa kimya, akaniambia bc kuanzia Sasa nisizime cm tena coz atakuwa ananiuliza mara kwa mara,, nikamwambia sawa,, akaniuliza uko wapi sasa?? Nikamwambia Mwanza,, akasema ulifata nn huko?? Nikamuhadisia mkasa wangu wote,, akaniambia nikifika Dar tu nifungue akaunti benk ili anitumie pesa nipange nyumba nikamwambia sawa,, akasema yaan nikifika tu nimjulishe kupitia wtsap na yeye atanipigia ili ajue kama nimefika salama,,, bc nikala zangu pale nikalala,,, kweli alfajiri nikagongewa mlango ili tupelekwe stendi,, nilifika stendi nyegezi Mwanza nikapanda gari Dar lux Safari ya Dar ikaanza tena kwa mara ya pili,, Mamujee kama Mamujee
Itaendelea like na comment ndio zitanishawishi kurudi
 
Back
Top Bottom