Ndoa ilimpa kilema cha maisha binti

Ndoa ilimpa kilema cha maisha binti

16
Bc Mahamood alisafiri akaniacha pale pale nyumbani kwangu na kuniachia jukumu la kusimamia ujenzi wa nyumba yangu Salasala, alinunua vitu vya ujenzi vya kutosha na kuwaacha mafundi na kuniachia pesa ili mafundi wakihitaji chochote niweze kununua,, maisha yaliendelea mimba yangu ilikuwa ilitimiza miez mitano iv nipo tu mwenyewe ila Mahamood tunawasiliana kila cku,, Mahamood akiwa Dubai anakuwa hana shida mnawasiliana kama kawaida,, nakumbuka siku hio nimeamka zangu najiandaa niende Salasala nikakae na mafundi nilipigiwa cm na shangazi,, aliniuliza uko wapi nikamdanganya mjini, akaniomba sana niende nyumbani kwake, nikamuahidi nitaenda nikitoka huko,, bc niliendelea na ratiba yngu nikaenda kwa mafundi nikahakikisha kila kitu kipo sawa maana Mahamood lzm anipigie cm anataka ripoti
Nikarudi zangu nyumbani kwangu nikapaki gari nikachukua bajaji nikaenda kwa shangazi ckutaka ajue kama nina gari,, hata kuhusu ujauzito sikutaka ajue, tumbo langu lilikuwa dogo mno huwezi kujua kama nina mimba hadi nikuambie mwenyewe, nimefika kwa shangazi alinipokea vzr jmn tena kwa kuwaambia wanae mkaribisheni Dada mhhhh, bc niliingia ndani vzr,, wakaniletea kinywaji lkn nilikataa nikawaambia nimetoka kula muda sio mrefu,, bc akaanza kuniambia alichoniitia kuwa Kaka yangu wa Arusha anapiga cm mara kwa mara anataka kuongea na mm,, nilifurahi kusikia habari za Kaka yangu ila sikufurahishwa kwann hakumpa namba zangu wakati anazo?? Nikamwambia sawa shangazi nashukuru sana ila naomba namba zake,, akanijibu namba zake sikupi ila nampigia hapa kwenye cm yangu uongee nae mhhhh, nilitulia kimya, nazani alim beep maana gafra cm ya shangazi iliita alipokuwa akaanza kuongea nae yeye kwanza walikuwa wanaongea kiruga,, then akamwambia Amamu huyu hapa ongea nae, ila nilishangaa shangazi anaongea na Kaka kistarabu mnoo nikajiuliza kulikoni?? Bc nikaanza kuongea na Kaka yangu, nikajikuta nalia nikamwambia Kaka mbona umeniacha mwenzio? Hata kunitafuta hakuna?? Akaniambia mbona napiga cm mara nyingi kwa shangazi ananiambia umetoka? Mara upo jikoni?? Nikabaki kusema haya sawa maana shangazi alikuwa ananikata jicho balaa,, akaniambia anakuja kesho kutwa kutusalimia mara moja ana mambo mengi sana ya kuongea na mm,, bc tuliagana na Kaka nikampa cm shangazi wakaendelea kuongea,, cm ilivyokata shangazi akaanza kuniambia ni kweli Kaka yangu alikuwa anapiga cm ila yeye hakujua nilipo ndio sababu akawa anamdanganya ,, bc nikasema sawa mm niende,, akaniambia mbona haraka ivo,, nikamjibu tu naenda kupumzika nimechoka sana,, bc tuliagana huku akinisisitiza kesho kutwa niwahi mapema ili Kaka akija anikute pale,,, Niliondoka lkn nilikuwa na hamu sana ya kukaa na Kaka yangu ili ajue mapito yangu yote nilifika kwangu nikajikuta mawazo yamenishika nawaza kuhusu wazazi wangu, Cm yangu ikaita Mahamood alipiga akaniambia washa data nikupigie WhatsApp,, bc nikawasha, tukaanza kuongea, akaniambia kavae mtandio ufunike hiko kichwa, nikaingia chumbani nikajifunika, kumbe alitaka niongee na mkewe mkubwa bc nikashangaa tu cm imeshikwa na mwanamke, mzuri huyo muarabu, akanisalimia assalamualaikum!! Nikaitika, nikamuamkia, akaniambia ww ndio Mamujee?? Nikamwambia ndio, akasema karibu kwenye familia yetu mdogo wangu , Mm ndio Dada yako mkubwa, ila yupo anae nifata, karibu sanaa,, Mhhhh!! Nilishangaa sana jmn,, nikamwambia asante nimekaribia,, akaniambia hongera kwa kutubebea mtoto tumboni ,, nikaona kama anajifuta machozi,, akaniambia mdogo wangu ww ndio umepata bahati, kabla hujaingia umebeba mimba?? Akaniambia nina mwaka wa kumi na Mume wangu sijabahatika uzazi mhhhh, nikajiuliza kurikoni Mambo haya jmn?? Bc nikamwambia usijali Dada Mungu atafungua milango,, akanijibu inshallah!! Tuliagana pale cm akachukua Mahamood,, akaanza kuniambia kweli Mamujee wake zangu wote hawajabahatika uzazi hata bi mdogo nae kumbe hajazaa,, mhhhh nilijiuliza sn,,, bc tuliagana na Mahamood,, niliwaza sana jmn, nikaogopa, nikasema hawa watu wa aina gn?? Mamujee umasikini unaniponza mie, kuingia sehemu hata siijui vzr,,,
Bc cku zilipita ikawadia cku ambayo Kaka yangu anakuja dar, nilitamani sana cku hii ifike jmn, niliona kama cku haziendi,, niliamka mapema sana, nikaenda Salasala nikahakikisha mafundi wapo vzr,, shangazi akanipigia cm niwahi, nikatoka Salasala moja kwa moja hadi kwa shangazi na gari langu, sikujari wala nn,, nimefika napaki gari tu, namkuta shangazi amekaa nje na mjomba,, walikuwa wanakodoa macho kuangalia anashuka nani kwenye gari,, c mnajua vioo vya giza,, nikazima gari nikashuka kisha nikaroki, kumaanisha hakuna mtu mwingine ndani ya gari ujue shangazi alipata kigagaziko Amamu ni ww mwanangu?? Nikatabasamu tu , nikawasalimia akamwambia mwanae mletee Dada kiti,, nikaletewa kiti nikakaa, nikatoa cm yngu nikaingia mitandaoni sikuongea chochote,,, bc mjomba akainuka kwa aibu kuingia ndani,, shangazi akaniuliza Mamujee una biashara gn mwanangu?? Nikamwambia hizi hizi ndogo ndogo,, akaniuliza hilo gari lako,, nikamwambia ndio langu ujue aliniangalia kisha akahema mhhh tumekaa pale hadi jion frani iv,, shangazi akapigiwa cm na Kaka akawa anampa maelekezo mara nashangaa gari prado inaingia, inapaki nilipopaki gari yangu,, kuangalia namuona Kaka yangu anashuka,, yupo peke yake, amependeza kawa bonge la braza meni,, nikanyanyuka nikamrukia tukaanza kulia,, nikajiuliza Kaka huyu ni Mwita au naota,, shangazi akaja kutukumbatia wote kwa pamoja,,,
Nitarudi niwaambie Kaka yangu gari kapata vp




17


Tulikumbatiana pale na Kaka yangu huku shangazi nae akitusii tunyamaze, shangazi akamkaribisha Kaka ndani , tuliingia ndani yaan tunaangaliana na Kaka hatumalizani kila mtu ana mengi kwa mwenzie, Kaka aliandaliwa chakula akala, mie sikutaka kula cha mtu, mjomba akatoka akakaa nae sebleni maongezi yanaendelea, nilipigiwa cm na Mahamood nikatoka nje kuongea nae, nikamwambia nipo kwa shangazi yangu na Kaka yangu amekuja, bc alifurahi sana akasema bora amepatikana mtu wa kupokea mahari yangu, nirirudi ndani, Kaka akaanza kunitania Amamu umekuwa mrembo, kweli dar haiongopi tulicheka pale yaan ilikuwa raha tu, mda ulifika nikawaaga niende kwangu, Kaka akashangaa Kwan hukai hapa? Shangazi akajibu c umesema amependeza sasa atakaaje hapa wakati amekuwa sasa? Mhhhh bc Kaka akasema twende nikupeleke hadi kwako, shangazi akarukia utampeleka vp wakati na yeye ana gari lake? Jmn shangazi anajibu kila kitu, Kaka akashangaa Amamu una gari?? Embu njoo nje kwanza tuongee vzr unipe Siri ya mafanikio yako,, tukatoka nje ila shangazi akili yake yote ipo kwetu,, akaniuliza hii ndio gari yako? Nikamwambia ndio, nikaifungua tukaingia ndani, akaniuliza vp ulimaliza kusoma hio kozi yako?? Nikamuuliza kozi gn tena? Wakati tangu afe Baba shule ilinishinda? Akasema kwan hukumaliza form 4?? Nikamwambia Kaka bhana usinichoshe kumaliza huko ananisomesha nani? Kaka alishangaa, akasema mbona aliambiwa na shangazi kuwa nimemaliza F4 na nipo tu nyumbani ndio Kaka kutoa hela niende chuo kumbe shangazi alichukua pesa kwa Kaka ili niende chuo niliumia sana nikamwambia Kaka elimu yangu ni ile ile aliyoniacha nayo Baba sina Zaid, bc akaniambia tutaongea vzr kesho maana shangazi alikuwa hana amani mara katoka nje mara kaingia ndani
Nikarudi ndani kuaga then nikaenda zangu kwangu,, tulihaidiana na Kaka atakuja kwangu mapema tu,, nilichukua namba ya cm ya Kaka, bc asbh nimeamka nikafanya zangu usafi, nikaenda buchani nikanunua samaki sato wangu ili nimpikie kaka ugali, kwetu chakula chetu kikubwa ni ugali tena wa mtama
Kaka alinipigia nimuelekeze kwangu nikamuelekeza akafika, yaan alifika mapema hata chai hakunywa nikamuuliza mbona mapema, akasema Amamu umenivuruga ulivyoniambia hujamaliza hata F4 , nikamwambia ndio ivo Kaka, nikamuuliza kwan shangazi ajakuambia chochote nilivyoondoka? Akasema aliongea kuwa ww umeamua kuhama nyumbani ila anahisi umepata mwanaume mwenye pesa, nikamwambia bc unywe kwanza chai, akaniuliza Amamu hapa unaishi na nani? Nikamwambia kunywa chai kwanza then tutaongea,, alikunywa tukamaliza tukaanza maongezi,, nilimuhadisia jinsi nilivyoondoka kwa shangazi na nilivyobakwa na mjomba Kaka angu alilia kwa sauti akaniambia Amamu, mbona hukunitafuta? Nikamwambia ningeanzia wapi? Nikamwambia hadi nilivyorudi kijijini, Baba mdogo alivyonipiga nusu kuniua eti kwann nimechelewa kufika nilikuwa wapi? Na walivyonigeuzia kesi eti mm ndio nilitaka kumbaka mjomba aisee Kaka alilia kama mwanamke , ikabidi nimnyamazishe Kaka yangu, akaniambia, kila cku nilikuwa nakuwaza mdogo wangu ila shangazi ananiambia upo chuo, nimemtumia milion mbili ya kukulipia ada ya chuo kumbe muongo,, bc tukanyamazishana na Kaka, akaniuliza kuhusu pale ikabidi nimwambie tu ukweli kuhusu Mahamood, ila kuhusu kutolewa marinda sikumwambia jmn hii ni aibu yangu mwenyewe ndio maana namwambia adimin furaha asiniweke hadharani ctaki, wamama mtanichamba Mamujee mm
Bc tuliongea mengi kunihusu na Kaka, ndipo na yeye akaanza kuniambia ya kwake,, kumbe Kaka yangu nae kapitia mazito ( wanawake muombeni Mungu awape maisha marefu mlee wanenu Uyatima mbaya sana ) Kaka yangu nae alichukuliwa na shangazi yangu mwengine, tulifanywa kugawanywa mie kuja dar yeye Arusha, alifika Arusha mwanzoni maisha yake yalikuwa mazuri tu, yeye mwenzangu alifanikiwa kumaliza F4 , bc aliishi kwa shangazi pale Arusha ila kama house boy shangazi wa Arusha nae ni mfugaji ko Kaka alikuwa anachunga mifugo,, Sasa cku moja kapeleka ngombe malishoni, cjui ikawaje ngombe mmoja akapotea, alitafuta kote, kwa wenzie wote anae chunga nao bila mafanikio, ndipo kumuambia shangazi, ila shangazi alishindwa kuelewa akampeleka Kaka polisi, akakaa sero wiki tatu hata wa kumuwekea dhamana hayupo, ndipo mapolisi kwa huruma wakamtoa, akawa hana pa kuishi anaishi stendi, ndipo akakutana na vijana wenzie wa mitaani wakaamua waende migodini kwenye machimbo,, Miaka miwili kasota machimboni ila Mungu si Mwanadamu, Kaka yangu katusua
Itaendelea



18


Tuliongea mengi na Kaka yangu akaniambia kuhusu biashara zake na nyumba yake kubwa anayoishi Arusha Maeneo ya Unga limited, nikamwambia na mm nyumba yangu ya Salasala, kuhusu Mahamood Kaka hakuwa na shida aliniambia tu mm ni mtu mzima hawezi kunipangia maisha, wakati tupo tunaongea na Kaka, shangazi akampigia cm Kaka kumuuliza upo wp? Kaka akamjibu nipo mjini huku nitakuja huko muda c mrefu niwaage, naanza safari ucku huu, shangazi alikataa cm,, Kaka akaniambia sina hamu hata ya kwenda pale kwa shangazi, nitafute hotel nzuri nikae siku mbili tatu, nikamwambia kwann usikae hapa kwangu? Alikataa kata kata, bc tulitoka na gari yake hadi maeneo ya mwenge tukalipia hotel, akarudi kwa shangazi kuaga lkn shangazi akawa hataki Kaka aondoke pale, ilibidi kaka alazimishe tu, alimpa laki moja akasepa zake
Tulihaidiana na Kaka asbh atakuja kwangu ili nimpeleke kwenye ujenzi wa nyumba yangu Salasala, bc alinifata kwangu tukaelekea, tukakuta mafundi wanaendelea na kazi, Kaka alishangaa kuona Dada yake naenda kumiliki ghorofa, akaniambia Amamu hongera sana, nataka na mm nitoe mchango wangu hapa kwenye nyumba yako,, nikamwambia Kaka kwnn sasa? Akasema ww ni mdogo wangu wa damu nisipo kusaidia ww bc nitakuwa mchawi, ungekuwa huna gari bc ningekununulia ila gari unayo tena mpya kabisa, acha nichangie ujenzi,, nikamwambia Kaka asante sana na Mungu azidi kukufanikisha, akaniuliza nina akaunti benk gn, nikamjibu, nikampa namba za akaunti yangu, Kaka yangu aliniingizia milion kumi cash akaniambia nikikwama chochote bc nimjulishe, nilimshukuru sanaa,, hatimae cku zikaisha Kaka akasepa zake Arusha
Mawasiliano na Mahamood yalizidi kushamili cm kutwa kucha, mimba yangu inazidi kukua tu,, nilikuwa napendwa hadi naona kero, ilifika mahari akawa hataki niendeshe gari mwenyewe nikitaka kutoka bc niite uber au nimwambie yeye anitumie dereva
Nakumbuka siku hio nimeamka zangu asbh kama kawaida yangu lazima nitapike kwanza ndipo maisha yaendelee, nipo chooni, Cm yangu ikawa inaita, nikasema nikitoka nitaichukua acha iite tu, nikaendelea na yangu ila cm inazidi tu, nikasema nani huyo jmn? Nikatoka kwa hasira kuchukua cm kuangalia namba shangazi, mhhhh nikasema kulikoni tena?? Nikaipokea, shangazi akaanza kilio Amamu mwanangu nipo hospital hapa mjomba wako kapata ajari ya pikipiki hee!! Makubwa haya tena, nikamuuliza hospital gn akaniambia muhimbili,, nikamwambia sawa nakuja,, nikamcheki Mahamood watsp kumpa zile taarifa akaniambia anamtuma mfanyakazi wake anifate anipeleke, nikaamua kumcheki Kaka kumpa zile taarifa kumbe na yeye aliambiwa na shangazi tena akamuomba hela ila Kaka akamjibu sina, ndipo kunipigia mm,, Kaka akaniambia usiende popote achana nao, ila roho ya huruma ikaniingia nikamwambia Kaka ngoja nikaone tu,, bc tulimalizana na Kaka, nikajiandaa fasta nilivaa baibui langu hadi nikabu ukiniona hunijui Mamujee mm
Dereva akaja tukaenda hospital, nilivyofika kwanza hakunijua nilimkuta nje ya wodi ya Moi anatia huruma kajishika shavu nikasema ngoja nijifanye sijamuona nimpite nikakae mbele yke nimchore kwanza ila roho ya huruma ikaniingia, nikamfata nikamwita shangazi akaitika kwa sauti kubwa Abeee huku ananitazama usoni, maana naonekana macho tu nikaona isiwe shida nikatoa nikabu, hee Amamu mwanangu sijakujua Mama nikamuamkia sikutaka mambo mengi, nikamuuliza vp ilikuwaje, akaanza kuniambia chanzo cha ajari, mjomba alibebwa nyuma cjui ikawaje akajikuta yupo uvungu wa lory,. Na miguu hainyanyuki, hapo wameletwa tangu jana yake ila bado hajapelekwa Opareshen eti kuna foleni wagonjwa wa ajari wapo wengi kwa hiyo asubiri, au alipie Emmegency, nikamwambia sasa c walipie hio kuliko kuendelea kusubiri mguu c utaoza?? Akaniambia Amamu mwanangu hao wanataka hela cash na mm sina hio hela, nikamuuliza sh ngp?? Milion moja na laki saba,, nikamwambia sawa bc ngoja niende benk nikampe,, shangazi alibaki kaduwaa hata jibu hana,, nikavaa nikabu yangu nikatoka kumfata dereva anipeleke benk,, hatukuchelewa kurudi nikampa shangazi milion mbili cash, kisha nikamuaga, akaniuliza huingii ndani kumuona mgonjwa?? Nikamwambia nitakuja cku nyingine,, bc shangazi machozi yakamtoka huku kawa mdogo,, mie huyo nikasepa zangu
Nilikaa kama wiki iv shangazi akanipigia mumewe anaendelea vzr ila wamemuweka vyuma
Maisha yakaendelea nipo zangu kwangu huku mimba yangu inazidi kukua gafra tumbo likawa kubwa ajabu, mhh mbona tumbo linakuwa haraka iv,, sikuanza kliniki coz Mahamood hakuwepo na aliniambia nimsubiri yeye anipeleke, bc nakumbuka mimba yangu ilifika miez sita kwenda saba sijaanza kliniki,, cku hio Mahamood akanipigia akaniambia anakuja kesho kutwa nijiandae, kweli alifika nikampokea vzr zawad kibao zingine nimetumiwa na mke mkubwa, cheni ya gord, pete na kikukuu vyote gord, nirifurahi nikaongea nae kwa cm kumshukuru,, nikapelekwa kliniki pale kairuki wala hatukusemwa kwa nn tumechelewa Mahamood aliongea na doctor sababu ya kuchelewa kuanza clinic, bc nilifanyiwa vipimo vyote hadi ultrasound,, mhhhh niliogopa ultrasound ilionesha nina mapacha,,,,,,,
Itaendelea


