Uchaguzi 2020 Ndugu Mwita Waitara hautoshi Ukonga. Umefeli ukiwa mpinzani, umeshindwa ukiwa CCM!

mbande hadi msongola mpaka kilimo
HAKUNA LAMI sio hakuna lami tu BARABARA INA MAHANDAKI MAKUBWA YASIOVUMILIKA
 
kama angepiga kazi hata atokee kona ipi ya dunia bado angekua ana nafasi kubwa ya kugombea na kupita.
tuna imani na CCM tunaamini watatupa mtu makini
Then CCM waliwapa mtu makini kabisaaa ndg. Waitara,aki-reflect akili za wananchi wake per se.
 
nashukuru kwa kuufungua huu uzi japo mlikaa nao muda mrefu mods sio vizuri
Hivi Watanzania lini ujinga huu utatutoka? Mbunge hana fedha za maendeleo ya jimbo! Mwenye fedha ni serikali na kupitia halmashauri na taasisi za serikali miradi inajengwa. Sasa kumdai mbunge ni kumuonea au kumbebesha mzigo usio wake.
 
Wabunge wengi wa CCM waliopo mikoa ya Dar es salaam,Iringa na Arusha wanajisahau kutokana na mfumo wa uongozi ulivyo katika hiyo mikoa. Ni kazi sana kujua majukumu ya wakuu wa mikoa hiyo tajwa na viongozi wengine katika hizo sehemu. Wakuu wa mikoa wanataka kufanya kila kitu,usipokuwa makini watu wanaweza jua unazingua kumbe wakuu wa mikoa husika wamepora majukumu ya wengine.
 
Bila kusahau barabara ya kitunda shule kuelekea kibeberu magole ni mbaya kabisa,daraja linalounganisha mwanagati na magole limeshindikana kujengwa ni mwendo wa kuogelea mto mzinga.mheshimiwa mbunge kimyaaaaaa
 
CCM CCM Ahhaaa chama cha mafisadi ccm namba 1 kwauchawi Tunajua ccm namba 1 eeehhh mnisamehe wajameni japo namimi ni mwanaukonga ila imebidi niimbe wimbo pendwa sikujua huko Mwanzo Kama mbunge wangu anapenda Sana nyagi [BAPA]
 
Hilo jimbo nasikia kesha kabidhiwa makonda
 
Hivi Watanzania lini ujinga huu utatutoka? Mbunge hana fedha za maendeleo ya jimbo! Mwenye fedha ni serikali na kupitia halmashauri na taasisi za serikali miradi inajengwa. Sasa kumdai mbunge ni kumuonea au kumbebesha mzigo usio wake.
Alitoa ahadi mwenyewe. Na kwa taarifa yako bora alipokuwa cdm jitihada angalau zilionekama. Mfano culvert pale jirani na majphe mpaka leo zipo na enep lile linapitija.

Huko alikohamia malalamiko ndio haya. Sasa nini kuita wa TZ wenzakp wote wajinga ila wewe.
 
Ujinga hapa nimetumia kuonyesha uelewa wetu ni mdogo.

Sasa kama aliahidi kuwa atafanya hizo kazi ni kwa sababu alifahamu uelewa wa watu aliokuwa anawaahidi hawana uelewa, yaani ni wajinga.
 
waitara jitathimini kabisa hali jimboni ni mbaya.
barabara ya msongola haipitiki hali ni mbaya sanaa.
makorongo yamekua makubwa sana
Msongola niliwahi kwenda 2013 hali ilikua ni duni sana, inasikitisha mpk sasa barabara bado
 
Mwita should https://jamii.app/JFUserGuide off!!!! Hana maana yoyote.
 
Naona ngumu kukubaliana na wewe unaemtetea Waitara kwasababu wakati yuko CDM alitoa ahadi na kutekeleza angalau huko CCM alikohamia anatoa ahadii hatekelezi kabisa.
Ujinga hapa nimetumia kuonyesha uelewa wetu ni mdogo.

Sasa kama aliahidi kuwa atafanya hizo kazi ni kwa sababu alifahamu uelewa wa watu aliokuwa anawaahidi hawana uelewa, yaani ni wajinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…