Ndugai amefuata utaratibu wa kujiuzulu Uspika kwa mujibu wa Katiba. Mbatia hayupo sahihi na kesi yake haina mashiko

Ndugai amefuata utaratibu wa kujiuzulu Uspika kwa mujibu wa Katiba. Mbatia hayupo sahihi na kesi yake haina mashiko

Nafasi ya U spika inahudumia Watanzania regardless tofauti zetu za kiitikadi,means hawezi akawa anawajibika katika system's za kichama ,speaker alitakiwa awasiliane na Bunge sio political party ndio maana halipwi na political party,tatizo ni KATIBA na mbaya zaidi ccm wamejimilikisha nchi yetu,yaani wanaiona ni sehemu ya Lumumba na wengineo wote ni wakimbizi,Tanzania it belongs to all of us na wote tunawajibika kwa ustawi wake.
Mkuu una hoja tena hoja mujarab kabisa ila kidogo imetoka nje ya mada. Hoja ya msingi kwenye mnakasha huu as per mleta mada ni; "Je, Bunge limepata taarifa ya kujiuzulu kwa Spika au halijapata?". According to mleta mada ni kwamba Katiba inaeleza tu Bunge lipewe taarifa ila kwa utaratibu upi, Katiba iko kimya.

Sasa kuna hoja mbili tu za kujibu ku-prove wrong kwamba "Spika hajajizulu"; mosi, Bunge halijapata taarifa; na/au pili, Bunge limepata taarifa ila utaratibu haukuwa sahihi. Tujikite kwenye hoja mbil hizo.
 
Kwamba Bunge ndo' lilipelekewa copy, ila 'orijino' alipewa katibu mkuu wa CCM[emoji848]
... sidhani kama kuna tatizo kwa sababu unapoletewa copy ni kwa ajili ya nini? "KWA TAARIFA"; so Bunge lina taarifa.
 
Mbatia anatembelea matukio kutafuta kiki,
Katiba imekanyagwa mara nyingi sana huko nyuma,hakuwahi kujitokeza kufungua kesi,
Leo hii ameona Nini?
Kipi ni Bora , kuendelea katika makosa au kuanzia upya bila makosa , au mtu akikosea njia huko nyuma hatakiwi kurudi kwenye njia sahihi , Bali aendelee katika makosa ? Hakuna mtu sahihi duniani kote, hata mbinguni wapo wa kuhesabu
 
Kumekuwa na mjadala kutoka baadhi ya watu mbalimbali mtandaoni juu ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Spika Mh Job Ndugai.

Ulianza mjadala kwamba kwanini ktk barua yake ameandika herufi kubwa pekee? KIMSINGI kilichosambaa mtandaoni siyo barua bali ni TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA HABARI ambayo ni sawasawa tu na TANGAZO. Katika uandishi TANGAZO/TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NI KAWAIDA SANA KUANDIKWA KWA HERUFI KUBWA PEKEE. Barua za kujiuzulu zimewasilishwa katika bunge na katika Chama cha Mapinduzi.

Jambo la Pili nimeona Ndg James Mbatia amesema anakusudia kupeleka kesi mahakamani kupinga utaratibu uliotumika ktk kujiuzulu kwa spika. Kwamba kwa maelezo ya Mbatia ni kiwa Spika alitakiwa aende bungeni kujiuzulu kupitia ktk kamati ya bunge na bunge lenyewe.

Kimsingi hoja yake siyo sahihi. Kwa maoni yangu Mh Spika amefuata utaratibu wa kikatiba na ametimiza matakwa ya kisheria katika mchakato wa kujiuzulu.

Ukisoma katiba ya JMT sura ya 11 ibara ya 149(1)(c) imeeleza wazi kuwa endapo Spika au Naibu spika anataka kujiuzulu anatakiwa kuwasilisha taarifa hiyo katika bunge. Katiba haijatoa masharti kuwa taarifa hiyo iwe ktk mkutano, kamati au kwa barua original au nakala ya barua? Katiba imetaka tu kuwa Spika atoe taarifa katika Bunge.

