Ndoa kama chaguo bora zaidi kwa vijana wa kike

Ndoa kama chaguo bora zaidi kwa vijana wa kike

Willima

Member
Joined
Jul 27, 2022
Posts
26
Reaction score
39
Watafiti wamezungumzia suala la ndoa kwa vijana wa kike, kasikazini mwa Tanzania, wameonyesha sababu za kupamba moto kwa matukio hayo na athari zake kwa waathirika wa mitazamo na mawazo hayo (wanawake).

Sababu za kupamba moto kwa matukio haya ni ukosefu wa elimu ya kutosha juu ya masala ya ndoa kwa vijana wa kike, kufikiri kuwa ndoa ndio heshima kwa mwanamke, pia ndoa imechukuliwa kama kitega uchumi kwa wazazi wa watoto wa kike, na pia masala ya ndoa yanajitokeza sana kwasababu ya kutokuona umuhimu wa kumsomesha mtoto wa kike hivyo akifanikiwa kuhitimu elimu yake ya msingi hulazimika kuingia kwenye ndoa katika umri mdogo kwakuangalia kigezo cha kupevuka kwa mtoto huyo wakike na kutozingatia umri wake.

Athari za ndoa za utotoni kwa watoto wa kike, ndoa za utotoni hupunguza upatikanaji wa elimu kwa wasichana, pia ndoa za utotoni husababisha mimba za utotoni na husababisha matatizo wakati wa kujifungua na hata kusababisha kifo kwa mama na mtoto.
 
Binti akishapevuka haitwi mtoto tena.
Hapa ndo shida ilipo, unakuta binti ana miaka tuseme 19, kisa yupo chuo anaonekana mtoto asiye na maamuzi binafsi.....kwamba mtu akiwa naye au ku propose kumuoa anaonekana gaidi. Bora sasa tukubaliane huo umri mnaoona ni sahihi ili kupunguza haya maneno maneno....
 
Sema binadamu wa sasa tuna miili midogo mtu ana miaka 20 ila unaweza kusema ana miaka 15 ... Ebu fanya kwena kweny vyuo mbalimbali wengi ni above 20 ila miili midogo
 
Watafiti wamezungumzia suala la ndoa kwa vijana wa kike, kasikazini mwa Tanzania, wameonyesha sababu za kupamba moto kwa matukio hayo na athari zake kwa waathirika wa mitazamo na mawazo hayo (wanawake).

Sababu za kupamba moto kwa matukio haya ni ukosefu wa elimu ya kutosha juu ya masala ya ndoa kwa vijana wa kike, kufikiri kuwa ndoa ndio heshima kwa mwanamke, pia ndoa imechukuliwa kama kitega uchumi kwa wazazi wa watoto wa kike, na pia masala ya ndoa yanajitokeza sana kwasababu ya kutokuona umuhimu wa kumsomesha mtoto wa kike hivyo akifanikiwa kuhitimu elimu yake ya msingi hulazimika kuingia kwenye ndoa katika umri mdogo kwakuangalia kigezo cha kupevuka kwa mtoto huyo wakike na kutozingatia umri wake.

Athari za ndoa za utotoni kwa watoto wa kike, ndoa za utotoni hupunguza upatikanaji wa elimu kwa wasichana, pia ndoa za utotoni husababisha mimba za utotoni na husababisha matatizo wakati wa kujifungua na hata kusababisha kifo kwa mama na mtoto.
Wazazi siku hizi wanawatumia watoto wa kike kama kitega uchumi inapofika swala la kuchumbiwa kwa mahali ndefu isiyo na mfano.

Aiseh!.
 
Hapa ndo shida ilipo, unakuta binti ana miaka tuseme 19, kisa yupo chuo anaonekana mtoto asiye na maamuzi binafsi.....kwamba mtu akiwa naye au ku propose kumuoa anaonekana gaidi. Bora sasa tukubaliane huo umri mnaoona ni sahihi ili kupunguza haya maneno maneno....

Binti wa miaka 15 anafaa kuitwa Mama na akaendelea na majukumu mengine.
 
Back
Top Bottom