19

Bc bhana yale majibu ya Dactari yalitupa mshituko sana hasa mie, nikamwambia Mahamood itakuwaje? Mahamood akanitia moyo akaniambia ngoja turudi nyumbani KWANZA,, nilihisi kudata jmn, bc hatukwenda hata nyumbani tulienda hotel pale Mahamood anapenda kufikia, alinitoa wasiwasi sana akaniambia yeye ni Baba na hatahakikisha watoto wake wanazaliwa salama kwa gharama yeyote ile labda iwe mapenzi ya Mungu,, bc alimpigia cm bi mkubwa kumpa zile taarifa walikuwa wanaongea kiarabu,, nikashangaa napewa cm niongee na bi mkubwa, nikazungumza nae anaongea Kiswahili kama cha mombasa ila ni muarabu, akaniambia Mamujee usijali itabidi MUME wangu akuoe rasmi kisha uje huku Dubai ukae hadi ujifungue ndipo urudi Tanzania, nikabaki. Mhh!! mhhh!!! Mhhhh, haya!! Kiufupi nilishikwa na kigugumizi japo kuwa kwa maumbile yangu harisi nina kigugumizi ila pale kiliongezeka bc nikarudisha cm kwa Mahamood
Nakumbuka siku hio nilikuwa kama mfalme wa inchi za kiarabu, mara nabebwa, mara nashushwa, mara naulizwa nikufanyie nini yaan tafrani tu nikaulizwa km nipo tyr kufunga ndoa nikasema ndio, akaniomba namba za Kaka yangu, akampigia akajitambulisha , akamuambia kuhusu ndoa, Kaka hakupinga kabisa ila akamwambia utaratibu ufanyike, bc Mahamood akamwambia kaka kama yupo tyr ampelekee mahari Arusha, Kaka akamwambia asubiri kwanza atampa majibu, wakakubariana ndani ya cku mbili majibu yatakuwa tyr
Tukiendelea kusubiri majibu ya Kaka ndipo Mahamood akaamua amuambie mkewe mdogo wa Uingereza coz hawezi kufunga ndoa bila ya kumpa taarifa, kabla hajamwambia akaniambia Mamujee huyu mke wangu ni mkorofi balaa cjui kama atanielewa, ila vyovyote vile mm ni mwanaume,, bc akampigia cm, Mhhhhh cjui ikawaje maana Mahamood alitoka nje kuongea na cm mm kaniacha ndani ila alivyorudi kapoa kawa mwekunduu,, mhhhh niliogopa nikamuuliza vp,, kabla hajajibu cm yake ikaita ni huyo mkewe,, Mahamood akapokea bc ile halow aliishia hapo hapo mwanamke anaongea yeye tu, Mahamood akitaka kuongea anakatishwa,,, nikasema Amamu mie mbona mikosi kwangu haiishi jmn,, bc waliongea mwisho Mahamood akapaniki akakata cm,, nilivyoona ile hali nikanyanyuka nikachukua pochi yangu nikashuka chini,, nikahisi moyo unaenda mbio htr,, mara namuona Mahamood nae ananifata Mamujee, Mamujee, sikugeuka nyuma hadi nje ya geti, alivyoona vile akarudi ndani nadhani alifata funguo ya gari,, nikatoka nje nikaita bajaji, nikamwambia nipeleke mwenge, hapo nimepanga niende ile hotel aliyofikia Kaka, bc ikanipeleka hadi mwenge nikapata wazo, nikamwambia nishushe hapa hapa sikutaka aone ninapo elekea maana ile bajaji nilichukulia pale Hotelini chini nikahofia anaweza kuuliza,, nikamlipa hela yake nikarudi nyuma kidogo nikachukua bajaji nyingine hadi pale Hotelini, nikaripia nikaingia room, hapo cm yangu inaita hatari,, nikavua nguo zote nikawasha AC nikaanza kulia, nililia hadi nikajiona mwepesi cm yangu iliendelea kuita tu ni Mahamood anapiga wala sikupokea, kumbe na yeye alitoka akaanza kunifatilia akaenda hadi kwangu akakuta cjafika, akaamua apaki gari nje anisubiri maana funguo nilikuwa nazo, akapiga cm weeee wala sikupokea, Mara naona cm ya Kaka yangu, nikapokea akaniuliza upo wp nikamjibu nipo mwenge kwan vp akasema amna nilitaka kujua then nikwambie mwanaume wako anataka kuleta mahari ila nimemwambia anipe mda wa cku mbili,, nikamwambia sawa, kumbe Kaka ametumwa na Mahamood anipeleleze,, tukaongea na Kaka akaniambia Sasa mwenge unafanya nn mida hii ww mtoto wa kike, nikamwambia leo nalala Hotelini kwako ulipo fikia ukiwa dar,, kumbe Kaka ananichora tu,, akaniuliza room gn upo hapo, nikamtajia, bc akaniaga akaniambia tu kesho nenda kwako,, nimekaa kama nusu saa mlango wangu ukagongwa nikajua Muhudumu, nafungua tu nakutana na Mahamood,, akanibeba huku analia, nisamehe mke wangu,, naomba usipate presha ukaharibu huo ujauzito,, hujui ni kiasi gn nimetafuta mtoto,, imefikia hatua hadi kutaka kupandikiza,, naomba Mamujee nielewe nitakupa hakuna wa kunizuia kama mke wangu atakuwa tayari nimpe taraka bc nitafanya ivo lkn lzm nikuoe Mamujee,, nililia mm tukalia wote,, tukasameheana, , cm ya bi mdogo ikazidi kuita Mahamood hakupokea, tulilala pale hadi asbh,, tukajiandaa kuondoka kwetu
Nikawa namtafakari bi mdogo, kwann hataki mi niolewe?? Mbona yeye hakukataliwa na bi mkubwa?? Nilimuwaza sana,. Hapo ndo hajui kama mm mjamzito,, bc bi mdogo alivyoona Mahamood apokei cm yake akampigia bi mkubwa,, bi mkubwa akampigia cm Mahamood wakaongea kiarabu huku wanachanganya na Kiswahili kidogo,, kumbe bi mdogo kasema ole wake amuoe huyo mwanamke, kama shida ni mtoto yupo tyr akapandikizwe, bi mkubwa akamwambia muache aoe tu kwan shida nn?? Akasema akilazimisha kumuoa bc sitakuwa radhi leo hadi kesho kiama mhhhh cjui nitamuweza mie huyu bi mdogo??? Vita ni vita Muraa
Itaendelea


20

Bc bhana vita ikaanza rasmi kati yangu na bi mdogo, nilikuwa naogopa balaa, nashukuru Mahamood na bi mkubwa walikuwa upande wangu na walinitia moyo sana, hasa Mahamood hakutaka kabisa nipate presha, cm zilizidi kupigwa kutoka kwa bi mdogo akimpigia mume wake akimsisitiza asioe,, zile cku mbili walizokubaliana Kaka na Mahamood zikafika na Kaka alipiga cm kwa Mahamood na kumpangia mahari, bc ilibidi tusafiri na Mahamood kwenda Arusha kwa Kaka, Mahamood alichukua watu wake watatu wawili walikuwa wa ofisini kwake na mmoja ni muarabu mwenzie, tuliondoka na magari mawili hadi Arusha, Mungu alitusaidia tulifika salama kabisa, tulikuta Kaka anatusubiri alishaandaa watu wake, mhhhh nilivyofika kwenye nyumba ya Kaka,, kweli Mungu c Mwanadamu,, nilikuta nyumba kubwa ina kila kitu, magari yake matatu kapaki hapo kwake, mhhhh nikamtania Kaka, angalia usijekuwa Freemason Kaka akanijibu umejuaje na lazima nikutoe ww kafara tulicheka pale nikaingizwa chumbani,, nilikuta house girl wawili na house boy mmoja,, Mahamood hakutaka kuchelewa alisema anatoa mahali na ndoa hapo hapo, bc ikabidi Mahamood mwenyewe atoke akatafute mashehe,, ikabidi nisilimishwe kwanza ndipo ndoa ifungwe, tukafanikiwa kufunga ndoa rasmi na Mahamood,, vitu vyote hivo tunafanya hatujashirikisha ndugu yetu yeyote nipo mm na kaka tu,, ndoa ilipita salama bc Mahamood akaongea na Kaka kuhusu ujauzito wangu unahitaji mtu wa kuniangalia na yeye haishi Sana Tanzania , so anaomba aondoke na mm kwenda Dubai,, Kaka yangu alikataa kata kata akamwambia hapana shemeji,, huyu ndugu yangu ndio mimba yake ya kwanza inabidi ajifungulie kwetu isitoshe tupo wawili tu kama macho,, cwez kumruhusu ndugu yangu kwenda huko kwa hali yake hii japokuwa ni mkeo,, bc Mahamood akakubali mm nibaki Arusha hadi nijifungue, ila yeye atakuwa anakuja kuniona,, tulikubaliana hivo,, wale wageni wakaondoka kuja dar nikabaki na Mahamood tukawa tunakaa Hotelin wiki Mahamood anarudi dar anakaa kama wiki mbili anakuja Arusha,,
Nilivyokaa na Kaka ndio nikajua vzr maisha yake,, alikuwa na Maisha ya starehe htr, pombe sana wanawake ndio usiseme kila cku naletewa wifi mpya kutambulishwa nadhani mnawajua watu wa madini,, Kaka yangu ni mfanya biashara mkubwa wa madini,, yaan pale Arusha anajulikana htr yupo kwenye kundi la watu wenye pesa,, Sasa wanawake nao hawapo nyuma kila cku analeta mpya,, nikaona hapana,, cku moja Kaka karudi mapema amerudi peke yake cku hio, mzima hata pombe hana kichwani,, kwake pia kuna kaunta huwa kama ajanywa nje bc analewea ndani Sasa cku hio karudi mkavu,, huwa anakawaida akirudi hata iwe saa ngapi lazima aite Amamuuuu tena kwa fujo,,,. Njoo ndugu yangu wa damu, wewe ndio unajua thamani yangu kuliko mtu yeyote yule njoo mdogo wangu,, cku hio karudi kimya kimya, nikajiuliza kulikoni?? Nikamfata chumbani kwake kugonga,, nikasikia analia tena sauti kubwa,, nikamwita Kaka vp? Unaumwa?? Akaniambia hapana Amamu,, nikamwambia bc fungua mlango,, akanifungulia huku analia, nikasema vp, kapoteza pesa?? au kaachwa?? Mhhhh,, nikamuuliza vp mbona unaniogopesha mwenzio? Akaanza kuniambia, nawakumbuka wazazi wetu sana,, nakumbuka maisha niliyopitia mm,, na ww Dada yangu?? Eti ulibakwa na mjomba na wakakupiga nusu ya kukuua?? Nikamwambia Kaka tuyaache hayo achana nayo tuangalie maisha yetu upya,, akaniambia hapana,, kesho naenda Musoma, nataka nikamfate Baba mdogo aniambie kwann alitaka kukuua?? Nikamwambia hapana Kaka,, nikamuomba sana apunguze starehe sio nzuri, hata wazazi wetu huko walipo hawawezi kufurahia wakijua unaishi haya maisha,, bc alinihahidi kubadilika ila kuhusu Baba mdogo lazima akaonane nae
Mahamood alisafiri kwenda kwa bi mdogo mm kabla cjajifungua ila nilikuwa mwishoni sana,, alikuwa anawasiliana na mm kwa shida sana kama kawaida yake,, inaweza kuisha wiki bila salamu, cku akikutafuta sory zinakuwa nyingi,, nikawa ctaki kujipa presha na ukizingatia nimechoka,, Kaka yangu alikuwa ananipa kila kitu ( kasoro sex) nilijikuta nina amani ya moyo wala sikuwaza kuhusu Mahamood,, nakumbuka siku hio nimeshika cm yangu ile nafungua wtsap tu nakutana na voice note, nikaifungua, hee! Mke wa Mahamood cjui namba yangu kapata wapi,, nikaisikiliza ni matusi jmn,, tena anatukana Kiswahili anachanganya na kingereza,, eti ww malaya,, huwezi kuolewa na Mume wangu, na ole wako uendelee kudil na Mume wangu utajua ujui,, yaan vitisho vingi na matusi,, kiukweli niliumia sana nikasema shida yote hii ya nn?? Kwanza huyo mumewe wala sikumpenda kwa hiali yangu, kukosa kunibaka ningekuwa nae mm?? Niliumia nikaanza kulia nikasema Mahamood akinitafuta namwambia ckutaki na anikome,, ilipita wiki hakunitafuta nikamtumia voice note na mm Mahamood,, nikamwambia kwann ulinibaka wakati ulijua fika upo na wake zako?? Na kwa nn uliniingilia kinyume na maumbile yangu?? Nakuchukia!! Mwambie huyo mkeo ukweli,, asinitukane mm, sina makosa,, pia naomba unitumie taraka yangu kwenye cm pindi tu utakapo upokea ujumbe huu,, na nikijifungua hawa watoto nitawaambia ukweli Baba yenu alinibaka kwanza kabla sijampenda,,,,,, nilivyomaliza kuongea nikatuma,, nikatuma na ile voice note ya mkewe,, nikakaa zangu kimya haikupita nusu saa cm ya Mahamood inaingia
Itaendelea
 
Pamoja sana BHOKE, ninashindwa kuacha kuwashangaa wanaokulalamikia kuhusu uandishi wako wakati wewe kama mhusika mkuu elimu yako ilipoishia umesema sijui darasa la nne B.
 
( 21- 35 ) MWISHO

21
Cm ya Mahamood ikaingia, nikajiuliza nipokee au niachane nayo? Nikasema ngoja nipokee maana ni Mume wangu, halow Mamujee unaendeleaje? Nikamwambia cjambo, eti mke wangu naomba univumilie, najua unaumia sawa, ila nivumilie mama, huyu mwanamke ni mkorofi sana, amechukua namba yako kwenye cm yangu, ctaki kumwambia kuhusu swala la mimba, nahofia anaweza kufanya hata kitu kibaya, ndio sababu nipo kimya kwa sasa, nasubiri ujifungue kwanza,, nilimuoa huyu mwanamke sababu ya bi mkubwa kukosa uzazi , ckujua kama hata yeye atachelewa kuzaa, wakati namuoa yeye nilimuhakikishia kuwa sitaoa tena yeye ndio wa mwisho, Sasa ningefanya nn na yeye uzazi umekuwa wa shida kwake? Ina maana nikae bila mtoto kweli?! Hapana naomba univumilie,, kama unashida yeyote ya pesa bc nikutumie, naomba utulie, acha presha, ujifungue kwanza,
Aliongea mengi sana kunibembeleza nikamwambia sawa inatosha, maana tyr nilikuwa naona kabisa presha yangu iko juu
Nikamuuliza tu vp ujenzi wangu kule Salasala, maana alimuachia mtu ausimamie, akaniambia unaendelea vzr na wameanza kupaua,, bc nikamwambia sawa bye
Niliendelea kukaa pale kwa Kaka ila akawa amepunguza kidogo Mambo ya wanawake, anawaleta ila wawili, wenyewe hata hawajuani kila mtu anajijua yupo mwenyewe na mm nilikuwa hata siwaopoi maana mie kwangu tupo watatu maisha yaliendelea na cku zikazidi kuisha,, tulikubaliana na Mahamood kabla kuwa nisubiri uchungu niombe Opareshen coz tulihofia watoto wawili harafu marinda sina mhhhh, bc tukawa tyr tunajua mm ni Opareshen tu, hata wakati nipo dar doctor wangu aliniandikia ivo so kwenye fairi langu ilikuwa ipo wazi kuwa nataka opp, nazani mnajua hospital za kulipia hazina shida zinakusikiliza mteja unataka nn,, na nilivyofika Arusha tyr nilishatafuta hospital ya kujifungulia, trh yangu ya opp ilifika nikaenda hospital vzr nilipelekwa na Kaka pamoja na wifi mmoja, nilifika hospital nikalazwa ili kuandaliwa kwa opp,, Kaka alimtafuta Mahamood ila hakupatikana, nikafanyiwa opp vzr nikajifungia salama watoto wa kiume,, nilifurahi sana pamoja na Kaka yangu maana tyr tumeongezeka, tulikuwa wawili ila sasa tupo wanne bc nilikaa hospital kama cku tano iv nikaruhusiwa kurudi nyumbani, niliendelea kula uzazi pale kwa Kaka wala sikuwa na hofu tena kuhusu Mahamood nilisema akinitafuta sawa ila asiponitafuta pia sawa , nilikaa hadi namaliza 40 Mahamood kimya ukimtafuta pia hapatikani, nikasema mhhhh hii sio kawaida kulikoni? Namba ya bi mkubwa sina huwa naongea nae kupitia cm ya Mahamood, nikaona hii hali sio ya kawaida,, namtafuta vp sina njia nyingine? Ila namba ya bi mdogo ninayo aliyonitumia matusi, ila cwez mtafuta!! Nikaongea na Kaka kuhusu ile hali na wasiwasi wangu,, Kaka aliniuliza tu ile ghorofa hati yake jina la nani?? Yaan Kaka unaacha kufikilia wanangu kuhusu Baba yao unawaza ghorofa?? Akaniambia Amamu hao watoto ni wangu, Baba yao awepo au asiwepo wala usijali, niambie tu hati ya nyumba yako inajina la nani?? Nikamwambia inajina langu,, akaniuliza tena una uwakika?? Nikamwambia ndio, akasema bc achana nae yaaan Kaka mipombe imemuaribu jmn,, cjui na mirungi pia, maana anaongea kihuni tu, aliniuliza kuhusu gari yangu nimeacha wap nikamwambia pale pale kwangu ila usalama upo tu, huwa nampigiaga jirani yangu ananiangalizia, bc Kaka akasema kama huumpati huyo mumeo achana nae nikamwambia bc mm nikifikisha miezi mitatu narudi kwangu, akaniambia sawa, kula uzazi kwanza kwa Kaka yako,, bc niliendelea kukaa kwa Kaka ila ckuacha kumtafuta Mahamood ila mafanikio hakuna
Cku moja nipo zangu tu sina hili wala lile, nishaanza kupendeza uzazi umenipenda mwenyewe kuhusu mengine nimemuachia Mungu,, nashangaa mlinzi wa Kaka ambaye ndio house boy, anakuja kuniita eti kuna mgeni wangu,, nimetoka namuona Mahamood, alivyoniona alifurahi, akaniambia nilijua tu tyr umejifungua, nikamwambia kwahyo ulifanya makusudi?? Nikamwambia karibu ndani,, akasema hapana siingii ndani, naomba toa maelekezo kwa watu wako humo ndani tutoke mara moja,, bc nikawaaga madada nikatoka na Mahamood, tukaenda kwenye hotel moja iv, tukaagiza chakula na vinywaji hatukuchukua room,, wakati tunakula na kunywa ndipo akaanza kuniomba samahani, kumbe bi mdogo alivunja cm na alikata kata laini zote za cm, kwahyo alikosa mawasiliano kabisa, mhhhh nikaamua kumuelewa tu, ndipo akaniuliza umejifungua watoto gn?? Nikamwambia wa kiume, maana mda wote huo alikuwa hajauliza chochote kuhusu watoto, akaniambia naomba picha nikamuonyesha ,, Watoto wangu wote machotara nywele Sasa kama Baba yao Mahamood alifurahi akasema nilitegemea hili,, bc alikuwa na cm nyingine kweli tofauti na ile ya mwanzo, akampigia cm bi mkubwa,, yaan bi mkubwa alifurahi jmn yule mwanamke cjui ana roho gn jmn, nikaongea na bi mkubwa akanipa hongera,, Mahamood akamtumia bi mkubwa picha,, bc Mahamood akaweka status yake watoto wake akaandika inshallah, hatimae nimekuwa Baba,, nikamwambia huogopi?? Akasema nilikuwa nasubiri wazaliwe salama tu mm sio mjinga wa kupelekeshwa na wanawake he mara ananionyesha status ya bi mkubwa nae kawaweka watoto kaandika My babies , nikasema bi mdogo lazima aue mtu
Itaendelea