Mh Spika Job Ndugai katika kujiuzulu ametoa taarifa katika bunge na chama cha mapinduzi na kwamba KWA KUWA BUNGE LIMEKIRI KUPOKEA TAARIFA YA KUJIUZULU KWA SPIKA (KAMA TAARIFA YA KATIBU WA BUNGE INAVYOJIELEZA) Basi tuhitimishe kwa kusema Spika amewasilisha taarifa yake ktk bunge na amefuata taratibu za kisheria za kujiuzulu kwa spika.

Kwa lugha rahisi Spika amejiuzulu kisheria na uchaguzi wa Spika mwingine utafanyika mwezi Februari kama ilivyotangazwa na BUNGE katika taarifa yake ya vyombo vya Habari.
View attachment 2072949
Toa taarifa na si nakala ya taarifa, sijui unatumia kiswahili cha wapi!
 
Kipi ni Bora , kuendelea katika makosa au kuanzia upya bila makosa , au mtu akikosea njia huko nyuma hatakiwi kurudi kwenye njia sahihi , Bali aendelee katika makosa ? Hakuna mtu sahihi duniani kote, hata mbinguni wapo wa kuhesabu
Sorry uliwahi kuishi Mbinguni?
 
Mbatia anatembelea matukio kutafuta kiki,
Katiba imekanyagwa mara nyingi sana huko nyuma,hakuwahi kujitokeza kufungua kesi,
Leo hii ameona Nini?
Ni kweli kabisa.Ndugai amenajisi katiba kwa kuwakumbatia wabunge 19 walio jichagua bila ridhaa ya chama Chao.Mbatia atuambie kama taratibu zimefuatwa,kama Sheria, kanuni na taratibu hazikufuatwa, nadhani hapa ndiyo angeshitaki kwa kutofuata Sheria.Kinyume Cha hapo ni usanii tu.
 
Yawezekana unajua kusoma na kuandika vizuri ila umekosa analytical thinking.

Kwa fikra zako, na kwa uelewa tu wa kawaida, hivi tuseme umeajiriwa na kampuni fulani, kabla ya kuajiriwa ulidhaminiwa na Baba yako, unaweza kujiuzulu kazi kwa kumwandikia barua baba yako, na anakala ukampelrkra mwajiri wako?

Katiba ipo wazi, spika akitaka kujiuzulu anapeleka taarifa Bungeni, huko kwenye chama chake, hakuna mahali popote katiba imetamka. Unaacha kitu kilichotamkwa kikatiba, unaenda kufanya upuuzi halafu unasema katiba imefuatwa!
Asante Sana Mkuu. Umefunga kazi
 
Watu wanasema lile sio bunge la CCM ni bunge la wananchi sasa kwanini Ndugai amwandikie Chongolo.


Umeelewa au bado?
Alimwandikia Chongolo lakini pia alimpa nakala katibu wa bunge, kwanini? Kwasababu alitaka pia katibu wa bunge ajue.
 
Kikubwa ni Bunge kupata taarifa ya kujiuzulu kwake.

