NDOA: Zamani vs Siku hizi

NDOA: Zamani vs Siku hizi

sread nzuri sana ngoja nipike nikimaliza na mie nije kujaribu kuchanganua miaka yangu minne ya ndoa na miaka 36 ya mamaangu na babaangu ya ndoa yao

Halafu nitaomba uje na mawazo yako juu ya hii dhana,

Je onja onja inayofanyika sana kabla ya ndoa siku hizi ina madhara yoyote kwenye ndoa??

Naamini wadau watatoa msaada wao pia!
 
Asante ila nitakuwa peke yangu ndo hivo

Pole sana AD,

Sasa, kwa nini unadhani wazee wetu walifanikiwa kwenye haya mambo ya malavi davi na sie tunafeli??

Please tupe mawazo yako...Not a case study!!
 
Sijui kwanini unanichanganya na Afrodenzi? Au hangover?

Naomba nisiombe hata msamaha kwa sababu kila ninapojaribu kuwa makini ndivyo ninavyozidi kukosea!!

Anyway,

Tupe basi uzoefu wako dada!
 
Nionavyo mie ni tabia ya watu kutothamini umuhimu wa ndoa au maisha ya kuwa na mwenza wa kudumu.kuishi na mtu kweli kazi, lakini kama unathamini uwepo wake utajitahidi kufanya vitu mnavyokubaliana ili msiachane.mfano zamani baba kutokula nyumbani lilikuwa kosa kubwa anatozwa faini.sasa vijana anapita baa anakula mbuzi akija home anabeuwa kweli jamani.mwanamke kwenda kwao kusalimia mpaka ruhusa na mume anacommunicate na wazee wife atakaa siku ngapi.siku hizi mtu anaaga akiwa airport au stendi.na akiwa huko mume au mke hapigi simu hata kusalimia wazee.matokeo yake mama anaaga anaenda kigoma anaishia Sinza.
 
Nionavyo mie ni tabia ya watu kutothamini umuhimu wa ndoa au maisha ya kuwa na mwenza wa kudumu.kuishi na mtu kweli kazi, lakini kama unathamini uwepo wake utajitahidi kufanya vitu mnavyokubaliana ili msiachane.mfano zamani baba kutokula nyumbani lilikuwa kosa kubwa anatozwa faini.sasa vijana anapita baa anakula mbuzi akija home anabeuwa kweli jamani.mwanamke kwenda kwao kusalimia mpaka ruhusa na mume anacommunicate na wazee wife atakaa siku ngapi.siku hizi mtu anaaga akiwa airport au stendi.na akiwa huko mume au mke hapigi simu hata kusalimia wazee.matokeo yake mama anaaga anaenda kigoma anaishia Sinza.

Kweli ndugu,

Kukosa uvumilivu, heshima na ubinafsi ni hatari sana!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Marriage is no longer linked to comfortable life mkuu! Ndo haswaa maana ya moskwito! Walio kwenye ndoa wanalalamika kila kukicha, hadi walioko single hawatamani kuingia ndoani tena! Ukiskia dunia hadaa ulimwengu shujaa ndo hii sasa!
kweli king...

that is why nimeiweka kama option... maana yake ni kwamba if it is not comfortable people have other options na kuiacha katikati, so rather than an opt in bad stuff, it has become kinda like opt to stay in if it is comfortable

kwa kiswahili labda, ndoa imekua kitu kingine ambacho unabaki ndani tu pale inapokua comfortable, au unaingia tu ili uwe comfortable na mtazamo wako au wa jamii .... we are searching for comfort so if ndoa makes you comfortable unaingia au unabaki, kama inaboa unaiacha zake na ku-move on to other comfortable options
 
kweli king...

that is why nimeiweka kama option... maana yake ni kwamba if it is not comfortable people have other options na kuiacha katikati, so rather than an opt in bad stuff, it has become kinda like opt to stay in if it is comfortable

kwa kiswahili labda, ndoa imekua kitu kingine ambacho unabaki ndani tu pale inapokua comfortable.... we are searching for comfort so if ndoa makes you comfortable unabaki, kama inaboa unaiacha zake na ku-move on to other comfortable options

Sure,

That's my very basic and simple principle....

