Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian inakimbilia kwenye talaka

Numbisa

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2016
Posts
301,221
Reaction score
1,172,274


Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian yapumulia mashine na kutaka kutalakiana. Kwa mujibu wa media za Marekani kwa muda Sasa ndoa yao Haina afya nzuri na ilidhoofu kwa kiasi kikubwa mwaka 2020 ambapo mastaa hao wamekuwa wakiishi Kila mtu kwake huku Kim akiwa na watoto

Kwa mujibu wa taarifa Kim hasa ndie anataka waachane baada ya mambo kumshinda ila anataka waachane kwa amani sio migogoro kwani wameshajaribu kwenda mapumzikoni pamoja na hata kwenda kupata ushauri maalum kuipa afya ndoa yao lakini mambo ndio yameonekana kutibuka zaidi Kim tayari ameripotiwa kumchukua mwanamama Laura ambaye Ni mwanasheria maarufu wa migogoro ya mastaa ili aweze kumsaidia suala hilo kuimaliza ndoa kwa amani
 
Kanye West itamkosti Sana. Kardashians hawatamuacha salama
... akiwa staa anajua kuishi na staa kama Kim ni gharama so kwa vyovyote amejiandaa kwa kila hali kuanzia kisaikolojia n.k.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…