....wakati nikijiandaa kuwasha mishumaa kusubiria mwaka 2012, hebu tutafakari na kujadiliana hili. Wazee wetu walidumu kwenye viapo vya ndoa zao kwa kuzingatia misingi ya mila na tamaduni zao, imani za kidini na mitazamo ya kijamii tofauti na kasi ya kuvunjika kwa ndoa kwa miaka hii ya sasa. Nini mtazamo wako kuhusiana na janga hili la kitaifa na kimataifa...
mfano; haijalishi mmeoana kijijini, mnapokuja mjini na mke anapoacha msingi wa ndoa aliyokuzwa nayo, ndoa itayumba, ...na hili pia lishawakumba hata wale waliokwenda ng'ambo na wake zao..." kipofu kaona mwezi, au alalaye usimwamshe?"....
Je, mporomoko wa NDOA ZA KISASA unachangiwa na wanawake kujua haki zao dhidi ya mifumo dume iliyotawala tangu enzi za mababu, na misingi ya imani za kidini, au?
Jadili
Swahiba/.... wakati wewe unajiandaa kuwasha mshumaa,
Mie nawasha tochi kabisa kuupa heshima yote mwaka 2011... A YEAR THAT WAS/IS, which has been the most exciting year in my life, positively, negatively and every between
My response to this (yet another platinum release) thread of your ni kama ifuatavyo;
Ndoa za zamani hazikua na mikito ya sasa, lakini nazo zilikua na misukosuko yao... waweza pata hayo kuanzia nyimbo za enzi ya shingo ya upanga, moyo wangu, dereva fanya upesi, nalia na moyo, usiondoke you name it; whatever we experience now, ilikuwepo but in a different density
tuonacho sasa ni kuendana tu na kukua kwa technology na knowledge among us (of course with unfortunate muanguko wa wisdom kidogo
KUFUPISHA... MPOROMOKO WA KISASA UNACHANGIWA NA YAFUATAYO
akina mama kujua haki zao zaidi
power of knowledge and alternative life style ambazo zamani zilikua hakuna
public flexibility
Mwisho kabisa ni ile necha ya binadamu kuendelea kuvumbua alternatives, tunaona haki za ndoa za jinsia moja, sayansi hasa IT ilivyoweza kufumua mambo ya tabia na vichocheo vya mwili ambavyo havikuwepo, utundu wa asili wa binadamu na pia ile nafasi ya mwanaume kuwa neutralized na vitu kama ajira, shule, sinema, redio nk... (i guess zamani mume/mke alikua ndio source primary ya habari, mbinu mpya na kila kitu
sometimes huwa nawaza, je Yesu au Mtume Muhammad (SAW) wangekuwepo enzi hizi za twitter, facebook, JF, satellite nk wangekua wana hali gani??? kwani hata akipiga ushuzi tu, dunia itajua
In short current world is dynamics and people have more options than just a MARRIAGE.... AND MARRIAGE IS SLOWLY TURNING INTO "JUST ANOTHER OPTIONS FOR LIVING A COMFORTABLE LIFE"
nakuacha na swali: Kama sio uchoyo wa watawala wa mwazo (werevu) ndoa ingekuwa nucleus ya human reproduction?