22
Adimin sory sana pamoja na wajumbe, nilitamani kurudi ila bize sanaa walah! Hii sikukuu kwa sisi wafanya biashara ndio wakati wetu wa kupata chochote, sasa nimejikuta hata muda wa kushika cm sina kabisa!!! Natamani kuimaliza hii story......
Bc tulikaa pale Hotelini tukimaliza chakula chetu,,, tulirudi nyumbani ili Mahamood akawaone watoto wake, bc alifurahi sana kuwaona wanae akasema hii kweli damu yngu,, alikaa pale akimsubiri Kaka ili amshukuru,, akaniambia Mamujee naomba turudi dar, nikamwambia sawa ila tulipatana na Kaka watoto wafikishe miezi mitatu, akaniambia hapana, nataka tuwahi nikasimamie ile nyumba iishe kwa haraka, kabla sijarudi Dubai muwe mmehamia na watoto, nikamwambia sawa, MUDA uliisha Kaka hakurudi mapema cku hio, Mahamood aliondoka kulala Hotelini,, bc Kaka aliporudi nilimpa zile habari akakubali mm kurudi dar na Mahamood,, bc asbh tuliamka mapema sana tukajiandaa kuondoka, Kaka akanipa msichana wa kazi mmoja nije nae, Mahamood alitufata tukaanza safari ya kurudi
Tumefika dar vzr tukaanza maisha mapya ya ulezi wa mapacha ( Mtanisamehe majina ya watoto wangu sita yataja kurinda heshima ya familia yangu maana humu tupo wengi na tayari nishajitaja jina langu Mamujee so watu watanijua) bc Mahamood alinitafutia msichana mwengine kwa watu wa makampuni nikawa na wasichana wawili,, tuliishi vzr sana Mahamood alipenda sana watoto wake, nyumba yangu iliisha kabisa, namshukuru Mungu mnoo, nikahamia kwenye nyumba yangu na familia yangu,, kipindi hicho chote choko choko za bi mdogo zinaendelea, mara anitumie matusi, yaan shida tupu, Mahamood alinisisitiza sana nisimjibu kitu hadi pale atakapo yaweka sawa
Nipo zangu kwangu Salasala nishaanza kuzoea maisha yangu na Mahamood yupo anaenda kwenye biashara zake anarudi jioni,, nakumbuka cku moja shangazi yangu alinipigia cm nimuelekeze kwangu anataka aje anishukuru,, mumewe amepona,, nikamwambia shangazi usijali haina haja akasema hapana nielekeze kwako nije,, nikaongea na Mahamood kwanza akaniambia sawa mwache aje,, nikamwambia shangazi kwa sasa mm naishi Salasala, akasema sawa nitakuja jumapili nikitoka kanisani, bc jumapili ilifika kweli shangazi akaja na familia yake , amefika pale kwangu hakuamini akakosa furaha akawa mnyonge sana,, watoto wake wakawa wananiuliza Dada hapa ni kwako? Nikawaambia ndio,, shangazi alishangaa mm kujifungua bila kumjulisha, nikamwambia nilikwenda Arusha kwa Kaka, bc Mahamood alionana na shangazi yangu wakafahamiana ,. Ila shangazi alishikwa na butwaa sana hakuamini Amamu mm kuishi nyumba kama ile na Mume wangu Muarabu bc tuliongea mengi akanishukuru kwa ile pesa niliyompa kumuuguzia mumewe, nikamwambia shangazi usijali sisi ni ndugu uwe na amani,, muda wao wa kuondoka uliisha wakaondoka zao
Kumbe yale maisha yangu aliyoyaona shangazi yangu hapa kwangu yalimpa maswali sana na akaingia na chuki moyoni mwake, shangazi yangu ana mtoto wake wa kike mkubwa tu, tunalingana na mm kiumri ila mm ni mkubwa kama mwaka,(anaitwa Roby) pia na yeye alikuja nyumbani kwangu na mama yake, nashangaa Roby ananipigia cm Dada naomba nije kwako nina shida na ww,, hapo sijui chochote wala sifikirii kama anaweza kunifanyia jambo baya,, nikamwambia sawa njoo,, hapo Mahamood anajiandaa kusafiri kwenda Dubai,, alikuja kwangu vzr nilitegemea labda anakuja na kuondoka kumbe amekuja kuishi nashangaa amefika na begi kubwa, nikajiuliza kulikoni? Dada wa kazi akampokea vzr akaingiza room kwao,, hee kumbe mgeni kaenda kuoga kabadilisha na nguo kabisa Sasa nguo aliyoenda kuivaa jmn bora aliyovua,, kavaa kipensi kifupii na kisingrendi tumbo lote nje,, kaja kakaa sebleni hapo sebleni nimekaa na Mume wangu,, yaan mara ashushe mguu mara apandishe juu hadi Mahamood akashindwa kukaa akaenda chumbani,, kweli sikujua lengo lake ila kwa vitendo vile tu nilijua hapa ametumwa na Mama yaje anichukulie Mume
Itaendelea

23
Wapenzi nataka kuimaliza hii story,, nitapunguza baadhi ya sehemu, nipo bize mnoo na nyinyi nazidi kuwachosha
Nikashangaa sana roby kujiachia kiasi kile tena mbele ya Mume wangu?? Mahamood hakusema chochote aliingia chumbani akalala,, nikamwambia Roby ulisema unashida na mm bc njoo tuongee, akanijibu mbona unaharaka Dada? Tutaongea tu ucjal, bc nikakaa zangu kimya sikutaka kuendelea kuongea,, usiku ulifika tukaingia kulala, Mahamood akaniambia Mamujee, unajua huyo mdogo wako alichofata hapa?? Nikawaambia bado hajaniambia ila amesema ana shida na mm,, akaniambia hana shida yeyote Zaid ya kunitaka mm na ametumwa na Mama yake,, na hajaja mikono mitupu yupo na dawa za kienyeji kwenye begi lake uwiiiii wee Mahamood umejuaje haya yote na Roby ndio kwanza amefika,,??? Au hutaki ndugu zangu waje hapa??? akaniambia Mamujee subiri kesho pakuche uende ukakague begi lake,, mhhhh haya, tukalala, ila akili yangu yote ilikuwa juu ya roby, na yale maneno aliyoniambia Mahamood,, nikajiuliza hivi Mahamood ni nani?? Ni mtu wa aina gn?? Mhhhh, nikasema ngoja pakuche nikaangalie hilo begi nijihakikishie ni kweli au,, bc palikucha vzr, Mahamood alitaka kutoka maana alikuwa kwenye maandalizi ya safari ya kwenda kwake
Nakumbuka hio cku ilikuwa cku ya kuwapeleka watoto kliniki, nikaongea na Mahamood akaniambia Dada awaandae watoto dereva atakuja kuwafata awapeleke, bc nikamwambia Dada tukawaandaa watoto fasta, Mahamood akaniambia nimwambie na Roby aende akasaidiane na Dada, then Dada mwingine abaki kwa kazi za nyumbani, bc roby hakuonyesha kukataa alijiandaa na yeye na nguo zake za uchi,, tumekaa tunamsubiri dereva afike, roby akanifata, Dada Amamu, mwambie shemeji twende wote na yeye kliniki huyo dereva asije, nikamwambia shemeji yako ana mambo mengi nyie nendeni tu, akaniambia bc sawa ila hatuchelewi, nikamwambia sawa, dereva akafika wakaondoka zao,, nikamwita Dada nikamwambia niletee begi la roby, hapo tupo na Mahamood,, tukaanza kulifungua, mhhhh sikuamini jmn, madawa kama yote tena yanamaelekezo yake,, dawa za mvuto,, matumizi,, nawia usoni asbh na jioni,, nyingine tafuna,, nyingine ya mfarakano, weka kwenye chakula na chumbani kwao yaan jmn dawa kibao, cjui shangazi ananichukia kwa nn?? Utasema sijazaliwa na Kaka yake jmn,, mbona mm siringi? Hata sikumbuki walio nifanyia? Wakipata shida nawasaidia tu?? Mahamood akaniambia c nilikwambia?? Umeamini sasa?? Nikawaambia sasa tutafanyaje na dawa ndo izo?? Akaniambia subiri,, akaingia chumbani akatoka na viunga unga navyo ni dawa,, akamwagia kwa kila dawa, kisha akamwambia Dada rudisha hilo begi na msimwambie chochote akirudi,, Mahamood akatoka zake, nikabaki na Dada, akaanza kuniambia walivyokuwa chumbani usiku Roby alikuwa anaongea sana na cm yaan kama anapokea maagizo iv,, mara ile nyingine nitafune mara ngp au kila wakati?? Yaan mambo kibao,, nikabaki mdomo wazi, shangazi, shangazi shangazi, kwann unanichukia kiasi hiko??
Waliporudi kliniki kitu cha kwanza,, shemeji yupo wapi?? Nikawaambia katoka na leo usiku anasafiri,,, hee anaenda wapi tena?? Nikawaambia Dubai,, nikamuona kapooza aliduwaa utadhani kamwagiwa maji akanyanyuka akaenda nje kuongea na cm,, alivyomaliza akaja kuniuliza tena, eti atarudi lini shemeji akiondoka leo?? Nikawaambia Roby kwan vp? Umenifuata mm hapa au shemeji yako?? Kwan akisafiri ww unapata tabu gn wakati mm nipo?? Akanijibu amna nampenda shemeji Sasa akiondoka hapa kutapooza nikamwambia ndio kutapooza sana tu kwa sababu harudi leo wala kesho,, akanyanyuka akaenda chumbani kwao akalala
Chakula kilipoiva akaamshwa aje ale alitoka kavaa dera vzr, wamekaa mezani wanakula,, Mara Mahamood anaingia tunasalimiana na Mahamood, yeye kanyanyuka kaenda chumbani kwao, ametoka kavaa kimini kifupii na kiblauz kitovu chote nje,, huku mdomoni anatafuna mzizi wake wa dawa,, akawa anamsogelea Mahamood kumpa mkono, eti shikamoo shemeji,, Mahamood akakataa mkono akamwambia nina uzu naingia kuswali akabaki hee jmn
Itaendelea

24
Cjui shangazi yangu nilimkosea kitu gani kikubwa ambacho ameshindwa kunisamehe, kadri ninavyoandika hii story ya maisha yangu ndipo nazidi kukumbuka vitu vingi sana nilivyopitia, niliishi na shangazi yangu wa damu ila kama nilikuwa naishi na mtu baki, mara nyingi usiku alikuwa ananilaza njaa eti chakula kimepikwa kidogo niwaachie watoto wale, mm ni mtu mzima naweza kuvumilia njaa bc nilikuwa nalizika tu naingia chumbani nalala wao nawaacha mezani wanakula,, asbh chai sipewi eti vitafunio vichache niwaachie watoto ,,, leo nimepata kwangu bado anaendeleza chuki juu yngu?? Niliumia sana,,, mumewe kanibaka ila hakujali wala nn ,, maisha ni safari,,,,
Tuliingia chumbani na Mume wangu, maana ucku alikuwa anasafiri sasa nikaenda kumpa haki yake habari za kwa mparange hazikuwepo kipindi hiko tena nilimuandalia vitu vyake vzr akakaa na wanae huku anawasemesha maneno utadhani labda walikuwa wanamuelewa,, bc tukiwa tunaendelea kuagana, mara bi mdogo akapiga cm kwa mumewe, kama kawaida yao wakaanza kuongea kiarabu wenyewe, mara namsikia Mahamood, naenda Dubai leo natoka Tz, mwanamke alikuwa anamuambia mumewe asiende Dubai aende tena kwake maana amekaa sn Tz, wakaanza kuzozana, Mahamood akaanza kuongea Kiswahili, akamwambia, ww ni mke wangu sawa, na Shakira nae ni mke wangu ( bi mkubwa) ana haki zote kama ulivyokuwa ww,, tena ngoja nikwambie tu, huku Tz nimeoa, na nina watoto, Sasa kuanzia Sasa naomba uelewe nitapanga ratiba iwe sawa sawa, heee bi mdogo kapaniki mbona umeoa bila kunishirikisha?? Njoo unipe taraka yangu Mahamood akamwambia kama unataka taraka bc sio lazima mm nije huko naweza hata kukutumia kwenye cm ila uwe na uhakika kweli unataka taraka,, mhhhh, bi mdogo akakata cm nikasema hii ligi itahamia kwangu jmn ,, nikamwambia Mahamood asifanye ivo, akaniambia amechoka sana ataki tena kusumbuliwa na wanawake,, akaniambia alikuwa anataka watoto, amehangaika sana na wake zake kutafuta uzazi, amepoteza pesa nyingi sana, hadi wakafikia wapandikize , ila Mahamood alikuwa hataki kupandikiza, alitaka achukue yatima hata wawili awafanye kuwa wake,, ila tatizo alikuwa bi mdogo hataki yatima anataka apandikize ndipo wakawa wanapishana na Mahamood,, yeye bi mkubwa alikuwa tyr kupokea yatima,, bc Mahamood akaniaga kuwa anaenda Dubai then atarudi tena Tanzania nikamwambia vip kwa bi mdogo c uende kwanza? Akaniambia yeye apangiwi cha kufanya, amesha panga,, mhhhh nikasema ngoja ninyamaze bc muda ulifika dereva akamfata akasepa zake
Asbh kumekucha natoka sebleni nakutana na roby kavaa kanga moja ndani ana chupi tu tena bikini,, tukasalimiana , eti ananiuliza shemeji yuko wap?? Nikawaambia kasafiri, hee mbona kimya kimya,, nikamwambia kwako ndio kimya kimya ila me mkewe kaniaga jmn, nikashangaa ananisonya, nikamwambia roby vp mbona unanisonya?? Nimekukosea nn?? Au Mume wangu kusafiri kunatatizo gn?? Akaondoka akaingia ndani,, nimekaa zangu nakunywa chai nikashangaa anashuka na mabegi yake,, eti kwa heri mm naondoka,, nikamwambia mbona gafra?? Akasema nitakuja cku nyingine,, nikamwambia sawa msalimie shangazi,, katoka hadi getini, akarudi eti naomba hela ya nauli nikapandisha juu kumchukulia hela nikampa elfu 50,, hata asante hana akasepa zake
Nikasema huyu simsemeshi ngoja aondoke na asirudi tena hapa,,
Bc tumekaa na familia yangu, hapo bado sijaanza biashara zangu,, imepita kama wiki nawasaliana na Mahamood vzr hadi bi mkubwa,, nashangaa nashika cm yangu nakutana na vitisho vya bi mdogo eti nisipo achika labda sio yeye,, nikamjibu vzr, nikamwambia pambana na Mume wako achana na mm,, nikamblok,,
Niliamua kujiongeza nilikuwa na hela kwenye akaunti yangu na zile alizonipa Kaka nikaamua nitafute kiwanja ili nijenge nyumba ya kawaida nipangishe,, nikaongea na mtu maana tyr nilikuwa nishafahamiana na watu, nikapata kiwanja, mbele kidogo na kwangu, nikaanza ujenzi wangu kimya kimya
Shangazi akanipigia cm eti Mamujee nashukuru sana, kisa pesa zako ndio umeamua kumfukuza ndugu yako ,, eti usijisahau haya maisha tu,, umesahau nilivyokutoa kijijini kukuleta mjini? Eti nisingekuwa mm huyo mwanaume ungempata vp
Itaendelea










25
Ile sim ya shangazi wala haikunistua, nilishazoea lawama mie, nilimuacha aongee hadi alivyochoka yeye akakata cm, nikatafakari yale maneno ya Mahamood, kuwa huyu ndugu yangu kaja kwangu kwa nia mbaya,, na nilivyoona zile dawa kwenye begi la roby niliamini kabisa kuwa shangazi hana nia nzuri na Maisha yangu,, nilimpigia cm Kaka yangu nikamueleza kila kitu kinachoendelea, alinishangaa sana, akaniambia Mamujee hayo yote umeyataka mwenyewe, iv hao watu kwa wema upi waliokufanyia hadi una waweka karibu yetu?? Nilikwambia tangu mwanzo achana nao,, akaniambia subiri kwanza,, akakata cm,, kumbe akampigia cm shangazi akamwambia achana na Mamujee please, ni ndugu yangu, kama umeona hakuna umuhimu wa kutupenda bc tuachee,, Kaka akanipigia cm, akaniambia shangazi akinipigia cm nisipokee, nikamwambia sawa,, niliendelea na Maisha yangu , Mahamood tulizidi kuwasiliana na alizidi kuwapenda wanae sanaa,, ilipita kama miezi miwili iv Mahamood bdo yupo Dubai kwa mke wake, alinipigia cm akaniambia ananifanyia mpango wa visa na passport ili niende huko nipeleke watoto akawatambulishe ndugu zake maana asilimia kubwa ya ndugu wa Mahamood wapo huko,, nikamwambia sawa,, ila nilikuwa muoga mnoo but sikuwa na jins lazima wanangu wapajue kwao , akaniambia nichague Dada mmoja kwa ajili ya kunisaidia watoto, namshukuru Mungu sana Dada zangu wa kazi wote nimeishi nao vzr kama ndugu zangu, yaan ukifika kwangu huwezi kumtambua Dada wa kazi ni yupi na ndugu ni yupi,, nikamchukua yule nilietoka nae Arusha kwa Kaka, tukaandaa picha kila kitu Mahamood alimuagiza mtu akawa anashuhurikia hilo jambo,, nilitafuta mlinzi wa getini kutoka kwenye kampuni ili nikiondoka niache usalama nyumbani kwangu,, nilimtaarifu Kaka yangu kuhusu safari, alinitakia kila la heri,, bc tukaendelea kusubiri vitu vikamilike ili tuondoke,,, nakumbuka siku hio nipo tu nyumbani kwangu nilikuwa nafua,, huwa nafanya kazi za nyumbani kwangu japo kuwa nina wasichana wawili, napenda sana kufanya kazi,, cm yangu ikaita kuangalia namba ngeni,, nikapokea nikasikia sauti ya mwanaume,, Halow Amamu hujambo?? Nikamsalimia vzr, nikamuuliza nani mwenzangu?? Akaniambia mm ni Baba yako mdogo nikamsikiliza,, akaniambia yupo dar amemleta mtoto wake hospital ya oshen rod anasumbuliwa na kansa, walikuwa Bugando hospital Mwanza ndipo wamepewa rufaa kuja huku,, na amepimwa amekutwa na kansa ya utumbo nikampa pole,, akaniambia anaomba akutane na mm tuongee vzr,, nikamwambia sawa ila nitakujulisha,, nilishangaa sana, nikajiuliza namba yangu kapata wapi,, nikapata jibu ni shangazi tu,, nilikumbuka kile kipigo cha mbwa mwizi alichonipiga hadi nikapoteza fahamu,, wakaniburuza hadi chumbani,, mhhhh!! Dunia hii jamani, haina mwenyewe kwa kweli,, leo hii Amamu mm najulishwa kwenye matatizo,, mhhhh,, nikasema hapa nikimwambia kaka hili Jambo, atampandia gari amfate maana ana uchungu nae sana huyu Baba mdogo, nikanyamaza zangu,, na wao pia wanamuogopa matatizo yao yote wanaleta kwangu mie mnyonge wao,, bc niliendelea kusubiri vitu vikamilike vya safari yetu,, ikaisha kama wiki mbili, sijamjulisha Baba mdogo kitu chochote wala sim sijampigia,,, Mahamood alituambia kila kitu tyr tujiandae kwa safari wiki inayofata tunaondoka, bc tukazidi kufanya maandalizi mimi na Dada, huku tunacheka wenyewe na Dada, tunaambiana huko kwa waarabu tutaenda kuongea vp na watu bc tunacheka wenyewe,, mara tunaulizana iv tukichunwa ngozi jee tunachekaa huku tunajipa moyo, bhana wee liwalo na liwe
Safari iliwadia ilibaki kama cku tatu iv,, nipo zangu kwangu napiga story na madada zangu pamoja na mlinzi,, tupo nje,, nakumbuka siku hio tulikuwa tunabishana Kati ya Diamond na Kiba nani mkali wawili wanamtetea kiba, wawili wapo kwa Mond,, yaan tuligawana, bc ikawa kelele tunabishana haswa,, gafra geti likagongwa,, mlinzi akafungua kuangalia, wakaanza kujitambulisha, maana mlinzi alikuwa mgeni,, akaniuliza niwaaingize? Wanasema ni shangazi yako,, nikamwambia waache wapite,, jamani jamani,, alikuwa shangazi,, Baba mdogo, Roby,, eti wamemleta Baba mdogo nyumbani kwangu aje akae kwa kipindi chote anachouguza mtoto wake, na niwe nampa nauli kila cku ya kutoka Salasala kwenda oshen rod na ya chakula chake na mgonjwa,, kiufupi niwahudumie,, niliwasikiliza vzr hata sikujibu kitu,, nikamwambia Dada awape chakula,, nikaingia chumbani kumlaza mtoto alilala,, nikampigia cm Kaka nikamueleza kila kitu,, akaniambia waache hapo hapo usiwaambie chochote,, Naanza safari mda huu kuja huko,, nataka nionane nao mwenyewe,, usiwaambie chochote kama mm nakuja maana watakimbia,,
Itaendelea