Suala la kukitaarifu chama kilichomdhamini ni hiyari yake na wala siyo kosa na haiathiri ukweli kuwa bunge limepewa taarifa ya kujiuzulu kwa spika na bunge lenyewe limekiri
Soma vizuri hiyo ibara ya 149 kifungu kifungu kidogo cha kwanza tangu mwanzo kisha soma hiuo 1(c) na uunganishe. Msharti yaliyoainishwa ya kujiuzulu kwanza ni kuandika barua ya kujiuzulu na kuitilia saini kwa mkono wake, kisha kuipeleka hiyo taarifa / barua kwa bunge. Maana yake ni kuliandikia bunge (barua zote zinazoelekea bungeni huandikwa kwa katibu wa bunge), na si vinginevyo!!
Ndiyo maana pamoja na kupokea nakala ya barua hiyo, katibu wa bunge hawezi kuanzisha mchakato wa kupata spika wa bunge!! Katibu mkuu wa ccm hana mamlaka ya kupokea barua ya kujiuzulu ya spika!! Spika angekuwa amejiuzulu uanachama wa ccm hapo ndipo angepaswa kumwandikia katibu mkuu wa ccm!!
Wala katibu mkuu wa ccm hana mamlaka ya kikatiba kumwandikia katibu wa bunge akimtaarifu juu ya kujiuzulu kwa spika maana barua hiyo lazima iwe na saini ya spika KWA MKONO WAKE!!
Wasipolizingatia hili unaweza kuzuka MGOGORO MKUBWA WA KIKATIBA, iko hivi: Kama wakipuuza utarstibu huu wa kikatiba kama inavyoelekea kutokea, katibu mkuu wa ccm atamwandikia barua katibu wa bunge akimtaarifu kuwa Ndugai kajiuzulu, na katibu wa bunge akaikubali taarifa hiyo na kuanzisha mchakato wa kuchagua spika mpya, KIKATIBA MCHAKATO HUO NI BATILI, NA SPIKA ATAKAYECHAGULIWA NI BATILI, NA VIKAO VYOTE VYA BUNGE NA KAMATI VITAKAVYOKAA CHINI YA SPIKA BATILI. I BATILI PIA, NA MAAMUZI YOTE YATAKAYOFIKIWA CHINI YA SPIKA BATILI NI BATILI PIA!! Mgogoro wa kikatiba utaanzia mtu atakapogoma kutekeleza maamuzi au wito wa spika kwa madai kuwa hayatambui maamuzi ya bunge maana nj BATILI na hautambui wito wa spika maana naye ni SPIKA BATILI!! Mwisho wa siku ngoma ITATUA MAHAKAMA KUU, kwa maana mtu huyo atashitakiwa!! Huko mahakamani atatoa sababu kwa nini maamuzi hayo ni batili!! Kuna uwezekano mtu huyo wataogopa kumshitaki ili kuepusha MGOGORO, lakini watu watajua na maamuzi ya bunge yatapuuzwa na watu wengi mwisho wa siku mgogoro utafika mahakamani tu!! Huko mahakamani ITATAMKWA RASMI SPIKA NDUGAI BADO NI SPIKA HALALI MAANA BADO HAJAMWANDIKIA KATIBU WA BUNGE KIHUSU KUJIUZULU KWAKE NA IKAO VYOTE VYA BUNGE VILIVYOKAA CHINI YA SPIKA BATILI NI BATILI PIA!!!! Ifanyike jitihada ya kuepusha mgogoro huo mkubwa wà kikatiba!! Soma tena ibara hiyo ya katiba kwenye post #1.
 
Mbatia anatembelea matukio kutafuta kiki,
Katiba imekanyagwa mara nyingi sana huko nyuma,hakuwahi kujitokeza kufungua kesi,
Leo hii ameona Nini?
Anachekesha na anasikitisha.
 
Tukisema vyuo vya Tanzania vinatoa Premature mnakasirika. Kwa akili yako Ndugai angeweza kupiga Simu tu ikawa taarifa?
Punguza hasira. Spika ametoa taarifa katika bunge na bunge limekiri kupewa taarifa hiyo; hivyo spika amezingatia matakwa ya kisheria ktk kujiuzulu

Nakutakia makasiriko mema
 
149(1)(c) Mimi nimeelewa kwamba taarifa ya kujiuzulu inatokewa iwasilishwe bungeni, yaani kwenye mkutano/kikao cha Bunge
Kwa hiyo asubiri hadi kikao ndipo ajiuzulu? We uliona wapi?

Kwenye bunge tafsiri yake ni bunge kupewa taarifa
 
Back
Top Bottom