Huwezi kung'ang'ania kuishi na mtu ambaye inaonekana kabisa mambo yamekwama. Mmekutana mkiwa wazima na kwa hiyo ni upuuzi kufikiria kuwa huwezi kuishi bila yeye!!
 
Swahiba/.... wakati wewe unajiandaa kuwasha mshumaa,

Mie nawasha tochi kabisa kuupa heshima yote mwaka 2011... A YEAR THAT WAS/IS, which has been the most exciting year in my life, positively, negatively and every between

My response to this (yet another platinum release) thread of your ni kama ifuatavyo;
Ndoa za zamani hazikua na mikito ya sasa, lakini nazo zilikua na misukosuko yao... waweza pata hayo kuanzia nyimbo za enzi ya shingo ya upanga, moyo wangu, dereva fanya upesi, nalia na moyo, usiondoke you name it; whatever we experience now, ilikuwepo but in a different density
tuonacho sasa ni kuendana tu na kukua kwa technology na knowledge among us (of course with unfortunate muanguko wa wisdom kidogo

KUFUPISHA... MPOROMOKO WA KISASA UNACHANGIWA NA YAFUATAYO
akina mama kujua haki zao zaidi
power of knowledge and alternative life style ambazo zamani zilikua hakuna
public flexibility
Mwisho kabisa ni ile necha ya binadamu kuendelea kuvumbua alternatives, tunaona haki za ndoa za jinsia moja, sayansi hasa IT ilivyoweza kufumua mambo ya tabia na vichocheo vya mwili ambavyo havikuwepo, utundu wa asili wa binadamu na pia ile nafasi ya mwanaume kuwa neutralized na vitu kama ajira, shule, sinema, redio nk... (i guess zamani mume/mke alikua ndio source primary ya habari, mbinu mpya na kila kitu

sometimes huwa nawaza, je Yesu au Mtume Muhammad (SAW) wangekuwepo enzi hizi za twitter, facebook, JF, satellite nk wangekua wana hali gani??? kwani hata akipiga ushuzi tu, dunia itajua

In short current world is dynamics and people have more options than just a MARRIAGE.... AND MARRIAGE IS SLOWLY TURNING INTO "JUST ANOTHER OPTIONS FOR LIVING A COMFORTABLE LIFE"

nakuacha na swali: Kama sio uchoyo wa watawala wa mwazo (werevu) ndoa ingekuwa nucleus ya human reproduction?

Hivi Mbu hizo sheria zinamsaidia mwanamke kwasababu tu ni mwanamke au kwasababu anakua anastahili?

Kwanini mnalalamika sana kwamba hizi mpya zinawanyanyasa nyie wakati za zamani ziliwanyanyasa wanawake zaidi? Kwanini msikae chini na kutafuta balance badala ya kutaka nyie ndio muwe wanyanyasaji? Usipompa mtu sababu, hatokua na sababu.Huwezi kuwa mwanaume mnyanyasaji alafu mke akaamua kukuacha na sheria ikamuunga mkono alafu wa kulalamika ukawa wewe.Heshimu uheshimiwe, tenda haki utendewe haki. Hapa naona ubinafsi ndio unaotawala zaidi, ile dhana ya "kwanini mimi ndio ninyanyasike" ndio inayochangia ndoa kutofika popote.Anzeni kufikiria "kwanini tunyanyasane" muone kama hakutakua na mabadiliko.

....nimeipenda hiyo swahiba! ...hivi kuna mtu atayekubishia kweli hapa?
tofauti ya zamani kwamba ndoa ilikuwa mtu anaoa/olewa kwenda kuanzisha mji/familia yake...sasa hivi
panaangaliwa wapi penye unafuu wa maisha bila kuangaliwa athari za maisha ya pamoja na sacrifices zake.

safi sana mkuu... umeliweka sawa kabisa kamanda
.

Ndoa is a two way street, ila kwa ubinafsi (bora ninyanyase mimi kuliko ninyanyaswe) baadhi ya watu wanataka kuifanya one way street.Mwenzi atangulie mbele wao nyuma kufuatilia na kumuendesha. Hata ikimbidi kugeuka na kurudi nyuma unamzuia kwasababu uko kwenye nafasi ya kufanya hivyo. Badala ya kumlazimisha mtu aendelee kuwepo kwanini nguvu msiweke kwenye kumshawishi taratibu na kumpa sababu za kuendelea kuwepo? Msipobadilika nyie kama wanaume inabidi tuandike hasara linapokuja swala zima la ndoa, kubalini mabadiliko and make the best of it badala ya kuona hamtendewi haki kwakua mmenyang'anywa haki ya kunyanyasa.