26
Jmn wanawake wenzangu nimepitia Coment zote leo, najua wengi wananilaumu kuwa mm nashindwa kujitetea mwenyewe,, kiufupi mm sio muongeaji sn,, tangu nikiwa mdogo najulikana na ndugu wote kuwa Amamu sio muongeaji, nimerithi kutoka kwa Mama yangu, alikuwa mpole mnoo,, ndugu wa Baba walimfanyia kila aina ya vituko lkn Mama yangu hakuwai kunyanyua mdomo,, bc nimerithi kila kitu cha Mama yangu na iv watu wanasema cha kurithi kinazidi bc naona mie nimezidi
Bc nikarudi sebleni baada ya kuongea na Kaka,, nikawakuta wageni bado wanakula,, yaan Roby ndio kamuona Mama yake ndio anazidi kufanya makusudi, mara ashike hiki mara aulize hiki yaan ilimradi tu,, Mara da Amamu nifundishe kuendesha gari kwa gari yako,, au nimpigie rafiki yangu aje kesho anifundishe,, nikamjibu usijali nitakupa,, tumekaa tunaongea namuona Baba mdogo jicho halitulii Mara kangalia huku mara kageukia huku yaan anaonekana ni mtu mwenye maswali mengi kichwani kwake,, nilikaa zangu kimya nawaangalia tu,, ucku umefika nashangaa shangazi na mwanae hata hawaagi kuondoka maana walisema wamemleta Baba mdogo?? Nikashangaa hadi saa nne bdo wapo nikamuita Dada nikamwambia akaandae chumba cha mgeni wa kiume,, hao wengine watalala nao chumbani kwao,, niliwaaga nikawaambia naingia kulala,,, shangazi akaniambia na wao watakao hapa ili asbh tuwahi hospital kwa pamoja nikamwambia sawa,, nikaingia zangu chumbani kwangu,, niliwasiliana na Mahamood kama kawaida huku alinishangaa nisibebe minguo mingi nichukue chache au nisibebe kabisa eti kwenye ndege mizigo inapimwa uzito sasa nisije acha mizigo mingine airport,, bc tuliongea mengi ila sikumwambia kuhusu ule ugeni,, nilivyomaliza kuongea nae nikampigia Kaka nijue kafika wap maana ilikuwa kama saa sita ucku IV, akaniambia ndio anaitafuta charinze,, bc nikamwambia Mungu amlinde nikalala zangu
Asbh kumekucha hata sebleni sijashuka Roby kanifata chumbani,, eti Dada fungua,, nikamuuliza vp kwani?? Eti Mama kasema muanze kujiandaa,, hata sijamjibu na mlango sikufungua nikaendelea kulala,, mara mlinzi ananipigia cm, kuna mgeni getini amejitambulisha ni Kaka yako, nikamwambia aingie, bc kaka akawa amefika kwangu tyr, nikashuka hadi chini, nilifurahi sana kumuona Kaka, akaniuliza vp huyo Baba yako mdogo yupo wp?? Nikawaambia chumbani, akasema nenda kamwambie namwita nikamwambia atatoka mda c mrefu , hadi shangazi yupo hapa,, akasema na shangazi kalala hapa?? Nikawaambia ndio,, akasema kwa sauti,, HUU UKOO MASIKINI HUU nikamwambia Kaka usiseme ivo watasikia,, akaniambia unamuogopa mtu??? Mara shangazi anashuka kwa mbwembwe mwenyewe huku anaimba ( nimeuona mkono wa Bwana nimeuona) ghafra anakutana uso kwa uso na Kaka eti Mwita umelala hapa?? Upo dar hii hii?? Yaan Mwita hajajibu hata swali moja tyr kashamuuliza kumi Mwita akamjibu nimekuja leo,, Mara Baba mdogo nae huyoo,, alivyomuona Mwita akawa mpole,, eti shangazi ananiambia mie, Amamu bado haujajiandaa, nikawaambia bado,, Kaka akauliza kwani mna safari asbh yote hii?? Akasema ndio, Obara anaumwa amelazwa oshen rod wiki ya tatu sasa amegundulika ana kansa ya utumbo,, Kaka akasema sasa Amamu ndio anahusika nn huko hospital?? Shangazi kabla hajajibu, Kaka akamwambia, shangazi iv kwa nn mnapenda sanaa kunyanyasa watu?? Huyu Amamu ana watoto wadogo bado mbaya aende huko kwenye magonjwa ya hatari hatari aje alete shida kwa watoto?? Shangazi akasema amna sio lazima aingie ndani,, Kaka akamwambia shangazi sikia,, huyu Mamujee haendi kokote,, iv we Baba mdogo unakumbuka ulivyompiga huyu Amamu kiasi cha kutaka kumtoa uhai wake?? Sasa ungemuua leo hii ungelala nyumba ya nani? Nani angekupeleka huko hospital?? Baba mdogo kimya,, akamgeukia shangazi, akamwambia shangazi naomba muachane na Amamu please, mumempitisha kwenye shida mnoo na mateso, leo Mungu amempa nafuu bado mnamfata tena? Shangazi akasema Mwita mwanangu, tusikumbushe yaliyopita tugange yajayo,, Mwita akasema yajayo ndo kumfata fata nyumbani kwake? Iv hamuoni hata aibu kuja kujazana hapa? Mnadhani mumewe Amamu atawachukuliaje? Bc walijitetea ila aibu ikawashika,, Kaka akamuuliza Baba mdogo kwani ulivyotoka nyumbani kuja hapa dar ulimtaarifu amamu kama unakuja dar?? Akasema hapana,, Sasa kwa nn unamwambia kwa kumshtukizia kuwa unakaa kwake?? Ba mdogo, kimyaa,, Kaka akawaambia hapa kwa Amamu hakai yeyote kila mtu atakaa kwake au alipofikia, kama msaada unahitajika bc niambieni mm sio Amamu,, acheni kujitia aibu,, mnajidharirisha tu,, mhhhh Kaka aliongea jmn wote kimya,, Kaka akanigeukia mm,, ww Amamu sio unapokea pokea watu tu hapa kwako, umeolewa juzi tu leo mumeo anakuta ukoo wako wote umejaa hapa c atakuzarau?? Acha huruma ya kijinga, hapa mjini kila mtu apambane na familia yake heee Kaka anaongea kihuni tu bc walikubaliana shangazi amchukue ndugu yake akae nae kama misaada tutamsaidia huko huko
Bc tulipanda gari ya Kaka hadi hospital tukamuona mgonjwa kweli hali mbaya
Kaka akasepa zake nikarudi zangu kwangu
Safari ikawadia haoo tukaondoka zetu Dubai
Itaendelea

27
Hayaaaaa mjeeeeeee tumalize
Tulifika Dubai salama salmini, tukapokelewa vzr, bonge la jumba jmn waarabu kibao humo ndani ila wafanyakazi wako wa ndani wapo wanne, wawili wa Tz, mmoja mkenya,, mwengine wa Msumbiji,, nikapewa chumba changu cha kukaa na watoto ila Dada akapelekwa kwa wenzie, mhhhh nilikuwa naogopa jmn, nikimtazama bi mkubwa alivyo na mm nilivyo vitu viwili tofauti bi mkubwa masharah! Mzuri kaumbika haswa na rangi yake tamu,, yupo soft yaan ananukia balaa , nikajitazama mm na weusi wangu huu nikasema huyu Mahamood kipo alichofata kwangu sio bure,, nyumba imejaa watu, ukitambulishwa hadi unachoka,, mtoto wa shangazi, mara huyu mjukuu wa Dada yaan ndugu kibao wote weupe,, ila nashukuru walinipokea vzr kwa kuniheshimu sana mm na wanangu, tumekaa km cku tatu iv za kuondoa uchovu, cku ya nne nikaamka zangu asbh nikaenda kusaidiana na wadada kazi,, maana nishaoga kazi jmn, kukaa bure cwez tena kwa watu ndio kabisa, nikafika uani nikaanza kazi,, wale wadada wakawa hawataki niwasaidie, eti Dada acha hizo ni kazi zetu,, yule binti yngu akawa anawaambia huyu kazoea hata kwake tunafanya nae kazi , cjui ikawaje akaniona ndugu mmoja wa mule, mbio hadi kwa bi mkubwa,, wee bi mkubwa akashuka chini, a aniita Mke mdogo,, mbona?? Kwann unafanya kazi na watu wa kazi wapo?? Hayo sio majukumu yako,, unataka Mumeo akukute hapo atulaumu sisi huku sisi hatufanyagi kazi,, kumbe hawafanyi kazi yeyote jmn hata chupi wanafuliwa mhhhh mie cwez hivo vitu aka,, bc niliacha nikaingia ndani,, niliendelea kukaa pale huku najiona kama nipo kifungoni tu, cku hio nimekaa zangu chumbani kwangu nipo peke yngu maana asbh watoto wanatolewa wanakaa huko kama kulishwa, kuogeshwa kila kitu huko mm narudishiwa watoto usiku wakiwa wamelala,, bc nipo zangu chumbani, mara hodi bi mkubwa akaingia,, akaniuliza vp mbona huna raha? Nikawaambia amna Dada nipo sawa mbona? Akasema hamna bhana sifurahii ww kuwa ivo?? Niambie bi mdogo au umemmiss Mumeo?? Nikamjibu mbona kila cku namuona tu , akaniambia unakataa tu ila mm ni mtu mzima najua umemiss Mumeo mhhhh nikamwambia Dada hapana mm nipo vzr tu ondoa hofu,, bc tukawa tunapiga story ananiambia walivyokutana na Mahamood, kumbe alichumbiwa tu bila kuonana na Mahamood, wala walikuwa hawajuani ila wazazi wa Mahamood ndio walimpenda bi mkubwa, wakamuomba aolewe na mtoto wao,, akaniambia alikuwa bikra kabisa alivyoingia kwa ndoa, tuliongea mengi sana hadi alivyomruhusu Mumewe kuoa mke wa pili alipo jiona yeye uzazi umekuwa wa shida kwake,, akasema hata Yule bi mdogo wa Uingereza kumbe bi mkubwa ndio alimtafutia Mumewe ili amuoe Akaniambia nilivyojiona uzazi umekuwa wa shida kwangu nikawaambia Mume wangu AOE ila Mume wangu alikuwa hataki hata kusikia, nilimlazimisha sana hadi kushirikisha ndugu zake ndipo akakubali kuoa ila kwa sharti mm nimtafutie huyo mke, bc nilimuahidi kumtafutia, akasema cku moja alivoenda kwenye shughuri ya Mama ake mdogo alikuwa anaozesha mwanae ndipo akakutana na bi mdogo na yeye alikuja harusini upande wa Bwana harusi,, bc bi mkubwa akampenda yule Dada, akamuomba mawasiliano wakabadilishana vzr, bc wakaanza kuwasiliana taratibu ndipo kumuuliza kama kaolewa, akamwambia hajaolewa,, ndipo bi mkubwa kumuomba aolewe na mumewe Kama bi mdogo,, ndipo yule bibi kukubali akakutaniswa na Mahamood , wakaridhiana ndipo ndoa ikafungwa,, ndipo yeye kupelekwa kuishi huko Uingereza maana Mahamood anabiashara zake huko pia na nyumba zake mbili , nilimshangaa huyu mwanamke nikasema huyu mwanamke ana moyo wa dhahabu jmn,, mhhhh, bc tuliongea mengi mnoo,, akanitania leo nitakuachia Mumeo ulale nae ingawa ni zamu yngu ila acha nikupe mdogo wangu uondoe uchovu uchangamke nikaona aibu, nikamwambia Dada hapana bhana,, bc tukatoka kwenda kula,, ucku umefika nikaingia chumbani kwangu nikaletewa wanangu, nikawalaza kwenye kitanda chao, nikaingia bafuni ili nioge nilale,, natoka bafuni mlango wangu unagongwa, kufungua Mahamood, nikamwambia vp mbona ucku, akasema amekuja kulala,, nikawaambia kivp c upo kwako?? Akasema bi mkubwa amemuomba alale kwangu wiki nzima mhhhh,, nikamwambia c zamu yake?? Akasema ndio ni zamu yake ila amekuruhusu,, Mahamood akaniambia akiwa Dubai bc ni zamu ya bi mkubwa,, akiwa Tz ni zamu yngu,, na kwa bi mdogo ivo ivo,, bc tukaenjoy kwa penzi la ugenini,, Mahamood ananiambia nilivyokumiss nilikuwa najikaza tu nitafanyaje sasa ,, bc asbh Mahamood kaenda kazini kwake,, bi mkubwa akaanza kunitania,, Leo bi mdogo umechagamka,, kumbe kweli ulimmiss Mumeo , eti c ungeniambia Dada namuomba Mahamood anifanyie massage nitoe uchovu, mm wala nisinge kunyima nikacheka sana huyu Dada ana moyo wa tofauti
Itaendelea



28
Daah hadi naona haya natamani ingekuwa wtsap nikatuma voice note nimalize,,
Nilikaa pale Dubai kwa raha sana outing kama zote kiufupi nilienjoy sana sana, wakati wa kurudi Tz uliwadia, nikaanza kujiandaa kurudi, bi mkubwa akanishauri nisikae bure nitafute kitu cha kufanya, akaniambia nikifika Tz nitafute frem nzuri ya kuuza nguo then yeye atakuwa ananifungia mizigo Dubai ananitumia Tz, kweli nilikubari wazo lake,, jion ilivyofika Mahamood alirudi bi mkubwa akamwambia kuhusu wazo la biashara, Mahamood hakubisha akamwambia tu bi mkubwa aanze kunitafutia huo mzigo coz mm nikifika Tz tu naanza kutafuta flem,, kweli nilijiona mwenye bahati mnoo wala sikuwahi kuwaza kwenye maisha yangu kama ipo siku na mm nitakuwa mtu kwenye watu , niliendelea kukaa pale nikisubiri Mahamood anashuhurikia tiket,, ila nikiwa pale nikawa sielewi,, kuna chumba maalumu ambacho hakifunguliwi ovyo,, na ikitokea kimefunguliwa bc Mahamood yupo hapo au bi mkubwa anaingia ila mara moja moja mno labda kufanya usafi,,. Mhhhh mara ya kwanza nilikuwa sijali, ila kadri nilivyozidi kukaa pale nikawa natafakari sana,, mara nyingine watu wanakuja watu wenye hela ukiwaona mwenyewe unakubali kuwa hawa watu pesa wanayo,, yaan hao watu wanakuja wakati Mahamood yupo na wakija tu wanaingia kwenye hiko chumba,,, nikajiuliza hawa watu niwakina nani?? Na humu ndani wanaenda kufanya nn?? Kweli mwanzo niliumiza kichwa sana na sina wa kumuuliza,, japokuwa mm ni mke wa Mahamood ila nilikuwa sijamzoea sana kumuuliza uliza vitu ovyo nilikuwa cwez, nikasema moyoni hapa hadi nijue humo ndani kunafanyika nn,, hiko chumba kiko chini, nyumba ni ghorofa moja ila ina vyumba vingi,, iko chumba Sasa kipo chini na mm nalala juu, kwenye hio nyumba kuna sebure mbili, juu na chini,, hio sebure ya chini kiufupi haitumiki,, inafanyiwa usafi kila cku ila hawakai wote wanakaa juu,, hiko chumba chenyewe kilichonipa hofu kipo chini pembeni mwa sebure,, nikaanza uchunguzi wangu wa kimya kimya sikumuuliza bi mkubwa wala Mahamood,, chumba changu cha juu dirisha lake linatizama geti kubwa la magari,, nikiona gari linaingia getini watu wakishuka tu, nasogea hadi karibia na ngazi nachungilia kwa chini bc nawaona hao wageni wanavyoingia kwa hiko chumba,,, nilifanya upelelezi wangu ila sikugundua kitu,, nikawa na hofu nikakosa amani najiuliza hawa ni wakina nani hasa?? Mbona wana siri zao wanazificha kwangu??
Bc safari ya kurudi Tz ilizidi kuwadia zilifika kama cku tatu safari ianze, na hapo sijajua chochote kuhusu hiko chumba,,, Waarabu wanapenda sana mambo ya kutoka out sana,, kwenda kwenye pikinik,, mara kula Ice cream, yaan wanapenda sana,,, mm tangu nifike Dubai walishanipeleka sana izo sehemu,,, nakumbuka ilikuwa cku ya jumapili,, wamejiandaa vzr wote wanataka kutoka, kasoro madada wa kazi tu,,, nilikuwa chumbani kwangu,, akatumwa mtoto aje aniambie nijiandae,,, wala sikumbishia nilijiandaa vzr nikajipodoa hasa kisha nikalala,, wakaja kuniita nikawaambia kichwa kunauma sana,,, bi mkubwa akaja hadi chumbani kwangu akaniuliza Mamujee vp? Nikawaambia Dada kichwa kinaniuma sana cwez kutoka leo,, bc akaniletea dawa akaniambia nipumzike kama kuna shida yeyote niwapigie cm,, bc nikamwambia sawa,, Mahamood akuwepo cku hio
Walivyoondoka tu nikamwita Dada yangu wa kazi,, maana kabla alikuja kuniambia kuwa kuna madada wale wa kazi, Sasa wale wawili wa Tz,, wameomba cku tukiondoka bc watupe mizigo kidogo na pesa tuwapelekee ndugu zao,, nikamwambia aniitie mmoja wao,, bc alimwita nikashuka chini maana wao wanalala nje kuna vyumba sio mule ndani,, alivyokuja nikaanza kumuuliza kuhusu kwao akanielekeza vzr nikamwambia sawa nitakwenda,, nikamuuliza kuhusu pale na watu wanavyokuja,, akaniuliza kwan hujui?? Ww c mkewe?? Kwann ajakwambia Mumeo?? Nikawaambia wala hajaniambia na mm sijaolewa mda mrefu sana,, akaniambia bc nikikwambia usimwambie hadi akwambie mwenyewe,, nikawaambia wala usijali mm shida yangu kujua tu bc
Akaniambia Mumeo ni MGANGA Tena Mganga mkubwa sana Dubai,, anatubu watu wakubwa,, Viongozi na Matajiri anafahamika sana sana heeeee Mamujee mm nimeingia wapi?? Tobaaaa,,, nikaishiwa pozi mwili wote ukaingia baridi,,, nikajiuliza kumbe mara ya kwanza nilivyokutana na Mahamood akaniambia nina nyota kali sana tena ya utajiri sikujua ana maana gn kumbe yeye ni mganga??? Hata Roby alivyokuja kwangu na dawa aliziona nilijiuliza amejuaje kama roby ana madawa kumbe ni mganga??? Hata nilivyojifungua wanangu kipindi nipo Arusha alivyokuja hakuwa na haraka ya kujua watoto jinsia gn kumbe alishawaona kwa uganga wake???
Nilikosa raha kwann amenificha hakuniambia mapema?? Nikamchukia kuanzia hapo
Vipenzi nipo bize sana nikipata mda nitaandika tena,, ila ndo ivo


