Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,420
- 18,298
Mkuu mi nipo ila nahisi we ndo umeadimika na una siku special za kujitokeza humu.
...umeadimika aisee, kwema?
well,...sasa huu usasa unafaida kweli na ndoa kwenye kizazi hiki na
vinavyokuja, au ndio tutaishia kuzalishana watoto na kuishia na u single parent?
...hii taasisi si inapoteza muelekeo mama/baba anapojiona ana kibri cha kulea mwanawe bila mwenza?
Tunatafakari athari ya jambo hili kwa vizazi vijavyo jamani?
Usasa hauna faida na kwa upande mwingine una faida pia,unaweza kufanya nini kama mtu amechoka kukaa na wewe
na ana uhuru wa kukuacha?na kwa upande mwingine amekupunguzia mzigo,ila tunakoelekea ndoa za kufunga kwa
mkataba wa miaka kadhaa itakuwa na nguvu zaidi kuliko zakufunga forever.
Mi nadhani tunakoelekea ndoa hazifungwi,na zikifungwa hazitadumu mana watu hawapendi kubughudiwa.
Mi namfahamu mama mmoja anatembea na rafiki wa mwanae,sasa hapo unategemea nini,hakuna malalamiko na
maisha bado yanasonga.