Ndugu Polepole, nitajie kituo Cha mabasi cha Wilaya au mkoa chenye Hoteli yenye hadhi Kama hoteli binafsi zinazohusu abiria wa safari ndefu

Ndugu Polepole, nitajie kituo Cha mabasi cha Wilaya au mkoa chenye Hoteli yenye hadhi Kama hoteli binafsi zinazohusu abiria wa safari ndefu

Sasa kwa Ile stendi ya matope bukoba magari yasimame wap.

Mpaka makampuni mengine kama friends hayaitumii hiyo stendi mbovu na finyu
 
Kwa hiyo unataka kudhania kuwa wakiwa wanakaa stendi ili kupata chakula hawatakula bure? Tumia akili bro kabla ya kutetea upuuzi.
Nafikiri upuuzi mkubwa wa binaadamu tena mtu mzima ni kufikiria kuwa yeye atakula bure bila kutoa jasho, ni ushenzi uliopitiliza kuwalazimisha watu wazima wafanye kile unavyotaka hata kama ni cha kipuuzi hivyo watu au wasafiri hivi sasa ni wakati muafaka wa kuchagua ale nini na wapi
 
Dah! Ila binadamu bwana tuna mambo!

Malalamiko si yamekuwa yakitolewa humu humu 'repeatedly' kwamba hoteli ambazo mabasi husimama chakula ni ghali sana, hakuna value for money na hakuna options? Kwa hiyo mabasi yatakiwe kuimama sehemu zinazowafaa wananchi wote.

Sasa malalamiko yamefanyiwa kazi, kabla hata utekelezaji haujaanza, waja tunalalamika tena? Eti kwa nini mapendekezo ya walalamikaji yamefanyiwa kazi. Duh!

Kwa hili polepole yuko sahihi sana na amekuwa very efficient. Kama kuna wa kulaumiwa kwenye hilo, basi ni waliolalamika ambao sasa wamepewa wanachotaka kisha wanalalamika tena.

Ni vyema tukawa tunajiridhisha kuwa tunataka nini au hatutaki nini kabla ya kuomba, vinginevyo kama kila ambacho mtu hupewa (hata kama kaomba) analalamika, mwishowe mfanya maamuzi huchanganyikiwa na kuamua chochote ili iwe vyovyote na chanzo cha tatizo la namna hiyo ni 'consumers'.

Mwisho wa siku kulalamika wakati mwingine nayo ni tabia, kuna mtu vyovyote itakavyokuwa tu, atalalamika na kulaumu, yaani ni sehemu ya maisha yake.
Hoja sio repeatedly,hoja ni kwa nini kaitoa polepole??mnafiki
 
wahamie stend tu kwa kweli italeta ushindan.nimesafir from dar to arusha pale korogwe tumeipita vuuu vuuu kwenda kusimama kwenye hoteli mbele.kuuliza sasa menu buffet wal maharag 10,000. chips elfu 10,000, andaz 1000 chai 1000 nikasafir mpkaa arusha bila kula kitu.zaid nikala mosh mjin tena parachich
 
kwanza washenz wao wakikubwagen kwenye hayo mahotel yao.wao sijui hawanaga haja ndogo.moja kwa moja mbio dereva na konda wake kuchkua hela na chakula.nyie wanawapa dk 10 za chakula na choo.anakula yeye haraka haraka unasikia mahoni sasa pippiiii piiii nachukiaga
 
Kutakuwa na ushindani. Na kukiwa ma ushindani bei na huduma zitakuwa rafiki. Kumbuka mabasi yakiwa yanasimama stendi basi mfanya biashara yoyote ana uhuru wa kufungua huduma kwenye eneo husika. Tunarudi kule kule kwenye kanuni yetu. Supply itakuwa kubwa na demand ndogo hivyo bei na huduma zitakuwa nzuri. Sasa hivi wanapotupeleka kwenye hizo hoteli zao ndiyo wanatupiga bei wanayotaka tena kwa kuringa. Umezaliwa lini? Zamani wakati mabasi yanasimama stendi huduma zilikuwa nzuri na bei pia.
muelimishe huyu.hajui tu.
 