29
Nilijikuta namchukia Mahamood, kwann amenificha hakuniambia mapema kama yeye ni mganga?? Nirirudi ndani nikaingia chumbani kwangu nikalala, mara wakarudi waliokwenda matembezi, bi mkubwa akaja chumbani kwangu kunijulia hali, nikawaambia naendelea vzr, bc aliniletea Ice cream na zawad nyingine,, tukatoka hadi sebleni tukawa tunapiga story,, akawa ananipa mbinu za biashara na jins ya kuliteka soko,, bc nilimsikiliza,, akazidi kuniambia jins ya kufanya biashara, kwanza nikae mwenyewe dukani hata km nitakuwa na wasaidizi,, nilimshukuru sana,, akawa anasema atawakumbuka sana mapacha wangu,, anatamani wakue awachukue akae nao, nikawaambia usijali wakikua tu atakaa nao,,
Cku iliwadia safari ya kurudi Tz ikafika,, wakati tunajiandaa kuelekea airport, Mahamood alinitazama usoni akaniambia Mamujee NAKUPENDA SANA MHHH nikajiuliza au amejua nimejua? Bc nikajiandaa fasta watoto wameandaliwa, na Dada nae, hao tukaelekea airport,,
Tumefika Tz salama kabisa, ila nikawa sina amani na Mahamood,, kwann hakuniambia?? Tulikuwa tunawasiliana vzr ila sikumwambia kuhusu uganga wake,, bc nilipumzika kama wiki mbili tu, Mahamood alikuwa ananisisitizia kuhusu flem,, nikawaambia sawa naanza kutafuta,, akaniambia niende mliman cty nikatafute flem pale ndani,, kweli niliuliza nikapewa utaratibu wa kupata pale,, nilifanikiwa kupata flem pale mliman cty,, Mahamood alinitumia pesa nikalipia,, ndio duka langu la kwanza nililofungua na lipo mpaka leo,,,
Bi mkubwa alinitumia mzigo, ulikuwa mzigo mzuri wa kutosha, nguo za watoto tu kiume na wakike,,, namshukuru Mungu sana sana ndio biashara yangu ya kwanza,,, bc nikawa na biashara yangu,, niliwasiliana na Kaka yangu nikamueleza kuhusu nyumba yangu ambayo najenga mm mwenyewe,, Kaka aliniongezea tena hela ili nimalize ujenzi,, kweli nilimaliza kila kitu na kuipangisha,, kiukweli namshukuru Mungu sana,, hata kama Mahamood anaitumia Nyota yangu bc na mm nafaidika,, nyumba ya Salasala ni jina langu kwenye hati,,, gari jina langu kwenye kadi,, duka ni jina langu,, nikasema hata ivo nashukuru
Niliendelea na biashara zangu ilipita kama miezi miwili na nusu iv Mahamood akaja Bongo,,, nilipunguza mapenzi kwake nikawa namuogopa sana,, cku hio nimekaa zangu dukani kwangu nipo na mdada mfanyakazi wangu,, Mahamood alikuja dukani,, akazunguka mle dukani kama Kuna vitu anavifanya,, nilimuoa ila nikakausha,, bc kuanzia muda huo wateja wakaanza kuingia mfululizo,, tena nikauza sana tofauti na cku zote,, nikasema hili silinyamazii lazima nimuulize,,, tulirudi nyumbani tukala, wakati tupo chumbani nikamuomba nimuulize jambo, akasema niulize mke wangu,, nikamuuliza naomba uniambie pale dukani ulikuwa unafanya nn na ulipomaliza tu wateja wakajaa dukani?? Kwanza alicheka, then akataka kukataa, nikawaambia niambie ukweli na ukinificha tu mm na ww bc hatuwezi kuwa mke na Mume then tunafichana vitu,,,, ndipo akaanza kufunguka,,, yeye ni mganga amerithi kutoka kwa marehemu Baba yake,, alikuwa hapendi kufanya hio kazi ila alilazimishwa sana,,, kumbe bi mkubwa wazazi wa mwanaume walimuona anafaa ndio wakamuolea mtoto wao,, ananiambia uganga wa Baba yake umewasaidia wengi sana. Na alivyofariki mikoba akapewa yeye,, nikawaambia sasa kwa nn umenificha?? Akaniambia angeniambia tu,, akazidi kuniambia anatibu watu wengi mnoo nikamuuliza kwahyo utajiri wako unahusiana na uganga?? Akaniambia sio asilimia kubwa,, akaniambia wao ni Matajiri sana kuanzia Babu yake akaja Baba yake Sasa amerithi yeye ,, nilimsikiliza akaniambia vitu vingi sana
Akaniambia cku ya kwanza niliyokuona niliona Nyota yako, nilitaka nikutumie tu kama wanawake wengine ila nilivyomaliza kufanya nilichofanya nikaambiwa nisikuache,, nikajiuliza nitakupataje tena?? Ndio sababu nikakupa cm na zile pesa,, ila ulivyokuwa hujanitafuta nikauliza wakubwa wangu wakaniambia kila kitu kuhusu ww,, nikawa nakufanyia dawa hadi ukawasha cm Akaniambia nimekupenda hadi wakuu wangu wamekupenda ndio sababu sijakufanya tena kinyume na maumbile ni ww tu ambaye sikufanyi hivo tena coz nakupenda sana na wakuu wangu wamekupenda,, ila bi mkubwa namfanya kinyume na maumbile pamoja na bi mdogo daaahh niliishiwa nguvu

30
ml wapenzi nimepitia comments zenu,, bi mkubwa na bi mdogo walikuwa wanaingiliwa kinyume na maumbile na Mume wao, ila sio mara zote au sio nyuma tu hata mbele kwenye njia ya uzazi walikuwa wanaitumia pia ndio sababu walitafuta watoto,, binafsi Mahamood aliniingilia kinyume mara mbili tu yaan cku mbili tofauti ila kwa kiasi gani sijui coz alikuwa ananiwekea madawa maana nilikuwa sijitambui kabisa ila nikiamka ndio najikuta nimechafuka na maumivu makali
Bc alivyoniambia vile nikashikwa na butwaa, akaniambia Mamujee NAKUPENDA SANA , ww ni mwanamke ambaye nimekupenda mm mwenyewe, nilikuona nikakufata, sio kama sijawahi kuwa na wanawake wengine kabla yako? Nilikuwa nao wengi tu ila ww nimekupenda kutoka ndani ya moyo wangu, nikawaambia sasa kwann unaendelea kuwaingilia hao wake zako kinyume?? Akaniambia wao wenyewe wamezoea wanaona kawaida tu mhhhh nikaziacha hizo habari maana nilikuwa naona kama naumiza moyo wangu nikikumbuka alivyoniingilia na mm
Akaniuliza Mamujee mbona unafanya vitu vyako kimya kimya na hunishirikishi mm?? Mhhh nikashangaa nikamuuliza vitu gn? Akaniambia ww mwenyewe unajua ni vitu gn unavifanya,, nikamwambia niambie ni vitu gn bhana,, akaniambia mbona umejenga nyumba bila kunishirikisha?? Mhhh, nikamwambia kweli Kaka yangu alinipa hela kwa mara ya kwanza nilivyokutana nae ndio nikanunua kiwanja na kujibana ndio nikajenga, akasema wala sikulaumu kujenga,, ni vzr na una akili nzuri, tatizo kwa nn umenificha?? Nikamwambia nilitaka nije nikwambie, bc akanyamaza, kiufupi Mahamood ni mtu muelewa sana,, kuhusu uganga wake ulizidi kunipa mashaka sana, niliogopa sana, kiufupi siwapendi waganga wa kienyeji nawaona kama wachawi tu,
Maisha yaliendelea huku nipo bize na biashara yangu, Mahamood nae yupo bize na biashara zake,, akiwa huku Tz hafanyi uganga wake,, Mahamood alikaa sana Tz kama miezi minne iv, mzigo dukani kwangu ukapungua, nikamuagiza tena bi mkubwa akanitumia, mawasiliano yangu na bi mkubwa yalizidi kuongezeka, tukatoka kwenye uke wenza tukawa marafiki wakubwa tu, bi mdogo akazidi kumsumbua mumewe anataka taraka,, Mahamood akaniambia Mamujee ngoja niende kwa bi mdogo nikampe taraka yake nikamwambia sababu nn ya kumpa taraka?? Akasema sitaki kupangiwa maisha, mhhh nikayaacha km yalivyo,, wakati Mahamood anajiandaa kusafiri,, nilipatwa homa kali sana, nikapimwa nikagundulika mjamzito,, hapo mapacha wangu wana miaka miwili kama na nusu iv,,. Mahamood alifurahi mapenzi yakazidi kwangu,, akajisahau kabisa kama ana wanawake wengine,, safari ya kwa bi mdogo iliwadia akaondoka zake,, mimba ilinisumbua sana tofauti na mimba ya mapacha, nikawa mtu wa kulala ndani tu,, dukani ikanibidi niongeze mtu mwingine,, nashukuru Mungu nilipata watu waaminifu sana,,, bc Mahamood alifika kwa bi mdogo akamwambia umetaka taraka nimekuja kukupa, bi mdogo akaanza kulia akimlaumu Mahamood kuwa yeye ndio chanzo cha yeye kuomba taraka,, hata ivo hataki taraka bado anampenda mumewe , bc waliyazungumza wao wakasameheana ,, Mahamood alikuwa ananipa taarifa zote za huko,, bi mdogo akakubali Mamujee kuwa mke mwenzie na kuniachia cheo cha bi mdogo
Bi mdogo alinipigia cm tukaongea akanikaribisha nyumbani kwake kwanza then yeye ndio aje kwangu,, tuliongea vzr, ila kuhusu mimba yangu hakuwa anajua chochote
Kiufupi mm sikuwa na shida na yeyote yule wote nilikuwa nawaona sawa, Mahamood hakukaa sana kwa bi mdogo alikaa kama wiki tatu tu akarudi Tz,, akakaa kwangu hadi mimba yngu ikafika miezi sita,, ile hali ikamkasirisha bi mkubwa,, nikashangaa tu nikimpigia cm hapokei, nikimtumia msg hajibu kwa wakati,, sikumwambia Mahamood kama bi mkubwa hapokei cm zangu, nikaanza kupata nafuu kidogo kidogo,, nikaongea na Mahamood nikamwambia nipo sawa Sasa aende kwake,, Mahamood akawa hataki kabisa kuniacha,, nakumbuka siku hio karudi zake nyumbani vzr,, nikakaa nae chini nikaongea nae kwa hekima,, nikamwambia Mume wangu,, ukumbuke ww una wanawake watatu,, sio Mamujee peke yake,, Sasa hao wanawake wengine nao wanakuhitaji nenda kawape haki zao,, nilimbembeleza sana mwisho akakubali kwenda Dubai,, akaniambia ila hatokaa sana,, nikamwambia hapana nenda kakae na mkeo

31
Mahamood aliondoka zake kwenda kwake, nikabaki mwenyewe najiuguza huku nikisaidiwa na madada zangu wa kazi, hali yangu iliendelea vzr, ilipita kama wiki tangu Mahamood aondoke ila tulikuwa tunawasiliana mara kwa mara, nikashangaa napigiwa cm na bi mkubwa, nikajiuliza kulikoni tena? Maana yeye CM zangu alikuwa hapokei, nikapokea vzr nikamsalimia wala sikuwa na shida, akaniitia Mama wawili, eti ww mjamzito?? Nikawaambia ndio Dada, akaniambia sasa kwa nn umenificha?? Nikawaambia Dada nilimuachia Mahamood akwambie mwenyewe kwan hakukwambia?? Akaniambia wala hakuniambia,, Sasa kwa nn umenificha mdogo wangu?? Mm nakulaumu kwa kosa la kuruhusu Mume wetu akae kwako mda mrefu, kumbe upo na shida? Bc nisamehe sana mdogo wangu, sikujua kama mjamzito na inakusumbua kiasi hicho, nikawaambia Dada usijali, nisamehe na mm kwa kukosa kukwambia mapema, akaniambia Mamujee huyu mwanaume ni Mume wetu wote, ukiona anafanya kitu cha kumuonea mwingine inabidi uikemee hio hali, usiiache ikakomaa, tumekubali wote kuwa wake wenza, bc tupendane tuishi kwa kupendana, ungeniambia mapema kama ni mjamzito wala nisinge kulaumu,, bc tuliongea mengi na Dada tukasameheana,
Nilipigiwa cm na shangazi kunipa taarifa za msiba, yule mgonjwa mtoto wa Baba mdogo amefariki, nikampigia Kaka kumpa taarifa kumbe na yeye tyr amazipata, msiba utasafirishwa kupelekwa nyumbani Musoma, bc nikamwambia kaka hali yangu ya afya tukakubaliana Kaka ndio ataenda mm nipumzike, bc nikawa nipo tu nyumbani kwangu,. Shangazi akawa anapiga cm kama ugomvi, we Amamu kwann huji msibani? Maana msiba waliweka nyumbani kwake kwanza taratibu za kusafirishwa zikiendelea, nikamwambia shangazi mm naumwa, bc kama nilimchokoza, unaumwa? Kuumwa ndio kukufanye usije msibani?? Nyie watoto mnaringa sana, mnajiona mmefanikiwa ndio mmekuwa na dharau, Sasa itajulikana tu, kwanza nyie sio damu yetu ingekuwa damu yetu bc mngekuwa mnatusikiliza na kutuheshimu,, shangazi aliongea hadi alichoka,, cm ilivyokata nikampigia Kaka nikamueleza, Kaka akaniambia Mamujee tulia niachie mm, mm nakuja huko leo, nikawaambia mbona mda umeenda sana utaanza safari usiku? Akasema atakuja kwa ndege,. Bc nikamsubiri Kaka aje ili tujadiriane tunafanyaje, nikampigia cm Mume wangu kumpa taarifa za msiba, alinipa pole akaniambia atanitumia pesa ya mchango ila mm nisiende popote,,
Kaka alifika alikuja moja kwa moja nyumbani kwangu, tukakubaliana yeye ataenda hadi Musoma, bc nikamwambia awahi kwenda msibani maana shangazi asizidishe lawama zake, Kaka alienda, shangazi alipomuona Kaka akapumua maana alichanganyikiwa kuhusu msiba ila alitaka huzuni zake azilete kwangu, nikajulishwa kuhusu mchango, wakati huo Mahamood alikuwa tyr amenitumia na mm nikatuma mchango wangu, walisafirisha msiba hadi nyumbani, wakazika vzr, Kaka alinipigia na kunipa wazo la kuwajengea wazazi wetu makaburi nikamwambia kaka sawa, ngoja nikutumie hela, Kaka akaniambia ni vzr na ww utoe hela ili wazazi wetu huko walipo waone tunawathamini, bc nilimtumia Kaka hela na yeye akatoka yake tukawajengea wazazi wetu , makaburi ya wazazi wetu yapo karibu,, tulimshukuru Mungu kutupa uwezo na akili ya kuwakumbuka wazazi japokuwa wametangulia mbele za haki,,
Biashara yangu iliendelea vzr mauzo yakawa makubwa cjui Mahamood alifanya kitu gn jmn ila nikazidi kumshukuru Mungu, na watu niliowaweka dukani walikuwa waaminifu kwa kiasi furani
Mimba yangu ilipofika miezi 8 hapo bado Mahamood yupo Dubai, Mahamood alinipigia cm akaniambia bi mkubwa anakuja kwangu kunihudumia hadi nijifungue, nikashukuru nikamwambia sawa, bc bi mkubwa nae akaniambia kuhusu safari yake, ila ananifungia mizigo kabisa anaanza kuusafirisha, bc tukakubaliana ivo,, kweli nilipokea mzigo wangu, wiki iliyofata bi mkubwa akaingia Tz, nilienda kumpokea airport na mimba yangu, aisee bi mkubwa alifurahi kuniona mie mjamzito, tulikumbatiana pale safari ya nyumbani ikaanza tuliongea mengi maana bi mkubwa hakutaka kabisa kulala chumba cha wageni tulilala pamoja, mtoto tumboni akicheza bc anashika tumbo langu anafurahi mwenyewe ananiambia cku akipata mimba bc Dubai nzima itajua ilikuwa raha sana bi mkubwa alivyo kuja kwangu, akanipa wazo la biashara lingine, akaniambia Mama wawili, iv unaonaje hapa kwako ukajenga fremu? Then ukawa unauza vitu vya umeme kutoka Dubai?? TV, friji, brenda NK? Nikawaambia Dada wazo zuri, akaniambia bc lifanyie kazi, hata sikuchelewa nikawaita mafundi wakaanza kunijengea fremu
Itaendelea

33
Shangazi yangu mkorofi sana namjua vzr ananitafutia sababu na hii mimba niliyonayo sijui yukoje anafahamu fika mm na Roby hatuwezi kukaa pamoja hata nusu saa ila ameamua kumuacha nyumbani kwangu wala hafikilii kuhusu hali yangu, niliwatizama mtu na mama yake wanaenda kusengenya tena nyumbani kwangu
Roby akarudi baada ya kuachana na mama yake, akaanza kunikejeri vp da Amamu unaenda kuzalia wp Ulaya au Buza? Nikaishia kumtazama tu, nikamwita Dada wa kazi aniletee matunda nile maana kula yangu ilikuwa ya tabu sana akarukia yeye mletee ale si unajua tena mke wa muarabu anatakiwa ale ashibe huko leba si mchezo kuwekwa mitambara?? Nikamwambia Roby naomba tuheshimiane kama umekuja nyumbani kwangu kwa heri bc ukae kwa heri ila kama umekuja na yako yatakurudia mwenyewe
Bhana eee kwani uongo? Si mnafirwa nyie? Nani asiyejua kama waarabu wafiraji?? Nikamwambia ndio kwani nikifirwa mkundu si wangu? Ww kinakuwasha nn?? Kama kufirwa kunalipa na ww c ukafirwe kwan mkundu huna? Nilimjibu wala sikumkawiza sikujali hata kama Dada yangu wa kazi anatuangalia
Eti bana ee mm ndio nishakuja kwako hata ukichukia sitoki ww ulivyokuwa unakaa kwetu? Malipo ndo haya shoo kama hupendi kunya huyo mtoto atoke
Dada yangu wa kazi akaniambia Dada acha usijiumize
Basi roho iliniuma yaan natukanwa nyumbani kwangu? Nikanyanyuka nikamuacha Roby nikaenda chumbani nikamkuta bi mkubwa amelala na watoto nikatoka tena nikashuka chini nikaenda nje kwa mafundi waliokuwa wananijengea frem nikakaa kimya
Nimekaa nje na mafundi wao wanajenga mie nawaangalia vp Dada mbona kama una mawazo sana? Hapana nimetoka kupunga upepo tu bc tukawa tunapiga story na mafundi
Bi mkubwa alitoka alikuwa akinitafuta akanikuta nipo na mafundi, Mama Wawili mbona huko huku? Nikamwambia nipo tu nimeona wote mmelala nikaona nisiwasumbue,
Tulirudi ndani tukaenda kukaa sebleni mara Dada wa kazi akaniletea yale matunda niliomuagiza, tupo sebleni na Roby nae akaja sijui alitoka kuoga maana alikuwa kabadilisha nguo kavaa kikaptura kifupi vile vinaitwa vikumanina nadhani mnavipata kavaa na kitop tumo lote wazi, kaona nipo na mtu na hamjui ila hata salamu hajampa kafika katukuta tunaangalia mieleka kaja nilipokaa kachukua limoti kabadilisha kaweka miziki
Nilibaki namuangalia, Bi mkubwa akaniuliza huyu ndugu yako? Nikamwambia ndio ni mtoto wa shangazi yangu bi mkubwa aliguna tu mhhh
Jioni nikiwa nimejilaza kwenye kochi nipo na huyo Roby alikuwa bize na cm yake bi mkubwa yupo juu anawapa chakula cha usiku watoto mara cm yangu ikaita kuangalia ni bi mdogo wa kati nikasema mama mama mama nafwa na hivi kapewa taraka moja mbona hasira zake zote juu yangu mie Mamujee? Niliogopa kupokea ila nikasema ngoja nipokee tu sina jinsi halow habari za mida? Nikaduwaa maana kanisalimia kwa heshima na utulivu, nikamjibu salama Dada,, mdogo wangu nisamehe sana kwa nilivyokwambia mara ya kwanza nikamwambia haina shida Dada wala usiombe msamaha mm sina tatizo na ww, Sawa Mamujee ila nataka nikuambie jambo ila uniambie kama utakuwa na kifua? mhhh nikamwambia Dada kama unahofu na mie bc usiniambie ila mie sina shida, haya ngoja nikwambie huyo mke mwenzio hapo hakuja kwa bahati mbaya usione amekuja huko ukadhani kweli unapendwa kaja kukuuguza huyo mwenzio kafata huyo mtoto akishirikiana na mumeo lengo lao ni KAFARA na damu ya Mahamod ndio inatakiwa itoe alitakiwa atoe hio kafara mda tu kwa hao mapacha ila Mumeo alikataa kwa sababh hana watoto wengine ila ulivyopata ujauzito ndio wameamua wamtoe huyo wa tumboni na huyo mke mkubwa yupo kusubiri mtoto,,,, nimeamua nikaambiwa ukweli si wamejifanya kunipanda kichwani wameshauriana nipewe taraka sasa nimekwambia ukweli akili kichwani mwako ukimtaka mtoto huyo bc nenda kajifungulie kwenu huyo mke mwenzio sio mtu mzuri pamoja na huyo mumeo
Daaahhh nilichoka hapo Roby ananitazama usoni nilivyokuwa naongea na cm
Itaendelea