Yani kwa vyovyote vile, mmoja akifikia kujiona bora kuliko mwenzake, akaona yeye ana haki kuliko mwenzake kiwango cha kufanikiwa pamoja nacho kinashuka.

...dahhh, kwahiyo Lizzy wadhani ile miongozo ya vitabu vya kiimani iliyowaongoza wazee wetu karne na karne na kwa kiwango kikubwa ilisaidia kusimamia misingi ya familia weye waiona haifai kwa kizazi hiki? Hapa kwa makusudi kabisa nimekuunga mkono zile mila potofu zilizokuwa zinamkandamiza mtoto wa kike na mwanamke, lakini hata maandiko ya kidini yamesisitiza uongozi wa mwanaume na jinsi mwanamke anavyotakiwa aishi kwenye ndoa...


Marriage is no longer linked to comfortable life mkuu! Ndo haswaa maana ya moskwito! Walio kwenye ndoa wanalalamika kila kukicha, hadi walioko single hawatamani kuingia ndoani tena! Ukiskia dunia hadaa ulimwengu shujaa ndo hii sasa!

...shabaash!....

huu nao ni mtazamo mwingine unaokinzana na wa MTM, yaani ni sawa na muono wa bilauri kama ni half full, au half empty...kamanda alitaja ndoa kama an option ya comfortable life, nawe wasema not linked anymore....nyote mko sawa kabisa... NDOA IMEPOTEZA MAANA YAKE!
 
mimi nadhani wazazi muwaelimishe watoto kuhusu ndoa tusisubiri mpaka kitchen party, na tutumie vitabu vya dini pia kuwaelewesha watoto, tukae nao mara kwa mara na kuwaelewesha maisha jinsi yalivyo including ndoa ili mtoto aone dhamani ya kuwa mke/mume, na nyyie wazazi muache ubusy.
*pia wazazi muwe mifano mizuri kwa watoto wenu vyo mnagombana mpaka watoto wanajua kama mama na baba wanagombana.

...yanafanyika sana tu haya majumbani, ila ndio kama wachangiaji wengine waliopita walivyotanabahisha, utandawazi nao umeleta athari zake kubwa tu kwenye jamii yetu hii ambayo inatupelekea kutafuta maisha kwa kwa majibu rahisi...mzazi akiwa mtu wa kukemea sana kwa mujibu wa maandiko matukufu ataambiwa ni old fashioned!
...ni wangapi miongoni mwetu tunaozingatia kuhudhuria nyumba za ibada angalau mara moja kila wiki? hofu ya Mwenyezi Mungu imepungua....
nini kifanyike sasa? .....


Ila kuna siku dunia itakuja jua mahali mwanadamu alipoteleza,na itaku too late,kama kweli unataka ulitumie gari vizuri ni lazima usome "manyuo buku"!Kama ukilitumia vile unavyotaka wewe kisa hutaki "utumwa" kubali matokeo yake ambayo lazima yatakua hasi tu!Ukiyakataa lazima kifaa ulichopewa kuchambua mambo(ubongo)kitakua na mushkeli.

....sasa mkuu hiyo manual book si ndio hivi vitabu vya kiimani vinavyopigwa vumbi makabatini bana? misahafu, biblia, nk...nk...ila kwa sie kujifanya twajua sana, tunajaribu ku link tafsiri za maazimio ya Beijing katika maisha yetu ya kila siku kuzitafsiri haki za mwanamke...au ni wanaume wamepoteza uwezo wao wa kuwa kichwa cha familia kama mafundisho yalivyotaka?

nani alaumiwe?