Hakuna ndoto mkuu serikali ikiamua itakua tu,tena hao jamaa wa hovyo sana hawaruhusu hata watu kuingia na chakula ndani ya Bus. Pale ni udikteta mwanzo mwisho usipokula unakufa na njaa,bei ya chini chakula buku 8. Labda unywe chai au biskuti.
niliteseka safar moja asee.ndio mara ya kwanza kutumia njia ya arusha af nikapanda hio ngoma.ile tunashushwa hotelin kwao bajet yangu ikawa ndog.nilienda na njaa mpaka arusha
 
kwanza washenz wao wakikubwagen kwenye hayo mahotel yao.wao sijui hawanaga haja ndogo.moja kwa moja mbio dereva na konda wake kuchkua hela na chakula.nyie wanawapa dk 10 za chakula na choo.anakula yeye haraka haraka unasikia mahoni sasa pippiiii piiii nachukiaga

Hawa madereva ni wapumbafu na hawana ubinaadamu kabisa, kwanini wasiige kwa wenzao wanaosafirisha ng'ombe kutoka kanda ya ziwa kwenda dar wao wakifika maeneo ya morogoro dumila hushusha ng'ombe wote na kuwalisha kwa siku mzima kabla ya kuendelea na safari
 
Kuna hoja ameiwasilisha Polepole kwenye television (chanel 10) kipindi cha papo kwa papo nakuungwa mkono na Mhe Waziri kwamba mabasi badala ya kwenda kwenye hoteli zenye hadhi na chakula salama wawapo safarini Basi mabasi hayo yasimame kwa muda mrefu stand watu wale chakula nakupata huduma nyingine.

Haya maamuzi ni maamuzi yanayosukumwa na watendaji ambao wanatumia mashangingi ya serikali na chama na ambao hawapandi bus kwenda popote. Leo hii vituo vya mabasi vinafahamika, havikujengwa kwa lengo lakutoa huduma ya chakula kwa abiria bali vimejengwa kama points zakusubirua abiria wapande na kushuka. Vituo hivi vina matundu machache sana yakujisaidia na huduma hii inagharamiwa huku kukiwa hakuna usafi Wala maji yakutosha.

Standard yavituo vyetu haikidhi viwango vyakuhudumia abiria labda tuingie kwenye uwekezaji mpya wa kuvikarabati

Turudi kwenye gharama ya chakula, gharama ya chakula inategemea na eneo unapopata huduma. Inashangaza Leo hii uniambia gharama ya Serena hoteli ilingane na gharama ya mama ntilie kisa wananchi wamelalamika.

Kama tutataka kuweka usawa tufike pointi tujadiliane na watoa huduma, wale wamiomiliki wanaopenda wakae stand muda mrefu wajitangaze ili abiria wajue bus ili linasimama stand kwa ajili ya chakula na bus ili linasimama hotel binafsi kwa ajili ya chakula....abiria wachague watapanda gari gani lakini si kulazimisha watu wote waishi, wasafiri na kula kwa maelekezo ya Waziri.

Polepole umechemka acha siasa kwenye huduma, pokea kero wakabidhi vijana wa chama wazifanyie utafiti the waishauri serikali njia inayofaa siyo kumlazimisha Waziri atoe msimamo wa kisera kwenye media.....w
Una hoteli nini? Au yawezekana haujawahi kukumbana na usumbufu huu.
 
Cha msingi hapo.

Kwa maoni yangu. Hayo mabasi yasimame kote.

Kwenye hotel na stend ili kuwasaidia na wale ambao hawana pesa ya kumudu kununua chakula hotelini.
Na ndivyo Waziri alivyosema wakati akiongea na Babu Pole Pole
 
Mnataka kutuletea migahawa ya NANGURUKURU huku kaskazini.? Bakini nayo huko huko njia ya Kusini. Kuna siku nilienda Mtwara magazine 2 yakasimama nangurukuru vyoo vya wanaume ilikuwa kwa foleni. Kuna mama alikuwa na visamaki kumi havikutosha kitu abiria wrote waliondoka na njaa zao. Chonde chonde tuacheni KASKAZINI na ustaarabu wetu
 
Sasa kwa Ile stendi ya matope bukoba magari yasimame wap.

Mpaka makampuni mengine kama friends hayaitumii hiyo stendi mbovu na finyu
Kunamajani ya migomba mengi sana wanaweza wakayatandika Bukoba yote na hapo kituoni, kama wahaya waliweza kubuni kufunga tai hilo la kutandika majani ya migomba litawashinda?
 
Watu najua solution ikitolewa na Mwana CCM itapingwa kwa sababu ya Uchama. Mimi nimeshawahi bus likasima sehemu flani ya kawaida sana chai kikombe kidogo ya rangi tsh 1,000 na chapati ya kawaida ambayo mtaani ni tsh 500 wao wanauza tsh 2,000. Sababu ni kuwa Bus ndo linasimama pale na ni huo Mgahawa mmoja upo peke yake.
 
Back
Top Bottom