34
Yale maneno ya mke mwenzangu yalinifanya nitafakari anayosema ni kweli au ameamua kugombanisha sababu kapewa taraka? Nikazidi kuchanganyikiwa mbona kama asemacho ni kweli mbona adui zangu wanazidi kuongezeka Mamujee mm? Nilibaki na bumbuwazi sijui nifanye nn? Nimuamini mke mdogo wa Mahamod? Au nimuamini Mahamod kwa kumleta mkewe nyumbani kwangu anisaidie kazi? Nilipooza nikawa mnyonge sana huku shangazi na mwanae sijui wanapanga nn juu yangu? Huku nako naambiwa haya?
Sikuongea chochote maana Roby alikuwa ananiangalia kama anataka kujua nimeongea na nani na nimeongea nn
Nikaanza kupata wasiwasi cjui ulitokea wapi ila nilipata hofu sana
Roby alikaa kwangu kama siku tatu iv akaniaga anaondoka nikamwambia sawa wasalimie sikumpa hata mia
Aliondoka zake nikabaki napambana na maisha yangu,, bi mkubwa sikumwambia chochote kuhusu ile cm ya mke mwenzetu nilikaa kimya
Maisha yakaendelea hatimae mimba ilifika miez tisa na ujifunguaji wangu ni Opp nikaandikiwa cku ya kufanyiwa opp bc nilikaa kujiandaa ila nipo nimechanganyikiwa nafikilia maneno ya bi mdogo bado yapo kichwani hata nijisaulishe vp ila hayatoki,,,, mume wangu ananipigia cm kunitia moyo maana presha ndio lilikuwa tatizo kwangu inapanda mara kwa mara nilitamani nipate mtu wa kumuhadisia yale maneno ila sikumpata nimwambie nani? Kaka yangu? Hapana sina uhakika nayo kama sio ya kweli huoni nitakuwa nimeweka doa kwa kaka yangu juu ya Mahamod?? Cjui nimwambie nani matatizo yangu sina Wazazi hata shangazi yangu simuamini yeye ndio yupo tayari kufurahia kifo changu
Nikapata wazo ngoja nimuhadisie Dada yangu wa kazi yeye nipo nae kwa mda mrefu ananifahamu vzr na anawafahamu vzr wakina Mahamod nilishaenda nae Dubai
Zilibaki kama wiki mbili ndio tarehe yangu ya Opp nilimuaga bi mkubwa kama nanyoosha miguu kidogo nafanya mazoezi, huwezi kufanya mazoezi kipindi hiki huoni unajitafutia matatizo Mamujee?? Bi mkubwa alikuwa ana wasiwasi na hali yangu, nikamwambia siendi mbali nanyoosha miguu tu pia sitakuwa peke yangu naenda na Dada, bc aliruhusu ila kishingo upande nikamwita Dada nikamwambia twende tukafanye mazoezi
Tukiwa njiani na Dada nikaanza kumsimulia yale maneno niliyoambiwa na bi mdogo, Dada akaniambia Dada Mamujee usikatae wala simuamini Mwanadamu yule unaemuamini ndio huyo ana kuhumiza? Aisee Dada wa kazi alinipa kauli ambayo ilinifanya niamini kuwa inawezekana bi mkubwa na mumewe hawana nia nzuri na mm na hivi Mahamod ni mganga na chumba chake cha Uganga haruhusiwi kuingia mtu yeyote zaidi ya Mahamod mwenyewe na bi mkubwa tu
Nikamuuliza Dada sasa mm nifanyaje? Akaniambia nenda kwenu kama ulivyoambiwa,, mhh kwetu wapi? Inamaana niende Musoma? Kwa nani yule Baba mdogo aliyeshirikiana na mkewe kunipiga hadi kunusurika kifo?? Nilijiuliza mwenyewe baada ya Dada yangu wa kazi kunambia niende kwetu,, nikawaza au niende tena kwa Kaka Arusha nikajifungue huko kama hawa mapacha?? Lkn kaka namwambia nn? Hata ivo kaka mwenyewe hata mke hana kila cku kunibadirishia wanawake tu mara waje wanipe makesi yao niwasuruhishe yaan ni shida tu
Bc nikasema liwalo na liwe nitakaa hapa hapa nione
Nilirudi nyumbani na Dada nikamkuta bi mkubwa ana wasiwasi kweli vp mbona mmechelewa nilijua umepata shida bado kidogo nikupigie cm kumbe cm hukubeba? Nikamwambia Dada ondoka shaka nipo sawa
Cku zilikimbia hatimae cku ya kujifungua ilifika nikapelekwa hospital nikalazwa ili kesho yake nifanyiwe opp nikiwa pale hospital nikaanza kuota mandoto ya ajabu ajabu mara nimejifungua mtoto kafa mara mtoto wangu kaibiwa
Usiku presha ikapanda sana nikapewa vidonge Dactar akaniambia Mamujee acha kupaniki relax, nikamwambia docta mbona najiona nipo sawa? Akaniambia presha ipo juu sana so jitahidi kutoa mawazo, bc asbh palikucha kabla sijaingia kwenye chumba cha Opp nimeingia kwenye vipimo mapigo ya mtoto hayaonekani nikawaisha kwenye operation presha bado ipo juu ikabidi nipewe vidonge kwanza operation isubiri presha ishuke, badala ya saa 4 asbh nimekuja kufanyiwa opp saa kumi jioni,,, nimekuja kupata fahamu nipo wodini kitu cha kwanza nikaomba mtoto nikaambiwa subiri upate nguvu nimekaa mtoto sipewi jmn mwisho nikaamua kuuliza mtoto wangu yuko wapi? Nimekuja kupewa jibu usiku kwamba mtoto wangu amefariki
Itaendelea


35
Mtoto wangu alizaliwa amekufa alikuwa ni mtoto wa kike iliniuma sn nikakumbuka yale maneno ya bi mdogo ndio yalizidi kuniumiza nilikaa hospital kwa muda wa siku tatu then nikarudi nyumbani tatizo la presha halikuniacha likazidi kunisumbua but sio kama wakati wa ujauzito, nilikosa amani nukimfikiria mtoto wangu kwann amekufa??
Bi mkubwa hakukaa sana tangu nimejifungua alihakikisha nipo vzr bc akaanza maandalizi ya safari kurudi nyumbani kwake
Muda mwingi Mahamod alikuwa akinipigia cm kunitia moyo sikutaka kumwambia chochote kama mke wake mdogo ameniambia kuhusu wao na mtoto wangu,,, bi mkubwa alisafiri kurudi nyumbani kwake nikabaki na familia yangu zilipita kama cku tatu tangu bi mkubwa aondoke bi mdogo wa kati alinipigia cm kunipa pole na kuniambia si nilikwambia Mamujee? Mbona hukunisikiza? Nilikwambia nenda kajifungulie nyumbani kwenu? Ona sasa umepoteza mtoto wako? Nikamwambia sawa ila kama binadamu ndio amenifanyia haya bc Mungu atamlipa ila kama ni kazi ya Mungu bc acha nishukuru akaniambia nakutumia hela ya pole ndugu yangu ila ipo cku nitakuja Tz ngoja tumalize mgogoro na Mume wangu nikamwambia nashukuru sn
Maisha yangu yaliendelea nikapata nguvu nikapona kabisa nikarudi kwenye mishe zangu watoto wangu wawili walifika miaka miwili na nusu nikaamua kuwapeleka shule
Nikajikita san kwenye kufanya biashara zangu bi mkubwa bado alikuwa ananigizia mzigo kutoka huko kwao nikaona nifungue duka lingine la nguo
Nikaongea na Mahamod aniongezee pesa nataka kufungua duka la nguo jumla na rejareja bc hakusita sana akaniambia subiri
Bc pale nyumbani kwangu zile fremu ziliisha nikaamua niweke duka la vyakula (Duka laMangi) kwakuwa nilikuwa na wasichana wa kazi wawili bc mmoja nikamuweka dukani hapo nje mmoja akabaki ndani na watoto wanashinda shule,,,, wasichana wangu nilikuwa naishi nao kama ndugu niliwafanya kuwa ndugu zangu na walikuwa waaminifu sana hata ukisahau pesa bc utaikuta
Niliamua nizidi kupambana nijisimamie mwenyewe kuhusu kuzaa niache kwanza
Mume wangu alinitumia pesa ya kuongeza mtaji wangu hapo ndio nikafungua duka kariakoo na mzigo wangu wa kwanza wa hapa dukani kwangu nilichukulia China, nakumbuka hii safari nilisafiri kimya kimya bila ya kumuaga Mume wangu nilifika china nikakaa kama wiki mbili nikarudi Tz niliwaaga wasichana wangu wa kazi wa nyumbani kwangu tu
Lkn nikiwa China Mahamod alinitumia msg Whtsp ukirudi huko ulipo utaniambia nije Tanzania nione watoto nilishangaa nikasema amejuaje kama mm sipo Tz?
Nilirudi Tz nikapumzika kama wiki nikaanza biashara kariakoo sikumtafuta Mahamod nikawa niko bize nashukuru Mungu nilianza biashara kariakoo kipindi sikukuu zinakalibia na nilikuwa na mzigo wa kutosha nauza jumla na rejareja biashara ikapamba moto
Mahamod alinipigia cm anataka kuja Tanzania nikamwambia sawa bc niliendelea na maisha yangu
Mahamod alifika Tz, alifurahi na watoto wake nilijiwahi nikenda kuweka vijiti vya uzazi wa mpango sikutaka kuzaa na Mahamod tena kila nikikumbuka nilivyoteseka na mimba then mwanangu kufariki nilikuwa nachukia kuzaa na Mahamod
Mahamod aliniuliza kwann umeenda China bila ruhusa yake? Nikamwambia nilifata mzigo wa biashara bc alikasirika akafoka kwamba kuniacha nifanye biashara kusinipe kiburi anauwezo wa kuniachisha hio biashara nikakaa nyumbani,, nikamwambia nisamehe Mume wangu bc alikubali yakaisha tulienda nae hadi kariakoo akaona biashara
Itaendelea
Mamujee
Furaha naomba nijibu baadhi ya comment, maana story yangu nakaribia kumaliza,, kuna watu wanacoment eti sina marinda, ni kweli kabisa ndio sababu nimeleta kisa mjifunze wengine, maana kuna baadhi ya wasichana wanavunja utu wao kwa makusudi kuingiliwa kinyume na maumbile bila ya kupata chochote, then wapo wengine wanadhani hii story ni ya kutungwa, wapenzi hii ni true story tena ni yangu mm mwenyewe, maisha yangu niliyopitia hadi sasa nilipo, leo ukiniona natembelea gari nzuri naishi nyumba nzuri unaweza ukatamani maisha yangu ila nilipotoka huwezi kupita,, then kuna mtu amecoment kuwa kwann naandika kwamba akanipeleka hadi kwenye hard yake ya magari?? Naandika ivo ili watu wote wanielewe maana uwelewa tumetofautiana, ningeweza kuandika TU akanipeleka kwenye hard yake,,, haya maisha nimepitia mm Amamu,, ni kama past tu, ila kwa Sasa nina maisha tofauti kabisa, wengi hawajui nilipotoka ila wakiniona naendesha prado wananiona mchawi tutaendelea tulipo ishia kesho

MWISHO S01/ S02 SOON
 
(36-41)
36

SEASON TWO,
Wapenzi wasomaji pole nimewachelewesha sana kupata msimu wa pili, nilikuwa naumwa kwa kipindi kirefu ila sasa alhamdulillah namshukuru Mungu naenderea vizuri.

Tuendelee
Mimi na Mahamood tuliendelea kuishi kwa kipindi kirefu huku akionekana hataki kwenda kwa wake zake wengine, ikafika kama miezi 3 nikamuomba aende kwa sababu sikutaka ugomvi mimi na wake wenza ambao walikuwa wamenitangulia, akasema hatokwenda ndio nikamuuliza kwanini
Mahamood aliniambia kwamba hataki kwenda kwa sababu kuna masharti mke mkubwa ameweza kuyavunua hivyo ingeweza kuleta matatizo kati yake na mizimu kwa sababu alikuwa amewakosea

Nikamuuliza kwanini unanificha mambo yako, si uniambie ni masharti gani hayo? Akasema mke mkubwa kaamua kushika mimba bila ridhaa yake wakati masharti kipindi anamuoa basi alikuwa anatakiwa asizae na mwanamke huyo.

Nilishangaa nikamuuliza kwa hiyo alivyokuwa ananiambia kwamba hana uzazi ilikuwa ni uongo? Akasema ndiyo ni masharti

Kwa hiyo mbona mimi ulinizalisha watoto akasema haikuwa kwenye mpango wake kuzaa lakini nilipokataa asiniingilie kinyume basi ilitokea kwa bahati mbaya na hata alivyojaribu kuongea na mizimu aliambiwa mimi ni mwanamke mwenye nyota kali hivyo asiniache kabisa

Kwa hiyo mkeo huyo utaacha kumfuata? Akaniambia ili aende lazima huyo mwanamke atoe kwanza hiyo mimba maana akienda kule na mwanamke yule ana mimba basi atapata matatizo makubwa sana.

Nilishangaa mno na niliogopa nikasema ile ni familia ya aina gani mbona ina mambo magumu kiasi hicho? Ghafla tukiwa tunaongea, mke mdogo wa kati ya bi Fatima ambaye alikuwa anaishi Uingereza, alimpigia simu Mahamood.

Mahamood akasema huyu vipi ananisumbua, anataka kuniambia nini? Mimi nilikaa kimya sikuongea lakini Mahamood alipokea simu na kuongea naye.
Walianza kuongea kiswahili kilichochanganyika na kiarabu na kiingereza humo humo, mwanamke akasema "Mahamood tafadhali nahitaji taraka yangu sasa, nimechoka kupoteza muda duniani
Mahamood akamuuliza kwanini mnanitesa hivi nyie wake zangu? Yaani hamniachi nipumue muda wote visa tu? Mbona huyu mdogo yeye hana mambo mengi

Huyo si ni mwafrika ni maskini unadhani ataweza kukuacha wakati una hela? Mimi nnahitaji talaka yangu nataka nikaanze maisha yangu nimechoka maisha ya kuishi miezi mitano bila mum
Maneno ya kwamba mimi mwafrika nina maisha magumu siwezi muacha yaliniuma, nikajikuta nalengwa na machozi.

Mahamood alinitazama machoni, alipogundua natokwa na machozi akakata simu na kuniwekea mkono begani akaniambia "mke wangu nakupenda sana, na ndio maana niliondoka Dubai badala niende uingereza nikaja kwako ni kwa sababu wewe ni mke bora" niliendelea kulia

Najua maneno ya Fatima yamekuudhi lakini naomba usilie piga moyo konde kumbuka tulipotoka
"Ameniita mimi maskini? Nilisema kwa uchungu huku kilio kikiongezeka"

Kwa hasira, Mahamood aliinuka akaenda chumbani na kutoka akiwa na kalamu na karatasi, akaanza kuandika talaka ya yule mwanamke, halafu akaipiga picha.

Nikamuuliza unafanya nini akasema anamtumia kweli talaka maana si kaitaka nikajaribu kumkataza lakini alimtumia kupitia whatsapp huku ikisindikizwa na voice note kwamba original copy atampelekea wiki inayofuata akiwa anaelekea uingereza kuzifuatilia biashara zake

37
Ilikuwa kama masikhara lakini pale ndiyo talaka ilikuwa imeshatoka hivyo, akaniambia Mamujee nafanya hivi kwa sababu nataka uishi kwa amani sipendi mtu yeyote akuudhi wewe, napenda muda wote uwe na furaha sawa mke wangu

Sawa, ila usichukue maamuzi ya haraka sana nilisema akasema ni muda mrefu alikuwa akitamani kumuacha huyo mwanamke mwenye kiherehere

Basi tukawa tumeishia pale, sasa siku ziliposogea Mahamood aliniaga kwamba anaenda Uingereza ili akaziweke biashara zake vizuri maana yule hakuwa mke wake tena hivyo alihisi anaweza akamfilisi.

Mahamood alijiandaa akaondoka kuelekea Uingereza, sasa, akaniacha peke yangu nalea watoto pamoja na kuendeleza biashara zangu.

Cha kushangaza mawasiliano yangu mimi na Mahamood yalikosekana tangu alipokuwa ameondoka na kuelekea uingereza, zaidi ya miezi miwili nikawa simpati na hakuwahi kunitafuta

Nilipata wasiwasi sana kuhusiana na yule mwanaume, nikajiuliza au alifariki au amekumbwa na nini kwa huyo mke Fatima wa uingereza, sikupata jibu

Namba ya Fatima niliyokuwa naijua ilikuwa haipatikani kipindi chote, na hata mke mkubwa ambaye ni Shakira alikuwa hajibu message zangu kabisa kila nilipomtumia message alinipiga blue tick na kuendelea na maisha.

Nilijua dhahiri kuna tatizo kubwa limetokea ila sikuwa na cha kufanta, ndiyo ikabidi nimshirikishe dada wa kazi akaniambia kwamba ni heri nifunge safari niende Dubai kule nyumbani nikaone kinachoendelea.
Niliona ni wazo zuri hivyo nikamuuliza kaka yangu Mwita akaniambia niende nikajue kilichotokea, kwa kuwa nilikuwa napafahamu Dubai nilianza kujiandaa na safari kwa kukata tiketi na kuandaa vitu vyote vinavyohusika.

Ikiwa ni siku moja tu imebaki ili nisafiri, nilienda dukani nikafanya kazi tangu asubuhi mpaka jioni muda wa saa kumi na mbili na nusu nikasema niondoke nikajiandae ili kesho tuondoke.

Nilipofika nyumbani nilimkuta dada wa kazi akiwa anafundisha watoto sebuleni, mahesabu hesabu na kadhalika, nikawashika mikono kwa furaha nashangaa wananiambia
"Daddy daddy" mi najiuliza Daddy kafanya nini ndipo dada wa kazi akasema Mahamood amekuja yupo ndani, nilishtuka na kudhani ni masihara, nikaondoka haraka kuelekea chumbani kumuona Mahamood

Nilipofika nilishangaa kumuona Mahamood kalala kitandani kifua wazi, macho yake yanatazama juu darini, huku yakiwa yamejawa na machozi anaonekena mwenye huzuni kubwa moyoni mwake, kilichonishtua zaidi ni namna ambavyo Mahamood alikuwa amekonda yaani mwili wake umedhoofika sana ni mifupa tupu ilikuwa imeshabaki ikifunikwa na ngozi, nikaogopa kwanza
ITAENDELEA

38
Mume wangu! Niliita kwa mshangao mkubwa maana sikutarajia, nilikuwa nimesimama sehemu moja nimeigwa butwaa
Mahamood, niliita tena ndipo akageuka huku akifuta machozi, akanitazama na kusema "uko salama mke wangu?"

"Ndiyo" nilisema huku nikisogea na kuketi kitandani namtazama hata siamini "kuna tatizo gani?" Nilimuuliza "unaumwa?"

Akatikisa kichwa kumaanisha haumwi, nikamuuliza mbona umekonda sana halafu pia unalia, kuna tatizo gani niambie"
Nimepitia mengi sana magumu mke wangu, naomba umisamehe sijakutafuta kwa kipindi chote hiki, ndipo na mimi nikamuuliza "sasa kwani ulikuwa na shida gani huko ukashndwa kunitafuta

Akasema kule uingereza kuna sheria ngumu sana, mke wa pili, bi Fatima alinipeleka mahakamani talaka yake iliendana na kugawana mali zangu nusu kwa nusu nimeparangana na hiyo kesi miezi miwili baada ya kuimaliza tu nikapigiwa simu kutoka dubai, mke wangu mkubwa amechukua fedha na kupotea.

Mhhhh nilishtuka sana nikawaza mbona magumu yanatokea kwa wakati mmoja nikamuuliza kwani ulikuwa umegombana mke mkubwa akasema tatizo lilianzia kwenye ile mimba
Nikamuuliza mimba ilisababishaje? Akasema mle alitaka naye aitwe mama ndio maana aliamua kubeba mimba bila kumshirikisha

Niliduwaa kwanza, "kwa hiyo mke ushajua alipo?"
Alasema hajajua alipo, ndipo nikamuambia si atumie madawa yake kujua alipo, akasema mkewe mwenyewe alikuwa ashaujua uchawi hivyo amejisindika ili nisijue yuko wapi. Niliogopa sana

Sasa mbona umekonda? Akasema ni mateso yamenikondesha nimeteseka sana
"Basi kaa hapa nitahakikisha nakuhudumia hadi unenepe sawa? Akasema sawa, maisha yakaendelea vizuri yeye hakutaka tena kurudi dubai.

Siku ya kwanza niliamua kumpikia chakula mwenyewe, nilikuwa najua anapenda nini hivyo nikamuandalia vizuri kisha akaja tukala kwa pamoja huku nikimtia moyo.