Nionavyo mie ni tabia ya watu kutothamini umuhimu wa ndoa au maisha ya kuwa na mwenza wa kudumu.kuishi na mtu kweli kazi, lakini kama unathamini uwepo wake utajitahidi kufanya vitu mnavyokubaliana ili msiachane.mfano zamani baba kutokula nyumbani lilikuwa kosa kubwa anatozwa faini.sasa vijana anapita baa anakula mbuzi akija home anabeuwa kweli jamani.mwanamke kwenda kwao kusalimia mpaka ruhusa na mume anacommunicate na wazee wife atakaa siku ngapi.siku hizi mtu anaaga akiwa airport au stendi.na akiwa huko mume au mke hapigi simu hata kusalimia wazee.matokeo yake mama anaaga anaenda kigoma anaishia Sinza.

...umezungumzia ya maana sana sana, heshima na uthamani wa taasisi hii....no wonder leo hii kuna hata malalamiko ati kuna baadhi ya wake majumbani wameacha kabisa majukumu yao na kuyakabidhisha kwa wasaidizi wa ndani (house girls)....lakini pamoja na hayo, je? ni wanawake tu wanaohusika katika kuporomosha maadili ya taasisi hii???
 
Sure,

That's my very basic and simple principle....

Huwezi kung'ang'ania kuishi na mtu ambaye inaonekana kabisa mambo yamekwama. Mmekutana mkiwa wazima na kwa hiyo ni upuuzi kufikiria kuwa huwezi kuishi bila yeye!!

...sasa mkuu kishindo kinakuja je?

kama ndoa zilikuwa ndio mhimili madhubuti wa familia, leo hii ndoa zinapuuziwa as if ni optional tu?
vipi athari zake kwa watoto na vizazi vijavyo? tunatengeneza taifa na watu wa aina gani, maana ikumbukwe... hapo zamani za kale, ndoa ilihusisha FAMILIA.
 
Aiseee hii mada tamu sana, ila wanaume wa siku hizi kwanza anaona kukuoa ni kama favour flan anakupa, ndo maana hata akiwa anatongoza tu anatanguliza ntakuoa, na akisha kuoa anategemea so much from you (to replace his mother) wakati huo yeye hayupo prepared to do anything hata vile vidogo anavyotakiwa kufanya.

Pili anaona amekupa favour kukubebesha minba, kwani anauwezo wa kuwapa wanawake wengine. now imagine living with a man with this kind of mindset ndo maana watu hawadumu na hizo ndoa,
 
Sababu ya ndoa za leo kutokudumu: This age we have a lot of negotiations. From the morning to the evening, from the sitting room to the bedroom, every where! Ni kwa wale tu ambao wako tayari kwa havoc hii ndo watadumu na ndoa.Ndoa za zamani wamama walikuwa kama ilivyo kwenye kile kipande cha movie la Eddy Murphy," COMING TO AMERICA". Mwambie mama kubweka atabweka,lakini leo thubutu yako,utashangaa una Asha ngedere ndani mwako. Let's go with the era!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Niliwahi kuelezea kitabu kimoja ambacho kinajadili haya mambo ya muhimu kwenye ndoa (marriage triangle...love, sex and living together) wapi pa kuanzia...Which to me, nakubaliana na mwandishi kwamba unaweza kuanza na lolote. Kama unajitambua, hakuna shaka kwamba ndoa yako itakuwa imara!!

Hebu chungulia hapa,


Amazon.com: I Married You (9780966396669): Walter Trobisch: Books


na hii ya kuanza na sex, mbona mara nyingi huwa zinafell tena hazifiki kabisa kwenye ndoa, na wanajamii watakwambia usingemvulia kwanza mpaka akuoe, nadhani kudumu kwa ndoa au mahusiano yeyote ni mpaka ukutane na mtu mnaendana, mnasikilizana
 
na hii ya kuanza na sex, mbona mara nyingi huwa zinafell tena hazifiki kabisa kwenye ndoa, na wanajamii watakwambia usingemvulia kwanza mpaka akuoe, nadhani kudumu kwa ndoa au mahusiano yeyote ni mpaka ukutane na mtu mnaendana, mnasikilizana
Kama mnaendana hata mkikutana leo na kuona kesho mtadumu, kama hamuendani hata mkikutana wote ni bikra, mkakaa kwenye uchumba muda mnaodhani unatosha na ndugu wote wakawaunga mkono bado kudumu kwenu kutakua kwa mashaka.
 
Back
Top Bottom