Safari ya Dubai nikawa nimeshaiahirisha kwa sababu niliyekuwa namfuata amekuja mwenyewe. Ilipofika saa tatu tu tulienda kulala.

Tulijaribu kufanya mapenzi lakini Mahamood alishindwa kwa sababu alikuwa na msongo wa mawazo sana akaniambia tutafanya kesho, hivyo tukalala.

Usiku saa nane nikashtuka kutoka usingizini, nilipotazama kitandani niko peke angu, nikajiuliza vipi mwanaume yuko wapi, au yuko bafuni lakini kwa kuwa chumba kilikuwa ni masta, nilitazama bafun hakukuonekana kama kuna mtu.

Nikaendelea kujilaza huku nikisubiri arudi dakika zaidi ya kumi mtu harudi ikabidi niwashe taa nitazame simu na laptop vyote kaacha kitandani sasa kaenda wapi?
Nikashuka huku naita "Mahamood...Mahamood" nikafungua mlango

Nilipofungua nilichungulia nikatazama barazani nikamkuta Mahamood amejilaza chini kwenye sakafu, anajiviringisha huku akiweweseka kama mtu anayepitia maumivu makubwa sana
ITAENDELEA

39
"Mahamood" nilisema kwa mshangao huku nikijaribu kumsogelea anazidi kujibaranguza kule na huku, ghafla kelele zikaanza analia kwa nguvu
"Niache.....Ya Allaaaaaaah aaaaii" alikuwa anasema hivyo Mahamood nikaanza kuogopa na kuita kwa nguvu
"Happy" hilo ni jina la dada wa kazi ambaye alikuwa anaishi pale, kweli haikuchukua muda akatoka chumbani kwake akamshangaa "eh eh"

Ubaya mmoja alikuwa kama vile ana mapepo mwanaume yule, Happy akaniuliza "Amekuwaje tena?"

Nikasema huku nikilia "mi sijui, sijui ana mapepo?" Mara happy akaanza kumuombea shindwa, shindwa.....kwa muda mrefu mpaka pale Mahamood alipotulia na kuwa sawa kabisa
Nikamuuliza "mume wangu vipi umepatwa na nini?" Akatikisa kichwa na kusema "hapana ni kawaida"

Nikamuuliza kawaida vipi mbona sijawahi kukuona na hii hali? Niambie ukweli una tatizo gani? Akaniambia tukaongelee chumbani tukiwa peke yetu.

Mi nilianza kuogopa hata chumbani naendaje naye lakini sikuwa na kipigamizi ilinibidi niende naye chumbani tukakaa na kuongea akaniambia kwamba hiyo ni adhabu anayoipata baada ya kumpa mimba yule mwanamke ambaye alikuwa haruhusiwi kuzaa naye
Nikamuuliza mbona mimi nilipopataga mimba ya mapacha na mtoto wa pili haikuwa hivyo? Akasema eti nyota yangu mimi inang'aa ndiyo maana
Niliwaza sana, kwa hiyo anatumia nyota yangu ili mambo yaende? Lakini sikuweza kumuambia kabisa, nilimuuliza tu sasa utafanyeje? Akasema anajua jambo la kufanya
Tuliendelea kulala japo sikusinzia tena mpaka asubuhi, maisha yakaendelea Mahamood akaogopa kurudi tena Dubai kwa kuhisi mizimu itaenda kumtesa.
Biashara za Mahamood zilianza kuwa ngumu ghafla, kule kwenye biashara ya magari wateja wakawa hawaji tena, afya yake naye ikazidi kudorora, mara kwa mara ile hali ya kuzimia ikawa inamtokea na kuwa kama vile ana mapepo.

Siku moja akajifungia chumbani mwenyewe akawa anaomba dua ili mambo yake yakawa sawa, mimi nikiwa sebleni na watoto pamoja na Happy tulisikia kama kishindo ndani, halafu ghafla akaanza kupiga kelele kwa nguvu chumbani

Nikaenda haraka nikajaribu kufungua mlango umebanwa kwa ndani, nagonga lakini yeye anazidi kulalamika kama vile anapata maumivu makali sana
Fungua mahamood, fungua tafadhali, lakini wapi hakunifungulia ikabidi happy aje anisaidie tukavunja mlango na kuingia ndani, nilimkuta amelala hoi anatoka damu puani na mdomoni halafu amepoteza fahamu.

Nikawaza mambo mengi, mimi naye nikajikuta nalia sana, tukajitahidi kumbeba tukashindwa hivyo tukatoka nje na kuomba msaada na kumtoa nikampakiza gari na kumuwahisha hospitalini haraka sana.

Tulipofika hospitali alifanyiwa matibabu, saa 10 usiku alishtuka mimi bado sijalala namtazama tu aliponitazama nikashtuka na kumshika mashavuni "umeamka?"
Hakunijibu nikasema Mahamood unajisikiaje? Una tatizo gani niambie ukweli? Akasema mke wangu wanataka kunichukua, wanataka kunichukua alisema huku akitokwa na machozi
Kina nani hao? Nilimuuliza akaendelea tu kulia huku akisema wanataka kuniua mimi, kiukweli nilichanganyikiwa
ITAENDELEA

40
Nilipomtazama alikuwa serious, afya yake imedorora namuangaria kitandani ni kama vile mifupa tu kitandani nikaogopa na kisema sasa nifanye nini, nilijuta kuingia kwa mganga nilijua kwamba uganga wake ndio chanzo cha matatizo yote yale.

"Mume wangu sasa utafanya nini?" Nilimuuliza
"Sijui, sijui ...... Shakiraaa.......Fatima mko wapi mbona mmeniachia adhabu kubwa kama hii?" Alisema
"Wao ndo wamekuroga Mahamood?"
Hapana ila wameniachia matatizo nifanye nini mimi? Nakupenda Mamujee nisaidie....naomba unisaidie alizidi kuongea huku akilia
Nikusaidie nini? Akaniambia huku akilia nisaidie bila hivyo sitaweza kupona
Nikamtazama vizuri nikamuuliza mbona sikuelewi akashindwa kujibu kabaki akilia.

Tulikaa pale hospitalini siku tatu, akaruhusiwa tukarudi nyumbani lakini alizidi kunyong'onyea kila siku, nikasema moyoni mtoto wa mtu asinifie, ngoja niwapigie ndugu zake
Nikachukua namba kwenye simu yake, nikampigia kaka yake mkubwa nikamueleza hali halisi akasema mapema kesho yake angekuja Tanzania, hata hivyo kesho yake hakuweza kufika kwani alikuwa amekosa ndege ya siku hiyo
Hivyo alifika siku tatu baadaye, nilimpokea akaniambia hana muda wa kupoteza anatakiwa aachwe yeye kaka yake chumbani pekee.

Mimi nikaenda nje na watoto pamoja na happy tukawa tunasubiri, zaidi ya masaa matatu ndo anatoka shemeji huyo akaniambia tayari.
Nilienda kumcheki bado hakuwa na nuru lakini shemeji aliahidi baada ya muda mfupi atakuwa na afya, shemeji hakuwa na nafasi ya kukaa sana tanzania hivyo baada ya siku mbili tu aliondoka kwenda kuendelea na kazi zake Dubai

Nikabaki na mume wangu kweli nuru ikamrudi akaanza kuwa sawa kuanzia kiakili na hata kimwili, nikamuuliza tatizo nini? Akaniambia tatizo tatizo mizimu inamtaka aingilie mwanamke kinyume na maumbile, hivyo hata hizo dawa alizopewa zingedumu kwa muda tu na angeweza kufariki.

Nikaogopa na kumuuliza "kwa hiyo itakuwaje? Akasema atajua la kufanya, hofu yangu nilijua atanisaliti na wanawake wengine maana mimi sikuwa tayari kufanya hivyo.
Baada ya wiki mbili aliondoka akaenda Dubai huko alikaa mwezi akiniacha peke yangu, baada ya muda akarejea tena Tanzania 🇹🇿, alipokuja aliniambia amenimiss sana

Baadaye usiku tulikula kisha tukaenda kupumzika, mimi mwenyewe nilikuwa nimemmiss sana, tukapanda kitandani tupeane raha, akaanza kunichezea

Mwili ukawaka moto akaanza kunipa raha kwa njia ya kawaida, baada ya kufanya dakika kam tano hivi, mi nimeshanogewa nikasikia kanigeuza akanipigisha magoti akaendelea kunifanya.
Akafanya akafanya, mwishowe nikashangaa kaingiza kidole huku nyuma, nilishtuka na kumpa onyo tafadhali usifanye huko, lakini hakunijibu aliendelea kukaa kimya akaendelea kunila mbele
Dakika tatu akachomoa nanii yake halafu nikashanga ameweka kichwa nyuma kwangu, we nikasema usinitanie niliruka chini kitandani nikasimama na kumuuliza "mbona unataka kufanya hayo tuliyokuwa tumeshaacha muda mrefu

Mahamood akaanza kulia "nisamehe mke wangu lakini naomba unisaidie, wewe ndiye uliyeshikilia uhai wangu"
Kivipi? Akasema bila kufanya hivyo sitaweza kuishi kabisa nitakufa au watoto wetu watakufa, maana ndiyo masharti niliyokuwa nayo tangu enzi za utajiri
Itaendelea

41
Nilishangaa sana maneno ambayo alikuwa ananiambia nikamuuliza unasemaje? Akasema ndivyo ninavyotakiwa nifanye ili niendelee na utajiri au watoto wetu wafe au mimi nifariki, kipi bora mke wangu?
Nikamuuliza "mbona tuliishi vizuri tu?"
Akasema kwamba kipindi yuko na mimi alikuwa anawafanya wale wake wengine kinyume ndio maana alikuwa hafilisiki, sasa inabidi anifanye mimi maana wale wengine walikuwa wameshamkimbia.

Mhhhh mhhhh mhhh niliguna tu maana sikuwa tayari kufanya hivyo akaniuliza "au unataka nikufanye kwa nguvu kama nilivyokufanya mara ya kwanza? Nikatulia kimya.

Mahamood akawa ananisogelea anataka anishike nikakimbia, nikawahi nguo yangu nikafungua mlango na kutoka, akabaki ndani peke yake.

Nilienda kulala kwenye chumba cha wageni mi sikutaka tena kutumika katika njia za kishirikina, niliamini anaponifanya vile anaondoka na nyota yangu ndio maana anapata pesa.

Nilijikuta namchukia sana, nikamuambia naondoka, akawa ananibembeleza sana ili nisiondoke pale, nikampa sharti kwamba ili nibaki basi asijaribu kuniingilia kinyume, akakubali

Maisha yaliendelea lakini akionekana hana furaha, nilipoona furaha kwake imepungua nikamruhusu atafute mwanamke mwingine wafanye hivyo mi sitakasirika.
Mahamood alisikitika sana akaniambia, basi anajua la kufanya, nikasema aamue analilotaka kuendelea kutanua nyuma kwangu hilo nooo!

Basi tukaendelea kuishi kawaida nampa mbele kwa machale machale asije akaniingiza huko, basi akawa analalamika ila nilikaza kweli kweli.

Siku moja nilienda kwenye duka langu la nguo nilikuwa na gari yangu ndani nimewabeba wanangu, nikawa naangalia mzigo ili niweze kujua naagiza mzigo gani, nikaandika vizuri kwenye diary kisha nikaongea ongea na wafanyakazi wangu halafu nikachukua gari na kurudi nyumbani

Nilipofika niliingia ndani, sikumkuta Mahamood sebuleni kama ilivyo kawaida yake hivyo nikaingia chumbani nikijua nitamkuta bado sikumkuta ila nilikuta simu yake kitandani.

Nikawaza yuko wapi, hivyo nikaona bora nimuulize Happy, hivyo nikasogea kwenye mlango wa chumba cha Happy, nikataka kugonga ila kabla sijagonga nilisikia sauti huko chumbani kama vile analalamika.

Nikapata wazo la haraka na kufungua, ile nimetazama ndani sikuamini kile nilichokiona
ITAENDELEA
 
( 42-46 ) MWISHO
42
"Mahamood" niliita kwa mshangao kwa sababu nilimkuta Mahamood amempigisha magoti dada wa kazi anamshindilia hongo lake kinyume,
Sijui alikuwa amemfanyaje mtoto wa watu alikuwa amekuwa kama mjina hata nilipoingia Happy hakushtuka, niliita happy, lakini hakushtuka nikasikia moyo umeniuma jumlisha presha yangu nikadondoka chini na kupoteza fahamu

Nilikuja kushtuka niko hospitalini, na Mahamood yuko kando yangu ananitizama ndio nikakumbuka tukio lililonikuta pale ndani machozi yakaanza kunitoka.
Mahamood akaanza kuniomba msamaha, nisamehe mke wangu, ilinbidi maana majini wananifuatilia wanataka nitoe mtoto mmoja kafara au nifanye hivyo ndio leo ilikuwa mwisho wa siku ningekufa mke wangu

Nikamuambia "ndio ufanye wewe na dada wa kazi kweli?"

"Nisamehe mke wangu" alinibembeleza sana lakini nilikuwa nimemchukia mno akasema mimi ndiye nilimruhusu afanye na mwanamke mwingine ila mi kilichoniuma ni kwa sababu yule ni mtoto wa kazi wa kwetu wenyewe halafu kwanini nijue si angefanya tu kwa siri.

Basi niliporuhusiwa siku ile ile nilirudi nyumbani, nilipofika sikumkuta happy alikuwa ameshaamua kukumbia baada ya lile tukio kilichonishangaza zaidi nilimkuta Roby ndiye yuko na watoto wangu nikakasirika sana na kumuuliza amekuja kitafuta nini kwangu akadai happy ndiye alimpigia simu aje amsaidie.

Nikamuambia sawa aondoke, mi nitakaa na watoto wangu mwenyewe, Mahamood akaniambia "basi ngoja nimpeleke na gari" nikasema hapana huwezi kwenda naye kaana nilijua kwa namna alivyowahi kumtega muda mrefu basi angeweza kuanza naye mambo mengine.

Nikachukua nauli nikampa Roby aondoke, sasa cha kushangaza Mahamood akazunguka kupitia mlango wa nyuma halafu akaenda kukutana naye mi nilipoona harudi nilichungulia kwa dirishani nikaona wakibadilishana namba

Roho iliniuma maana ni mume halali wa ndoa halafu mimi sikutaka magonjwa, hivyo aliporudi tu nikamuuliza kwanini amebadilika ghafla? Akasema mimi ndiye nimembadilisha,
Nimekubalisha na nini akadai kwamba simpi kile anachokitaka hivyo anatafuta akadai kwanza anataka aongeze mke mwingine nikamuambia kama ni kuoa oa lakini mi sitaki hao michepuko.
Tuligombana sna lakini hakuonekana kujali maumivu yangu, Mahamood akabadilika siku hadi siku, mara nyingine akawa halali tena nyumbani anakuja mara moja moja na hata hanijali kabisa

Siku moja ndipo Roby akanitumia message, kwamba nimeshindwa kulelea mume basi yeye anamlelea na anampa kile alichokitaka, nikaona naelekea pabaya sasa nikamtumia ujumbe Mahamood
"Ninahitaji talaka"
Akanijibu "sawa nitakuja baadae nitakupatia talaka yako" yaani alijibu bila kujali
Niliumia sana

43
Niliwakumbatia wanangu tukawa wote tunalia nikaanza kuwaza mambo mengi sana mpaka nikaanza kuhisi labda shangazi ndiye amenirogea mtu wangu, nikafikiria au ni wale wake wenza?
Ilinibidi nimpigie kaka yangu simu ili nimueleze hali halisi kinachoendelea kaka akaniuliza kwani umemkosea nini Mahamood ikabidi niseme ukwel, kwamba Mahamood ananitaka kinyume na maumbile

Mhhhh mhh kaka aliguna akaniambia hizo ndo za waarabu wanapenda sana kwa mpalange, nilikuwa nahisi kwanza labda ashakufanya hivyo, sasa kwanini anataka kufanya hivyo?
Nikamuambia anasema akifanya hivyo ndiyo utajiri wake unazidi pamoja na biashara zinatembea
Kaka akasema achana naye, nikamuambia poa, ila nitaishi vipi yeye ndiye anatunza watoto? Akasema watoto watatunzwa kisheria na asipotunza basi mimi nitakuwa nawatunza tena nawapenda sana wajomba zangu hao mapacha.

Kidogo hili lilinipa kiburi, na baadaye bila kufikiria Mahamood aliporudi alinipa talaka kisha akaniambia "hataki kuniona maana anataka aoe mke mwingine amuweke pale ndani"
Nikamuambia hapana haiwezi kuwa hivyo mimi nitaenda wapi na watoto? Akasema niondoke na watoto wangu, nikamuambia lakini nyumba ina hati miliki yenye jina langu, akasema hilo si tatizo kwani yeye si ndiye alijenga?
Nilichanganyikiwa nikalala pale ndani nawaza usiku kucha usingizi hauji, asubuhi nikashindwa kuvumilia nikaona wewe usinitanie naachaje utajiri.
Nikampigia Mahamood maana alikuwa halali tena pale nikamuambia kwamba talaka yake narudisha, akanicheka halafu akaniambia sharti la kuirudisha ni kwamba nikubaliane na hali ya kuingiliwa kinyume.

Nikafikiria wee nikakosa jibu nilipotazama kwenye simu rafiki yupi nimuaminie hapana ndipo nikaona namba ya mke mkubwa nikasema ngoja nicheki kama anapatikana
Nilimtext whatsapp na kumueleza hali halisi nikamuambia mume anataka nyuma akaniambia kwa kuwa ushazaa basi mpe tu sisi tumekimbia baada ya kuona hatupati watoto.
Nikamcheki Edina japo alikuwaga adui yangu muda mrefu lakini niliona naye anipe ushauri juu ya hilo Edina akaniambia acha ushamba siku hizi kuna mtu asiyetoa kwa mpalange kweli? Kikubwa ni mwanaume awe na hela ila mwili wako ni mali yake.
Nikasema mh mbona wote wananishauri nitoe mpalange? Maneno ya kuambiwa changanya na ya kwako nikaona kweli kama alishanifanya kipindi cha nyuma sasa nakataa nini?
Nikamtumia ujumbe Mahamood nikamuambia mume wangu nimekubali nitakupa unachokitaka

Acha message za mahaba zimiminike, kweli mke wangu? Siamini, nakupenda sana Mamujee una akili kuliko wanawake wote nakuja hapo nyumbani sasa hivi mpenzi"
Mi nikabaki nacheka tu najiuliza kwani kafurahia nini? Nikamsubiri kweli baada ya nusu saa akafika nyumbani alikuwa amebeba zawadi kem kem, za kwangu na za watoto akanikumbatia kwa nguvu halafu akaniambia ananipenda sana mim nikawa kimya kabisa.

Tuliketi tukaongea mengi akachukua ile talaka akaichana chana, siku ile hakutoka tena jioni nikaandaa chakula cha usiku tukala, tukiwa tumekula akaniuliza nikupe zawadi gani? Nikamuambia aniwekee tu pesa kwenye akaunti yangu nitakuwa nafurahi ili nikipata matatizo niwe nayatatua kwa haraka
Je nilifanya sahihi kumruhusu hilo? Naomba comment na likes za kutosha niendelee kuwasimulia kilichonikuta

44
Usiku ulipofika alinifanya kinyume baada ya miaka zaidi ya mitatu kupita, alinishukuru sana akaniweke milioni 20 kwenye akaunti akidai hiyo ni kunishukuru tu.

Kuanzia siku hiyo alikuwa ananijali mno, lakini mimi sikuridhika ni kile nilichokuwa nakifanya, nilikuwa nawaza hivi siku ikija kugundulika itakuwaje? Jamii itanionaje halafu pia kwa Mungu wangu siku ya kiyama nitaenda kujibu nini? Nilikosa furaha

Mchezo ukaendelea kila mwezi akawa ananiwekea hela kwenye akaunti tena pesa nyingi akiniambia nimeing'arisha nyota yake halafu akadai anataka tuhamie Dubai, nikakataa.
Siku moja ndio kaka akaniuliza mbona sikwenda tena kwake au nishakubali mpalange? Nikamuambia hapana nilikataa lakini kaka akasema we haya, nikakata simu najishtukia hatari

Maisha yakaendelea ila sikuwa napenda kile nilichokuwa nafanyiwa sasa ameshanitawala siwezi kumnyima tena, nilipochungulia kwenye akaunti nina pesa nyingi ninaweza kwenda kuanzisha maisha niondokane na dhahma ya kuingilia kinyume, ni hatari.

Nikajipanga taratibu nataka nikimbie zangu sasa nikawa nimepanga naenda zangu mbali huko Mbeya nikaanzishe maisha mapya nikatubu dhambi halafu maisha yaendelee.

Sikumuambia mtu yeyote zaidi nilikuwa nafanya kimya kimya ili asijue natoroka maana wambea wengi.
Wiki kama mbili zilipopita niliwachukua wanangu wote wawil tukatoroka kwa basi na kuelekea mkoani mbea, niliamua kuachana na biashara za kipumbavu hela napata lakini furaha sina sasa za kazi gan
Nikaelekea mbea huku nikiacha barua nyuma nimemuambia nisamehe mume wangu siwezi kuendelea kuwa na wewe, kitendo tunachokifanya hakinipendezi mimi wala Mungu wangu, naomba nikatafute maisha mengine, inshallah tutakutana tena ila naahidi kuwatunza watoto wako vizuri na watafurahia maisha huko niendako

Nikabadilisha namba halafu nikaondoka zangu ili asinipate tena kwenye simu. Nilipofika mbeya nilitafuta hoteli nzuri nikalipia kisha nikaingia mimi na wanangu tulale ili kesho tuanze kutafuta nyumba ya kuishi tukiwa na amani.

Tukala tukalala, ila watoto mara zote wananiuliza dady atakuja lini nawaambia atakuja tu wao hawaelewi nilichokikimbia.
Kesho nikaanza kuhangaika na madalali mpaka nikapata nyumba nzuri kwa mwezi laki nne, nkalipia miezi sita tu halafu nikanunua vitu vya ndani na kuanza maisha mapya mimi na wanangu tu.
Nikiwa naishi pale Mahamood hakuwahi kunitafuta zaidi ya miezi mitatu sasa nikaona nianze kufanya biashara kwa kuwa nilikuwa ninajua misingi ya biashara niliona nianze biashara kufuata bidhaa china niwe nauza.

Ilinibidi nitafute shule ya boarding nikawapeleka wanangu halafu mimi nikaanza biashara, kwani nisingeweza kusafiri nao kila mahali, mi nikawa naenda nachukua mzigo narudi, nikamshukuru mungu Biashara ilikuwa inatembea sana na hapo sikutumia hata uchawi wala uganga ila Mungu hakunitupa

Nilikuwa naishi maisha ya amani, sina stress na sikuwa na mwanaume kabisa, baadaye nikamuambia kaka yangu nishakimbia niko mbeya hivyo anitembelee siku moja aone napokaa ili hata likitokea tatizo ajue ananipata vipi.

Siku moja nilienda kuwatembelea wanangu shule, nilipofika nilikuta wanaendelea vizuri, kilchonishangaza watoto walikuwa na mabegi mapya nikawauliza vipi shuleni ndio wamewapa zawadi wakasema hapa baba ndiye aliyewaletea siku alipowatembelea
Nikashangaa baba yao kajuaje jamani, nikaanza kuogopa tena nikaona tunarudi kule kule

45
Nilikaa na watoto nawauliza waalimu nani alikuja wakasema ni muarabu jamani nikachoka, nikasema ule uganga wake ndiyou umemsaidia. Sikumtafuta kabisa kwenye simu maana sikutaka aijue namba yangu.

Baada ya muda kaka yangu alikuja kunitembelea, akaniuliza, umeamua kuacha zile mali zote ukaja kupanga huku
"Kaka unaona raha mdogo wako niingiliwe nyuma?" Akaniambia mi sijui ila ungejua namna kufanya zile mali zibaki upande wako, nikamuambia hati miliki ya nyumba zote ninazo hivyo ni mali zangu hakuna wa kunidhulumu kamwe.
Ghafla tukiwa tunaongea simu yangu iliita, nilipotazama hivi ni mwalimu wa shule ile waliyokuwa wanasoma watoto wangu.
Nikapokea "Hallo Mamujee wewe ndiye mama wa watoto mapacha?"
Nikasema ndiyo mimi, sawa naomba ufike shuleni mara moja, nikachukua gari yangu aina ya Prado Tx nikapanda na kaka tukaelekea shuleni
Tulipofika shuleni nilipokelewa nikapelekwa kwenye zahanati ya shule tulipofika nilishtuka mtoto wangu mmoja anaumwa ghafla, huyu mtoto ndiye alizaliwa wa kwanza yaani Dotto, nilishtuka mwili wa mwanangu ulikakamaa, alionekana kuota vipele mwili mzima.

Nilichanganyikiwa nikamuwahi na kumshika nikamuita mwanangu! Hakuitika alikuwa ananitazama tu, nikamtikiza halafu nikasema kipi kilichokutokea hadi uko hivi? Unaumwa? Mwanangu ee... nilizidi kulalamika huku nikitokwa na machozi, mwenzako yuko wapi?
Niliinuka na kumgeukia mwalimu, pacha yake yuko wapi? Akasema ngoja tumuite hivyo akatoka fasta na kwenda kurudi na kulwa, yeye alionekana kutokuwa na tatizo lolote lakini machoni alionekana amelia sana

Mlipompima alionekana ana tatizo gani? Nilimuuliza daktari akasema vipimo vinaonesha mtoto haumwi kitu chochote, nikasema msinitanie tumbo la uzazi linauma namuomba mwanangu nimpeleke hospitali kubwa, wakaniambia sawa

Tulifanya taratibu zote pale nikamchukua mwanangu na kumpeleka hospitali ya rufaa akatazamwe, alipotazamwa madaktari wakasema mtoto hana shida, mi nashangaa mtoto haongei hafanyo chochote halafu wanasema hana shida? Nikaanza kuwaza mengi ndipo wazo la mume wangu kwamba muda mrefu alitaka kutoa kafara ila akaachaga likanijia, nikaanza kulia huku nikimlaumu
Mahamood usikute ni wewe unamfanyia hivi mtoto wangu, kwa kuwa sikutaka Mahamood aijue namba yangu, hivyo basi niliomba namba ya kaka yangu na kumpigia Mahamood

Nikamuambia salam alaikum akasema walaykum salam halafu akakaa kimya hakuniuliza nikamuambia "usikute wewe ndiye unataka kuua mtoto wetu akaniuliza kwani uko wapi mke wangu? Nikamuambia usiulize niko wapi ila please naomba usimuue mtoto wangu

Hutaki kusema ulipo? Umenitafuta ili nini? Alisema na kukata simu nikabaki nalia huku nimemshika mwanangu kitandani, mara sauti ya mtoto wangu ikaniita 'momy' nikainua macho nikamtazama na kumuuliza "umeongea mwanangu? Umepona?" Akasema tu mama i love you halafu akafumba macho huku mkono wake ukilegea legelege, sikuamini macho yangu mtoto wangu mmoja alipoteza maisha pale pale, nililia sana hadi nikapoteza fahamu

46
Ninakuja kushtuka ni muda umeenda sana niko kwenye kitanda cha hospitali kando yangu kasimama kaka Mwita anatazama juu kwenye dari huku machozi yakimtoka akawa analalamika "kwanini lakini Mungu hivi wazazi wetu wangekuwepo tungepitia maisha haya? Tunapata starehe kwa muda mfupi tu lakini kila mara vilio? Sawa tu Mungu"
Kaka alikuwa anamlaumu Mungu nikajikuta natokwa na machozi namkumbuka mwanangu alivyokuwa mchangamfu sikuamini kama sitomuona tena akiwa hai.

Nilimtumia ujumbe Mahamood nikamuambia "asante sasa naamini umefurahi"
Mahamood akapanda hewani kwenye simu ya kaka, akisema "nimefurahi nini?"
Nikamuambia mtoto amefariki, akashtuka na kuniuliza kweli mwanangu amefariki? Nikamuuliza unajifanta hujui akasema wallahi sijui.
Wewe ndiye uliyehusika Mahamood sio kwamba nilikuwa sina taarifa kwamba muda mrefu ulitaka kuwatoa kafara watoto
Akasema siwezi kufanya hivyo sina watoto wengine je hao nitawafanyia hivyo? Naomba mumsafirishe mtoto tafadhali atazikwa huku huku. Nikamuambia haiwezekani
Akasema inabidi iwe hivyo mtoto hawezi zikwa nje na nyumbani kwake, akadai nisipomleta atamfuata na hata akizikwa bila ridhaa yake basi atamfukua.

Mahamood alipokata simu kaka aliniambia mamlaka ya mtoto anayo baba yake basi nikatulia sijui nichukue hatua gani, mtoto alitakiwa azikwe mapema sana lakini kesho yake asubuhi na mapema Mahamood alifika Mbeya akasema tujiandae wote, mimi, kaka na mtoto kurwa tuelekee Dar ili saa tano mtoto azikwe, nikasema sawa, tukajiandaa na kurudi Dar
Mtoto alizikwa lakini baadaye usiku nikamuambia Mahamood kwamba kesho yake ningeondoka akasema siwezi kuondoka ni njia Mungu aliyoituma kutuunganisha tena
"Tumeshampoteza mtoto wetu mmoja tumebaki na mtoto mmoja sasa tuishi pamoja tuongeze familia' nilisema hapana siwezi kuishi na wewe tena akaniambia wewe ni mke wangu wa ndoa
Nikamuambia hapana ninahitaji talala hata dini inasema kwamba mke akishasema apewe talaka, basi hiyo ni talaka tosha
Akasema bado hajaridhia akapiga magoti na kuniomba msamaha niweze kumsamehe turudiane, alikiri kutokunifanyia unyama tena, sikuelewa nifanye nini
Itaendelea

47
Kaka naomba unisaidie kuongea na huyu mwanaume mi nahitaji kukaa peke yangu, mwita hakuongea chochote zaidi alimtazama tu Mahamood akaongea
Nasema mara ya mwisho naomba tubaki wote, nikasema hapana sihitaji kuishi na wewe tena, akamaliza kwa kusema basi ondoka ukihitaji ila mtoto atabaki hapa.

Nikamuambia naondoka na mwanangu, akaniambia unataka akafe kama mwenzake? Umeshindwa kulea watoto miezi sita tu mmoja ameshafariki huyu mwingine ndiye utamuweza? Niachie mwanangu sina mwingine

"Kwa hiyo mimi ndiye nimemuua mtoto?" Niliuliza huku nikilia

"Mbona kipindi anaishi hapa hakutokewa na hivyo vilivyomtokea kwanini kwanza upeleke mtoto boarding? Unadhani wanaweza kumsimamia kama wewe?
Nikasema basi inatosha nashukuru kama nimemuua mtoto wangu, sawa Mahamood sawa" nilisema huku nikilia sana.

Sikuhitaji kukaa tena pale, niliondoka nikaenda kulala hotelini, na kesho yake asubuhi niliondoka kurudi mbeya nikiwa peke yangu maana kaka yeye alielekea Arusha akaendelee na kazi zake.

Nikabaki upweke nyumbani naishi peke yangu nikawa nafanya biashara taratibu siku zikawa zinazidi kusonga mbele, natamani nipate mtoto mwingine lakini nahofia nimeshachezewa sana kinyume na Mahamood sasa nifanye nini?
Nikazidi kupambana mpaka biashara zangu zikachangamka, nikawa kuuza laki tano nne mpaka sita ni kawaida kwa siku mwishowe nikazoea kabisa kuishi peke yangu

48
Takribani miaka 3 mi na Mahamood hatukuwasiliana kabisa lakini katika maisha unaambiwa usikumbuke tu ubaya mtu aliyokutendea, kumbuka na mazuri pia japo kiduchu, kiukweli licha ya kuwa na uchumi mkubwa sana, lakini mwanzo nilikuwa na maisha magumu sana, Mahamood ndiye aliyenitoa kwenye maisha mabaya na kunisaidia mimi nikawa mjanja na hata kuwa urahisi katika kufanya biashara kwani pesa alizokuwa akinipa mara zote nilizutumia kama mtaji na hatimaye nikafanikiwa.

Sikuwa na cha kumpa hata ningesema nimpe milioni kumi asingeona kama ni pesa kwa sababu alikuwa ni bilionea.

Niliondoka kwenye utajiri wake ili nikaishi kwa amani na ndivyo ilivyokuwa hivyo,
Zawadi ya pekee niliyokuwa nimempa ni ya mtoto, sikuwahi kuwasiliana na mwanangu lakini mpaka kipindi hicho alikuwa na miaka minane nilitamani sana nipate angalau nafasi ya kumuona,

Sikuamini tena kama yule mtoto nitamzingatia kama wa kwangu maana ni muda mrefu ambao alikuwa anaishi bila mapenzi yangu tena alizoea kuishi na watu wengine, nilikuwa na mimi natamani nipate angalau mtoto mmoja tu, na round hii nilitaka niwe na mtoto wa kike, lakini sikuwa na mwanaume kwa kipindi chote.

Nilimfuata rafiki yangu mmoja aitwaye vero nikamuomba anishauri nikapandikize au nitafute mwanaume nizae naye akasema ni heri nitafute mwanaume nizae naye ili hata likitokea la kutokea basi mtoto awe na baba.

Nikaanza mdogo mdogo kumnyemelea kijana mmoja alikuwa wa kichaga alikuwa na akili huyo nikaamini nikipata naye mtoto basi nimepata mtoto mwenye akili nyingi

Nilianza utani wa hapa na pale mara kumjali jali ili ajiongeze maana mimi sikutaka kutongoza mwanaume, hivyo nilifanya tu vituko mara kumkaribisha kwangu tunakaa ila aliheshimu hivyo hakuthubutu kunitongoza.

Sasa siku moja nilijua kabisa niko kwenye siku za hatari, halafu Mungu alivyo bwana acha mvua inyeshe siku hiyo baridi kama yote mi nimelala zangu nasikia baridi sana halafu nawashwa hatari,ni muda mrefu sijafanya
Nikaona mh mh ntakuja kufa na utamu wangu, nikaamua kumfungukia yule mwanaume aitwaye Arnold

"We mmachame"
Akajibu "unataka kupigwa wewe"
Nikamuambia kisa nini akajibu kwanini usiniite jina langu hadi utaje kabila?
Nikamuambia sasa basi njoo unichape sasa sijajua hujanichapa na fimbo gani, akasema ntakuchapa kwa fimbo yangu ya nyama, nikamuuliza ipi hiyo?
Akasema hii huku ndani ya boxer utalia kama mtoto
Mhhhhhh nilisikia hisia za tofauti zimeniamka nikamuambia sijafanya hayo mambo mda mrefu, akaniambia wewe si ustadhat bana unataka hadi ndoa? Nikasema ni kweli.

Arnold aliendelea kukaa kimya nikaona nimchokoze, "njoo basi tupige story nyumbani?"
Akaniuliza "na mvua hii?"

"Ndiyo niko peke yangu upweke kama wote"
Nikija utanikumbatia?"
Nikamjibu kwanini nisikukumbatie sasa mi nitamkaribisha mgeni halafu asipate joto kwa baridi hii ya Mbeya?"
Arnold akakaa kimya dakika kumi nikamchokoza, umefika wapi?"
Akaniuliza uko serious nije? Na mvua hii?" Nikajibu "wallahi nahitaji kampani yako njoo"
Nikija utanipa nini?" Nikamuambia we njoo tutaongea

Huwezi amini licha ya mvua kali lakini ndani ya dakika kumi nilisikia honi getini kwangu, akanipigia na kuniambia nifungue geti ashafika
Ila wanaume!!! Itaendelea

49
Nilicheka kwanza nikijifanya nilikuwa natania "hee umekuja kweli?"
Acha mambo yako njoo ufungue geti wewe" alisema Arnold
Nikachukua mwmvuli halafu nikatoka kwenda kufungua geti, akaingia na gari yake mpaka ndani, akaipaki halafu tukaingia ndani wote tukiwa kwenye mwamvuli.
"Sikudhani kama utakuja" nilisema
"Unajua nini? Kiukweli message zako huwa zinaharibu taswira kichwani mwangu, ni message tamu leo nimekuja nataka kumbato tu"
Mi ninacheka tu, angejua nachokitafuta kwake wala asingeongea sana.
Tukaketi kwenye sofa, "nikupe chai, akasema hapana, soda hapana juisi hapana, sasa nikupe nini? Akasema kuna kinywaji nakitaka kwako
Nikamuambia sasa si ndo utaje?
Arnold mwenyewe siku ile alionekana yuko vibaya aliinuka kwenye kochi akanifuata kwenye sofa nililokuwa nimekaa halafu akaniwekea mkono begani.
Mimi kimya ghafla akanivuta, nini bwana, nilisema lakini busu la shingoni tu aliponichapa nililegea na kumdondokea tukaanza kunyonyana denda pale kwenye sofa.

Nyonyana nyonya mwishowe tukapelekeana chumbani, weee shoow ya siku ile kweli sikuwahi kuipata kwa Mahamood hata siku moja, nikichapwa mtoto wa kikurya mie mpaka usiku saa saba ni fimbo tu nimechoka nyang'anyang'a
Asubuhi ndio Arnold anaenda nyumbani na mimi naenda kazini, najua nasubiri tu siku nije nione tumbo likiongezeka,

Sasa bana ubaya huu mchezo ukishaanza na mtu basi kila siku unasema nafanya mara ya mwisho, tukawa tunapeana, mapenzi yakakolea mi na Arnold mji mzima ukafahamu

Arnold alionyesha kunipenda na ilipofika miezi mitatu ndio namuambia ukweli kwamba nina mimba yake na sijawahi kuipima kabisa, alifurahi sana kijana yule maana hakuwa na mtoto hata mmoja.

Tukaenda hospital kupima duuh napimwa mimba hivi ni mapacha tena alloooo.....Itaendelea

50
Arnold alifurahi, na mimi pia nikawa na furaha, nikajua Mungu alinipitisha kwenye mitihani mingi ili mwishowe nikutane naye huyo ambaye angenipenda na ana maadili yale ya kitanzania haswa.

Tulianza kuilea mimba ugomvi kidogo na maisha yanaendelea raha moja wote tulikuwa na hela licha ya kwamba mimi nilimzidi kama mara tatu yeye kipato chake kwa mwezi alikuwa akipata milioni tatu mimi naelekea tisa kumi huko maana biashara zinaenda hatari hatari.

Alhamdulillah Mungu huwa hamtupi mja wake, round hii alinipa watoto mapacha lakini wa jinsia tofauti, Doto wa kike na kurwa wa kiume, nilifurahi sana nilimshukuru Mungu nikasema wale ndio wa mwisho sitaki kuzaa tena maana nilikuwa nazaa kwa operation hivyo mwili ulikuwa unakosa nguvu sana.

Mimi na Arnold tulipambania watoto wetu tukawa tunawalea kwa furaha, though hatukuoana kwa sababu mi nilikuwa bado kule sijavunja ndoa na Mahamood ingeweza kuleta shida halafu pili dini yangu na Arnold ilikuwa tatizo, Arnold mwenyewe aliniambia watoto wale wangemtosha asingetaka kuoa tena maana ndoa usumbufu

Licha ya mimi kusema kwamba kama anataka kuoa aoe tu maana mimi sitaki kuoelewa tena ndoa ni mateso makubwa nilitaka kufanya tu biashara

Tukaendelea na maisha kawaida na mapenzi yetu yakawa yana kasi ile ile siku zote, watoto tunawalea wamekuwa Mungu amesaidia wamekuwa na wameanza shule sasa

Ndugu msomaji nitangulize Shukrani kwako kwa kufuatilia kisa cha maisha yangu hiki, naomba uendelee kuniombea niishi maisha ya furaha na amani, nisirudi tena kwenye mateso
Na mimi ninawaombea nyie wote kwa Mungu ili msije mkapitia magumu kama niliyopitia mimi, awajaalie muwe na afya njema awape uhai ili muishi na watoto wenu msiwaache wakawa yatima wakapitia manyanyaso kwa wale waliobaki nao
Asanteni sana hapa ndio mwisho wa simulizi yetu hii ya kweli, kwa herini nawapenda
MWISHO
 
Leo ndio nimeimaliza,. Japo naona haina uhalisia sana au ni mwandikp tu wa msimuliaji haushawishi sana ila ni nzuri
 
Back
Top Bottom